TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, May 7, 2012

RAIS AWAHAPISHA MAWAZIRI IKULU LEO


 Rais Dk. Jakaya Kikwete akiwa katika viwanja vya Ikulu leo mara baada ya kumaliza kazi ya kuwaapisha mawaziri na manaibu waziri wapya aliowateua hivi karibuni, Mwandishi wetu ameshuhudia tukio hilo kwenye viwanja vya Ikulu  leo
 Naibu waziri wa Sayansi na Teknolojia January Makamba akihojiwa na mtangazaji wa BBC mara baada ya kuapishwa leo.
 Rais Dk Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Said Mwema.
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na mmoja wa watoto walliohudhuria na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo ya kuapishwa kwa mawaziri
 Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkuu wa Majeshi nchini Jenerari Davis Mwamunyange kushoto ni Waziri wa Ulinzi Shamsi Vuai Nahodha
 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk Fenela Mukangara akila kiapo mbele ya Rais Jakaya Kikwete leo.
 Naibu waziri wa Sayansi na Teknolojia January Makamba akila kiapo.
 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angela Kairuki akila kiapo
 Mwandishi wandamizi wa Magazeti ya Mwananchi Communication Bathoromeo Mkinga akisaidia mzee Sabodo kuelekea katika eneo la kukaa wageni waalikwa, kushoto ni Waziri wa Wanawake Jinsia na Watoto Mh. Sophia Simba.
Ridhiwan Kikwete akizungumza na aliyekuwa rais wa Yanga Jamal Malinzi wakati wa hafla hiyo katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es salaam leo.
 Miraji Kikwete akiwa na wadau wengine katika hafla hiyo
 Rais Jakaya Kikwete akipiga picha ya pamoja na mawaziri pamoja na manaibu waziri mara baada ya kuwaapisha leo.
 Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na manaibu Waziri mara baada ya kuwaapisha leo Ikulu.

RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA ATINGA KIZIMBANI KUTOA USHAHIDI KATIKA KESI YA BALOZI MAHALU

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo, kutoa ushahidi wake katika kesi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa  Costa Mahalu,  anayekabiliwa na shtaka la uhujumu uchumi.

Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa akiondoka Mahakama hapo baada ya kutoa ushahidi wake.

WABUNGE WA CHADEMA WADAI KUTOKUBALIANA NA UTEUZI WA BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI


NA PAULINE KUYE -NJOMBE
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakijakubaliana na baraza la Mawaziri ambalo limeapishwa leo na Rais wa Jamuhuri ya Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete.
 
katika Mkutano wa hadhara uliofanyika Mkoa mpya wa Njombe kwenye uwanja wa polisi Makambako uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi na viongozi mbalimbali wa CHADEMA akiwemo Mbunge wa Iringa mjini Mheshiwa Peter Msigwa, Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi na Mbunge wa Mbozi Magharibi ambaye pia ni katibu wa CHADEMA Tanzania Mheshimiwa David Silinde,wamesema uteuzi huo mpya wa baraza la mawaziri uliofanywa mei 4 mwaka huu sio suluhisho la matatizo ya Watanzania.
 
 Kwa upande wake Silinde amesema kuwa, kinachotakiwa kifanyike ni kubadilisha mfumo mzima na wale wote ambao wametajwa kwamba ni wezi wa mali za umma waende jela na wafilisiwe na si kuachwa bure.
  
Naye Mchungaji Peter Msigwa amesema kuwa Chama cha mapinduzi ni ukoo mmoja, wote wanafanana kitabia, kwa kubadilisha Baraza la Mawaziri kutoka nafasi moja kwenda nyingine haiwezi kusaidia kutatua ubadhilifu wa mali ya umma kwani bado ukoo ni ule ule.
 
Katika ziara hiyo matawi matatu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo pamoja na ofisi moja ya kata ilizinduliwa, huku zaidi ya wanachama wapya 600 walijiunga na chama cha CHADEMA

MKUU WA MKOA WA RUKWA AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU NNE YA UANDISHI WA HABARI ZA UCHUMI NA BIASHARA MKOANI RUKWA LEO

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na washiriki wa semina hiyo leo wakati akifungua mafunzo hayo rasmi yaliyoandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) na kuratibiwa na Klabu ya Waandishi wa Habari ya Rukwa (Rukwa Press Club). Mafunzo hayo yatadumu kwa muda wa siku nne na jumla ya washiriki 18 kutoka vyombo vya habari tofauti vya Mikoa ya Rukwa na Katavi wanashiriki. Katika maneno yake ya ufunguzi Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka waandishi wa habari wa Rukwa kuhakikisha kuwa wanatumia nafasi yao vizuri kutangaza vivutio na fursa zinazopatikana Mkoani Rukwa kwa wadau ili kuvutia wawekezaji.
Muwezeshaji wa mafunzo hayo Ndugu Mnaku Mbali ambaye ni Muhariri wa gazeti la Business Times la jijini Dar es Salaam. Lengo kubwa la mafunzo hayo alisema ni kuwajengea uwezo zaidi waandishi wa Rukwa waweze kuandika habari za biashara na uchumi katika uelewa chanya kwa maendeleo ya jamii ya Rukwa na Taifa kwa ujumla.
Mkurugenzi na muendeshaji wa Blog ya Pembezoni Kabisa ambaye pia ni mwandishi wa gazeti la Mwanachi Mussa Mwangoka kulia na Joshua Joel wa ITV na Radio One wakifuatilia mafunzo hayo.
Baadhi ya washiriki wengine kutoka Rukwa na Katavi wanaoshiriki mafunzo hayo. Wapili kulia ni mdau Ernest Kibada kutoka Katavi.
Washiriki wa Mafunzo hayo wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya leo.

MAMA TUNU PINDA APOKEA MICHANGO YA SH. 16M/-


Mke wa Waziri Mkuu Tunu Pinda pamoja na Kaimu Katibu Mkuu wa Chaneta Rose Mkissi wakipokea vifaa vya michezo kwa ajili ya timu ya taifa ya Netiboli-  Taifa Queens kutoka kwa Meneja wa Mahusiano ya Nje wa Vodacom Bw. Salum Mwalim. Vodacom imeipatia Taifa Queens vifaa mbalimbali vyenye thamani ya Shilingi Milioni Sita kuwezesha ushiriki mzuri wa timu hiyo kwenye mashindano ya Afrika yanayoanza kesho (Jumanne Mei 8, 2012) jijini Dar es salaam. Wa kwanza kulia ni mjumbe wa kamati ya maandalizi ya mashindano Shiza Mwakatundu.
 
 MKE WA WAZIRI MKUU Mama Tunu Pinda leo amepokea michango kutoka kwa kampuni za Vocacom na Zantel ikiwa ni mwitikio wa ombi lake kwa Watanzania kuwaomba waichangie timu ya Taifa ya Netiboli (Taifa Queens).
Mama Tunu Pinda amepokea vifaa vya michezo kwa ajili ya mashindano kutoka kampuni ya Vodacom Tanzania vyenye thamani ya  sh. milioni sita. Vilevile, Mama Pinda  amepokea simu za mkononi 300 zenye simcard na muda wa maongezi kwa ajili ya wachezaji na viongozi wao kampuni ya Zantel zenye thamani ya  sh. milioni 10/-.
Makabidhiano hayo yalifanyika leo mchana (Jumatatu, Mei 7, 2012) kwenye makazi ya Waziri Mkuu Oysterbay, jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi vifaa hivyo vya michezo hiyo, Meneja Mahusiano ya Nje wa VODACOM, Bw. Salum Mwalimu alisema wameitikia wito wa Mama Pinda wa kuichangia timu ya Taifa Queens kwa sababu wametambua umuhimu wa kuiunga mkono timu hiyo.
“Vifaa tulivyotoa ni jezi 20, tracksuit 20, raba pea 20 na bibs 20… tuna imani timu yetu ya taifa itaweza kupenya hadi ngazi ya fainali,” alisema.
Naye Meneja Biashara wa Zantel, Bw. Ahmed Mokhles akikabidhi simu hizo, alisema wametoa mchango huo kwa sababu wanaamini kwamba japokuwa watakuwa hapa nchini, wachezaji na maafisa wao wana haki ya kuwasiliana na familia zao.
“Kwa kutambua hilo, tumetoa simu 300 zenye muda wa maongezi ambapo mtu akiongeza muda wa maongezi, ataongezewa muda mwingine wa sh. 10,000/- kila mwezi kwa muda wa miezi mitatu.”
Pia Zantel walitoa router mbili kwa ajili ya ofisi za Chama cha Netiboli Tanzania (CHANETA) ili ziweze kuwasadia katika mawasiliano yao ya internet.
Mama Tunu Pinda aliwashukuru makampuni yote mawili kwa michango yao, na akatumia fursa hiyo kuwashukuru zaidi Watanzania waliojitokeza kwa wingi kuchangia mashindano hayo.
Akitoa ufafanunuzi kuhusu michango ambayo imekwishatolewa hadi sasa, Mama Pinda alisema jumla ya sh. 178,230,000/- zimekwishapokelewa hadi sasa zikiwa ni fedha taslimu na vifaa. Kati ya hizo, sh. milioni 114.8 ni fedha taslimu na sh. milioni 53.4 ni vifaa vilivyotolewa na wadau mbalimbali kuchangia mashindani hayo.
Alisema bajeti nzima ilikuwa sh. 158,439,000/- ambapo sh. 82,656,000 zilikuwa ni gharama za kuendeshea kambi ya maandalizi ya timu ya Taifa Queens na sh. 75,780,000/- zilikuwa ni kwa ajili ya kuendesha mashindano yanayotarajiwa kuanza kesho.
Tanzania kupitia CHANETA imepewa heshima ya kuandaa Mashindano ya Netiboli ya Kombe la Afrika ambayo yanatarajiwa kuanza kesho saa 8 mchana (Jumanne, Mei 8-12, 2012). Mashindano hayo yanayojumuisha nchi saba za Botswana, Lesotho, Zimbabwe, Zambia, Uganda, Malawi na Tanzania yatafunguliwa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.

Ziara ya Rais Dk. Mohamed Shein Kusini Unguja

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(kushoto) akipokea taarifa ya kazi za utekelezaji
wa Mkoa wa Kusini Unguja,kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa huo Abdalla
Mwinyi Khamis, leo alipoanza ziara yake na kutembelea miradi mbali
mbali ya maendeleo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati) na ujumbe aliofuatana nao wakitoka
kuangalia mnara wa Redio ulioanza kufungwa  na kampuni ya Ujenzi ya
Minara ya New Techinical Contractors Company ya Dar es Salaam,chini
Injinia Stivin Makange,(mwenye tai)huko Bungi Wilaya ya kati Unguja
 leakiwa katika ziara ya Moa wa Kusini Unguja.[Picha na Ramadhan
Othman,Ikulu.]
Afia Tawala wa Mkoa wa Kusini Unguja Sabri Mohamed,akisoma
taarifa ya Mkoa wa Kusini Unguja,mbele ya Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipowasili
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini huko Tunguu,katika ziara ya kutembelea
maendeleo ya miradi mbali mbali ya Mkoani humo iliyoanza leo.[Picha
na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar,walioshiriki katika ziara ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,wakisikiliza kwa Makini
taarifa ya Mkoa wa Kusini Unguja iliyosomwa na Afisa Tawala wa  Mkoa
Sabri Mohamed (hayupo pichani).[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) akipata maelezo kutoka wa Katibu Mkuu wa
Wizara ya Habari Utamadunu na Michezo Ali Mwinyikai alipotembela eneo
jipya linalojengwa Mnara wa Redio wa kurushia matangazo huko Bungi
Wilaya ya Kati Unguja,alipokuwa katika ziara ya Mkoa wa Kusini
leo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akisalimiana na Mzanzibar anayeishi nje
ya Nchi Dr. Ferouz Jafferji,alipowasili katika Skuli ya Sekondari ya
Unguja Ukuu alipotembelea madarasa  ya kusomea yaliyokarabatiwa na
umoja wa Diyasphora pamoja na kuweka jiwe la msingi nyumba ya
Madaktari iliyopo Jirani na Skuli hiyo leo,akiwa katika  ziara ya
Mkoa wa Kusini Unguja iliyoanza janakutembelea miradi mbali mbali ya
maendeleo katika ya  Mkoa huo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

SERIKALI YATAKIWA KUINGILIA KATI MGOGORO WA MAJI KATI YA DAWASCO NA WAKAZI WA MALAMBA MAWILI MBEZI


WAKAZI  wa Malamba Mawili  Mbezi  jijini Dar es Salaam, wameitaka   serikali  kuingilia kati  mradi wa maji katika eneo lao, baada ya Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka (DAWASO), kushindwa kutekeleza ahadi yake.
Wamefikia maamuzi hayo  baada ya mamlaka hiyo kukutana na wakazi  pamoja na uongozi wa eneo hilo ikiwataharifu kwamba inatarajia kujenga visima viwili vya maji safi na kuvikabidhi kwao ifikapo Aprili mwaka huu bila mafanikio.
 
Akizungumza na Fullshangweblog jana Mwenyekiti wa eneo hilo  Said Bakari alisema kuwa anashangazwa na hatua ya Dawasa   kukutana na wananchi wakiwemo viongozi  kwa madai ya kutatua tatizo la muda mrefu linalolikabili eneo hilo na kuwatelekeza.
Alifafanua kuwa  kabla mamlaka aijakutana na wakazi hao , awali ilikutana na uongozi wa eneo hilo na kuwapa  semina ya siku .. kwa lengo la kuutambulisha mradi kwa wananchi huku kwa maelezo  kwamba  tatizo hilo litatatuliwa ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu yake.
Alichanganua kuwa maelezo ya awali waliyopewa na shirika hilo yalisema fedha zitakazotumika kuchimbia visima hivyo  ni kutoka katika mfuko wa Rais wa Jamuhuru ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete  jambo ambalo halijatekelezwa hadi sasa.
“Dawasa walituahidi kutuchimbia visima viwili vya maji, ila kwa sasa wamechimba kimoja na hicho hakitoi maji bali kimekaa  na wala hakuna dalili za muendelezo wa zoezi hilo, hivyo basi ikiwa walidhamiria kututatulia tatizo la maji ni bora wangekamilisha malengo yao kuliko kutuacha njia panda tusijue la kufanya wala sehemu ya  kwenda”, Bakari.
Vile vile anafafanua kuwa  kikao kilichowakutanisha viongozi wa eneo hilo na Shirika kilifanyika kabla ya Desemba mwaka jana huku kile kilichowahusisha wakazi hao  kilifanyika 31mwishoni mwa mwaka huo kikitambulisha juu ya kuwepo kwa mradi huo.
“Sisi viongozi wahusika  akiwemo Diwani wa Kata hii hatujui gharama zitakazokamilisha mradi huo mpaka kukamilika kwake, kitu ambachop kinatupa wasiwasi hasa tunapotakiwa kutoa ufafanuzi na wananchi”.
Naye Ofisa Uhusiano wa Dawasa Mery Msuya alipotakiwa kutoa ufafanuzi juu ya mradi huo, awali alilitaka gazeti hili kufika ofisini kwao, hata hivyo, siku iliofuata alisema "Kwa sasa haitakuwa rahisi kwa kuwa niko njiani nikielekea kwenye mkutano Ubungo Plaza" alisema  Msuya. 

SERIKALI YATAKIWA KUWSHIRIKISHA WAFUNGWA KATIKA KUPIGA KURA

NA MWANDISHI WETU
 

SERIKALI imetakiwa kuwashirikisha wafungwa katika mchakato mzima wa kupiga kura, ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kupata haki ya kukutana na wenzi wao hasa wanapokuwa  kifungoni.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa Chama cha kurekebisha Mwenendo wa Watu waliomaliza Kifungo Tanzania (ERST),Dk. Alfred Kaaya alisema kwamba kuna haja ya serikali kushirikiana na chama hicho ili kusaidia kupunguza wimbi la uhalifu nchini.

Kaaya alisema kuwa kitendo cha serikali kutolishirikisha kundi hilo itakuwa haijawatendea haki hususan katika mchakato mzima wa upigaji kura sambamba na katiba mpya.

“Wajibu wa serikali ni kubadili mfumo wa magereza kutoka sheria ya mkoloni, ili kufuata sheria ambazo sio kandamizi zenye malengo ya kufunza zaidi, sanjari na elimu bora kwa watoto wanaoingia gerezani.

Vile vile alisema lengo la chama hicho ni kuwaunganisha wafungwa waliomaliza kutumikia vifungo vyao pamoja na kuwarekebisha kitabia sanjari na kusimamia haki zao zilizosahaulika.

Hata hivyo alichanganua kuwa chama kina mkakati wa kuwafungulia miradi mbalimbali wafungwa waliomaliza vifungo ili waweze kutumia ujuzi wao kwa manufaa ya jamii inayowazunguka.

“Lengo letu ni kuwaanzishia miradi mbalimbali itakayowapatia ajira na kupunguza uhalifu unaoweza kuwarudisha gerezani tena, hata hivyo jamii ielewe kwamba kuwapokea watu hawa ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo itasaidia kwa kiwango kikubwa kupunguza uhalifu ndani ya jamii yetu”.

Mbali na hayo alibainisha kwamba chama hicho kina zaidi ya wanachama 182 huku kikiwa na miradi mbalimbali ikiwamo upasuaji mbao na uselemala.

Kwa kiasi kibwa chama hicho kimeweza kusimama baada ya kupatiwa msaada wa shl. milioni 100 na Mwenyekiti wa Kampuni ya IPP Leginald Mengi mwaka 2009.  

MGOGORO WAFUKUTA UCHAGUZI JUMUIYA YA WAZAZI KATA YA NDUGUMBI KINONDONI

Na Mwandishi Wetu

UCHAGUZI wa viongozi wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi Tawi la Vigaeni, Kata ya Ndugumbi Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, unafukuta kutokana na kudaiwa kuwa na mchezo mchafu.
Uchaguzi huo bado haujajulikana utafanyika lini, ingawa zoezi la urudishwaji wa fomu za wagombea ulishakamalika tangu Jumapili iliyopita.
Baadhi ya wanachama wa jumuiya hiyo, wamesema zoezi la uchaguzi wa viongozi wao unaonekana kuwa katika zengwe kutokana na kurudishwa kwa majina ya wagombea.
Wanachama hao walidai kuwa kurudishwa kwa fomu ya mgombea wa nafasi ya uenyekiti wa Tawi la Vigaeni (jina linahifadhiwa) kunatokana na kutakiwa kuwepo kwa majina ya 'wateule' wao.
"Unajua kuwa kuna mambo ambayo hata hatuyaelewi kabisa, kwa mfano jina la mgombea wa nafasi ya mwenyekiti limetakiwa kurudi kisa liko moja, na mgombea hawezi kuwa peke yake," alisema mmoja wa wanachama hao.
Wakizungumza kwa nyakatio tofauti, wanachama wa tawi hilo wamedai kuwa kuwepo kwa tofauti ya jina moja kuondolewa, huku nafasi ya katibu ikiwa na mgombea mmoja, sambamba na nafasi ya mjumbe wa mkutano mkuu kata.
 lilipowasiliana na Ofisi ya Katibu Mkuu wa Tawi la Vigaeni, lilijibiwa kuwa katibu huyo hayupo kazini kutokana na kusumbuliwa na maradhi.
Mmoja wa wafanyakazi wa ofisi hiyo ambaye alijitambulisha kwa jina moja la Shida, alisema yeye si msemaji, na kumtaka mwandishi kuwasiliana na katibu, ambaye kwa wakati huo alidai yuko nyumbani kwake na anaumwa.
Tawi hilo linadaiwa kufukuta kutokana na baadhi wa wagombea kuwekewa kauzibe kwa vigezo vya kutokuwa wakazi, kitu ambacho kinavumishwa ikidai kuna mbinu kwa baadhi ya watu kutakiwa kushika baadhi ya nyadhifa.
Hata hivyo, wagombea wote wa nafasi tofauti walizoomba wamefanyiwa usaili jana, huku nafasi ya mwenyekiti ikitakiwa kutafutiwa mpinzani, baada ya awali kuwasilishwa jina moja hadi siku ya mwisho ya kurudisha fomu iliyokuwa Mei 6.

Speaker Makinda attends the seventh Meeting of the East African Speakers Bereau in Kigali Rwanda

Speaker of the National Assembly of Tanzania Hon. Anne Makinda arrives at the Rwandan Parliament to attend the seventh Speakers bereau of the East African Countries.. On her left is the EALAs Speaker Hon. Abdi Rahim 
Photo by Owen Mwandumbya
Speaker of the National Assembly of Tanzania Hon. Anne Makinda greats Hon. Ntawukuliryayo Jean Damascene, President of the Sanate of Rwanda when she arrives at the Rwandan Parliament to attend the seventh Speakers bereau of the East African Community today.
Hon. Ntawukuliryayo Jean Damascene, President of the Sanate of Rwanda presents a gift to the Speaker of the National Assembly of Tanzania Hon. Anne Makinda when she arrives at the Rwandan Parliament to attend the seventh Speakers Bureau of the East African Community today.
Speaker of the National Assembly of Tanzania Hon. Anne Makinda leads her countermets from EAC Member state to pray for the strong EAC intergration before the start of the seventh Speakers beareau of the East African Community today.
Chairman of the East African Speakers Bureau Hon. Rose Mukantabana, Speaker of the Rwandan Parliament welcomes the speakers from EAC members states after the officail opening of the one day meeting of the seventh meeting of the Speakers Bureau of the East African Community today. On her right is Hon. Abdi Rahim Speaker of the EALA and on her left is Hon. Rebecca kadaga, speaker of the Ugandan Parliament.

KAMPUNI YA SEMES YAJIDHATITI KUOKOA WANAWAKE ARUSHA

NA GLADNESS MUSHI -ARUSHA
KAMPUNI ya Semes ya jijini la Arusha imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa  inawaakomboa wanamke wa nchi ya Tanzania  kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali sanjari  na kuwapatia mitaji ili iwawezeshe kujikwamua kiuchumi.
Hayo yalisemwa na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bw Elias Seme alipokuwa katika sherehe za kuzindua kikundi cha kampuni hiyo jijini hapa
Alisema kuwa ili kuhakikisha kuwa wanawake wanaondokana na hali ya utegemezi kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha kuwa wanawake wanapewa kipaumbele katika kuwakomboa kwa kuwapatia mitaji mbali mbali .
Alieleza kuwa mwanamke ndie mwenye huruma na ana uwezo wa kupangilia mipango zaidi ya wanaume hivyo wanayo fursa kubwa ya kuwezeshwa ili waweze kujikwamua kiuchumi
Bw Seme aliongeza kuwa kampuni hiyo tayari.imeshatoa mitaji ya shilingi milioni tano kwa mwaka huu ambapo pia wameweza kuanzisha vikoba kwa  lengo la kukopeshana ili kuboresha maisha yao
Aliongeza kuwa mbali na hayo kampuni hiyo imefanikiwa  kutoa ajira kwa vijana 21 ambapo  lengo halisi ni kuweza kutoa ajira kwa watu 50-60 kwa mwaka .
Akielezea changamoto inayoikabili kampuni hiyo alisema kuwa ni pamoja na ushindani wa kibiashara ambapo kumekuwepo na makampuni mengi kutoka nchi ya nje  yanayohusiana na maswala ya  usafi hivyo kuwepo na upinzani    mkubwa.
Alitaja mikakati waliyonayo kuwa ni pamoja na kuongeza vitega uchumi zaidi na kujiboresha ili iweze kujiongezea mapato zaidi ili kuwawezesha vijana wengi kujipatia ajira.

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda awasili Kigali jana Usiku kuhudhuria Mkutano wa Saba wa Maspika wa Mabunge wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda awasili Kigali Rwanda kuhudhuria Mkutano wa saba wa Maspika wa Mabunge wananchama wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Hapa Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwasili jana katika Uwanja wa Ndege wa Kigali baada ya kupokelewa na Mwenyeji wake Spika wa Bunge la Rwanda Mhe. Rose Mukantabana (kulia). Mhe. Makinda yupo Kigali Rwanda kuhudhuria Mkutano wa Saba wa Maspika wa  Mabunge wananchama wa Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika leo
Picha na Owen Mwandumbya
 
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akizungumza na Mwenyeji wake Spika wa Bunge la Rwanda Mhe. Rose Mukantabana mara baada ya Kuwasili Mjini Kigali kuhudhuria Mkutano wa Saba wa Maspika wa Mabunge wa Nchi wananchama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utakaofanyika leo.
Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akipata maelezo  ya awali kuhusu Mkutano huo kutoka kwa maafisa wa Bunge la Tanzania. Wa kwanza Kushoto ni Bi. Justina Shauri , Afisa Dawati wa Bunge la Afrika Mashariki kutoka Bunge la Tanzania na Ndg. Charles Mloka, Mkurugenzi wa Kamati za Bunge anayemuwakilisha Katibu wa Bunge katika Mkutano huo.
 
Mhe. Makinda na Mwenyeji wake wakiondoka Uwanja wa Ndege mara baada ya Kuwasili.

TGNP YAWANOA WANAHARAKATI TOKA MIKOANI KATIKA MBINU ZA URRAGHBISHI

Mchoraji wa katoon magazeti ya The Guardian Muhidin Msamba, akimsawadia Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Zawadi ya picha ya kuchora wakati wa mafunzo hayo.
 
Leo TGNP imezindua warsha ya  uraghbishi ya wiki moja  kwa wanaharakati kutoka mikoani pamoja na Dar es Salaam, ili  kunoa uwezo wao wa kufanya kazi na   jamii husika kuibua masuala nyeti katika jamii hizo zikiwemo mafanikio na changamoto, kuchambua visababishi vya matatizo au mafanikio hayo kwa kina  na kupanga mikakati ya kushughulikia kero hizo  pamoja na wanajamii .
Warsha hiyo inalenga kuimarisha uelewa wa pamoja  wa mtizamo  ya  kiitikadi  kuhusu  dhana za ukombozi wa  wanawake kimapinduzi na makundi yaliyoko pembezoni  na kuitekeleza  kwa vitendo;  kujenga uelewa  wa pamoja  kuhusu  uraghbishi  na mbinu shirikishi  zinazotumika  katika uraghbishi,  kuongeza uelewa wa kampeni  ya hiaki ya uchumi  katika kudai kazi zenye heshima utu na kipato, uhifadhi wa kumbukumbu, mbinu za mawasiliano  na uwezo wa kuvitumia  katika Ujenzi wa  Vuguvugu la ukombozi wa wanawake kimapinduzi katika ngazi ya kanda.
Wawezeshaji wa warsha hiyo ni  Bw. Richard Mabala   Mkurugenzi wa TAMASHA  ambayo ni asasi  ya kiraia iliyobobea  katika kuwawezesha vijana  na jamii kwa ujumle  kutumia mbinu za uraghbishi  kama chachu ya kuleta mabadiliko chanya katika jamii husika.  Bw. Winston Chuchil Mkurugenzi Msaidizi wa TAMASHA ni mwezeshaji mwenza  ambaye naye pia amebobea katika mbinu za uraghbishi.
Washiriki wa Warsha hiyo wametoka katika mikoa ya Shinyanga, Morogoro, Arusha, Dodoma, Mwanza , Mbeya, Dar es Salaam na Pwani wakiwakilisha asasi mbalimbali za kiraia ambazo zimekuwa mstari wa mbele katika kuleta mabadiliko chanya katika jamii za mikoa husika.
Baada ya warsha  washiriki wakishirikiana wanajamii  na TGNP wataendesha zoezi la uraghbishi katika mikoa  husika ambapo watatumia mbinu mbali mbali za uraghbishi katika  kuibua  masuala nyeti yanayogusa jamii husika, kuyachambua kwa kina ili kupata kiini cha matatizo au mafanikio, hayo na  kutafuta  mbinu mbali mbali za  kutafuta ufumbuzi wa matatizo hayo, mbinu zitakazotumika, nani atafanya nini kuanzia ngazi binafsi, jamii  na taifa.


PINDA AKUTANA NA BALOZI WA SAUDI ARABIA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na Balozi wa Saudi Arabia nchini, Hani Abdullah Mominah kabla ya mazungumzo yao, ofisini kwake jijini Dar es salaam May 7, 2012.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Balozi wa Saudi Arabia Nchini, Hani Abdullah Mominah, ofisini kwake jijini Dar es salaam May 7, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

41,733 WASHUHUDIA MECHI YA SIMBA, YANGA


Watazamaji 41,733 walikata tiketi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya Simba na Yanga iliyochezwa jana (Mei 6 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, sh. 10,000 viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 VIP C, sh. 30,000 VIP B na sh. 40,000 VIP A. Watazamaji 36,980 walinunua tiketi za sh. 5,000 wakati 203 walikata za sh. 40,000.
 
Mechi hiyo ambayo ni moja kati ya saba zilizochezwa siku hiyo kufunga msimu wa 2011/2012 iliingiza sh. 260,910,000. Kila klabu ilipata sh. 62,646,395.85. Asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) ni sh. 39,799,830.51 wakati Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilipata sh. 19,908,361.95.
 
Gharama za mechi kabla ya mgawo ni nauli ya ndani ya waamuzi na kamishna sh. 20,000, posho ya kujikimu kwa kamishna sh. 40,000, mwamuzi wa akiba sh. 30,000, gharama za tiketi sh. 8,539,950, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, umeme sh. 300,000, ulinzi na usafi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (Beijing Construction) sh. 2,000,000.
 
Mgawo wa uwanja ni sh. 19,908,361.95, gharama za mechi sh. 19,908,361.95, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 9,954,180.97, Baraza la Michezo la Taifa (BMT) sh. 1,990,836.19 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 10,467,324.78.

Kumbukumbu

SLEYUM MOHAMED ZAHOR (1922-2003)
HATIMAYE leo umetimiza miaka tisa tangu ulipofariki dunia mwaka 2003 baada ya kuugua kwa muda mrefu na kuzikwa katika makaburi ya Kigilagila, Kiwalani, Dar es Salaam.
Kifo chako kimetuachia pengo na upweke mkubwa. Tunazikosa simulizi zako, maono yako, ucheshi wako, busara zako na hekima zako.
Unakumbukwa sana na mke, Bibi Fatuma Rashid na watoto wako, Rashid, Pili, Amisa, Shani, Asha, Saumu, Nuru na Hilali pamoja na wajukuu zako wote.
Hakika sisi zote ni waja wa Mwenyezi Mungu na kwake lazima tutarejea. Tunaamini maandiko ya kwamba kila chenye roho, lazima kitaonja mauti.
Mungu ailaze roho yako mahali pema, peponi. Amin

Uongozi wa azam waipongeza timu yao kwa kuibuka washindi wa pili ligi kuu ya Vodacom

Makamu Mwenyekiti wa timu ya AZAM FC.Bw Said Mohamed akitoa hotuba jana katika ukmbi wa hoteli ya JB Belimont  jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kuipongeza timu ya Azam Fc kwa kuwa mshindi wa pili wa ligi kuu ya Vodacom .
Kocha wa Azam Fc Bw;John Stewart Hall.nae akitoa msisitizo katika hafla hiyo
Katibu mkuu wa Tff Bw;Angetile Osiah akisisitiza jambo katika hafla ya kuipongeza timu ya Azam Fc.
MWENYEKITI wa Simba, Ismail Aden Rage nae akisisitiza jambo katika hafla hiyo.
Mtangazaji wa Radio One .Bw. Omari Katanga akikabidhiwa Tuzo na  Mbunge wa Kinondoni Idd Azan kwa  kuwa mmoja wa waandishi bora wa michezo Tuzo hizo zilitolewa na uongozi wa klabu ya Azam wakati wa hafla ya kuipongeza timu ya Azam Fc kwa kuwa mshindi wa pili wa ligi kuu ya Vodacom.
Mkurungenzi wa  michezo katika wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na michezo Bw. Leonard Thadeo katikati akimsikiliza Mbunge wa Kinondoni Idd Azan wakati wa hafla hiyo kushoto ni makamu mwenyekiti wa Azam FC  Bw Said Mohamed

Saturday, May 5, 2012

SPIKA WA BUNGE AWA MGENI RASMI KILELE CHA MAADHIMISHO YA ALBINO MKOANI LINDI


  Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) akipata maelezo kutoka kwa Ndg. Abdalah Omar kutoka Chama cha Albino Tanzania juu ya matumizi ya mafuta maalum ya ngozi kwa ajili ya watu wenye ulemevu wakati alipotembelea mabanda ya maonesho ya bidhaa na huduma mbalimbali za watu wenye ulemavu wa Ngozi. Spika alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi Jana.
(Picha zote na Owen Mwandumbya wa Bunge)

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) akipokea DVD maalumu kuhusu Albino na Maisha yao kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika lisilo la kiserikali la Under the Same Sun Bi. Vicky Mtetema wakati wa maadhimisho ya  Siku ya Albino yaliyofanyika Lindi. Shirika la ni mdau mkubwa wa watu wenye ulemavu wa Ngozi na linajishughulisha na kutoa elimu kwa watu wenye Ulemavu wa Ngozi pamoja na Misaada mbalimbali. Spika walikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi Jana.

Dk. Mashingo Lerise kutoka Taasisi ya Magonjwa ya Ngozi na Saratani (Ocean Road) akimweleza Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) juu ya huduma mbalimbali zitolewazo na taasisi hiyo kwa watu wenye ulemavu (Albino) baada ya Mhe. Spika kutembelea banda lao wakati wa kilele cha Siku ya Albino kitaifa iliyofanyika Lindi. Kulia ni baadhi ya madaktari wa saratani ya Ngozi kutoka taasisi hiyo katika Hospitali za KCMC na Mkoani Lindi.
  Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Ludovick Mwananzila, Spika wa Bunge  Mhe. Anne Makinda, Mweneyikiti wa Chama cha albino Tanzania Ndg. Ernest Kimaya, na Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Ndg. Danford Makala wakipokea maandamano wakati wa kuadhimisha siku ya Albino Mkoani Lindi ambapo Spika alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi Jana.
Bi. Zakia Matimbwa kutoka Albino Revolution Cultural Troup cha Dar es Salaam akighani Ngonjera iliyobeba ujumbe wa kulaani mauji ya Albino wakati wa katika maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi jana
  Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Lindi wakati wa maadhimisho ya saba ya siku ya Albino yaliyofanyika kitaifa Mkoani Lindi jana. Mhe Spika alikuwa Mgeni rasmi katika kilele hicho.

UWT KIVUKONI WATANGAZA NAFASI ZA UONGOZI


UMOJA wa Wanawake nchini (UWT),  Kata ya Kivukoni wilaya ya Ilala umetangaza nafasi mbalimbali za uongozi kwa wanachama wake katika kata hiyo ambapo uchukuaji fomu umekwishaanza tangu Mei 4 mwaka huu.Katibu wa Umoja wa Vijana Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Kata hiyo, Omary Omary alisema hayo jijini Dar es Salaam leo, kuwa mwisho wa uchukuaji fomu hizo utakuwa Mei 11 mwaka huu.
Alisema nafasi zinazopaswa kugombaniwa na wanachama wa chama hicho ziko nane (8), ambapo kila mwanachama hai anayo nafasi ya kujitokeza katika kuomba moja ya nafasi hizo.
Omary alizitaja nafasi hizo kuwa ni pamoja na Mwenyekiti nafasi moja, Katibu nafasi moja, wajumbe wa kamati ya utekelezaji wanatakiwa wanne, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kata nafasi moja.
Nafasi nyingine ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Wilaya nafasi mbili , mjumbe wa Halmashauri ya Kata nafasi moja , mwakilishi kutoka UWT kwenda Wazazi nafasi moja na mwakilishi kutoka UWT kwenda Uvccm nafasi moja .
Omary alitanabaisha kuwa fomu zinapatikana katika ofisi ya CCM kata ya Kivuko kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa 10:jioni ambapo kila fomu moja muombaji atapaswa kuilipia shil. 10,000/=.

WATANZANIA WAFANYA MATEMBEZI YA AMANI KATIKA JIJI LA YOKOHAMA NCHINI JAPAN

  Maafisa Ubalozi wa Tanzania nchini Japani, Jilly Maleko na Francis Mossongo wakijiandaa tayari kwa matembezi ya hisani yenye lengo la kuhamasisha juhudi za kufufua uchumi na utalii wa jiji la Yokohama.
      Maandalizi yakiendelea
Watanzania wanaoishi nchini Japani wakiwa kwenye picha ya pamoja na wadau wengine kutoka mataifa ya Afrika katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa matembelezi hayo.
Watanzani wakipeperusha bendera ya Tanzania katika Matembezi ya hisani yaliyoandaliwa na jiji la Yokohama
Matembezi yamekolea, Mwenyekiti wa watanzania wanaoishi nchini Japani Radhid Njenga (mwenye kanzu) naye alikuwemo.
Noboru Ninomiya (mwenye picha ya tingatinga) mwenyeji wetu katika matembezi haya akiwa sambamba na Francis Mossongo, Afisa Ubalozi.
Maafisa Ubalozi wa Tanzania nchini Japani, wamewaongoza watanzania wanaoishi hapa kushiriki katika matembezi ya hisani ya mji wa Yokohama, ikiwa ni moja ya hatua za kukuza urafiki kati ya jijini hilo na Tanzania.
 
Hii ni mara ya kwanza kwa Tanzania na hata mataifa ya Afrika kushiriki rasmi kwenye matembezi hayo ambayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka. Mwaka huu, Tanzania kutokana na historia yake ya kupenda, kusimamia na kutetea amani, umoja na mshikamano duniani.
Aidha katika siku za usoni, mji wa Yokohama una mpango wa kuanzisha uhusiano (Sistercity Friendship) na moja ya miji ya Tanzania, uhusiano ambao utajumuisha kupanda miti aina ya Cherry blossom katika mji utakaochaguliwa Tanzania.
Matembezi hayo yalianzishwa mwaka 1953 kwa lengo la kuhamasisha jitihada za kufufua uchumi na utalii wa mji wa Yokohama kufuatia uharibifu uliotokana na Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

Friday, May 4, 2012

RASMI SIMBA BINGWA, AZAM WATOKOTA UWANJA WA TAIFA BAADA YA KUCHAPWA GOLI 2-1 NA MTIBWA SUGAR


SIMBA leo wanaanza kushangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya Azam FC kufungwa mabao 2-1 na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Simba ina pointi 59, ambazo sasa haziwezi kufikiwa na timu yoyote msimu huu na imebakiza mechi moja dhidi ya watani wa jadi, Yanga Jumapili ambayo kwao itakuwa ya kulinda heshima tu.
 Lakini Azam tayari imejihakikishia nafasi ya pili kwenye ligi hiyo na hivyo kukata tiketi ya kushiriki Kombe la Shirikisho la Soka Afrika mwakani.
Waliokuwa mabingwa watetezi Yanga, hawana tena chao- kwani hata wakiifunga Simba keshokutwa watabaki nafasi ya tatu tu, hivyo mwakani hawavuki mipaka ya nchi.

Tumaini pekee la Yanga kucheza michuano ya Afrika mwakani ni iwapo Simba SC itaingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho mwaka huu- ikiwa imebakiza mitihani miwili kufikia mafanikio hayo.
Inatakiwa kuitoa Al Ahly Shandy ya Sudan- na baadaye iitoe timu itakayokutana nayo kwenye mchujo wa kuwania kucheza hatua hiuyo, ambayo itakuwa imetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa.
Hapo, Tanzania itakuwa na nafasi mbili kwenye Kombe la Shirikisho mwakani, kwa mujibu wa kanuni mpya za Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Tayari Simba imeifunga Shandy mabao 3-0 katika mchezo wa kwanza na inahitaji sare katika mchezo wa marudiano wiki ijayo ili kusonga mbele.

Katika mchezo wa leo, hadi mapumziko, tayari Mtibwa walikuwa wanaongoza kwa bao 1-0 lililowekwa kimiani na Awadh Issa dakika ya 25, wakati kipindi cha pili, Wakata Miwa hao wa Manungu waliokuwa wanashangiliwa kwa nguvu na mashabiki wa Simba, walipata bao la pili dakika ya 59, mfungaji akiwa ni Juma Abdul.

Awadh alifunga bao lake akiunganisha kona iliyochongwa na nyota wa mchezo wa leo, Juma Abdul ambaye naye alifunga bao la pili kwa mpira wa adhabu, baada ya Luckson Kakolaki kumchezea rafu Vencent Barnabas Saramba. John Raphael Bocco aliifungia Azam bao la kufutia machozi.

RAIS JAKAYAKI KWETE AKITANGAZA BARAZA LA MAWAZIRI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali na Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda baada ya kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012
(PICHA IKULU)
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wanahabari wakati wa kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012
Wapiga picha wakiwa kazini wakati Rais Jakaya Kikwete akitangaza Baraza la Mawaziri leo ikulu
Wanahabari wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa kutangaza Baraza la Mawaziri leo April 4, 2012

Rais Jakaya Kikwete Apangua Baraza la mawaziri



THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com
              press@ikulu.go.tz             

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
              P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
MAWAZIRI
1. OFISI YA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,
2.              OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H.  Suluhu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,
3.              OFISI  YA WAZIRI MKUU
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,
4.              WIZARA
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,
Waziri wa Ujenzi
Dr.  John P. Magufuli, Mb.,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,
Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,
Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof.  Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof.  Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
Waziri wa  Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,
Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,
Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,
Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,
Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,
Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,
5.              NAIBU MAWAZIRI
OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI
6.              OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,
7.              OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi  ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,
8.              WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo  ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,
Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,
Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,
Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
4 Mei, 2012

Tuesday, May 1, 2012

SHEREHE ZA MEI MOSI ZAFANYIKA ZANZIBAR


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk
.Ali Mohamed Shein,akizungumza na wanayakazi wa Sekta mbali mbali za
Serikali na Sekta Binafsi wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Kilele
cha Siku ya Wafanyakazi Duniani (MEY DAY)zilizofanyika jana katika
ukumbi wa Salama Bwawani Hotel Mjini Unguja,(kushoto) Mwenyekiti wa
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar,Zahrani Mohamed
Nassor,(kulia) Katibu Mkuu Kiongozi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee na
Waziri wa Kazi,Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika Haroun Ali
Suleiman, {Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk
.Ali Mohamed Shein,akimkabidhi   Fedha tasilim Margreth Peter Mathew
wa Nelia Hotel & Resort Zanzibafr, Shilingi za Kitanzania Laki
Saba,(700,000/=)  kupitia Chama cha wafanykazi (CHODAU) akiwa katika
miongoni mwa wafanyakazi bora kwa mwaka 2012,wakati wa sherehe za siku
ya wafanyakazi Duniani zilizofanyika leo katika ukumbi wa Salama
Bwawani Hotel Mjini Unguja. {Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.}
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk
.Ali Mohamed Shein,akimkabidhi   Fedha tasilim Kidawa Juma said
Shilingi za Kitanzania Laki Mbili na Hamsini Elfu (250,000/=)
Mfanyakazi Bora,wa Halmashauri  ya Wilaya ya Magharibi kupitia Chama
cha wafanykazi (ZALGWU) akiwa katika miongoni mwa wafanyakazi bora kwa
mwaka 2012,wakati wa sherehe za siku ya wafanyakazi Duniani
zilizofanyika leo katika ukumbi wa Salama Hotel Bwawani. {Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.}
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati ) akishikana mikono na viongozi wakati
wa Sherehe za  kilele cha Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi
Duniani,na kuimba wimbo wa (Solidariti Foreva) wakinyanyua juu mikono
kuonesha mshikamano katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja
zilizofanyika sherehe hizo  leo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(katikati ) akishikana mikono na viongozi wakati
wa Sherehe za  kilele cha Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi
Duniani,na kuimba wimbo wa (Solidariti Foreva) wakinyanyua juu mikono
kuonesha mshikamano katika Ukumbi wa Salama Bwawani Mjini Unguja
zilizofanyika sherehe hizo  leo.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
 

SHEREHE ZA WAFANYAKAZI MEI MOSI MKOANI DAR ES SALAAM LEO


Kaimu mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bi Mwnantum Mahiza akitoa hotuba wakati wa sherehe za MEI MOSI leo zilofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es salaam ambapo kitaifa sherehe hizo zimefanyikia mkoani Tanga mgeni rasmi akiwa Rais  wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Jakaya Kikwete.Kushoto ni Mwenyekiti wa TUCTA mkoa wa Dar es salaam Bw Hassan Kaumo.
Wafanyakazi kutoka Vyama mbalimbali vya wafanyakazi wakiwa wamefurika katika viwanja vya mnazi mmoja kusherekea MEI MOSI leo huku watu wengine wakijaribu kuingia katika viwanja hivyo kama wanavyoonekana katika uzio.
 Baadhi ya wafanyakazi wakiwa katika viwanja vya Mnazi Mmoja wakisubiri kuanza kwa sherehe hizo jijini Dar es salaam.
Unaweza ukafikiria huyu ni mlemavu Lah. siyo mlemavu ila kijana huyu aliyetambulika kwa jina la Hashimu Ibrahimu aliamua kutoa burudani kwenye sherehe za Mei Mosi ili kujipatia kipato.kama usemi unaosemwa mgeni njoo mwenyeji apone.

RAIS DK. JAKAYA KIKWETE AONGOZA SHEREHE ZA MEI MOSI TANGA


Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo Mei 1, 2012
(PICHA NA IKULU)
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akishiriki kuimba wimbo wa wafanyakazi akiwa kashikana mikono na Rais wa Jumuiya ya Vyama vya wafanyakazi (TUCTA) Mh, Waziri wa Kazi na Ajira Mh Gaudence Kabaka (kulia) na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mh Galawa katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo Mei 1, 2012
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akimkabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni tatu kama zawadi kwa  Mfanyakazi bora wa Tanesco Bi Anetha Chengula  katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo Mei 1, 2012
Wafanyakazi wa Ofisi za Bunge wakiigiza kikao cha bunge wakati gari lao lilipokuwa linapita mbele ya Rais Dkt Jakaya Kikwete katika sherehe za Mei Mosi katika Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga leo Mei 1, 2012 
 Viongozi mbalimbali wakiwa katika jukwaa kuu wakati wa sherehe hizo kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga leo
 Hii ni sehemu wa wafanyakazi waliojitokeza katika uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga leo.
 Viongozi mbalimbali wakiwemo mawaziri na wabunge pamoja na viongozi wa siasa wakiwa katika wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete wakati alipokuwa akiwahutubia wafanyakazi katika sherehe za Mei Mosi Mkoani Tanga leo.
Baadhi ya Wafanyakazi na wananchi waliojitokeza kwenyesherehe hizo wakiwa wamefurika kwenye uwanja wa Mkwakwani leo.