TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, March 21, 2013

Tigo na Kabang yazidi kutikisa Anga

 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Mr.Blue akifafanua Jambo wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari kuhusiana na Tigo Kabang hivi karibuni.
Msanii akizungumzia Kabang inavyozidi kutikisa
 Chege akifafanua jambo
 Mwandishi wa Habari Ahamad Michuzi akiziweka hewani habari hizi za Kabang na Tigo

 Wasanii wakishangaa jambo kuhusiana na huduma ya Kabang na Tigo
Picha Zote kwa Hisani ya Miss Demokrasia Tanzania.

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAM CHADHAMINI FAINALI YA TAIFA MISS UTALII TANZANIA 2012/13



CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAM CHADHAMINI FAINALI YA TAIFA  MISS UTALII TANZANIA  2012/13

Chuo Kikuu cha Dar es salaam ni miongoni mwa taasisi mbalimbali nchini zilizoitikia wito wa kudhamini fainali za taifa za Miss Utalii Tanzania 2012/13 ikiwa ni baada ya kupata taarifa ya kuwapo kwa mapungufu mbalimbali ambayo yamepelekea kusogezwa mbele fainali zake kutokana na upungufu na ufinyu wa bajeti kiasi cha shilingi milioni 170 zilizotokana na kushindwa kwa baadhi ya wadhamini kutimiza ahadi zao.
udhamini huo ambao unalenga moja kwa moja kwa washindi, ni pamoja na kulipiwa gharama za ada ya masomo katika musimu wa 2013/14  kozi ya uandishi wa habari  katika chuo kikuu cha dar es salaam ,school of journalism and mass communication( sjmc).
akizungumza jijini dar es salaam kuhusu udhamini huo , rais wa miss utalii tanzania, gideon chipungahelo alisema kwamba ni jambo la kupendeza kwa kuwa kuna  ufinyu wa bajeti katika kukamilisha fainali za taifa za miss utalii tanzania.
“tunashukuru kuona taasisi kama chuo kikuu cha dar es salaam kinajitokeza kuunga mkono juhudi za miss utalii tanzania katika harakati za kufanikisha fainali za taifa za miss utalii tanzania 2012/13 ambazo zinalenga kuutangaza utalii wa tanzania, ikiwa ni pamoja na chuo kikuu cha dar es salaam ambacho kina historia ukilinganisha na vyuo vingine katika ukanda wa afrika mashariki na kati, hivyo nazidi kusisitiza kwa wadau, taasisi na makampuni binafsi kujitokeza kuunga na kusaidia juhudi hizi ili fainali za mwaka huu ziwe tofauti na fainali za miaka ya nyuma” alisema chipungahelo
Na kuongza kwamba ahadi kwa wadau na wapenzi wa mashindano haya iko pale pale, kwa kuwa dhamira ipo na nia ya kulifanya shindano la Miss Utalii Tanzania kuendelea kuwa bora na lenye mafanikio makubwa kuliko jingine lolote nchini na afrika iko pale pale, na hili litadhihirika wakati wa fainali kuu ya mashindano  mwishoni mwa mwezi huu, hivyo wadau,wafanyabiashara, makampuni binafsi na ya umma, hasa ya kizalendo watakaojitokeza siku hiyo watashuhudia burudani ya aina yake kutoka kwa Warembo mbalimbali wanaowakilisha Mikoa yao,na wawakilishi wa Kanda za Vyuo Vikuu Tanzania bara na Zanzibar.

Miss Utalii Katavi akionekana mwenye Furaha wakati akipozi kwa ajili ya Picha















Wednesday, March 13, 2013

Washtakiwa kesi ya uchochezi, wizi wakana waelezo ya awali

 
Posted: 12 Mar 2013 12:12 AM PDT

Rehema Mohamed na Rehema Maigala

WASHTAKIWA wa kesi ya wizi na uchochezi inamkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shekhe Issa Ponda na wenzake, jana waliendelea kujitetea baadhi yao wakikana maelezo ya awali waliyotoa katika Kituoa cha Polisi Mabatini, Kijitonyama.

Katika kesi hiyo, washtakiwa hao wametoa utetezi wao kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, mbele ya Hakimu Victoria Nongwa wakiongozwa na wakili wao, Bw.Juma Nassoro.
Mshtakiwa Alawi Musa, alikana maelezo yake na kudai kuwa, alikwenda katika Msikiti wa Changombe Markaz, kwenye ibada ya Itikafu kwa ajili ya kukomboa eneo la Waislamu lililouzwa. Alawi alikana maelezo ya kuhusika kujenga Msikiti wa muda
katika eneo la Markaz, linalomilikiwa na Kampuni ya Agritanza Ltd, wakati wakati akihojiwa na wakili wa Serikali Tumaini Kweka. Katika maelezo aliyotoa polisi, mshtakiwa huyo alidai yeye ni mzaliwa wa Zanzibar, Kijiji cha Ole na alikuja Dar es Salaam mwaka 2008, lakini wakili huyo alipomuhoji kuhusu  maelezo hayo pia aliyakana. Kwa upande wake, mshtakiwa Ramadhani Rashidi katika maelezo aliyotoa polisi, alidai kuwa yeye ni mkazi wa Mlandizi na alipata taarifa za kusaidia ujenzi wa Msikiti katika kiwanja cha Chang'ombe Markaz kutoka kwa imamu wake wa Msikiti wa Nuruh.
Katika maelezo hayo, alidaikuwa baada ya kupata taarifa hizo alikuja Dar es Salaam na kwenda Chang'ombe Markaz, Oktoba 15,2012 na walikamatwa na polisi Oktoba 16 mwaka huo usiku. Hata hivyo, mshtakiwa huyo alikana maelezo hayo na kudai polisi walimuhoji jina lake, umri na anapoishi ambapo suala la kwenda Chang'ombe Markaz, kujenga msikiti halijui hivyo huenda polisi wamejiandikia. Shekhe Ponda na wenzake wanakabiliwa na makosa matano  ambapo Oktoba 12 ,2012 wanadaiwa kula njama na kuvamia kiwanja kinachomilikiwa na Kampuni ya Agritaza Ltd  kwa nia ya kujimilikisha isivyo halali.
Katika kosa la uchochezi, inadaiwa Shekhe Ponda na Salehe Mkadam wakiwa katika eneo la Chang'ombe Markaz na viongozi
wa taasisi hiyo, waliwashawishi wafuasi wao ambao ni washtakiwa katika kesi hiyo kutenda makosa hayo.
Posted: 12 Mar 2013 12:11 AM PDT

Na Yusuph Mussa, Korogwe

MKUU wa Wilaya ya Korogwe, mkoani Tanga, Bw. Mrisho Gambo, ameungana na vyama vya upinzani kuikataa taarifa ya Kaimu Ofisa Elimu Sekondari wilayani humo Bw. Shabaan Shemzigwa, kuhusu chanzo cha kufeli kwa wanafunzi wa kidato cha nne mwaka 2012 na kudai haina mashiko.

Akizungumza mwishoni mwa wiki kwenye Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC), Kaimu Katibu wa Chama cha Wananchi (CUF), wilayani humo, Bw. Ibrahim Abdillah, alisema taarifa hiyo haioneshi matatizo yaliyochangia wanafunzi kufanya vibaya zaidi.
“Mwenyekiti (DC), naomba tuikatae taarifa ya Ofisa Elimu kwani haioneshi tatizo lililofanya wanafunzi kufeli zaidi ya kuja na asilimia ya watoto waliopata sifuri, pia hawaoneshi ni jitihada gani ambazo watafanya ili kumaliza tatizo hili,” alisema Bw. Abdillah.
Kwa upande wake, Bw. Shemzigwa alijitetea na kudai kuwa, alipata taarifa kikao hicho siku moja kabla hivyo ameshindwa kuingiza vitu vingi kwenye ripoti yake na kukiri kasoro hizo lakini alimtibua Bw. Gambo baada ya kusema kuwa, tatizo la kufeli ni la kitaifa.
Bw. Gambo alimwambia Bw. Shemzigwa kuwa, asilete taarifa ambazo zinazungumzia Taifa katika kikao hicho bali yeye anapaswa kusema ni nambna gani wataweza kumaliza tatizo la watoto kufeli wilayani humo.
“Taarifa iliyotolewa na Ofisa Elimu inaonesha kama funika kombe mwanaharamu apite, haioneshi mkakati au jitihada gani zitafanyika kupunguza matokeo mabaya kwa wanafunzi... taarifa hii ni sawa na utani, dharau na mazoea.
“Acha kusema wanafunzi kupata sifuri ni tatizo la Taifa, kwani mimi, mke wangu na mtoto wangu tumepata zero...zungumzia nini kifanyike ili kuondoa tatizo hili, kama ningekuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ningemuandikia barua Ofisa Elimu ya kujieleza kwa nini asishushwe cheo,” alisema Bw. Gambo.
Aliongeza kuwa, anaungana mkono msimamo wa vyama vya upinzani kuikataa taarifa hiyo na kumtaka Bw. Shemzigwa aiondoe kwenye kumbukumbu za DCC na kuiwasilisha wakati ujao.  Alisema kama Watanzania tunataka ufaulu mzuri kwa watoto wao, wanapaswa kuacha kuingiza siasa na haki za binadamu kwenye masuala ya elimu kwani kuacha kuwachapa viboko wanafunzi kupunguza nidhamu shuleni ambayo ndio msingi wa mafanikio. taarifa hiyo ilisema wanafunzi 1,727 waliomaliza kidato cha nne wilayani humo mwaka 2012, walipata sifuri sawa na asilimia 83.269. 
Akizungumza na gazeti hili baada ya kikao hicho, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wilayani humo, Dunstan Mdoe, alisema kuwe na masharti magumu kwa wakuu wa shule za sekondari kuwa atakayeshindwa kufikia
kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wake afukuzwe.
Posted: 12 Mar 2013 12:10 AM PDT
Na Kassim Mahege

SIKU moja baada ya Waziri wa Mambo ya ndani Dkt.Emmanuel Nchimbi kuwasimamisha kazi maofisa wa Jeshi la Polisi kwa tuhuma mbalimbali, Mwenyekiti wa Chama Cha Democratic Party(DP) Mchungaji Christopha Mtikila amempongeza kwa hatua hiyo na kumtaka asiishie hapo.
Akizungumza na gazeti hili jana alisema kuwa hatua hiyo inaonyesha ishara nzuri kwa Jeshi la polisi lakini Dkt Nchimbi anatakiwa achimbuwe mizizi ya uhalifu kwa jeshi hilo na hatua kali za kisheria zichukuliwe kwa watakaobainika.
"Kuwasimamisha kazi pekeyake haitoshi tunataka ukweli ukibainika kwa maofisa hao hatua kali sana za kisheria zifanyike dhidi yao,maana hao ndio wanaolipaka matope Jeshi la Polisi."na kuongeza kuwa hao ndio wanaowaumiza wananchi."alisema Mtikila.
Akitolea mfano wa aliyekuwa waziri wa fedha Basil Mramba,Amatus Liyumba na Yona wa benki kuu mahakama yenyewe ilithibitisha kuwa hakuna makosa yoyote ya wizi walioyafanya ispokuwa makosa yao yalikuwa ni kutumia vibaya madaraka yao na kuongeza kuwa leo hii watu hao wanasota kisutu,hivyo anataka na maofisa hao pia wapelekwe mahakamani ili iwe fundisho kwa wengine.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dkt.Wilbroad Slaa alisema haoni kama kuna jipya kutokana na hatua hiyo.
"Mimi sitaki kuzungumzia uamuzi huo wa Dkt.Nchimbi kwa sababu ni dhahiri kuwa kuna double standard,Nchimbi aliwahi kuunda tume kwa ajili ya kufuatilia mauaji ya Mwangosi lakini hakuna hatua yoyote alioichukua mimi sioni kama kuna jambo jipya."alisema Slaa.
Alisema hatua hiyo imechelewa kutokana na kukithiri kwa vitendo vya uhalifu kwa jeshi la polisi na kutolea mfano kuwa Dkt.Nchimbi aliwahi kuunda tume yake kwa ajili ya kuchunguza mauaji ya mwangosi,Ripoti zote zilizotolewa zilionyesha kuwa Jeshi la polisi lilitumia nguvu isio ya lazima na kuongeza kuwa mpaka hivi leo Nchimbi hajasema chochote.
Posted: 12 Mar 2013 12:09 AM PDT

Na David John

MWENYEKITI wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Bw. James
Mbatia, amemshauri aliyekuwa mgombea urais nchini Kenya
kwa tiketi ya Chama cha Muungano CORD, Bw. Raila Odinga kuheshimu matokeo ambayo ndio maamuzi ya wananchi.
Alisema kinachohitajika baada ya Bw. Uhuru Kenyatta kushinda nafasi ya urais nchini humo kwa tiketi ya Chama cha Muungano
wa Jubilee ni kukaa mezani ili kuijenga nchi hiyo kwa pamoja. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam jana, Bw.  Mbatia alimpongeza Bw. Kenyatta kwa ushindi alioupata na kusisitiza kuwa, Wakenya wamefanya uamuzi mgumu ambao haukutarajiwa na watu wengi. “Hali nii inatokana na ukweli kwamba, Bw. Kenyatta anakabiliwa
na kesi mahakamani lakini bado wananchi wameendelea kumuamini na kumpa nchi ili aweze kuwaongoza kama rais wao.
“Ni vyema Bw. Odinga akaachana na nia yake ya kutaka kwenda mahakamani kuweka pingamizi la matokeo yaliyotangazwa badala yake aheshimu maamuzi ya Wakenya ambayo wameyafanya kwa kumchagua Bw. Kenyatta,” alisema.
Alisema Wakenya wameandika historia mpya duniani hasa katika Bara la Afrika inayopaswa kuigwa na mataifa mengine na kufafanua kuwa, kama Bw. Odinga atakwenda mahakamani kuweka pingamizi ajue wazi huko ni kutaka kuwagawa Wakenya, kuhatarisha amani ambayo tayari wameionyesha, kusababisha machafuko na chuki.
Bw. Mbatia aliongeza kuwa, ushindi wa Bw. Kenyatta ni kielelezo kuwa si kila kitu watakacho wazungu, waafrika wakifanye lakini ufike wakatiAfrika iweze kufanya maamuzi yake wenyewe bila kuingiliwa na taifa lolote duniani. “Namuomba Bw. Odinga na wagombea wengine walioshindwa katika uchaguzi huu waheshimu makubaliano ya kulinda amani ambayo walikubaliana ili kuivusha Kenya kwenye demokrasia
ya ukomavu,” alisema Bw. Mbatia.
Katika hatua nyingi, Bw. Mbatia alizungumzia mchakato wa Katiba Mpya unaondelea nchini na kusisitiza nchi inapaswa kujifunza kwa yale mazuri ambayo Wakenya wameweza kuyatumia katika Katiba yao ambayo wameipata miaka michache iliyopita.
Posted: 12 Mar 2013 12:06 AM PDT

KUJIAJIRI ni suala linalopewa kipaumbele na mamlaka mbalimbali nchini pamoja na mataifa yaliyoendelea. Mabadiliko makubwa katika mifumo ya uchumi, yamechangia
wananchi wengi kukosa kazi za kuajiriwa ambapo ajira binafsi 
ndizo zinazoonekana kushika kasi katika maeneo mengi. Nchini Tanzania, idadi kubwa ya wananchi wameamua kujiajiri wenyewe wakiwemo wastaafu kwa kufungua vitega uchumi mbalimbali  pamoja na kufanya biashara ndogondogo ili waweze kujipatia kipato. Cha kukidhi mahitaji yao.
Kujiajiri katika biashara ni jambo jema lakini sisi tunaona kuwa, tatizo kubwa linalowasibu wadau wengi wanaofanya shughuli hizo ni kukosa mafunzo ambayo yatawawezesha kuendesha biashara pamoja na kukuza mitaji yao.
Wafanyabiashara wengi nchini hawabadiliki kwa sababu shughuli wanazofanya ni zile za mazoea bila kuwa na ujuzi wa namna ya kuziendesha hivyo upo umuhimu wa Serikali, kubeba jukumu hilo ili kuwawekea msingi mzuri wa maisha.
Baadhi ya wastaafu waliopewa viinua mgongo na kuwekeza kwenye biashara, wanakabiliwa na wakati mgumu wa kutafuna mitaji yao kwa sababu ya kufanya biashara zisizoendelea. Wanaofanya biashara ya kuuza maandazi na vitumbua, hawana mtazamo wa kutunza ziada wanazopata kwa kufungua akaunti bali wanachokipata kinakwenda tumboni bila kujua senti 50 inayobaki, ilipaswa kuwekwa akiba ili kuendeleza biashara zao.
Hili ni jambo hatari sana, wafanyabiashara kama hawa mbali ya kufanya biashara hizo kila siku, bado wataendelea kubaki maskini bila mafanikio yoyopte kama Serikali haitachukua hatua za haraka kuwasaidia kwa kuwapatia mafunzo ya kuendesha biashara zao.
Ni wajibu wa Serikali na wadau wengine, kutambua kundi hili ni watu wenye vipato vidogo na vile vya kati ambao hawawezi kulipa maelfu ya pesa kugharamia mafunzo ya uendeshaji biashara.
Wito wetu kwa Serikali ibuni mkakati wa kushirikisha wadau wengine na kuandaa mpango maalumu wa kutoa mafunzo ya usimamizi na uendeshaji shughuli za ujasiriamali bure
kwa wananchi waishio mijini na vijijini.
Kwa kufanya hivyo, italeta mwamko kwa wajasiriamali kujua namna ya kuendesha shughuli zao na kuwapa ubunifu zaidi wa biashara mpya tofauti na sasa.
Hivi sasa, wajasiriamali wengi wanafanya biashara kwa kumwiga mwenzake, utakuta kila mahali biashara ni saloon, grosari, maduka ya dawa, chakula na nguo. Je, hivi hizi ndio huduma pekee wanazohitaji wananchi?

Thursday, February 7, 2013

UTUNZAJI CHADEMA kuwashtaki Makinda, Ndugai *Dkt. Slaa adai wameshindwa kuliongoza bunge Hukumu ya vigogo Shirika la VUKA kutolewa Machi 11 NYANYA Mgogoro Moravian wachukua sura mpya Mabaharia 6 wahofiwa kufa maji Serikali yajipanga kukomesha ujangili nchini MADAFU Mtendaji anusurika kifo akidaiwa kuiba mahindi Wakazi waishio mabondeni Tegeta waomba viwanja Jela miaka 2 kwa kuua akidai sh. 4,000 MKATABA Jela miaka 2 kwa kuua akidai sh. 4,000 Wapema mafunzo kupunguza viwavi jeshi Mradi wa 'Niache Nisome' usambazwe nchi nzima

Posted: 06 Feb 2013 01:27 AM PST

Mchuuzi wa Samaki, Bw. Aloyce Sebastian akimfunga samaki na mpira (rubber band) ili maji yasiingie katika mapezi, kama alivyokutwa kwenye Soko la Samaki la Kimataifa Feri, Dar es Salaam hivi karibuni. Wateja wengi huamini samaki mwenye mapezi mekundu kuwa ni salama kwa kitoweo. (Picha na Asia Mbwana)
Posted: 06 Feb 2013 01:24 AM PST

Na Goodluck Hongo

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Slaa, amesema chama hicho kitatumia ngumu ya umma kupeleka hoja zote za wabunge zilizokataliwa bungeni kwa wananchi.
Dkt. Slaa aliyasema hayo Dar es Salaam jana wakati akizungumza na waandishi wa habari na kusisitiza kuwa, hakuna mahakama nyingine za kuwashtaki Spika wa Bunge Bi. Anne Makinda na Naibu wake, Bw. Job Ndugai.
“Hakuna mahakama yoyote ya wananchi iliyowahi kushindwa, nasi tutapeleka hoja zote zilizozimwa na bungeni na Spika Makina pamoja na Naibu wake Ndugai kwa wananchi,” alisema
Alisema chama hicho kilishatangaza mwaka huu ni wa nguvu ya umma hivyo kitendo cha Spika na Naibu wake kushindwa kuliongoza Bunge ambalo ndiyo linaisimamia Serikali kwakuzima hoja muhimu kwa masilahi ya nchi na Watanzania,wananchi watatoa hukumu kwa Serikali na CCM.
“Wananchi wanashindwa kupata haki zao mahakamani, polisi na sehemu zingine na hivi sasa vitendo hivi vimehamia bungeni kwa kuzima haki za wananchi.“Ipo siku uvumilivu utakwisha na kujua kwa nini nchi za Rwanda na Burundi waliingia vitani...nchi hizi hazijaingia katika vurugu kwa kupenda bali kutokana na ukandamizaji kama huu,” alisema.
Alisema mwaka 2011, aliwahi kusema Tanzania haitatawalika na kuitwa mchochezi lakini leo maamuzi ya Spika ni ya kukandamiza wananchi kwani hoja zilizozimwa ni kwa manufaa ya Watanzania ambapo Spika na Naibu wake, wanaongoza Bunge kwa chuki.
Aliongeza kuwa, kutokana na hilo amewaagiza wabunge wote wa CHADEMA kutokwenda kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge hadi Spika atakapoweka wazi rufaa 10 zilizokatwa na wabunge hao.
Aliwataka wajumbe wote ambao watakwenda katika mabaraza ya kutoa maoni ya Katiba Mpya, watoe mani ya kutaka Spika na Naibu wake wasitokane na chama chochote cha siasa ili Bunge liweze kufanya kazi kwa niaba ya wananchi si kwa matakwa ya CCM.
Dkt. Slaa alisema, hivi sasa viongozi wanaoliongoza Bunge hilo, wameshindwa kutekeleza wajibu wao kwa kupindisha kanuni za Bunge wazi wazi na kama zingefuatwa, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dkt. Shukuru Kawambwa, angejiuzulu.
“Samuel Sitta (Mbunge wa Urambo, mkoani Tbaora na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki), aliongoza Bunge kwa aibu pale alipotaka kupindisha sheria lakini Spika wa sasa na Naibu wake ni balaa zaidi,” alisema Dkt. Slaa.
Alisema cham hicho kinawapongeza wabunge wote wa upinzania waliosimama bungeni kupinga maamuzi ya Spika na hiyo ndio njia pekee ya kutafuta haki za Watanzania.
Posted: 06 Feb 2013 01:23 AM PST

Na Rehema  Mohamed

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaaam, Machi 11 mwaka huu, inatarajia kutoa hukumu ya kesi ya wizi wa zaidi ya sh. milioni 100, inayowakabili vigogo wa Shirika la VUKA-Tanzania, linalohusika kuendesha miradi ya UKIMWI.Washtakiwa hao ni Mwenyekiti wa shirika hilo Bw. Adolf Mrema, Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Utawala, Bi. Hilda Urassa pamoja na mshauri Bw. Straton Simon, ambao wanadaiwa kutumia fedha za miradi ya UKIMWI.
Jana kesi hiyo ililetwa mahakamani hapo kwa ajili ya utetezi ambapo washtakiwa hao, walijitetea mbele ya Hakimu Sundi Fimbo na kufunga ushahidi wao.Wakitoa utetezi wao, washtakiwa hao walikana kutumia isivyo halali fedha hizo kutoka Shirika la Maendeleo la Denmark (DANIDA) na Shirika la SAT-Tanzania.
Kwa nyakati tofauti, washtakiwa hao walidai fedha hizo walizitumia kwa ajili ya matumizi ya ofisi kama dawa kwa ajili ya waathirika wa VVU, kuendesha semina na kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.
Hata hivyo, washtakiwa hao hawakuwa na nyaraka za kuthibitisha matumizi ya fedha hizo na kudai kuwa, nyaraka hizo zilichomwa moto na mwenye nyumba aliyewapangisha ofisi kwa kuwa waliifunga.Walidai mwenye nyumba baada ya kuona wamefunga osifi, aliamua kumpangisha mtu mwingine hivyo kutoa vitu vyao na kusababisha nyaraka zao kupotea na nyingine kuchomwa moto kama uchafu.
Katika kesi hiyo, washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 37 likiwemo la kugushi, wizi na matumizi mabaya ya fedha.Inadaiwa kuwa, washtakiwa hao walitenda makosa hayo kati ya Juni11,2006 hadi Desemba 2007, Temeke, Dar es Salaam.

NYANYA
Posted: 06 Feb 2013 01:20 AM PST

Dalali wa nyanya katika Soko la Ilala, Kaniki Ramadhani akiwa ameshikilia 'kitita' cha fedha wakati kifanya hesabu za biashara hiyo, kama alivyokutwa Dar es Salaam jana. Sanduku moja la nyanya lilikuwa likiuzwa kwa sh. 18,000. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 06 Feb 2013 01:14 AM PST

Na Charles Mwakipesile, Mbeya

MWENYEKITI wa Kanisa la Moravian nchini, Jimbo la Kusini, Mchungaji Clement Mwaitebele, mewataka wachungaji 14 ambao alitangaza kuwafukuza baada ya kukiuka kiapo chao cha utumishi Misheni ya Dar es salaam, kuondoka katika nyumba za kanisa.Akizungumza na Majira jana, Mchungaji Mwaitebele ambaye alionesha kukerwa na wachungaji hao kuvuruga amani ndani ya kanisa hilo kwa kujitangazia Halmashauri Kuu yao kinyume na Katiba, alisema uongozi wa kanisa umechukua hatua stahiki kwa watumishi hao kwa kuwa wasaliti katika jimbo mama.
Alisema inashangaza wachungaji hao kudai hawaitambui mamlaka iliyowafukuza badara yake wanasubiri maelekezo ya uongozi wa Bodi ya Dunia (Unity Bord) ulio na Makao Makuu nchini Ujerumani hali inayoonesha kuwa, pamoja na usomi wao bado wameshindwa kutambua taratibu.“Kwa kuwa wameonesha kiburi cha kutoitambua mamlaka yangu kikatiba, natangaza rasmi kuwa kuanzia leo (jana), nimefuta ujio wa Bodi ya Dunia kuja nchini kuzungumzia tatizo hili kwa sababu tayari limekwisha hawana umuhimu wa kuja,” alisema.
Mchungaji Mwaitebele alisema Ofisi la Dunia ni Makao Makuu ya Jumuia ya kanisa hilo kama ilivyo Umoja wa Mataifa ambao hauwezi kuingilia mambo ya ndani nchini Tanzania hadi unapopewa taarifa na uongozi wa nchi.
“Sisi kama viongozi wa jimbo mama, hatuoni umuhimu wa hawa viongozi Bodi ya Dunia kuja kusikiliza mazungumzo kwa sababu tayari tumemaliza mgogoro uliokuwepo na taratibu za kisheria zinachukuliwa,” alisema.
Aliwataka wachungaji hao kuhama mara moja katika nyumba za kanisa kwani hivi sasa si watumishi tena wa kanisa hilo kwa mujibu wa katiba baada ya kushindwa kulinda kiapo chao kilichowataka kuwa watii uongozi badala yake wanatumika kuleta mipasuko.Aliongeza kuwa, wao walifuata utaratibu wa kanisa wa kukaa mezani ili kusikiliza matatizo ya Misheni hiyo baada ya Sinodi ya eneo hilo kumuondoa madarakani aliyekuwa Mwenyekiti wao.
“Wakati mazungumzo yakiendelea, Mwenyekiti huyo alitangza Halmashauri Kuu yake jambo lililoonesha wazi usaliti mkubwa katika kanisa,” alisema Mchungaji Mwaitebele.Aliwaonya Watunza Hazina wa kanisa hilo kuepuka kushirikiana na wachungaji hao kwa kuchukua fedha za matumizi yao binafsi kwani uongozi wake utawaburuta mahakamani kwa kosa la wizi wa fedha za umma jambo ambalo asingependa litokee.
Alisema Mamlaka iliyowafukuza wachungaji hao ni halali ambayo ilichaguliwa na Mkutano Mkuu wa Kanisa na hivyo madai kuwa walipaswa kufukuzwa kwa pendekezo la Askofu ni upotoshaji  wawanaoufanya ili kuliyumbisha kanisa.
Posted: 06 Feb 2013 01:13 AM PST

Na John Gagarini, Pwani

MABAHARIA sita wanahofiwa kufa maji baada ya jahazi walilokuwa wakisafiria kwenye Habari ya Hindi kuzama.Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei, alisema mabaharia hao walipanda jahazi la mizigo na walikuwa saba lakini mmoja ameokolewa.
Alisema jahazi hilo linalofahamika kwa jina la Soweto, lilizama katika Visiwa vya Koma, eneo la Mwamba wa Chokaa, wilayani Mkuranga.
“Usajiri wa jahazi hili bado haujafahmika na lilikuwa na shehena ya mbao na mirunda likitokea Kyasi kwenda Zanzibar,” alisema.Aliwataja baadhi ya mabaharia wanaohofiwa kufa maji kuwa ni Ally Hasan, Hassan Mamba, Nasoro Isa, Abdala Said na Husein Huku wakati Hasan Rajab, aliokolewa na wanaendelea kutafutwa.Aliwataka wananchi kutoa taarifa polisi kawa wataziona maiti zinazoelea majini.
Posted: 06 Feb 2013 12:57 AM PST

Na Godfrey Ismaely, Manyara

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amesema baada ya Rais Jakaya Kikwete kuona matukio ya ujangili nchini yanaongezeka siku hadi siku, muda wowote ataagiza majeshi yote kushirikiana ili kudhibiti matukio hayo.Hatua hiyo inatokana na Serikali ya Tanzania kusaidi dikezo maalumu na Serikali ya Marekani ambalo kushirikiana katika kudhibiti matukio ya ujangili nchini.Balozi Kagasheki aliyasema hayo jana mkoani Manyara katika hafla maalumu ya uzinduzi wa Kituo cha Mapokezi kwa watalii ambacho kipo chini ya Jumuiya ya Usimamizi wa Hifadhi ya Wanyapori Burunge (WMA), Wilaya ya Babati, mkaoni Manyara, kilichojengwa na Marekani kupitia Shirika lake la  USAID.
Jana (juzi) mimi na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Marekani Bw. David Hayes, tulisaini dokezo hili kwa lengo la kukomesha matukio ya ujangili nchini,” alisema na kuongeza kuwa, matukio ya ujangili yanaichafua nchi pia ni mateso kwa wanyama.Alisema mapambano dhidi ya majangili yanawezekana ambapo Serikali imeanza kujipanga ambapo Rais Kikwete, wakati wowote atatoa uamuzi kamka Amiri Jeshi Mkuu wa nini kifanyike kudhibiti hali hiyo nchini.
Alisema suala la kucheleweshwa fedha zinazotokana na makusanyo ya WMA ambayo ni asilimia 50 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo kwa wananchi, litafanyiwa kazi na wakati wowote mambo yatakuwa mazuri.Kwa upande wake, Bw. Hayes ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, alisema lengo la nchi yake kutoa ufadhiri kwa jumuiya za WMA nchini, mbali ya kulenga kukomesha ujangili pia jamii zitanufaika kupitia mapato mbalimbali.
“Kufanikiwa kwa WMA ni fursa moja wapo ya kukomesha kabisa matukio ya ujangili yanayotokea Tanzania, vitendo hivi vinachangia kuhatarisha usalama wa binadamu, wanyamapori na hata kutatiza shughuli za utalii,” alisema Bw. Hayes.Balozi wa Marekani nchini, Bw. Alfonso Lenhardt's, alisema utaratibu wa wanajamii kuanzisha WMA nchini umeweza kuwa na mafanikio makubwa, kuboresha miradi ya shule, zahanati na kusomesha watoto kutokana na mapato yanayopatikana kutoka kwa wawekezaji walioingia nao mikataba.
“Tangu mwaka 2006, WMA tisa zimeweza kuingia mikataba na wawekezaji binafsi katika sekta ya utalii ambapo zimefanikiwa kupokea zaidi ya dola za Marekani milioni tano kutokana na shughuli za uwindaji na upigaji picha. “Hatua hii imewezesha zaidi ya wanajamii 400,000 kunufaika kwa namna moja ama nyingine pamoja na kupata ajira hivyo Marekani itaendelea kuzijengea uwezo jumuiya hizi mara kwa mara ziweze kufikia malengo ya uhifadhi na maendeleo kwa wananchi,” alisema.

MADAFU
Posted: 06 Feb 2013 12:52 AM PST

Wasamaria wakisaidia kuidhibiti baiskeli baada ya kuangukia gari namba T 309 AWU. Kushoto ni dereva wa gari hilo akiangalia sehemu iliyoharibika katika gari hilo, kama walivyokutwa katika Barabara ya Sokoine Posta, Dar es Salaam jana. (Picha na Prona Mumwi)
Posted: 06 Feb 2013 12:48 AM PST

Na Masau Bwire, Bunda

OFISA Mtendaji wa Kata ya Iramba, Wilaya ya Bunda, mkoani Mara, Bw. Simon Katikizu, amenusurika kifo baada ya wananchi wenye hasira kumshambulia kwa mawe wakimtuhumu kuiba mahindi ya msaada.
Tukio hilo lilitokea juzi saa 4 asubuhi, Kijiji cha Isanju ambacho ni Makao Makuu ya kata hiyo ambapo wananchi walikusanyika ili kugawiwa mahindi ya msaada.Wakati kazi ya kugawa mahindi hayo ikiendelea, wananchi hao walibaini upotevu wa magunia zaidi ya 40 na baada ya kufanya uchunguzi, wakagundua wizi huo ulifanywa na Bw. Katikizu hivyo walianza kumshambulia kwa mawe na marungu.
“Tumemkamata na mahindi ya msaada akiwa ameyaficha nyumbani kwake, katika Ofisi ya Elimu, kilimo na mengine aliyaweka katika nyumba za rafiki zake, wakati akijaribu kukimbia lilipigwa yowe,” alisema Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM, katika kata hiyo, Bw. Mohamed Gamba.Alisema Serikali ilipeleka msaada wa magunia 318 ya mahindi kwa ajili ya vijiji vitano vya kata hiyo ambapo kila kijiji kilipaswa kupata magunia 63 kutokana na njaa inayowakabili wananchi.
Vijiji vilivyokumbwa na tatizo la njaa ni Isanju, Mugara, Sikiro, Nyarugoma na Mwiruruma, lakini Bw. Katikizu aliiba kiasi kikubwa cha mahindi ambapo kijiji cha Nyarugoma, kiliambulia magunia 26 ndipo wananchi walipokuja juu na kugundua wizi huo. Mkuu wa Wilaya hiyo, Bw. Joshua Mirumbe, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudai kuwa, tayari amemwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri amsimamishe kazi Bw. Katikizu kwa kosa hilo.
“Huyo Ofisa Mtendaji habari zake ninazo, aliwahi kuiba na kuuza mitumbwi 20 iliyokamatwa katika uvuvi haramu hivyo kutokana na tukio hili, nimeagiza Mkurugenzi amsimamishe kazi kuanzia leo (jana) na ashitakiwe kwa wizi,” alisema Bw. Mirumbe.Alisema viongozi wa namna hiyo hawafahi kuendelea kuongoza na wanaitia doa Serikali hivyo hawana budi kuondoka wabaki viongozi waaminifu na waadilifu watakaowaletea wananchi maendeleo.

“Siko tayari kuona viongozi wezi, wabadhilifu na wababaishaji wakiendelea kuwanyonya wananchi kwa kuwaibia, kama wapo wajiondoe kabla sijawafikia, nitaanza na huyo Ofisa Mtendaji ili iwe mfano kwa wengine,” alisema.Majira lilipomtafuta Bw. Katikuzu na kumuuliza juu ya tuhuma hizo alidai madai hayo ni uzushi uzushi na hakuna wizi wowote aliofanya bali yeye ni miongoni mwa Watendaji waadilifu wilayani humo wanaoaminiwa kiutendaji na Bw. Mirumbe.
Posted: 06 Feb 2013 12:41 AM PST
Na Miriam Sarakikya

BAADHI ya wananchi wanaoishi mabondeni eneo la Tegeta kwa Ndevu, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam, wameiomba Serikali iwasaidia kuwapa viwanja ili waweze kuondoka katika maeneo hatarishi kutokana na kero wanayopata kipindi cha mvua.Wakizungumza na Majira kwa nyakati tofauti Dar es Salaam juzi, wananchi hao walidai wanashindwa kuondoka maeneo hayo kutokana na ukata wa fedha za kununulia viwanja.
“Baadhi yetu wamejenga nyumba zao katika maeneo haya na wengine wamepanga, tunaiomba Serikali isikilize kilio chetu ili tuweze kuhamia maeneo salama tofauti na sasa kwani tunaishi kwa wasiwasi mkubwa,” alisema mkazi wa eneo hilo Bw. Edgar Msanganzila.Mkazi mwingine ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema hivi sasa eneo lao linafurika maji kutokana na mto uliopo jinani na makazi yao hivyo kuhatarisha maisha yao na familia zao.
Hivi karibuni wananchi hao waliitisha mkutano wa hadhara na kukubaliana kuupanua mto huo maarufu 'Mto Tegeta', ili kupata njia ya kupitisha maji kirahisi pindi mvua zinaponyesha lakini hadi sasa mpango huo haujafanikiwa.

Jela miaka 2 kwa kuua akidai sh. 4,000
Posted: 06 Feb 2013 12:40 AM PST

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma, juzi ilimuhumuku mkazi wa Dodoma Mjini, Yohana Chipini (23), kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua Alord Ndeshio, bila kukusudia wakati akidai sh. 4,000. Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mary Shangali baada ya mshtakiwa kukiri kosa na kumtia hatiani.
Jaji Shangali alidai kuwa, amezingatia maelezo yaliyotolewa na upande wa mashtaka pamoja na utetezi kuhusu chanzo cha mauaji hayo ambacho ni ugomvi uliotokea kati yao wakati mshtakiwa alipokwenda kumdai marehemu fedha zake.Aliongeza kuwa, baada ya ugomvi huo mshtakiwa aliokota kipande cha ubao au kitu kinachoaminika kuwa kipande cha chuma na kumpiga nacho marehemu kichwani.
“Adhabu ya kuua bila kukusudia ni kifungo cha maisha lakini kutokana na mazingira yalivyoonyesha na utetezi wa mshtakiwa, Mahakama imempunguzia adhabu na hivyo atatumikia kifungo cha miaka miwili gerezani,” alisema. Kabla ya hukumu hiyo, wakili wa mshtakiwa, Steven Kuwayawaya, aliiomba mahakama impunguzie adhabu mshtakiwa akidai kosa hilo ni la kwanza na amekiri kosa. Awali, ilidaiwa na upande wa mashtaka kuw,  mshtakiwa alitenda kosa hilo mwaka 2012 katika barabara ya Bahi, Manispaa ya Dodoma.
Posted: 06 Feb 2013 12:38 AM PST

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Tarakea, mkoani Arusha, Bw. Martin Kija (kushoto) na Balozi wa Japan nchini, Bw. Masaki Okada wakitia saini makubalino, Dar es Salaam jana, ambapo Serikali ya Japan itajenga  mabweni ya wasichana ya shule hiyo. Ujenzi wa mabweni hayo utawaondolea tatizo la kutembea umbali mrefu kutoka maeneo wanayoishi. (Picha na Asia Mbwana)
Posted: 05 Feb 2013 10:33 PM PST

Na Pendo Mtibuche, Dodoma

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma, juzi ilimuhumuku mkazi wa Dodoma Mjini, Yohana Chipini (23), kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua Alord Ndeshio, bila kukusudia wakati akidai sh. 4,000. Hukumu hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mary Shangali baada ya mshtakiwa kukiri kosa na kumtia hatiani. Jaji Shangali alidai kuwa, amezingatia maelezo yaliyotolewa na upande wa mashtaka pamoja na utetezi kuhusu chanzo cha mauaji hayo ambacho ni ugomvi uliotokea kati yao wakati mshtakiwa alipokwenda kumdai marehemu fedha zake.
Aliongeza kuwa, baada ya ugomvi huo mshtakiwa aliokota kipande cha ubao au kitu kinachoaminika kuwa kipande cha chuma na kumpiga nacho marehemu kichwani.“Adhabu ya kuua bila kukusudia ni kifungo cha maisha lakini kutokana na mazingira yalivyoonyesha na utetezi wa mshtakiwa, Mahakama imempunguzia adhabu na hivyo atatumikia kifungo cha miaka miwili gerezani,” alisema.

Kabla ya hukumu hiyo, wakili wa mshtakiwa, Steven Kuwayawaya, aliiomba mahakama impunguzie adhabu mshtakiwa akidai kosa hilo ni la kwanza na amekiri kosa.Awali, ilidaiwa na upande wa mashtaka kuw,  mshtakiwa alitenda kosa hilo mwaka 2012 katika barabara ya Bahi, Manispaa ya Dodoma.
Posted: 05 Feb 2013 10:30 PM PST

Na Mariam Mziwanda

MAOFISA Kilimo zaidi ya 20 kutoka Wilaya tano nchini, wapo kwenye mafunzo ya mradi shirikishi wa kupunguza wimbi la viwavi jeshi ambavyo ni kero sugu kwa wakulima na kusababisha njaa katika baadhi ya maeneo nchini.Akizungumza katika mafunzo hayo Dar es Salaam juzi, mwezeshaji wa mafunzo hayo ambaye pia ni Ofisa Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Kanda ya Kaskazini, Bw. Didas
Moshi alisema mafunzo hayo yatawasaidia maofisa hao kuwatambua na kuwaangamiza kabla ya kukua.
“Tumeanza mafunzo haya na Wilaya tano ambazo ni Kisarawe, Nachingwea, Masasi, Lindi Vijijini na Kilwa, mafunzo haya yanaendeshwa kwa msaada wa watu wa Marekani ambao wameona viwavi jeshi ni kero kwa wakulima,” alisema.Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi Msaidizi wa Afya ya Mimea kutoka katika Wizara hiyo, Cornelius Mkondo, alisema mazao mengi ya wakulima nchini yamekuwa yakiathiriwa na milipuko ya wadudu sugu wanaoshambulia mazao kwa haraka.Alisema viwavi jeshi wamekuwa wakipoteza nguvu kazi za wakulima hivyo imeamua kutafuta mbinu za kuwatokomeza.
Aliongeza kuwa, maofisa hao watafundishwa mambo mengi hususan jinsi ya kufahamu mlipuko unavyotokea na kuimarisha mawasiliano kati ya vijiji, kata, Wilaya hadi Taifa.“Lengo ni kujilinda na viwavi, katika kuhakikisha operesheni hii inakuwa endelevu, tutashirikiana na kampuni za simu ili wakulima waweze kufahamu utabiri wa hawa wadudu waharibifu,” alisema na kuongeza kuwa, mradi huo mbali ya Tanzania pia unaendeshwa katika nchi za Kenya na Ethiopia.

Posted: 05 Feb 2013 10:29 PM PST

Na Rose Itono

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imekabidhiwa majukumu ya kuweka viwango vya ubora wa elimu na mafunzo ya ufundi katika ngazi zote za elimu kuanzia awali mpaka sekondari.Sambamba na hilo wizara pia ina wajibu wa kuhakikisha kuwa elimu ya awali,msingi,sekondari na ile ya watu wazima inatolewa kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika.
Wizara pia ina jukumu la kusimamia utekelezaji wa utoaji wa elimu kwa kufanya ufuatiliaji na tathmini pamoja na kufanya mapitio,kuandaa na kutoa mapendekezo ya marekebisho ya Sera, Mipango, Sheria na kanuni za elimu zilizopo,kulingana na mabadiliko ya dhima na dira ya Serikali huku ikiandaa mikakati ya utekelezaji wake.
Aidha, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ndiye msimamizi mkuu wa masuala ya taaluma katika ngazi zote za elimu na mafunzo.Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inatekeleza mipango mbalimbali ili kuinua ubora wa elimu Ili yote hayo yaweze kufanikiwa juhudi za wazazi na walezi kwa kushirikiana na wanafunzi zinahitajika kwa kiasi kikubwa katika kuleta matokeo mazuri.Nimeongea hivyo kwa makusudi kwani kumekuwa na baadhi ya wazazi,walezi ambao wamekuwa wakiwakatisha masomo wanafunzi hasa wa kike kwa kutaka kuwaoza kwa nguvu kwa nia ya kujipatia fedha ama mali.


Nionavyo hii ni ukiukwaji wa haki za binadamu kwa kumyima haki yake ya msingi ya kupata elimu mtoto wa kile na kumjengea .Kutokana na hali hiyo ipo haja ya serikali kuianzia ngazi zake za mtaa kuielimisha jamii matatizo na madhara ya watoto wa kike kuolewa kabla ya umri wao na umuhimu wa watoto kusoma.
Nionavyo kwa kufanya hivyo kutalipunguza tatizo la wazazi ambao wana tamaa za kujipatia pesa kwa mahari kupitia watoto wao bila kuangalia madhara na vitu vya msingi ambavyo mtoto wa kike atavikosa kutokana na kuolewa bila kuwa na elimu.
Hivi karibuni tumeshuhudia mtoto wa kike ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Tongani kata ya Mkaramo wilayani Pangani akitoroka kwao na kukimbilia kujificha porini akikwepa kuachishwa shule.Nionavyo hali hii ni hatari kiusalama kwa mtoto huyo ambaye angeweza kupata madhara ya kukutana na wanyama wakali na hata kupoteza maisha.Hali ya mtoto huyo kuamua kulala porini ilimuwezesha kufika kwa Mkuu wa Wilaya ya handeni kuomba msaada ambao utamuwezesha kuweza kuendelea na masomo.
Nionavyo kulingana na hali hiyo ni wanafunzi wangapi wenye ujasiri kama aliouonyesha msichana huyo ambaye aliamua kujitoa muhanga na kuamua kulala porini ili kukimbia kuolewa.Kwa maelezo ya mtoto huyo anasema aliamua kukimbilia kwa Mkuu wa Wilaya baada ya kusikia kuwa kuna mradi wa 'Niache Nisome' ambao umeanzishwa kwa ajili ya kumkomboa mtoto wa kike dhidi ya mimba na ndoa za utotoni.
Nionavyo kwa mfano wa mradi huu ni wazi serikali ikaona umuhimu wa mradi huo kusambaa nchi nzima ili kuwawezesha vijana wa kike kujikomboa na ndoa na mimba za utotoni.

Monday, February 4, 2013

Lowasa awakonga nyoyo Walimu na Wanafunzi katika Shule ya Benjamini Mkapa Sekondari

 Mgeni Rasmi katika Mahafali ya kuwaga wanafunzi wa kidato cha sita shule ya Benjamini Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu-na Mbunge jimbo la Monduli Edward Lowasa, akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo
 Mgeni Rasmi katika Mahafali ya kuwaga wanafunzi wa kidato cha sita shule ya Benjamini Mkapa, Waziri Mkuu Mstaafu-na Mbunge jimbo la Monduli Edward Lowasa, akifafanua jambo wakati wa hafla hiyo
 Mhitimu wa Kkidato cha Sita katika shule ya Sekondari Benjamini Mkapa na Msanii wa Commedy,Daudi Festo, akionyesha moja ya vichekesho wakati wa hafla hiyo kwa mgeni Rasmi
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa, akipiga picha na Wanafunzi wa Shule hiyo
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa, akipiga picha na Viongozi wa Shule hiyo
 washiriki wa Onyesho la Miss Demokrasia Tanzania-Benjamini Mkapa Sekondari katika miondoko ya kimiss
 wanafunzi wa shule hiyo katika picha
washiriki wa Onyesho la Miss Demokrasia Tanzania-Benjamini Mkapa Sekondari-wakijibu maswali
 Wwashiriki wa Onyesho la Miss Demokrasia Tanzania-Benjamini Mkapa Sekondari katika pozi
 Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowasa, akipiga picha na Wwashiriki wa Onyesho la Miss Demokrasia Tanzania-Benjamini Mkapa Sekondari
 Wanafunzi wa Kidato cha Sita wakifuatilia kwa makini
 Wazazi wa wanafunzi wakifuatilia hafla hiyo
Wahitimu wa Kidato cha Sita katika Shule ya Sekondari Benjamini Mkapa, wakiimba Shairi(Picha kwa Hisani ya Miss Demokrasia Tanzanzania)