TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, July 15, 2014

MADUKA YANAUNGUA MUDA HUU MWANANYAMALA JIJINI DAR

Zaidi ya nyumba 3 za Biashara zilizopo karibu na Hospitali ya Mwananyamala  jijini Dar es Salaam zinateketea kwa moto ambao bado unaendelea kuwaka kwa kasi na kutishia nyumba zingine zilzopo jirani. Zimamoto wamefika eneo la tukio na kuanza kuzima moto. Endelea kufuatilia kwa taarifa 

Habari na picha zaidi endelea kutufuatilia 

Sunday, June 29, 2014

TMAA YAOKOA BILIONI 15 ZA MADINI, YAPONGEZWA

                                          Na Saidi Mkabakuli
Afisa Habari wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini nchini (TMAA), Mhandisi Yesambi Shiwa (Kulia) akitoa maelezo juu ya utendaji kazi wa TMAA kwa Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Hab Mkwizu (Kushoto) wakati alipotembelea kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.

Mashine ya kisasa ya kupimia ubora wa sampuli za madini ikioneshwa kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Hab Mkwizu (Kushoto) akizungumza na watumishi wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) alipowatembelea kwenye Banda lao. Wanaomsikiliza ni Afisa Habari, Mhandisi Yesambi Shiwa (Kulia) na Afisa Utumishi, Bibi Fatma Chondo (Katikati).

Makaa ya mawe yakioneshwa kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya sampuli za madini yapatikanayo nchini yakioneshwa kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Hab Mkwizu (Kushoto) akihimiza kufanya kazi kwa uzalendo kwa watumishi wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA) alipowatembelea kwenye Banda lao.
=======================================================================
Serikali imeupongeza Wakala wa ukaguzi wa madini nchini (TMAA) kwa kufanikiwa kuokoa kiasi kikubwa cha madini yaliyokuwa yakitoroshwa kinyemela katika viwanja vya ndege nchini hivyo kuokoa zaidi ya bilioni 15 zilizolipwa kama mrahaba tangu ilipoanzisha ukaguzi maalum kwa wasafiri waendao nje ya nchi.
Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Hab Mkwizu alipokuwa akikagua utendaji kazi wa Wakala katika maonesho ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Bw. Mkwizu alisema kuwa kwa muda mrefu sasa wafanyabiashara wasio waaminifu wamekuwa wakiitia hasara Serikali kwa kukwepa ulipaji wa kodi wa madini yaendayo nje ya Tanzania kinyume na utaratibu uliowekwa.
“Hongereni sana kwa kuweza kuokoa kiasi kikubwa cha madini yaliyokuwa yakisafirishwa bila kufuata taratibu zetu za usafirishaji wa madini yaendayo nje ya Tanzania,” alisema Bw. Mkwizu.
Naibu Katibu Mkuu Mkwizu aliwasihi viongozi na watumishi wa Wakala kuongeza uchapaji kazi na uzalendo ili kuweza kukomesha kabisa tabia ya wafanyabiashara hao wasio waaminifu.
Akikaribishwa kwenye banda la Wakala kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja na Afisa Habari wa Wakala hiyo, Mhandisi Yisambi Shiwa, Bw. Mkwizu alijulishwa kuwa moja kati ya mafanikio yaliyofikiwa na Wakala mara baada ya ukaguzi wa ziada kwa wasafiri waendao nje ya Tanzania, ni pamoja na kubainika mamia ya wafanyabiashara wa madini ambao wamekuwa wakitorosha kinyemela madini ya thamani kubwa ya fedha bila kufuata taratibu.
“Katika kuboresha utendaji kazi wa Wakala, tulitambulisha mpangokazi mpya wa ukaguzi wa ziada katika viwanja vyetu vya ndege vikubwa vya Dar es Salaam, Kilimanjaro na kile cha Mwanza lengo ni kubaini wafanyabiashara wasio waaminifu na ndipo tulipobaini wizi huu,” alisema Mhandisi Shiwa.
Akizungumzia thamani ya madini hayo, Mhandisi Shiwa alisema kuwa kufuatia ukaguzi huu, mpaka sasa Wakala imeweza kuokoa madini yenye thamani ya zaidi ya shilingi za kitanzania bilioni 15.
“Ukaguzi huu umesaidia kuokoa kiasi kikubwa cha madini yenye thamani ya shilingi bilioni 15.3 hadi kufikia mwaka na hivyo kuiongezea serikali yetu mapato ambayo yalikuwa yatoroshwe na wafanyabiashara hao wasio waaminifu,” aliongeza.
Kwa mujibu wa Mhandisi Shiwa, kiasi hiki cha fedha ni sehemu ya mrahaba wa kisheria unaostahili kuchangiwa na wafanyabiashara hao kwa umiliki wao wa madini hayo kabla ya kusafirisha nje ya nchi.
Mhandisi Shiwa aliongeza kuwa katika kuendelea kudhibiti tabia hizi, Wakala kwa kushirikiana na taasisi nyingine za serikali imekuwa ikishikilia na kutaifisha madini yanayotiliwa shaka ama kumilikiwa isivyo halali yanayopatikana katika viwanja hivyo.
Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania ni Wakala wa Serikali ulioanzishwa tarehe 2 Novemba, 2009 chini ya Sheria ya Wakala wa Serikali, Sura ya 245. Tamko la Waziri la kuanzisha Wakala lilichapishwa kwenye Gazeti la Serikali Namba 362 la tarehe 6 Novemba, 2009.
Lengo la Wakala ni kuhakikisha kwamba, Serikali inapata mapato stahiki kutoka kwenye shughuli za uzalishaji na biashara ya madini nchini kupitia usimamizi na ukaguzi makini wa shughuli za uchimbaji, na kuhakikisha kuwa shughuli hizo zinafanyika kwa kuzingatia uhifadhi na utunzaji thabiti wa mazingira katika maeneo ya migodi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Stephen Masato Wasira (Mb) Akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013

Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Dkt. Philip Mpango (Kushoto) pamoja na Naibu wake, Bw. Maduka Kessy wakifuatilia kwa umakini uwasilishaji wa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013 na Mpango na Maendeleo wa Taifa 2014/15.

Wageni wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Stephen Masato Wasira (Mb) ambao ni baadhi ya viongozi waandamizi wa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakifuatilia kwa umakini uwasilishaji wa Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013 na Mpango na Maendeleo wa Taifa 2014/15.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Stephen Masato Wasira (Mb) Akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013 na Mpango na Maendeleo wa Taifa 2014/15.

Tuesday, April 29, 2014

WAKULIMA WA ZAO LA TUMBAKU WATAKIWAKUFANYA KAZI KWA MALENGO ILI KUBORESHA MAISHA YAO CHUNYA


Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro akifungua  semina iliyoandaliwa na Benki ya NMB kwa wakulima wa zao la Tumbaku katika Ukumbi wa Sapanjo unaomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya Chunya

Mwakilishi wa Meneja wa NMB Kanda Sumka Mbuba amesema Benki ya NMB ina mkakati wa kuwa karibu na wakulima wa mazao mbalimbali na kuendesha semina mbalimbali zitakazowasaidia wakulima kujikwamua kiuchumi.

Meneja wa NMB wilaya Chunya Musa Mumba alisema Benki yake ipo tayari kutoa mikopo kwa wakulima wa zao la Tumbaku na kuwataka kuwa waaminifu katika kurejesha mikopo kwa wakati ili iweze kusaidia wakulima wengine.

Baadhi ya wwezeshaji tika NMB wakimsikiliza mgeni rasmi


Wakulima wa zao la Tumbaku wakiwa makini kumsikiliza mgeni rasmi




Picha ya pamoja


Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro amewataka wakulima wa zao la Tumbaku kufanya kazi kwa malengo ili kuboresha maisha yao na Watanzania ili kupata matokeo makubwa sasa(BRN).
Ameyasema hayo alipokuwa anafungua semina iliyoandaliwa na Benki ya NMB kwa wakulima wa zao la Tumbaku katika Ukumbi wa Sapanjo unaomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ili kuleta tija kwa wakulima ambao wamekuwa na maisha duni.
Kinawiro ameitaka Benki ya NMB kutoa mikopo nafuu kwa wakulima wa Tumbaku na kukopesha Pembejeo kwa gharama nafuu ili vyama viweze kujikwamua kiuchumi kwa ajili ya kupata majawabu sahihi na Serikali inaunga mkono juhudi zinazofanywa na Benki hiyo.
Aidha amewataka viongozi wa vyama vya Ushirika na Benki kufanya kazi kwa uadilifu na kuacha kukwepa kutorosha Tumbaku na kupeleka mikoa mingine na nchi jirani kwa nia ya kukwepa madeni wanayodaiwa pia kufanya hivyo kunakosesha serikali mapato yake yanayotokana na ushuru.
Pia amewataka wakulima wa zao la Tumbaku kuweka pesa benki na kuhakikisha wanapanda miti ili kutunza mazingira na kupata nishati mbadala ili kuhifadhi mazingira ya Wilaya ya Chunya.
Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Chunya alitumia fursa hiyo kuiomba Benki ya NMB kusaidia mazao mengine kama ufuta ambayo yamekuwa yakichangia kwa kiasi kikubwa pato la wilaya hiyo.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Meneja wa Kanda Sumka Mbuba amesema Benki ya NMB ina mkakati wa kuwa karibu na wakulima wa mazao mbalimbali na kuendesha semina mbalimbali zitakazowasaidia wakulima kujikwamua kiuchumi kama siku za hivi karibuni walifanya semina ka hii kwa wakulima wa zao la Kahawa ilyojumuisha wilaya za Mbeya,Mbozi,Rungwe,Ileje na Mbeya.
Meneja wa NMB wilaya Chunya Musa Mumba alisema Benki yake ipo tayari kutoa mikopo kwa wakulima wa zao la Tumbaku na kuwataka kuwa waaminifu katika kurejesha mikopo kwa wakati ili iweze kusaidia wakulima wengine.

Na Mbeya yetu 
Chunya

BASI LA AM LAMGONGA MWENDESHA BAISKELI ENEO LA MAJENGO ARUSHA


Mwendesha Baiskeri akiwa ameumia vibaya Mguuni baada ya kugongwa na Basi hilo
Picha na Arusha yetu Blog

Friday, April 18, 2014

MAMA AMSAMEHE NA KUMFUNGUA KITANZI MFUNGWA ALIYE HUKUMIWA KUFA KWA KUMUUA MWANAE

Wanasema uchungu wa mwana aujuae mzazi! Na kutokana na uchungu huo wa mama, ni vigumu kumshawishi akae meza moja na mtu aliyemuua mwanae kwa makusudi tena kwa kumpiga hadi kuhakikisha anakata roho.

Lakini imekuwa tofauti na jambo lililowaacha mdomo wazi umati wa watu uliohudhuria kushuhudia kunyongwa kwa mwanaume aliyemuua kijana mwenye umri wa miaka 18 nchini Iran ambako hukumu ya kunyongwa hadharani ni kawaida kwa mtu aliyepatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia, pale ambapo mama mzazi wa marehemu alipoingilia na kumfungua kitanzi muuaji huyo sekunde ya mwisho.
Kwa mujibu wa The Guardian, mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Balal alikuwa tayari amefungwa kitambaa cheusi na kuvalishwa kitanzi akisubiri amri ya kitanzi kufyatuliwa, ghafla mama huyo alimzaba kibao usoni na kuanza kumfungua kitanzi akisaidiana na mumewe!

“Mimi ni mtu wa imani.” Alisema mama huyo aliyefahamika kwa jina la Samereh Alinejad. “Nilipata ndoto ambayo mwanangu alikuwa ananiambia kuwa yuko katika sehemu nzuri na yenye amani…baada ya hapo, ndugu zangu wote, hata mama yangu, wakaanza kunihimiza nimsamehe muuaji huyu.”
Balal alihukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumpiga vibaya Abdollah Hosseinzadeh (18) hadi kumuua katika ugomvi uliotokea mtaani kati yao mwaka 2007.

Tuesday, April 15, 2014

Fredy Tony added 2 new photos. 7 hrs · Haya yaligongana moja likaingia chaka moja likapinduka ..kila moja na upande wake wa barabara Fredy Tony's photo. Fredy Tony's photo. Like · · Share Bana Kang'ata likes this. Mpalule Shaban Mwezi huu nimeshuhudia ajali nyingi sana barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na ile ya kwenda Mbeya baada ya Mikumi, lakini nahisi sema zilitokana na utelezi uliokuwa umeambatana na mvua za hapa na pale. lakini pia nawashauri madereva kwenda mwendo wa kawaida. kwani mwendo kasi ndo chanzo cha ajali.

Fredy Tony added 2 new photos.
7 hrs ·
Haya yaligongana moja likaingia chaka moja likapinduka ..kila moja na upande wake wa barabara
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Like · ·
  • Bana Kang'ata likes this.
  • Mpalule Shaban Mwezi huu nimeshuhudia ajali nyingi sana barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na ile ya kwenda Mbeya baada ya Mikumi, lakini nahisi sema zilitokana na utelezi uliokuwa umeambatana na mvua za hapa na pale. lakini pia nawashauri madereva kwenda mwendo wa kawaida. kwani mwendo kasi ndo chanzo cha ajali.

TIZAMA HAPA JINSI LOWASSA ALIVYOMKARIBISHA RAIS MSTAAFU MKAPA WILAYANI MONDULI

Rais mstaafu wa awamu wa tatu Mh Benjamin Mkapa amefanya ziara kutembelea shule ya msingi ya Manyara Ranchi inayofadhiliwa na shirika la kimataifa la uhifadhi wa wanyamapori la African Wildlife Foundation  Wilayani Monduli. Mzee Mkapa ni Makamu Mwenyekiti wa shirika hilo lenye makao yake mjini Washington Marekani. picha mbalimbali zinamuonesha Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akimuongoza Rais Mkapa kuzuru shule hiyo.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akizungumza Mzee Mkapa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akiagana na  Mzee Mkapa
 
NA: RWEYEMAMU BLOG

AJALI BARABARANI

:Liliacha njia
 
 
 
 
 
 
 
Like · ·

MAZIKO YA GUROMO ANGALIA MATUKION KATIKA PICHA

Monday, April 14, 2014

MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNGUMZIA TUKIO LA BOMU KULIPUKA KWENYE BAA USIKU APRILI 13, 2014

Usiku wa April 13 2014 kwenye baa iitwayo ‘Arusha night park’ iliyopo Mianzini Arusha ambayo siku zote ni miongoni mwa sehemu zinazokua na mkusanyiko wa watu wengi kuanzia jioni, limerushwa bomu wakati watu mbalimbali wakitazama mpira.
Blog hii imepata nafasi ya kuongea na mkuu wa mkoa wa Arusha ambae ni kiongozi
wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ambae amethibitisha kwamba ni
watu 15 wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Anasema
wote wamepelekwa hospitali ambapo uchunguzi wa awali umeonyesha bomu
hilo ni la kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa hajajulikana
alietekeleza shambulio hilo.
Kwenye sentensi nyingine pia amesema hakuna aliepoteza maisha kwenye shambulio hilo ambalo uchunguzi wa awali umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa rasmi pale uchunguzi kamili utakapokamilika.

ANGALIA PICHA ZA MUONEKANO WA DARAJA LA MTO RUVU LLILOJAA MAJI NA KUSABABISHA MAGARI KUSHINDWA KUPITA