Zaidi
ya nyumba 3 za Biashara zilizopo karibu na Hospitali ya Mwananyamala
jijini Dar es Salaam zinateketea kwa moto ambao bado unaendelea kuwaka
kwa kasi na kutishia nyumba zingine zilzopo jirani. Zimamoto wamefika
eneo la tukio na kuanza kuzima moto. Endelea kufuatilia kwa taarifa
TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Tuesday, July 15, 2014
Sunday, June 29, 2014
TMAA YAOKOA BILIONI 15 ZA MADINI, YAPONGEZWA
Na
Saidi Mkabakuli
| Mashine ya kisasa ya kupimia ubora wa sampuli za madini ikioneshwa kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. |
| Makaa ya mawe yakioneshwa kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. |
| Baadhi ya sampuli za madini yapatikanayo nchini yakioneshwa kwenye Banda la TMAA wakati wa Maadhimisho ya Utumishi wa Umma katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam. |
=======================================================================
Serikali
imeupongeza Wakala wa ukaguzi wa madini nchini (TMAA) kwa kufanikiwa kuokoa
kiasi kikubwa cha madini yaliyokuwa yakitoroshwa kinyemela katika viwanja vya
ndege nchini hivyo kuokoa zaidi ya bilioni 15 zilizolipwa kama mrahaba tangu
ilipoanzisha ukaguzi maalum kwa wasafiri waendao nje ya nchi.
Pongezi
hizo zimetolewa na Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa
Umma, Bw. Hab Mkwizu alipokuwa akikagua utendaji kazi wa Wakala katika maonesho
ya maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayofanyika katika Viwanja vya
Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Bw.
Mkwizu alisema kuwa kwa muda mrefu sasa wafanyabiashara wasio waaminifu
wamekuwa wakiitia hasara Serikali kwa kukwepa ulipaji wa kodi wa madini
yaendayo nje ya Tanzania kinyume na utaratibu uliowekwa.
“Hongereni
sana kwa kuweza kuokoa kiasi kikubwa cha madini yaliyokuwa yakisafirishwa bila
kufuata taratibu zetu za usafirishaji wa madini yaendayo nje ya Tanzania,”
alisema Bw. Mkwizu.
Naibu
Katibu Mkuu Mkwizu aliwasihi viongozi na watumishi wa Wakala kuongeza uchapaji
kazi na uzalendo ili kuweza kukomesha kabisa tabia ya wafanyabiashara hao wasio
waaminifu.
Akikaribishwa
kwenye banda la Wakala kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja na Afisa Habari wa Wakala
hiyo, Mhandisi Yisambi Shiwa, Bw. Mkwizu alijulishwa kuwa moja kati ya
mafanikio yaliyofikiwa na Wakala mara baada ya ukaguzi wa ziada kwa wasafiri
waendao nje ya Tanzania, ni pamoja na kubainika mamia ya wafanyabiashara wa
madini ambao wamekuwa wakitorosha kinyemela madini ya thamani kubwa ya fedha
bila kufuata taratibu.
“Katika
kuboresha utendaji kazi wa Wakala, tulitambulisha mpangokazi mpya wa ukaguzi wa
ziada katika viwanja vyetu vya ndege vikubwa vya Dar es Salaam, Kilimanjaro na
kile cha Mwanza lengo ni kubaini wafanyabiashara wasio waaminifu na ndipo
tulipobaini wizi huu,” alisema Mhandisi Shiwa.
Akizungumzia
thamani ya madini hayo, Mhandisi Shiwa alisema kuwa kufuatia ukaguzi huu, mpaka
sasa Wakala imeweza kuokoa madini yenye thamani ya zaidi ya shilingi za
kitanzania bilioni 15.
“Ukaguzi
huu umesaidia kuokoa kiasi kikubwa cha madini yenye thamani ya shilingi bilioni
15.3 hadi kufikia mwaka na hivyo kuiongezea serikali yetu mapato ambayo
yalikuwa yatoroshwe na wafanyabiashara hao wasio waaminifu,” aliongeza.
Kwa
mujibu wa Mhandisi Shiwa, kiasi hiki cha fedha ni sehemu ya mrahaba wa kisheria
unaostahili kuchangiwa na wafanyabiashara hao kwa umiliki wao wa madini hayo
kabla ya kusafirisha nje ya nchi.
Mhandisi
Shiwa aliongeza kuwa katika kuendelea kudhibiti tabia hizi, Wakala kwa
kushirikiana na taasisi nyingine za serikali imekuwa ikishikilia na kutaifisha
madini yanayotiliwa shaka ama kumilikiwa isivyo halali yanayopatikana katika
viwanja hivyo.
Wakala
wa Ukaguzi wa Madini Tanzania ni Wakala wa Serikali ulioanzishwa tarehe 2
Novemba, 2009 chini ya Sheria ya Wakala wa Serikali, Sura ya 245. Tamko la
Waziri la kuanzisha Wakala lilichapishwa kwenye Gazeti la Serikali Namba 362 la
tarehe 6 Novemba, 2009.
Lengo
la Wakala ni kuhakikisha kwamba, Serikali inapata mapato stahiki kutoka kwenye
shughuli za uzalishaji na biashara ya madini nchini kupitia usimamizi na
ukaguzi makini wa shughuli za uchimbaji, na kuhakikisha kuwa shughuli hizo
zinafanyika kwa kuzingatia uhifadhi na utunzaji thabiti wa mazingira katika
maeneo ya migodi.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Mheshimiwa Stephen Masato Wasira (Mb) Akiwasilisha Bungeni Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2013
Tuesday, April 29, 2014
WAKULIMA WA ZAO LA TUMBAKU WATAKIWAKUFANYA KAZI KWA MALENGO ILI KUBORESHA MAISHA YAO CHUNYA
| Mkuu wa Wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro akifungua semina iliyoandaliwa na Benki ya NMB kwa wakulima wa zao la Tumbaku katika Ukumbi wa Sapanjo unaomilikiwa na Halmashauri ya Wilaya Chunya |
| Baadhi ya wwezeshaji tika NMB wakimsikiliza mgeni rasmi |
| Wakulima wa zao la Tumbaku wakiwa makini kumsikiliza mgeni rasmi |
Friday, April 18, 2014
MAMA AMSAMEHE NA KUMFUNGUA KITANZI MFUNGWA ALIYE HUKUMIWA KUFA KWA KUMUUA MWANAE
Wanasema
uchungu wa mwana aujuae mzazi! Na kutokana na uchungu huo wa mama, ni
vigumu kumshawishi akae meza moja na mtu aliyemuua mwanae kwa makusudi
tena kwa kumpiga hadi kuhakikisha anakata roho.
Lakini imekuwa tofauti na jambo lililowaacha mdomo wazi umati wa watu
uliohudhuria kushuhudia kunyongwa kwa mwanaume aliyemuua kijana mwenye
umri wa miaka 18 nchini Iran ambako hukumu ya kunyongwa hadharani ni
kawaida kwa mtu aliyepatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia, pale
ambapo mama mzazi wa marehemu alipoingilia na kumfungua kitanzi muuaji
huyo sekunde ya mwisho.
Kwa
mujibu wa The Guardian, mwanaume huyo aliyejulikana kwa jina la Balal
alikuwa tayari amefungwa kitambaa cheusi na kuvalishwa kitanzi akisubiri
amri ya kitanzi kufyatuliwa, ghafla mama huyo alimzaba kibao usoni na
kuanza kumfungua kitanzi akisaidiana na mumewe!
“Mimi ni mtu wa imani.” Alisema mama
huyo aliyefahamika kwa jina la Samereh Alinejad. “Nilipata ndoto ambayo
mwanangu alikuwa ananiambia kuwa yuko katika sehemu nzuri na yenye
amani…baada ya hapo, ndugu zangu wote, hata mama yangu, wakaanza
kunihimiza nimsamehe muuaji huyu.”
Balal alihukumiwa kunyongwa hadi kufa
baada ya kupatikana na hatia ya kumpiga vibaya Abdollah Hosseinzadeh
(18) hadi kumuua katika ugomvi uliotokea mtaani kati yao mwaka 2007.
Tuesday, April 15, 2014
Fredy Tony added 2 new photos. 7 hrs · Haya yaligongana moja likaingia chaka moja likapinduka ..kila moja na upande wake wa barabara Fredy Tony's photo. Fredy Tony's photo. Like · · Share Bana Kang'ata likes this. Mpalule Shaban Mwezi huu nimeshuhudia ajali nyingi sana barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na ile ya kwenda Mbeya baada ya Mikumi, lakini nahisi sema zilitokana na utelezi uliokuwa umeambatana na mvua za hapa na pale. lakini pia nawashauri madereva kwenda mwendo wa kawaida. kwani mwendo kasi ndo chanzo cha ajali.
Fredy Tony added 2 new photos.
7 hrs ·
Haya yaligongana moja likaingia chaka moja likapinduka ..kila moja na upande wake wa barabara
- Bana Kang'ata likes this.
- Mpalule Shaban Mwezi huu nimeshuhudia ajali nyingi sana barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro na ile ya kwenda Mbeya baada ya Mikumi, lakini nahisi sema zilitokana na utelezi uliokuwa umeambatana na mvua za hapa na pale. lakini pia nawashauri madereva kwenda mwendo wa kawaida. kwani mwendo kasi ndo chanzo cha ajali.
TIZAMA HAPA JINSI LOWASSA ALIVYOMKARIBISHA RAIS MSTAAFU MKAPA WILAYANI MONDULI
Rais
mstaafu wa awamu wa tatu Mh Benjamin Mkapa amefanya ziara kutembelea
shule ya msingi ya Manyara Ranchi inayofadhiliwa na shirika la kimataifa
la uhifadhi wa wanyamapori la African Wildlife Foundation Wilayani
Monduli. Mzee Mkapa ni Makamu Mwenyekiti wa shirika hilo lenye makao
yake mjini Washington Marekani. picha mbalimbali zinamuonesha Waziri
Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akimuongoza Rais
Mkapa kuzuru shule hiyo.
Waziri Mkuu Mstaafu na
Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akizungumza Mzee Mkapa Waziri Mkuu
Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akiagana na Mzee Mkapa
NA: RWEYEMAMU BLOG
Monday, April 14, 2014
MKUU WA MKOA WA ARUSHA AZUNGUMZIA TUKIO LA BOMU KULIPUKA KWENYE BAA USIKU APRILI 13, 2014
Usiku
wa April 13 2014 kwenye baa iitwayo ‘Arusha night park’ iliyopo
Mianzini Arusha ambayo siku zote ni miongoni mwa sehemu zinazokua na
mkusanyiko wa watu wengi kuanzia jioni, limerushwa bomu wakati watu
mbalimbali wakitazama mpira.
wa Kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa ambae amethibitisha kwamba ni
watu 15 wamejeruhiwa kwenye mlipuko huo.
Anasema
wote wamepelekwa hospitali ambapo uchunguzi wa awali umeonyesha bomu
hilo ni la kutengenezwa kwa mkono na mpaka sasa hajajulikana
alietekeleza shambulio hilo.
Kwenye
sentensi nyingine pia amesema hakuna aliepoteza maisha kwenye shambulio
hilo ambalo uchunguzi wa awali umeshatoka, ila baadae itatoka taarifa
rasmi pale uchunguzi kamili utakapokamilika.
Subscribe to:
Posts (Atom)

























