TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, June 15, 2012

Mwanamke auawa katika fumanizi


Posted: 12 Jun 2012 11:48 PM PDT

Na Faida Muyomba, Geita                

MKAZI wa Kijiji cha Mwagimagi, Wilaya ya Geita, mkoani Geita, Bi. Dome Shaban (35), ameuawa kwa kupigwa na mumewe baada ya kumfumania akifanya mapenzi na mwanaume mwingine.

Akizungumza na waandishi wa habati, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Leonard Paulo, alisema tukio hilo lilitokea Juni 11 mwaka huu, saa nane usiku na kumtaja mtuhumiwa wa mauaji hayo kuwa ni Bw. Faida Anthony (45), ambaye ni mume wa mwanamke huyo.

Alisema mwanamke huyo alifumaniwa akiwa na mwanaume mwingine ambaye jina lake halikufahamika wakifanya mapenzi chumbani wakati mumewe hayupo.

“Mtuhumiwa aliporudi nyumbani aligonga mlango na kukuta mkewe akifanya mapenzi na mwanaume mwingine ambaye alifanikiwa kukimbia na hadi sasa hajulikani jina lake na mahali anapoishi,” alisema Kamanda Paulo.

Aliongeza kuwa, mtuhumiwa alichukua kitu chenye ncha kali na kumchoma sehemu ya jicho la kulia la kushoto kabla ya kumpiga sehemu mbalimbali za mwili hadi kusababisha kifo chake.

Alisema mtuhumiwa alitoroka baada ya mauaji hayo ambapo Jeshi la Polisi linaendelea kumsaka.
Posted: 12 Jun 2012 11:47 PM PDT

Na Salim Nyomolelo

SERIKALI imeanza kuchukulia hatua kwa taasisi, mashirika na watu mbalimbali wanaotumikisha watoto walio chini ya miaka 18 na kuwakosesha haki zao za msingi ikiwemo ya kupata elimu.

Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dkt. Makongoro Mahanga, aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika kilele cha Siku ya Kimataifa ya kupiga vita utumikishwaji watoto iliyoandaliwa na Shirika la Kazi Duniani (ILO).

Alisema tayari hatua za kisheria zimechukuliwa kwa watu wanaotumikisha watoto walio chini ya miaka 18, ambao  walichukuliwa na kupewa haki zao za msingi ikiwamo elimu.

Aliongeza kuwa, suala la malezi, matunzo na kuwalinda watoto dhidi ya vitendo vyote vinavyolenga kuhujumu haki zao ni jukumu la wadau wote kutokomeza vitendo hivyo.

“Utumikishwaji watoto katika kazi hatarishi ni hujuma kwa haki za mtoto kuishi, kukosa muda wa kupumzika, malezi bora, kucheza  na kupata elimu,” alisema Bw. Mahanga

Alisema utumikishwaji watoto ni tatizo la kitaifa na kimataifa, ambapo kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na ILO mwaka 2010, zinaonesha watoto milioni 215 wanatumikishwa katika sekta mbalimbali duniani kote.

“Katika Afrika nchi zilizo katika Jangwa la Sahara, zinakadiriwa kuwa na watoto milioni 65 wanaotumikishwa katika kazi za hatari, upande wa Tanzania kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa mwaka 2005/2006, asilimia 18.7 ya watoto wenye umri kati ya miaka mitano hadi 17, wanatumikishwa katika shughuli mbalimbali,” alisema Dkt. Mahanga.

Aliongeza kuwa, Serikali kwa kushirikiana na wadau imeandaa na imeanza kutekeleza mpango kazi wa kitaifa wenye lengo la kutokomeza utumikishwaji watoto.

Mpango huo umelenga kutimiza malengo ya milenia ifikapo mwaka 2015 ambapo Serikali imefanikiwa kuandaa orodha ya kazi hatarishi ambazo hazipaswi kufanywa na watoto chini ya umri wa miaka 18.
Posted: 12 Jun 2012 11:52 PM PDT
Mtoto ambaye jina lake halikupatikana akiangua kilio baada ya karanga na mayai aliyokuwa akiuza kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi eneo la Kawe kumwagika kutokana na upepo makali kama alivypnaswa na kamera yetu.Tukio hilo lilitokea jana ikiwa ni Siku ya Kupinga Utumikishwaji kwa Watoto Duniani yenye kauli mbiu "Haki za binadamu na usawa katika jamii tokomeza utumikishwaji wa watoto". (Picha na Blog ya Immatukio).
Posted: 12 Jun 2012 11:37 PM PDT
Na Godwin Msalichuma, Mtwara

WATUMISHI wawili wa Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, wamefikishwa mbele ya Hakimu Mkazi, Bi. Agnes Futakamba, wa Mahakama ya Wilaya hiyo wakituhumiwa kwa kosa la ubadhilifu wa sh. milioni 12.32 zilizotolewa kwa ajili ya kuendesha mafunzo ya makuzi na malezi ya mtoto.
Washtakiwa hao ni Bw. Hassan Mwakipa ambaye ni Ofisa Tabibu Msaidizi na Mhasibu Bw. Absolum Ntakandi ambaye hakuwepo mahakamani ambao wankabiliwa na mashtaka 15.

Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Bw. Sospeter Tyeah, alisema washtakiwa wote wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya Juni 11-16, 2009.
Alisema makosa hayo yamegawanyika katika maeneo matatu, ambayo ni kula njama za kumdanganya mwajiri wao na kubadilisha matumizi ya fedha kwa manufaa yao binafsi, kugushi nyaraka na kuhujumu uchumi.
Bw. Tyeah alisema katika kosa la kwanza, washtakiwa wanadaiwa
kutengeneza nyaraka za malipo ya washiriki 25 wa mafunzo ya makuzi na malezi ya mtoto Juni 11, 2009 na kila mmoja kulipwa sh. 320,000.
Kosa la pili, katika kipindi hicho washtakiwa wanadaiwa kutumia karatasi zisizo na tarehe kuwalipa washiriki saba sh. 450,000 kila mmoja maelezo ambayo ni ya uongo.
Mashtaka mengine ni kumlipa Bi. Elizabeth Macha, sh. 560,000 kwa madai ya kuhudhuria mafunzo hayo kama mwezeshaji na kuandaa stakabadhi namba R07584 ya Januari, 4, 2010.
Stakabadhi hiyo ilieleza kuwa, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo alimlipa Mkurugenzi wa Chuo cha Ushirika, tawi la Mtwara, sh. 129,000 kama gharama za ukumbi.
Bw. Tyeah ambaye alitumia zaidi ya dakika 20 kusoma tuhuma hizo, alidai washtakiwa walitumia tiketi ya ndege PW/MQQB7 ya Juni 9, 2009 wakidai ilitumiwa na Bi. Elizaberth Macha kwa ajili ya safari ambayo gharama yake ni sh. 368,000.
Stakabadhi nyingine haikuwa na tarehe ikionesha Mkurugenzi wa halmashauri hiyo alimlipa sh. 750,000, Mkuu wa Chuo cha Ushirika kwa ajili ya ukumbi.

Shtaka lingine ni kuwepo risiti inayoonesha Juni, 12, 2009,
Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo amemlipa mtu ambaye hakutajwa jina sh. 320,000 ili kununua karatasi kwa ajili ya kuendesha mafunzo hayo.

Bw.  Tyeah aliieleza mahakama kuwa washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kugushi nyaraka, kubadilisha matumizi ya fedha na kuisababishia halmashauri hasara ya sh. milioni 12.32.
Posted: 12 Jun 2012 11:35 PM PDT
Rais waZanzibar na Mwenyekiti wa Balaza la Mapinduzi, Dkt.Ali Mohamed Shein, alipokua akizungumza na wahariri na wahandishi wa habari wa vyombo vya habari mbalimbali vya Bara naVisiwani, kuhusu vurugu za kundi la uhamsho zilizotokea visiwani humo kwa siku tatu mfululizo (Juni 26,27 na 28 mwaka huu).Mazungumzo hayo yalifanyika mjini Zanzibar katika ukumbi wa Ikulu hivi karibuni ambapo Serikari ilisisitiza vurugu hizo kusitishwa mara moja.
Posted: 12 Jun 2012 11:26 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

KATIKA kile kinachoonekana kuguswa na sakata la usajili la beki wa timu ya Taifa (Taifa Stars) na Simba, Kelvin Yondani, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga, amesema suala hilo lina mwisho wake kwani chombo husika kitalifanyia kazi pale muda utakapofika.

Beki huyo hivi sasa amekuwa gumza si katika vyombo vya habari hata katika baadhi ya mitaa nchini kutokana na namna ambavyo inadaiwa kusajiliwa na Yanga akitoroshwa kambini usiku.

Kutokana na tukio hilo, uongozi wa Klabu ya Simba, ilitishia kuishtaki Yanga kwa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kutokana na kushindwa kufuata taratibu husika.

Akijibu swali kuhusu sakata hilo Dar es Salaam jana, Tenga alisema Yondani hajatoroshwa kama inavyodaiwa ila anachofahamu ni kwamba beki huyo ni mtu mkubwa ambaye anaweza kuamua lolote, hivyo hakutoroka ila aliondoka kambini.

"Mimi ninadhani tuna mambo mengi ya kufanya kuliko kuanza kuzungumzia hili la Yondani, hiki ni kipindi cha usajili la lolote linaweza kuzungumzwa, si kitu cha ajabu mchezaji kutoka timu moja kwenda nyingine," alisema Tenga na kuongeza;

"Ila hapa tatizo ni kwamba ametokaje kambini, je alipewa ruhusa na viongozi wake au alijiondokea tu na hilo tumewaachia viongozi wake walishughulikie na litakapokamilika watatupa majibu ya hatua gani wamechukua."

Alisema usajili una taratibu zake na muda wake hivyo kama mchezaji akiwa na mkataba atacheza lakini asipokuwa nao hawezi kucheza na kwamba ndio maana suala hilo la usajili lipo mikononi mwa klabu zenyewe.
Alisema ana imani muda ukifika hakuna shaka chombo kinachohusika kitalifanyia kazi na mwisho wa siku itajulikana atachezea klabu ipi lakini yanayoendelea hivi sasa ni 'unazi' wa mashabiki wa klabu hizo.

Aliongeza kutokana na tukio hilo, hivi sasa wameingia mikataba maalum na wachezaji wao ambao utakuwa ukiwaelekeza taratibu za kambi, hivyo mchezaji akienda kinyume na taratibu hizo hatua za kuchukuliwa zitakuwa wazi.
Mbali na hilo, Tenga aliipongeza timu ya Taifa (Taifa Stars) kwa ushindi walioupata wa mabao 2-1 dhidi ya Gambia na kwamba ameomba kikosi hicho kilicho na vijana wengi kilelewe ili baadaye ilete matunda kwa taifa.
Alisema amekoshwa na kiwango kilichooneshwa kwani hakuaimini kama wangeshinda katika mchezo huo lakini kutokana na kujituma katika dakika zote 90 ndivyo zilizosababisha kupata matokeo mazuri.
Posted: 12 Jun 2012 11:25 PM PDT

Na Victor Mkumbo

ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars),  Marcio Maximo, ameshindwa kuja nchini kama ilivyopangwa kutokana na kumalizia majukumu yake ya kuifundisha Democrata F.C ya Mjini Rio de Jeneiro, Brazil.
Kocha huyo alitarajiwa kutua nchini jana mchana kwa ajili ya kuja kusaini mkataba na mabingwa wa Kombe la Kagame, Yanga.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa timu ya Yanga, Luois Sendeu alisema kocha huyo ameshindwa kuja kama walivyopanga baada ya kutokea dharula na sasa atatua nchini mwishoni mwa wiki hii.
Alisema sababu kubwa iliyomfanya kocha huyo kushindwa kuwasili jana, ni kutokana na timu anayoifundisha kwa sasa ya Democrata F.C kukabiliwa na mchezo mgumu Jumamosi.
"Maximo tayari amekwishatumiwa tiketi ya safari ya kuja hapa nchini, ameshindwa kuwasili leo (jana) kutokana na Klabu yake anayofundisha kukabiliwa na mchezo mgumu,"
Sendeu alisema kuwa Marcio mara baada ya kuwasili nchini atafanya mazungumzo na Uongozi wa Klabu ya Yanga ikiwemo kusaini Mkataba na Klabu ya Yanga kabla ya kuanza kazi ya kukinoa kikosi hicho.
Wakati gazeti hili, likienda mitamboni lilipata taarifa kwamba timu hiyo haipo tayari kumuacha kirahisi kocha huyo, hivyo hawezi kuja nchini mpaka baadhi ya vitu waviweke sawa.
Posted: 12 Jun 2012 11:52 PM PDT
Posted: 12 Jun 2012 11:23 PM PDT

TATIZO la mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari nchini, linachangia kurudisha nyuma maendeleo ya elimu.
Takwimu za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi zinathibitisha kuwa tatizo hili limekuwa likiongezeka siku hadi siku hasa baada ya kuanzishwa shule za kata.
Pamoja na shule hizo kupunguza tatizo la wanafunzi kukosa nafasi za masomo, bado zinakabiliwa na changamoto nyingi.
Miongoni mwa changamoto hiyo ni tatizo la mimba kwa wanafunzi ambao wengi wao hulazimika kukatisha masomo, uhaba wa vifaa, vyumba vya madarasa, walimu na madawati.
Tafiti mbalimbali zimebaini kuwa, tatizo la mimba kwa wanafunzi hasa wa sekondari ni kubwa na linagusa hisia za kila mpenda maendeleo  lakini jamii kubwa bado haijahamasika kutoa ushirikiano wa karibu kwa vyombo vya dola ili kuwafichua wahusika wa vitendo hivyo.
Baadhi ya wazazi hupokea rushwa kutoka kwa watuhumiwa ili wasifikishwe katika vyombo vya sheria na kuchukuliwa hatua stahiki ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia za aina hiyo.
Sisi tunasema dhamira yetu ni kuona wazazi wanashirikiana na vyombo hivyo kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Kama jamii itaona umuhimu huu, Tanzania yenye wasomi wazuri waliobobea katika fani mbalimbali itawezekana na maendeleo yatakuwa kwa haraka.
Kitendo cha jamii kuendelea kuwaficha wahusika wa vitendo hivi, kinarudisha nyuma juhudi za Serikali na wadau wa elimu kuhakikisha mtoto wa kike anapata elimu bora.
Imani yetu ni kwamba, uwajibikaji wa viongozi wa vyama na Serikali unahitajika kwa kuhamasisha jamii iboreshe maendeleo ya elimu hasa kwa mtoto wa kike na kukomesha tatizo la mimba.
Umefika wakati wa wanafunzi wetu, kupewa elimu ya kujitambua na kufahamu wajibu walionao kwa jamii na Taifa ili waweze kujithamini na kuepuka vishawishi vinavyoweza kusababisha wapate mimba au kuacha shule.
Elimu ni nyenzo muhimu kwa maendelo ya Taifa lolote Duniani kwani mapinduzi mengi ya maendeleo, hutegemea kiwango cha elimu kwa jamii husika.
Posted: 12 Jun 2012 11:13 PM PDT

Na Sophia Fundi, Ngorongoro

MAMLAKA ya Hifadhi ya Ngorongoro, mkoani Arusha,  imewakamata watu wanne wanaodhaniwa kuwa majangili ambao huwinda wanyama kwa kuwapa sumu katika msitu wa mamalaka hiyo ulioko eneo la Kambi ya Simba, wilayani Karatu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Meneja Huduma za Uhifadhi wa mamlaka hiyo, Bw. Amiyo Amiyo, alisema watu hao walikamatwa juzi, saa ya nne asubuhi katika Msitu wa Sahata.

Alisema watu hao walikuwa na maboga 10 ambayo ndani yake waliyaweka sumu ya kuulia wanyama mbalimbali hasa tembo.

Aliongeza kuwa, hivi sasa majangili wamebadili mbinu ya kuwinda wanyama wakitumia sumu aina ya “aldicarb” ambayo kwa jina jingine hujulikana kama “temk”, kwa mujibu wa uchunguzi wa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Bw. Amiyo alisema sumu hiyo ipo kwenye kundi la “Carbametes”, ambayo huathiri mfumo wa ufahamu wa mnyama kama wataila hivyo kusababisha kifo chake.

Katika tukio hilo, majangili hao walikutwa wakilinda maboga waliyotega msituni ili yasiliwe na wanyama wengine zaidi ya tembo ambapo kutokana na hali hiyo, mamlaka imelazimika kuimarisha ulinzi katika misitu.

“Kutokana na doria tunayoifanya kila siku, tumefanikiwa kukamata majangili hawa na kukuta mizoga ya tembo wawili ambao tayari walikuwa wametolewa meno,” alisema.

Alisema majangili hao wanafahamika kwa majina ya Bw. John Lohay (62),  Bw. John Amisi (27), Bw. Isaya Arusha (36), Bw. Roman Amsi (23) wote wakazi wa Kambiya Samba, wilayani Karatu na wamekabidhiwa kwa Jeshi la Polisi.

Aliongeza kuwa, Februali mwaka huu mamlaka hiyo ilifanikiwa kukamata watu wawili katika Msitu wa Mangola Juu wilayani Karatu wakiwa na matikiti maji 60 ndani ya msitu huo.

Alisema matikiti hayo yalikuwa na sumu ya iina hiyo na tayari wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya mjini Karatu.

“Kimsingi majangili wamebuni mbinu mpya ya kuwatega wanyama na kuwaua kwa kutumia sumu, tutahakikisha ulinzi unaimarishwa dani ya misitu yetu ili kupambana na hawa magangili,” alisema.
Posted: 12 Jun 2012 11:12 PM PDT

Na Anneth Kagenda

MAMLAKA ya Usafirishaji wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) inashikilia daladala zaidi ya 126 kwa kukutwa na makosa mbalimbali, yakiwemo ya kutoa lugha ya matusi, kupandisha nauli holela na mengine kutokuwa na leseni.
Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari Dar es Salaam jana na kusainiwa na Ofisa Uhusiano wa SUMATRA Bw. David Mziray, ilieleza kuwa katika kipindi cha Mei na Juni, 2012 mamlaka ilikamata  ya daladala zenye  makosa mbalimbali, huku wamiliki wa mabasi hayo wakitozwa faini kati ya sh 100,000 na sh 250,000.

Alisema daladala nyingi zilikamatwa kwenye mkosa ya kutokuwa na leseni, kughushi nyaraka za Serikali, kuiba njia, kutokuwa na tiketi kutovaa sale, kupakia eneo ambalo si la kitu na mengine.

Bw. Mziray alisema kutokana na hali hiyo mmiliki ambaye basi lake litabainika na makosa hayo atachukuliwa hatua za kisheria.

"Pamoja na kulipa faini hiyo mmiliki atatakiwa kusitisha mkataba na kumbadilisha dereva wa basi husika ndipo aruhusiwe kuendelea na utoaji huduma ya usafiri," alisema.
Posted: 12 Jun 2012 11:11 PM PDT

Posted: 12 Jun 2012 11:09 PM PDT

Na Victor Mkumbo

MNYANGE atakayeiwakilisha Tanzania katika mashindano ya urembo ya dunia mwaka huu anatarajiwa kupatikana Jumamosi.

Mwakilishi huyo atapatikana katika mashindano yaliyopewa jina la Redd's Miss World Tanzania yatakayofanyika katika Ukumbi wa 327 Club jijini.

Akizungumza na Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Lino Agency ambao ndio waandaaji wa mashindano ya urembo nchini, Hashim Lundenga alisema mashindano hayo yanatarajia kushirikisha jumla ya warembo 10.

Alisema warembo 10 ndio waliothibitisha kushiriki katika mashindano hayo ambaye mmoja wao ndio ataiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss World yatakayofanyika Agosti, mwaka huu nchini China.

Lundenga alisema kuwa wameamua kuchukua warembo waliowahi kushiriki katika mashindano ya Miss Tanzania katika miaka iliyopita, kutokana na mabadiliko ya ratiba ya mashindano kwani awali yalikuwa yanafanyika Desemba.

"Tumeamua kuchukua warembo ambao walishawahi kushiriki katika mashindano ya Miss Tanzania miaka iliyopita kwa kuwa mashindano yetu huwa yanaanza Mei na kumalizika Septemba," alisema.

Lundenga alisema mshindi katika mashindano hayo anatarajiwa kuzawadiwa sh. milioni 10 pamoja na kufanyiwa maandalizi yote ya kwa ajili ya matayarisho ya safari.

Naye Meneja wa kinywaji cha Redd's, Victoria Kimaro, alisema wamejiandaa vizuri na mashindano hayo ambapo wanatarajia kuwa watapata mwakilishi mzuri.

Alisema kuwa shindano hilo litakuwa kwa ajili ya watu maalum ambao wataalikwa na kutakuwa na burudani ya aina yake.
Posted: 12 Jun 2012 11:08 PM PDT
Mkurugenzi wa Kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga (kushoto), akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) Dar es Salaam jana kuhusu shindano la Redd's Miss World Tanzania litakalofanyika Jumamosi. Kulia ni Meneja wa kinywaji cha Redd's, Victoria Kimaro (Picha na Victor Mkumbo)
Posted: 12 Jun 2012 11:04 PM PDT
Na Daud Magesa, MWANZA

BENDI mbili kongwe za Muziki wa Dansi zenye upinzani wa jadi, DDC Mlimani Park (Sikinde) na Msondo Ngoma, zinatarajia kutoa burudani katika maadhimisho ya sherehe za miaka mitano tangu kuanzishwa kwa  klabu ya starehe ya Villa Park Resort.

Sherehe hizo zitahusisha michezo ya soka, muziki wadansi, taarabu na disco zitafanyika kuanzia Juni 14 hadi 16, mwaka huu jijni.

Akizungumza na gazeti hili jana kuhusu sherehe hizo, Meneja wa hoteli ya Villa Park Resort, Shijani Mtunga, alisema sherehe hizo zimelenga kuwakumbuka wadau wanaofanya nao biashara na kujumuika nao ili kurudisha fadhila kwao.

Alisema kutokana na wadau hao kuwaunga mkono, ili kusherehekea vizuri wamewaandalia burudani mbalimbali za soka, muziki wa dansi, taarabu na disco kwa kila mtu.

Alisema wapenzi wa muziki wa dansi, watapata burudani ya muziki huo kutoka kwa Msondo Ngoma na Sikinde, zitakapopambana Ijumaa, zikisindikizwa na bendi mwenyeji ya Super Kamanyola, ambapo Jumamosi itakuwa ni mapumziko na fainali itafanyika Jumapili.

Alisema ufunguzi wa bonanza hilo utafanyika Alhamisi kwa msanii, Jokha Kassim maarufu kama Kanga Moko, atachengua kwa kutoa burudani ya muziki wa taarabu na Ijumaa kutakuwa na disko.

“Bonanza hili la miaka mitano ya Villa Park, si kucheza tu bali pia kufanya mazoezi ili kujenga afya.Kauli mbiu yake ni kula ni lazima, michezo ni afya," alisema Mtunga.

Posted: 12 Jun 2012 11:03 PM PDT


Na Zahoro Mlanzi

WAREMBO 12 wanaotarajia kuwania taji la kitongoji cha Kigamboni, mwaka huu 'Miss Kigamboni City 2012', leo wanatarajiwa kufanyiwa usaili kwa ajili kumpata mshindi wa shindano hilo litakalofanyika Ijumaa kwenye Ukumbi wa Navy Beach, Dar es Salaam.


Akizungumza Dar es Salaam jana, Mratibu wa shindano hilo, kutoka Kampuni ya K&L Media Solutions, Somoe Ng'itu, alisema maandalizi ya zoezi hilo yamekamilika na wanachosubiri ni siku ya shindano ifike.

Alisema kitongoji hicho kina warembo wenye sifa na wanaojiamini ambao wamepania kurudisha taji la Miss Tanzania kwenye Kanda ya Temeke.

Aliongeza ili kuboresha shindano hilo Bendi ya Muziki wa Dansi ya FM Academia 'Wazee wa Ngwasuma' na msanii na mchekeshaji mahiri hapa nchini, Mpoki watatumbuiza kwenye kinyang'anyiro hicho.

"Tunawaomba wadau wa sanaa ya urembo kufika kushuhudia mrembo wa Kigamboni atakavyopatikana, ni Kitongoji kilichoko sehemu pekee hapa nchini, hivyo ni vizuru kushuhudia shindano hilo," alisema Somoe.

Aliwataja warembo watakaochuana ni Susanne Jeremiah, Agness Goodluck, Elizabeth Boniface, Dorothea Kessy, Esther Albert, Edda Silyvester, Sophia Martin, Doreen Kweka, Khadija Kombo, Linnah David, Rosemary Peter na Winnie Karaya.

Aliwashukuru wadhamini ambao wamejitokeza kusaidia shindano hilo ambao ni Redd's, Dodoma Wine, hoteli ya Hope Country, Screen Masters, Global Publishers, Nobro Collections, Times FM na Clouds FM.

Aliongeza kuwa warembo watakaoshika nafasi tatu za juu kutoka katika shindano hilo wataungana na wenzao kutoka vitongoji vya Kurasini na Chang'ombe ili kuwania taji la Kanda ya Temeke baadaye mwaka huu.

Washindi wa tuzo za excel with Grand Malt kutoka Vyuo vya CBE na UDOM




Washindi wa tuzo za excel with Grand Malt kutoka Vyuo vya CBE na UDOM wakiwa katika Picha ya Pamoja na Wafanyakazi wa kampuni ya Bia ya Tanzania(TBL) na Mwakilishi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini

Wednesday, June 13, 2012

Redds Miss World Tanzania 2012



Washiriki wa shindano la Redds Miss World Tanzania 2012 wakiwa kwenye kambi yao iliyopo kwenye Hotel ya Kitalii ya Giraffe jijini Dar Es Salaam tayari kwa shindano lao la jumamosi hii kumpata mwakilishi wa Taifa.Toka kulia
1.Gloryblaca Mayowa (Lindi)2. Hamisa Hassan (Kinondoni)3. Queen Saleh (Ilala)4. Christine Willium (Iringa)5. Pendo Laizer (Arusha) 6.Lisa Jensen (Mara)7. Mwajuma JUma (Tmk)8. Neema Saleh (Ilala) 9.Jeneffer Kalolaki (Ilala) 10.Stella Mbuge (Kinondoni)

Akili za wasomi zitumike kuendeleza sekta ya elimu

Posted: 12 Jun 2012 12:52 AM PDT

Posted: 12 Jun 2012 12:48 AM PDT

Na Willbroad Mathias

MWISHONI mwa wiki  Waziri wa Mambo ya Nje, Bw. Bernard Membe, aliwakaribisha nyumbani kwake viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kula nao chakula cha mchana.

Wakati wa chakula hicho alizungumza na viongozi hao masuala mbalimbali ya kisiasa ukiwemo mwenendo wa upepo wa kisiasa nchini.

Katika mazungumzo hayo Bw. Membe alikitabiria ushindi CHADEMA katika uchaguzi mkuu unaokuja na akasema kwamba chama hicho kimetokea kupendwa na wananchi katika kila kona ya nchi na hata operesheni yao ya Kusini imekitikisa chama tawala.

Viongozi hao waliookutana na Bw.Membe ni Mjumbe wa Kamati  Kuu, Bw. Godbless Lema, aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha kabla ya kuhamia CHADEMA, Bw.James Millya na viongozi wakuu waandamizi.

Waziri Membe aliwaambia viongozi hao kwamba ameishi nchi mbalimbali duniani zenye demokrasia ya hali ya juu hivyo hatashangazwa hata kidogo kama CHADEMA itaingia Ikulu.

Katika mazungumzo hayo Bw. Membe alienda mbali zaidi na kugusia  kesi iliyotengua ubunge wa Bw. Lema  ambapo alidai kushtushwa na kusema kwa vile amekata rufaa anaamini mahakama ya rufaa itamrejeshea ubunge wake.

Kwa kitendo hicho nashawishika kumpongeza  Bw.Membe  kwani  ameonesha kukomaa kisiasa na anastahili kuwa mfano wa kuigwa na wanasiasa wengine nchini.

Mbali na kumpongeza  naweza kusema kuwa ameonesha ushujaa  kwa kusema ukweli  kwani ni wachache ndani ya CCM ambao wanaweza kusimama wakaeleza ukweli huku wakifahamu chama kinakoelekea siko.

Wana CCM wenye moyo wa dhati na chama wanatambua kuwa hali ya upepo kwa sasa ndani  ya chama sio shwari kutokana na wimbi  la wanachama wake kukimbilia CHADEMA, lakini ni wachache wanaoweza kutamka hili japo  moyoni wanajua ukweli wengine wanashindwa kutamka kwa kuhofia ugali wao, wengine kuhofia posho, huku hali halisi inaonekana wazi.

Kwa kuamua kuwa muwazi, Bw.Membe ameongea yaliyo moyoni mwake na pia, ameonesha busara, hata kuna baadhi ya mawaziri na wabunge kama Ezekiel Maige amewahi kutoa kauli kama hii zaidi ya mara moja.

Na kwa kufanya hivyo, basi ni mtu mkweli asiyetaka kuficha ukweli kwa mgongo wa kukipendezesha chama kinachoshindwa kuangalia maslahi ya umma, ubinafsi na umimi, hivyo hakuna haja ya kumshambulia.

Nasema hivyo kutokana na kwamba hakuna mtu anayekuwa mtenda dhambi wa milele, isipokuwa sheteni, huongea maneno yenye upako wa Mungu, tuyaheshimu na kuyafanyia kazi kwa tahadhali ya hali ya juu.

Nashawishika kusema hivyo  kutokana na kwamba kwa hapa nchini, nina uhakika itakuwa ni mara ya kwanza kwa mbunge kuwaalika wapinzani nyumbani kwake na kuwaandalia chakula huku akiwapa maneno ya faraja kama hayo.

Hii ni kutokana na kuwa baadhi ya wanasiasa ambao wamekuwa wakichukulia siasa kama uhasama huku wakiwabeza wapinzani kwamba hawana uwezo wa kuingia Ikulu, licha ya kuelewa uwezo mkubwa waliokuwa nao baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani.

Hali hiyo imekuwa ikitokana na baadhi ya wanasiasa  kutojiamini wakidhani endapo utamkaribisha kiongozi ama mwanachama wa upinzani nyumbani kwako utakuwa unaliweka jimbo lako rehani.

Imani hiyo ndiyo imekuwa ikiwafanya baadhi ya wanasiasa  kujenga fitina miongoni mwa wafuasi wao ili wawachukie wapinzani.

Pia imani  hiyo  imekuwa ikiwafanya kujiona miungu watu huku wakiwaona wapinzani kama maadui ambao muda wote wanatishia kukitia mchanga kitumbua chao.

Kwa sasa taifa letu linakabiliwa na  hali ngumu kiuchumi iliyosababisha pia kupanda kwa gharama za maisha ,lakini wapo wapinzani ambao wamekuwa wakitoa maoni yao yenye mwelekeo wa kulinusuru taifa, lakini matokeo yake wamekuwa wakionekana kuwa maadui kwa baadhi ya wanasiasa, wakati wangeweza kuwasaidia kufikia malengo.

Nichukue fursa hii kuwaomba viongozi wengine wa siasa kulitambua jambo hilo la kuwa upinzani siyo uhasama bali ni chachu ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo.

Viongozi wakikubali changamoto katika siasa hawataweza kuchukiana bali kujengana  kisiasa na kuongeza mshikamano baina yao.

Hii itawasaidia pia kusimama palipo na ukweli kwa maslahi ya wananchi na kuweka itikadi za kivyama mbali.

Siasa isichukuliwe kama uhasama ambao unaweza kuzaa migogoro isiyoisha, mnatakiwa kukaa pamoja na kujadili ni kwa jinsi gani mtatoa tulipo.

Hakuna kitu kinachonisikitisha ninapowaona wanasiasa wakongwe wakipanda jukwaani na kulumbana badala ya kutoa hoja za msingi kwa wananchi za utatuzi wa matatizo yaliyopo.

Tumechoshwa na siasa za uadui, siasa ni urafiki na kuiga mazuri anayofanya ama aliyofanya mwenzako hadi kukubalika na kupewa ridhaa na wananchi wake.

Hongera sana waziri Membe umekuwa  mfano wa kuigwa, wengine wafuate nyayo hizo.
Posted: 12 Jun 2012 12:40 AM PDT

Waimbaji wa bendi ya muziki wa dansi ya Msondo Music, wakiimba Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kutoka kushoto ni Eddo Sanga, Muhidini Gurumo na Juma Katundu. Picha na Rajabu Mhamila

Posted: 12 Jun 2012 12:37 AM PDT

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia yake ya Safari Lager imekabidhi vitendea kazi mbalimbali kwa wajasiriamali 11 walioshinda kupewa ruzuku za Safari Wezeshwa vyenye thamani ya sh. milioni 50.

Akizungumza katika sherehe za makabidhiano ya vifaa hivyo jijini Arusha jana katika viwanja vya Soweto Meneja wa Safari Lager, Oscar Shelukindo alisema mashindano hayo ya Wezeshwa na Safari Lager nia yake kubwa ni kuwapatia ruzuku wajasiriamali wadogo na wakati kuendeleza biashara zao.

Shelukindo alisema jumla ya sh. milioni 50 zimetumika katika kununulia vifaa hivyo kwa Kanda ya Kaskazini, ambapo mwaka 2011 ruzuku ilikuwa ni milioni 200 kama vifaa vya vitendea kazi kwa wajasiriamali hao walioshinda katika mashindano hayo.

Alisema utaratibu huo huo ulianzia Mbeya na Arusha na wanatarajia wiki ijayo kuwa Mwanza na mwisho watamalizia Dar es Salaam.

Naye Mgeni rasmi katika sherehe hizo, Niarire Magunda ambaye ni Ofisa Biashara Manispaa ya Arusha, aliipongeza TBL kupitia bia yake ya Safari Lager kwa kuanzisha programu hiyo yenye nia ya kuwasaidia wajasiriamali wadogo na wakati.

Katika sherehe hizo wajasiriamali 11 kutoka Arusha, Moshi na Tanga walikabidhiwa vifaa mbalimbali vya vitendea kazi.

Posted: 12 Jun 2012 12:35 AM PDT

Bondia Nassibu Ramadhani (kushoto) na Fadhili Majia wakioneshana ufundi wa kutupa masumbwi wakati wa pambano lao la ubingwa wa Taifa. Ramadhani alishinda kwa point. Picha na Rajabu Mhamila

Posted: 12 Jun 2012 12:31 AM PDT

Na Zahoro Mlanzi

MCHEZO wa timu ya Taifa (Kilimanjaro Taifa Stars) na Gambia, uliochezwa juzi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, umeingiza sh. 124,038,000.

Mechi hiyo ilikuwa ni ya Kundi D ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil, ambapo wenyeji Kilimanjaro Taifa Stars iliibuka na ushindi wa mabao 2-1.


Timu zingine za kundi hilo ni Ivory Coast na Morocco, ambazo nazo zilifungana kwa mabao 2-2.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura ilieleza kwamba mapato hayo yametokana na washabiki 31,122 waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo.

"Asilimia 18 ya mapato hayo ambayo ni sh. 18,921,050.85 ilikwenda kwenye Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) wakati gharama kabla ya mgawo zilikuwa (sh. 6,555,000) na bonasi kwa Taifa Stars (sh. 15,767,542.37)," alisema Wambura.

Alisema waamuzi sh. 13,372,000, usafi na ulinzi sh. 2,350,000, maandalizi ya uwanja ni sh. 400,000, Wachina ni sh. 2,000,000, umeme sh. 300,000 na mafuta ya jenereta sh. 200,000.

Aliongeza kwa upande wa mgawo asilimia 20 ya gharama za mechi ni sh. 12,834,481, asilimia 10 ya uwanja sh. 6,417,241, asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) sh. 3,208,620, asilimia 20 ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 12,834,481 na asilimia 45 ya TFF (sh. 28,877,583).

Wakati huohuo, Waamuzi 54 wameanza kozi ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Wambura, alisema kozi hiyo itamalizika Juni 14, mwaka huu na inaendeshwa na wakufunzi wawili kutoka FIFA wakisaidiwa na wakufunzi wengine wanne wa TFF. Wakufunzi wa FIFA ni Carlos Henriques na Mark Mizengo.

Wakufunzi kutoka TFF ni Kapteni mstaafu Stanley Lugenge, Leslie Liunda, Soud Abdi na Riziki Majala.
Posted: 12 Jun 2012 12:29 AM PDT
Vyakula vya kuoka maarufu kama burgers ambavyo vimeelezwa kuwa na madhara katika afya ya binadamu.

Posted: 12 Jun 2012 01:28 AM PDT


Darlin Said na Radhia Adam

TAASISI ya Mawasiliano (TCRA), imeliomba Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kuhamasisha wasanii kuongeza na kuboresha vipindi vyao, ili viweze kuleta maendeleo ya nchi katika tasnia ya sanaa na utamaduni.

Ombi hilo limetolwea na Mhandisi Mwandamizi wa masafa TCRA, Joel Chacha katika kongamano lililohusu teknolojia ya dijitali na faida zake kwenye sekta ya sanaa na wasanii, lililowasilishwa kwenye jukwaa la sanaa liliofanyika Dar es Salaam jana.


Chacha alisema katika mabadiliko ya utangazaji kutoka analogi kwenda dijitali sekta ya sanaa na wasanii nchini, watafaidika kwa kutangaza kazi zao za usanii na kuutangaza utamaduni wa Mtanzania ndani na nje ya nchi.

"Kupitia mabadiliko haya ya sanaa, Tanzania itapata soko kwa njia iliyo rahisi na kuwatangaza wasanii nje ya mipaka yetu, pamoja na kuutangaza utamaduni wetu na pia wasanii watapata ajira mbalimbali kutokana na kuongezeka kwa kampuni za sanaa," alisema.

Mbali na faida hizo, baadhi ya wasanii waliohudhuria kongamano hilo wameulalamikia mfumo huo mpya kutokana na changamoto watakazokumbana nazo ikiwemo upoteaji wa kazi zao za filamu na utamaduni wa Mtanzania.

"Kupitia mfumo wa dijitali, ambao unalenga kutumia ving'amuzi itakuwa rahisi kwa mtu wa nje ya nchi kuiba sanaa zetu kwa kunyonya kazi zetu na kwenda kutumia katika nchi zao," alifafanua Surchyang Raphael ambaye ni msanii na Mwenyekiti wa TASA, Ilala.

Naye msanii kutoka kundi la Kashkash, Amos Beda aliulalamikia mfumo huo kwa kusema kwamba mfumo huo ni wa gharama kwa mwananchi wa kawaida kuweza kuumudu katika kununua king'amuzi na kulipia gharama za uendeshaji.

Wakizungumza katika changamoto za mfumo wa dijitali wasanii hao, waliiomba TCRA kusimamia kudhibiti mfumuko wa bei ya ving'amuzi na pia kudhibiti uingiaji wa aina tofauti za ving'amuzi, ili iwe rahisi kwa mwananchi kumiliki king'amuzi kiurahisi zaidi ambacho kitaonesha chaneli zote.

Mfumo wa digitali ulizinduliwa rasmi Agosti mwaka jana na Rais Jakaya Kikwete, ambao ulienda sambamba na uzinduzi wa nembo ya dijitali kwa ambao utekelezaji wake unatarajiwa kuanza rasmi Januari 2013.
Posted: 12 Jun 2012 12:17 AM PDT

Posted: 12 Jun 2012 12:16 AM PDT


Na Elizabeth Mayemba

KAMATI ya Uchaguzi ya Yanga, jana ilitangaza majina ya wagombea wa uchaguzi mdogo wa klabu hiyo ya kujaza nafasi za waliojiuzulu baada ya kupitia vyeti vyao, hivyo yatabandikwa ubaoni keshokutwa ili kutoa nafasi kwa wale wenye pingamizi.

Uchaguzi huo unatarajiwa kufanyika Julai 15, mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana Katibu wa kamati hiyo, Francis Kaswahili alisema kati ya majina 29 ya walioomba kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, Abdallah Sharia ambaye ni mkazi wa Zanzibar vyeti vyake hakuwasilisha hivyo ametakiwa kufanya hivyo kabla ya usaili, baada ya mwenyewe kuiomba kamati.

Kaswahili alisema mgombea Mohammed Mbaraka, yeye ameondolewa katika kinyang'anyiro hicho kwa kuwa hana sifa.

Kwa upande wa wanaogombea nafasi ya Mwenyekiti wote wanne wamepita, ambao ni Yusuf Manji, John Jambele, Edgar Chibura na Sarah Ramadhan kwa nafasi ya Makamu Mwenyekiti waliopita ni Ayoub Nyenzi, Clement Sanga, Yono Kevela na Ally Mayai.

Wajumbe waliopita ni Lameck Nyambaya, Ramadhani Kampira, Mohamed Mbaraka 'Binkleb', Ramadhan Said, Edgar Fongo, Ahmed Gao, Beda Tindwa, Jumanne Mwamenywa na George Manyama.

Wengine ni Gadeuncius Ishengoma, Haron Nyanda, Omary Ndula, Shaban Katwila, Justine Baruti, Jamal Kisongo, Peter Haule na Stanley Kevela 'Yono'ambaye pia anagombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti.

Kaswahili alisema pingamizi kwa walioomba kugombea uongozi litaanza kutolewa Juni 14 hadi 18, mwaka huu na baada ya hapo Kamati za Yanga na TFF zitakaa kupitia pingamizi hizo.

"Tunatoa hadhari kwa wale wote ambao wataleta pingamizi zao wawe na ushahidi wa kutosha, kinyume na hapo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao," alisema Kaswahili.
Posted: 12 Jun 2012 12:13 AM PDT
Mkuu wa Chuo cha Aseki Dodoma, Bw. Omari Kiputiputi akizungumza katika mahafali ya kwanza ya chuo hicho yaliyofanyika hivi karubuni, ambapo wahitimu mbalimbali walitunikiwa vyeti katika fani za biashara, kushoto ni Mwenyekiti wa bodi ya mitihani ya chuo hicho, Balozi Job Lusinde na Mwenyekitu wa Bodi ya Wakurugenzi wa chuo hicho,Dk. Richard Mushi. (Picha na Mpiga Picha wetu)
Posted: 11 Jun 2012 11:58 PM PDT

Na Willbroad Mathias

ILI Tanzania iwe na maendeleo endelevu lazima kujenga utamaduni wa kujiendeleza kimasomo hasa katika fani za biashara na ujasiriamali.

Kwa kufanya hivyo, watakuwa wamejirahisishia mazingira ya kumudu ushindani unaolikabili soko la ajira ndani na nje ya nchi. Hakuna njia ya mkato zaidi ya watu kuwekeza katika sekta ya elimu.

Changamoto hiyo ndiyo imewafanya watanzania wengi kuwekeza katika elimu.

Mkuu wa Chuo Cha Biashara cha Aseki cha mkoani Dodoma,  Bw. Omari Kiputiputi, wakati akizungumzia maendeleo ya elimu na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo pamoja na umuhimu wa ujasiriamali.

Bw. Kiputiputi anasema ni mhitimu wa Shahada ya Elimu ya Chuo kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1979 na pia ana Shahada ya pili ya usimamizi wa biashara akiwa amebobea zaidi upande wa masoko MBA aliyopata mwaka 1998.

Anasema baada ya kuhitimu shahada ya ualimu wa masomo ya sayansi mwaka 1979 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam aliajiriwa na Chuo cha Biashara Dar es Salaam CBE na kufanya kazi katika chuo hicho kwa miaka 31 ambapo alistaafu kwa mujibu wa sheria mwaka 2010.

Anasema, miaka 10 ya mwisho licha ya kuendelea na kazi ya ufundishaji alipewa dhamana ya kuwa Makamu Mkuu wa Chuo cha CBE Dodoma.

Bw.Kiputiputi anasema, akiwa katika nafasi hiyo alikikuta kikiwa na wanafunzi 183, lakini hadi anaondoka aliacha wanafunzi zaidi ya 4,000.

"Uwezo wa kampasi ile ni wanafunzi 200 tu, lakini tuliweza kufanya yote haya kutokana na stadi za kijasiriamali," anasema.

"Nilipokea kampasi ile ikiwa inaendesha programu moja tu ya stashada katika fani tatu tu yaani uhasibu, uendeshaji biashara na uboharia, lakini nimeiacha kampasi ikiwa inaendesha programe tatu, cheti, stashahada na shahada katika fani tano za uhasibu, uendeshaji biashara, masoko, uboharia na TETAMA yaani Teknolojia ya Taarifa na Mawasiliano," anasema.

Anasema kwa kuwa alifanya kazi kwa bidii, utiifu, ubunifu na uadilifu mkubwa, alipostaafu mwajiri wake alimpa zawadi nyingi, ikiwemo cheti cha utumishi uliotukuka hivyo anawahimiza watanzania kujituma zaidi katika kufanya kazi.

Bw.Kiputiputi anasema, hata hivyo akiwa bado yupo kazini wazo lake kubwa lilikuwa ni kuanzisha chuo chake binafsi ili aweze kuwasaidia watanzania kufaidi matunda ya elimu yake.

Anasema kuwa hata hivyo ndoto zake zilikamilika mwaka jana baada ya kufanikiwa  kuanzisha chuo chake binafsi  cha Biashara cha Aseki cha mkoani Dodoma, ambapo anaahidi kutoa wahitimu bora wanaoweza kujiajiri wenyewe au hata kuajiriwa kila pembe ya dunia.

Anasema  kozi zinazofundishwa kuwa ni pamoja na cheti cha uhasibu, cheti cha uendeshaji wa biashara na cheti cha manunuzi na ugavi.

Bw. Kiputiputi anasema kwa upande wa stashahada wanatoa katika uendeshaji wa biashara, stashahada katika uhasibu na stashahada ya manunuzi na ugavi.

Anaongeza kuwa mwanafunzi yeyote aliyemaliza kozi ya cheti NTA 4 inayoendana na fani hizo kutoka kwenye chuo chochote kilichosajiliwa na NACTE au aliyemaliza kidato cha sita na kupata angalau 'pass' moja au 'subsidiary' pass mbili anaweza kujiunga na kozi ya stashahada.


“Tunajitahidi chuo hiki kiwe cha kipekee hapa nchini kwa kutoa wahitimu bora katika menejimenti, ujasiriamali na ujuzi kupitia mafunzo, utafiti, utumishi wa umma na huduma za kijamii katika kanda hii na hata nje ya mipaka ifikapo mwaka 2020,” anasema.

Anasema chuo kitahakikisha kinawaandaa wanafunzi katika misingi bora ya uendeshaji bora wa biashara wenye mafanikio makubwa kwa kuwatumia wanataaluma waliobobea katika gani husika.

Bw. Kiputiputi anasema chuo kimepata usajili kamili kutoka NACTE na hiyo inamaanisha kwamba mtu yeyote atakayesoma kwenye chuo hicho na kufanikiwa kupata cheti kitatambuliwa rasmi nchini na duniani kote.

Anasema ili kufikia malengo hayo wamedhamiria kutoa elimu ya kiwango cha juu na kwa gharama ambazo watanzania wengi wataweza kuzimudu katika kozi za usimamizi wa biashara, uhasibu na fedha, masoko, ugavi na manunuzi, masomo ya  kompyuta na kozi zingine zinazoendana na masomo hayo.

Anafafanua kuwa, iwapo wahitimu watapata mafunzo ya kiwango cha hali ya juu itarahisisha kupata maendeleo endelevu, kwani nchi itakuwa na wataalamu wa kutosha katika fani mbalimbali kama zinazotolewa na chuo hicho.

Ili Aseki ifikie malengo hayo, anasema wamepanga kufanya kazi kwa ushirikiano kama timu moja, kwa kuzingatia weledi wa taaluma, uadilifu, ubunifu, huduma kwa wateja na uwajibikaji wa pamoja.

Bw. Kiputiputi anawaomba watanzania kuchangamkia fursa ya kuanzishwa kwa chuo hicho kwa kuwa elimu ni ufunguo wa maisha pia hazina pekee kwa urithi wa baadaye.

Anasema wazazi au walezi ambao wana vijana waliomaliza kidato cha nne na kukosa sifa ya kuendelea na masomo ya kidato cha tano wasikate tamaa ili mradi tu wawe wamefaulu na kupata angalau alama tatu za D, hivyo wanaweza kujiunga na chuo hicho.

“Akija hapa sisi licha ya kumpa stadi muhimu za maisha tutampa pia sifa za kuweza kujiunga na chuo kikuu chochote nchini ndani ya miaka mitatu, tutampa stadi za kuweza kujiajiri yeye mwenyewe au kuajiriwa baada miaka hiyo mitatu ya kwanza endapo atashindwa au ataamua kutoendelea na masomo zaidi,” anasema, Bw. Kiputiputi.

Anasisitiza kuwa, “Tumepania kuwa kituo kilichotukuka, yaani kituo bora kwa kutoa elimu, mafunzo na stadi katika nyanja za biashara, uendeshaji na ujasiliamali kupitia mafunzo, utafiti, huduma kwa umma na shughuli za nje ya chuo katika kanda hadi kufikia mwaka 2020.”

Bw. Kiputiputi anasema walimu wote wa chuo hicho wana angalau shahada ya kwanza na stashahada ya juu, hivyo wahitimu wa chuo hicho wanakuwa na viwango vya elimu inayokubalika katika fani mbalimbali nchini.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho, Dkt. Richard Mushi, anawahimiza watanzania kuwa na utamaduni wa kuanzisha miradi kwa ubia kwani ndiyo njia pekee ya kuanzisha miradi mkubwa.

Anasema wengi hawapendi kuanzisha miradi ya ubia kwa kutoaminiana, lakini aliwatoa hofu kuwa walioanzisha chuo cha ASEKI kwa ubia wamefanikiwa na chuo kinazidi kusonga mbele siku hadi siku.

“Waanzilishi wa chuo hiki wanastahili pongezi. Baraza linaona fahari kuongoza chuo hiki kwani licha ya kuanzishwa na watu binafsi, chuo kimetimiza masharti yote ya msingi ya kuandikishwa yaliyowekwa na Baraza la Vyuo vya Elimu ya Ufundi NACTE na ndiyo maana kimepata usajili kamili,” anasema Dkt. Mushi.

Anasema baraza la chuo limedhamiria kuona wakufunzi wa chuo hicho wanapata elimu ya ngazi ya juu zaidi ili waweze kumudu majukumu yao ipasavyo na wawe na viwango vinavyokubalika popote.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Mitihani, Bw. Balozi Job Lusinde anasema Baraza lake limepania kuhakikisha linasimamia viwango vya juu vya taalum ili wahitimu watakaotoka Aseki wawe watu wa kupigiwa mfano.
Posted: 12 Jun 2012 12:14 AM PDT
Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), Imani Lwinga (kushoto)akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) jana kuhusu tuzo za Chama Cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA) ambazo zitafanyika kesho. Katikati ni Mwenyekiti wa TASWA Juma Pinto na kulia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Amir Mhando.(Picha na Victor Mkumbo)
Posted: 11 Jun 2012 11:52 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

BENDI ya muziki wa dansi ya Extra Bongo 'Wazee wa kizigo', inatarajia kunogesha tuzo ya Mwanamichezo Bora 2011 wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) zitakazofanyika Alhamisi kwenye Ukumbi wa Diomond Jubilee, Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam jana na waandishi wa habari, Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) ambao ndiyo wadhamini wa tuzo hiyo, Imani Lwinga alisema bendi hiyo itakasindika utoaji wa tuzo hizo kwa kutua burudani ya aina yake.

Alisema ana uhakika bendi hiyo itakonga nyoyo za wanahabari pamoja na watu mbalimbali watakaokuwepo siku hiyo.

"Tunatangaza rasmi kwamba bendi ya Extra Bongo ambayo ipo chini ya Ali Choki, ndiyo itakayotoa burudani siku hiyo, hivyo tunaomba wanamichezo, waandishi wa habari na wageni watakaoalikwa kujitokeza kwa wingi kuja kushuhudia tukio hilo kubwa kwa wanamichezo," alisema Lwinga.

Naye Mwenyekiti wa chama hicho, Juma Pinto aliishukuru kampuni hiyo kwa kuzidi kutekeleza waliyoahidi na kwamba kuhusu mgeni rasmi, watatangaza siku chache zijazo.

Mbali na hilo, alisema wanajipanga kuhakikisha wanajenga uhusiano na waandishi wa habari za michezo kwa Ukanda wa Afrika Mashariki, ambapo kwa mwaka jana walipata mwaliko wa kwenda kushuhudia tuzo katika nchi za Rwanda na Burundi.

Alisema kwa mwaka huu walipanga pia kuzialika baadhi ya nchi za ukanda huo, lakini walifanya jitihada za kuwapa ikashindikana kutokana na kubanwa na ratiba zingine.

Mwanamichezo bora kwa mwaka huu, anatarajiwa kupewa dola za Marekani 8,000 (sh. milioni 12 za Tanzania).

Pia kutakuwa na zawadi ya sh. milioni moja kwa kila mshindi wa kila mchezo.
Posted: 11 Jun 2012 11:50 PM PDT


Na Elizabeth Mayemba

TAWI la Chelsea nchini, limeandaa sherehe za kuipongeza timu ya Chelsea ambayo imenyakua ubingwa wa Klabu Bingwa Ulaya na Kombe la FA.

Akizungumza Dar es Salaam jana Katibu Mkuu wa Chelsea Tawi la Dar es Salaam, Cliford Ndimbo alisema sherehe hizo zimepangwa kufanyika Msasani Beach, Dar es Salaam Juni 24, mwaka huu.

"Tumeamua kuanzisha tawi letu la Chelsea hapa nchini, hivyo tumeona ni vyema tuipongeze timu yetu kwa vikombe hivyo ambavyo wamevipata, tunaamini sherehe zetu zitafana sana," alisema Ndimbo.

Alisema pia katika kunogesha sherehe hizo wamewaalika na wapenzi wa Manchester United na wale wa Arsenal, ambapo kutakuwa na mechi kati ya wapenzi wa Chelsea ambao watacheza na timu zote mbili na zawadi mbalimbali zitatolewa kwa washindi.

Ndimbo alisema wapo katika harakati za kusajili rasmi tawi lao, ili lijulikane kote duniani na wanaamini watapata wanachama wa kutosha katika kuliendeleza tawi lao.

Alisema kiingilio katika sherehe hizo ni sh. 10,000 kwa kila mtu, pia watoto nao watapata fursa ya kuhudhuria ambapo mwisho wao itakuwa ni saa 12 jioni.