TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, August 16, 2014

marufuku shughuli zote za upigaji wa disko katika eneo la kiwengwa

 Waziri wa Habari Utamaduni, Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk (wakatikati) katika ziara ya kutembele mabaa na mahoteli ya kitalii, kutokana na wananchi kulalamikia vitendo vya upigwaji wa ngoma na vitendo viovu, (kulia) Mkuu wa Wilaya Kaskani (B) Unguja Khamis Jabir Makame na kushoto ni Sheha wa Kiwengwa Bw. Maulid Masudi Ame huko Kiwengwa.
 Waziri wa Habari Utamaduni, Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk na Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B, Khamis Jabir Makame wakipapa maelezo kutoka kwa mmiliki wa Baa ya Vision Pub Francis Vicoguga juu ya undeshaji wa kazi zake katika Baa hiyo.
 Waziri wa Habari Utamaduni, Utalii na Michezo Saidi Ali Mbarouk,akizungumza na wananchi na wamiliki wa mahoteli na baa katika kijiji cha Kiwengwa mara baada ya ziara yake ya kutembelea hoteli hizo.
 Mratibu wa Wanawake na Watoto Bi Mtumwa Rashid Khalifa ,mkaazi wa Kiwengwa akizungumzia kero wanazozipata kutokana upigwaji wa madisko katika mabaa kijijini hapo.(Picha na Jamila Abdalla – Maelezo Zanzibar).
Na Ali Issa Maelezo-Zanzibar. 15/8/2014.
Waziri wa Habari,Utamaduni , Utalii na Michezo Saidi Ali Mbaruok amepiga marufuku shughuli zote za upigaji wa disko katika eneo la kiwengwa mpaka pale Serikali ya wilaya itapo toa maelekezo maalumu ya upigaji wa disko hilo kwa utaratibu unao faa.
Agizo hilo amelitoa leo huko kiwengwa Mkoa wa kaskazini “A”wilaya ya kaskazini B Unguja katika Ofisi ya umoja wa maendeleo wa kijiji cha kiwengwa wakati alipokuwa akifanya mazungumzo na wamiliki wa mabaa mikahawa,na kumbi na starehe juu ya kukithiri wa upigaji wa magoma kucha.
Amesema amelazimika kuzifunga shughuli zote za upigaji wa madisko usiku kutokana na kutokua na  utaratibu mzuri wa upigaji ngoma hizo usiku  haliambayo inapelekea wageni wa kitalii na wenyeji kuchukia hali hiyo kwa kukosa usingizi na kusumbuliwa wagonjwa wenye shindikizo la damu.
Amsema hali hiyo haiwezekani kuona inaendelea katika hali kama hiyo kwani inapoteza muelekeo na mstakabali mwema wanchi na  raia kwaujumla.
 “Nimepokea messsege ya kwamba watalii wamefika kusema wanaondoka na kutafutiwa sehemu nyengine wakapunzike kutokana na zogo kuwa jingi la madisko,hili hiliwezekani liendelee”lisema Waziri.
Aidha alisema haiwezekani kuona utamaduni wa burudani unavurugwa kituambacho ni kosa kufanya hivyo na kwenda kinyume na taratibuzao selka zao.
“kuazia leo napiga marufuku mpaka sheha wa shehia hii aridhie hata kama kuna kibali ,kwani sheha yeye ndio anae jua hali za raia wake kuna wagonja,na wenyemaradhi ya kuhitaji kupumzika hatutaki kuona masuala yasio na utaratibu.”aliongeza Waziri.
 “mimi kazi yangu ni kuutangaza utalii nasio utalii uharibiwe ,tufahamu kua ulalii Zanzibar ndio uchumi unao tegemewa kwa sasa kwa hivyo tulinde,”aliongeza Waziri Said.
Hata hivyo waziri huyo alichukia vitendo vya uwasharati vilivyo tapakaa katika kijiji hicho na kujenga mabaa karibu na nyumba za ibada kitu ambacho aliagiza kwa mkuu wa wilaya kuyafanyia kazi.
Nao wazazi wa kiwengwa Othumani mnyanja na mtumwa Rashidi walisema kiwengwa hivisasa imepoteza muelekeo kwani watoto wao wanaishia katika madisko na kukosa masoma kitiambacho ni hatari kwao.
Aidha walisema kua watoto wao wakiwa na umri mdogo na kujishughulisha na masuala ya kimapezi jambo linalo wafanya nialama ya kupotea na kuacha mila za kislamu.
Wakitaja maeneo ya nayopigwa miziki na watoto wao kwenda ni pamoja na  maeneo yanayo pigwa madisko hayo ni pamoja na ,kigorofani, vishani wazalendo pub, Kamili View,Obama Baa na kigorofani eneo la mafarasi.
 Nae miliki wa ukumbi wa Disko wa PERUU B, Peruce Osward Buhoma  akiulizwa swali na waziri kwanini anafanya mazogo usiku alikiri kwa kusema hufanya hivyo kwaajili ya kuvuta wateja na kufanya ushindani kila mmoja kwajili ya  kusikika zaidi kuliko mweziwe.
Bibbi huyo na wezake walisema wanaweza kujirekebisha lakini pawe na utaratibu wa kupiga madisko kwa zamu na utaratubu mzuri utakao wekwa na uongozi.

ANGALIA PICHA BAA YAGEUZWA KANISA HUKO SINZA DAR

Baa iliyopo Sinza-Lion jijini Dar ambayo imegeuzwa kuwa kanisa.
WAKATI matukio mengi ya kushangaza na kushtukiza yakiendelea kutokea kila siku duniani, neno la Mungu nalo linazidi kushika kasi kufuatia baa moja iliyopo Sinza-Lion jijini Dar kugeuzwa kuwa kanisa.Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa baa hiyo maarufu iitwayo The Don, ukumbi wake ambao ulikuwa ukitumika kwa watu kupiga ulabu, hivi sasa unatumiwa na waumini wa kanisa linalojukana kama Impact International Christian Centre kupata mahubiri. Lakini cha kushangaza ilibainika kwamba katika maandishi makubwa yanayolinadi jina la baa hiyo, chini yake ndipo limewekwa bango linaloonyesha kanisa hilo, kitu ambacho kwa mtu mgeni, ni vigumu kuelewa mara moja.
Muonekano wa karibu wa kanisa hilo.

 “Siyo baa hiyo kaka, hilo ni kanisa siku hizi, tumeshangaa ghafla tu waumini wanakuja na mhubiri wao na wanaendelea na sala kama kawaida. Hatujui kama huyu mhubiri ndiye alikuwa mmiliki wa hii baa au imekuwaje,” alisema jirani mmoja wa eneo hilo, aliyekataa kutaja jina. 

Hata hivyo, juhudi za gazeti hili kuzungumza na uongozi wa baa au kanisa hilo ziligonga mwamba baada ya kuambiwa na majirani kuwa ni nadra kuwakuta mahali hapo hivyo jitihada zinaendelea. 
Katika miaka ya hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la kuibuka kwa makanisa ya madhehebu mbalimbali, ambayo kila moja huwa na watumishi wao wanaopewa majina kama Mchungaji, Nabii, Askofu na kadhalika.

HOJA MPYA ZA KAMATI ZALICHANGANYA BUNGE MAALUMU LA KATIBA MPYA DODOMA.

 
Dodoma. Mapendekezo mapya yanayopelekwa kwenye Kamati za Bunge Maalumu kwa ajili ya kurekebisha baadhi ya Ibara za Rasimu ya Katiba, yamezua mivutano mikali kiasi cha baadhi ya sura kuwekwa kiporo au kurukwa na kamati husika.

Habari zilizolifikia gazeti hili zinasema mapendekezo hayo ni yale yanayozigusa taasisi kubwa za nchi, zikiwamo Bunge la Jamhuri ya Muungano na Mahakama, pamoja na nafasi za Makamu wa Rais.

Katika baadhi ya kamati yamepelekwa mapendekezo ambayo yanataka Bunge liwe na sehemu tatu ili kutoa fursa kwa mambo ya Tanzania Bara kujadiliwa bila wabunge kutoka Zanzibar kuwapo.

“Mapendekezo yaliyopo ni kwamba wanataka Bunge liwe na sehemu tatu ambazo ni Bunge la Muungano kwa masuala ya muungano na humohumo linakuwa na sehemu mbili ambazo ni wabunge wa Zanzibar kwa ajili ya masuala ya Wazanzibari na sehemu ya Tanganyika kwa ajili ya mambo ya bara,” kilisema chanzo chetu kutoka katika kamati moja ya Bunge hilo.

Hata hivyo, habari zinasema baadhi ya wajumbe wa kamati walikosoa pendekezo hilo kwa maelezo kwamba linashabihiana na muundo wa muungano wa serikali tatu ambao ulipendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba lakini ukapingwa na baadhi ya wajumbe wakiongozwa na walio wanachama wa CCM.

Jana Mwenyekiti wa Kamati Namba 8, Job Ndugai aliwaambia waandishi wa habari kwamba kamati yake imeshindwa kuafikiana kuhusu muundo wa Bunge la Muungano hivyo kulazimika kuliacha suala hilo ili kulifanyia uchunguzi kwanza.

“Mbali na sura ya 5 inayozungumzia uraia pacha ambayo ilitusumbua, lakini pia suala la Muundo wa Bunge la Muungano na Mahakama ya Muungano vilikuwa tatizo katika kamati yangu,” alisema Ndugai.

Licha ya kwamba Ndugai hakuzungumzia suala hilo kwa undani, lakini taarifa zilizolifikia gazeti hili zinasema muundo wa kuwa na sehemu tatu katika Bunge moja ndio uliozua mtafaruku kiasi cha kamati hiyo kuliahirisha.

Katika kamati namba 5, sura ya 10 inayozungumzia suala la Bunge na Mahakama imerukwa. Mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo alisema: “Tumeamua kuendelea na mambo mengine kwanza maana hilo limeonekana kuwa ni gumu kwa sasa.”

Habari zaidi zinasema katika kamati hiyo namba tano, mapendekezo ya kuwapo kwa makamu wa rais watatu yalizua mjadala mkali kiasi cha kusababisha kuwapo kwa wajumbe walioamua kuandaa maoni ya wachache.

“Wamekuja na mapendekezo kwamba awepo Makamu wa Kwanza wa Rais ambaye atakuwa mgombea mwenza, Makamu wa Pili wa Rais ambaye atakuwa Rais wa Zanzibar na Makamu wa Tatu wa Rais ambaye ni Waziri Mkuu,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya kamati hiyo na kuongeza:

“Lakini wapo waliokataa kama watano au sita hivi na wameamua kwamba wataandika maoni ya wachache kwa mujibu wa Kanuni ya 32 (10)”.

Hoja hiyo inafanana kabisa na ile iliyowasilishwa katika Kamati namba 10 na kusababisha mgawanyiko uliozalisha kuwapo kwa maoni ya wachache ambayo kwa mujibu wa taarifa zilizolifikia gazeti hili yataandaliwa na Mbunge wa Mpanda Mjini (Chadema), Said Arfi na mwenzake kutoka kundi la 201 Adil Mohamed Ali.

Katika Kamati Namba 11, habari zinasema suala hilo pia lilizua mvutano baina ya wajumbe wanaounga mkono mfumo wa Serikali mbili na wale wanaotaka Serikali tatu na kwamba aliyeokoa jahazi ni Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman ambaye alitoa mapendekezo kuhusu mifumo yote miwili.

“Katika kamati yetu wanasema eti tayari mfumo wa Serikali mbili umepitishwa maana ndiyo unaungwa mkono na wengi, lakini wengine wamekataa, kwa hiyo ndiyo maana masuala kama haya yanatupa shida kwelikweli,” kilisema chanzo chetu.

Hata hivyo, kwa mujibu wa habari hizo, kamati hiyo namba 11 iliunda kamati ndogo ya watu watatu akiwamo Naibu Waziri wa Kilimo, Godfrey Zambi ili kupitia mapendekezo ya Othman kabla ya kuyarejesha kwenye kamati nzima kwa ajili ya kufanya uamuzi.

Kaimu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk Christina Mnzava alipotafutwa jana kutoa ufafanuzi wa suala hilo alisema asingeweza kuzungumza kwani alikuwa kwenye kikao. Othman kwa upande wake naye alisema hakuwa katika nafasi ya kuzungumzia suala hilo kwani lipo kwenye mamlaka ya kamati.

Habari zaidi zinasema pia kumekuwa na mvutano pale kunapokuwa na mapendekezo ya kufutwa kwa maneno Tanganyika na Shirikisho, kwani baadhi ya wajumbe wamekuwa wakitaka yaendelee kuwapo kama yalivyopendekezwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, hadi pale Bunge zima litakapofanya uamuzi.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati Namba 10, Salmin Awadh Salmin, alikiri kwamba katika maeneo mengi ambako kulikuwa na maneno hayo wameyaondoa kwa kuzingatia kuwa ndiyo yalikuwa makubaliano ya wengi.

“Ingawa bado tuna watu ambao ni sehemu ya Ukawa, lakini ni wachache na pamoja na hoja zao za msingi, lakini zinaonekana kumezwa na wajumbe walio wengi ambao ndio wanaounga mkono Serikali mbili,” alisema.

Akizungumzia changamoto zilizowapata ndani ya kamati yake, alitaja kuwa ni suala la kutenganisha madaraka ya mawaziri na wabunge.

Kwa maelezo ya kiongozi huyo, jambo hilo lilitoa mvutano mkali ndani ya kamati yake na kuwa litaamuliwa Jumatatu ingawa wao kwenye uraia walipitisha uraia pacha.

Frederick Sumaye
Waziri Mkuu mstaafu Frederick Sumaye ameshauri kusimamishwa kwa Mchakato wa Katiba kutokana na mvutano kati ya wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi na wale wa kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) akionya kuwa bila ya maridhiano hakuna katiba bora.

Akifungua Kongamano la Kuombea Katiba Mpya na Uchaguzi na Amani nchini lililoandaliwa na Free Pentecostal Church in Tanzania (FPCT) na kufanyika mkoani Kigoma, Sumaye amesema kuwa Bunge ni nyumba ya kujenga hoja na siyo nyumba ya mapambano wala ubabe.

“Pamoja na umuhimu huu wa kupata Katiba Mpya, Watanzania tungependa katiba itakayopatikana kwa maelewano na maridhiano ya pande zote husika. Bunge ni nyumba ya kujenga hoja na siyo nyumba ya mapambano wala ubabe. Kinachotakiwa wabunge wote washiriki na hatima ya yote ni wengi wape na wachache wasikilizwe,” alisema Sumaye na kuongeza:

“Kama inaonekana dhahiri kuwa hatutapata katiba nzuri kwa wakati uliopo, ni busara mchakato huu ukasimama, Watanzania tukajipa muda zaidi tukayatafakari haya ili tuje tupate katiba mwafaka kwa muda mwafaka. Itakuwa ni ushindi batili kama tutang’ang’ania kutengeneza katiba ambayo siyo ya manufaa kwa Watanzania wote.

Sumaye ambaye ni mmoja wa makada wa CCM waliojipambanua kutaka kuwania urais mwakani, alisema mchakato huo umetumia fedha nyingi za walipakodi ambazo zingetumika katika kuboresha huduma mbalimbali za jamii kama vile afya, elimu, maji na miundombinu.

Alisema licha ya sura nyingi katika Rasimu ya Katiba, sura zinazozungumzia Muungano ndizo zimekuwa ngumu licha ya kila upande kutoonyesha nia ya kuuvunja.

Hata hivyo, Sumaye alipendekeza muundo wa serikali mbili, kwani kuongezwa kwa idadi ya Serikali hakutakuwa suluhisho.

Huku akionyesha kutoamini kama mchakato huo kuwa suluhisho la mwisho la maendeleo ya Watanzania, Sumaye alionya kuhusu ulafi wa madaraka:

“Kama tumefika hapa kwa sababu kuna matatizo ya madaraka au utawala kwa vyovyote jawabu lake siyo Serikali tatu kwa sababu kufanya hivyo kutafanya tatizo liwe kubwa zaidi. Kama tumefika hapa kwa sababu ya mivutano ya rasilimali, basi kuwa na mfumo wa Serikali tatu kutafanya hali iwe ngumu zaidi,” alisema na kuongeza:

“Kwa maoni yangu kama kuna mvutano wowote kati ya Serikali ya Jamhuri na Serikali ya Zanzibar katika muundo wa Serikali mbili, na tukaanzisha Serikali ya Tanganyika kabla hatujatatua mivutano iliyopo, hiyo mivutano itaendelea kuwapo na tutazalisha mivutano mingine mipya.”MWANANCHI

HOFU YA EBOLA DAR, MGENI KUTOKA BENIN ALAZWA TEMEKE

  Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au  namba +255767869133.

Watu wakikatiza kwenye lango la kuingilia katika Hospital ya Temeke, sehemu ambayo anayedaiwa kuwa mgonjwa wa Ebola amelazwa  
 Hofu ya ugonjwa wa ebola imeingia jijini Dar es Salam baada ya msichana anayedhaniwa kuwa na ugonjwa huo kutua nchini akitokea Benin, Afrika Magharibi na kulazwa katika Hospitali ya Temeke.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Amani Malima alithibitisha kuwapo msichana huyo mwenye umri wa miaka 14 aliyeingia nchini jana kuonekana akiwa na dalili hizo.
“Huko alikotoka alihisiwa kuwa na dalili hizo, alipofika hapa madaktari walipomhoji alisema ana maumivu makali ya viungo, miguu na mikono,” alisema.
Dk Malima alisema baada ya kupata maelezo hayo, walichukua vipimo vyote vya damu na majibu yake yatatoka leo kujua kama ana ugonjwa huo au la.
“Tumegundua kwamba ana malaria lakini vipimo vya ebola majibu ni kesho (leo), hivyo tunaangalia namna ya kumtibu na kama atakuwa hana ugonjwa huo tutamruhusu,” alisema Dk Malima.
 Chanzo;Mwananchi

RAIS KIKWETE AWAAPISHA MAJAJI WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA WAPYA 20 IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete,  Makamu wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilali, Waziri Mkuu Mhe Mizengo Pinda,  Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha-Rose Migiro, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu,  Katibu Mkuu Kiongozi  Balozi Ombeni Sefue, Mwanasheria Mkuu Jaji  Frederick Werema, Mtendaji Mkuu wa Mahakama Mhe Hussein kattanga  katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama kuu ya Tanzania baada ya kuapishwa leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na  Majaji wa Mahakama ya Rufaa Tanzania na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wapya
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na  Majaji wa Mahakama ya Kuu Tanzania na Majaji  wapya
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akiwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu pamoja na  majaji wapya 
  Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu na Jaji Kiongozi   Shaban Ally Lila wakiwa na Majaji wapya 
 Rais Kikwete na Waziri wa Sheria na Katiba Dkt Asha Rose Migiro wakiwa wa wanachama wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) na Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania wanawake wapya
  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe Mohamed Chande Othman, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe Omar Othman Makungu na Jaji Kiongozi   Shaban Ally Lila wakiwa katika pic ha ya jumla na Majaji wapya na wa zamani

[BREAKING NEWS] R.I.P Justin Timberlake Died Early Today in a Horrific Car Accident in L.A!

His driver was drunk did'nt see stalled truck ramming on it! How sad!
sauls.infieldvideo.pw

KAMATI TANO BUNGE LA KATIBA ZAKWAMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au  namba +255767869133.
Mwenyekiti wa kamati namba tano, Steven Wasira
 
Kamati tano kati ya saba za Bunge Maalumu la Katiba zimejikuta katika njiapanda ya kushindwa kufanya maamuzi kutokana na kukosekana kwa akidi kwenye vikao vya kamati hizo.
Kwa mujibu wa mjumbe mmojawapo wa Bunge hilo, Teddy Ladislaus, kukosekana kwa akidi katika kamati nyingi kumezifanya zishindwe kufanya maamuzi  ikiwamo upigaji kura kwenye ibara mbalimbali.

Ladislaus, ambaye ni kutoka kundi la 201 akiwakilisha wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, alisema mjadala ndani ya kamati hizo umekuwa mgumu na kamati zinashindwa kumaliza kazi kwa muda uliopangwa kutokana na kukosekana kwa akidi ya kuwezesha kufanya maamuzi kutokana na wajumbe kutohudhuria kwa sababu mbalimbali.

Hadi sasa kati ya kamati saba zilizotoa maendeleo ya mjadala wa rasimu ya katiba ni kamati mbili pekee zilizopigwa kura katika kile kilichojadiliwa.

Mwenyekiti wa Kamati namba moja, Ummy Mwalimu, juzi aliahidi kuwa upigaji kura ungefanyika siku hiyo baada ya kujadili sura nne za rasimu hiyo, lakini hadi sasa zoezi hilo halijafanyika.

Aidha, Mwenyekiti wa kamati namba tano, Steven Wasira, akizungumza na NIPASHE alisema upigaji kura haujafanyika kwenye kamati yake licha ya kujadili sura ya pili, tatu, nne na tano.

Kamati zilizotoa mrejesho wa majadiliano yao hadi sasa ni namba 9, 10, 11, 12, ambazo hazijaeleza kama wamepiga kura, huku kamati namba tatu wakipiga kura na kuwa na maoni ya wengi na wachache.

ATAKA BUNGE LIAHIRISHWE
Katika hatua nyingine, Ladislaus alisema viongozi wakuu wanapaswa kutambua kuwa katiba bora itapatikana kwa maridhiano na siyo kwa ushindani na ubabe wa kisiasa.

Aidha, alisema vilevile kuwa ni vyema bunge hilo likaahirishwa kwa kuwa hivi sasa, kamati zinajadili sura za rasimu ya katiba kwa muundo wa "bora liende" na hakuna matumaini ya kupata katiba mpya yenye misingi ya umoja wa kitaifa.

Ladislaus aliwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma jana kuwa ni vyema Rais akaona umuhimu wa kusitisha shughuli za Bunge hilo kwa sasa na kutafuta maridhiano ya pande zinazovutana.

Mjumbe huyo, ambaye katika mkutano huo alikuwa ameambatana na Rais Mstaafu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Hemed Mngwali na Mwanafunzi wa Chuo cha Mipango Dodoma (ARDP), Elisante Mfinanga, alisema tamko analolitoa ni kwa niaba ya wanafunzi wa vyuo vikuu anaowawakilisha ndani ya bunge la katiba.

Alisema kuwa hadi sasa, Bunge hilo lipo katika mkwamo mkubwa kwani licha ya kamati kuendelea na uchambuzi wa rasimu, ukweli ni kwamba (wajumbe) wanapata ugumu kufikia akidi ya kuwezesha vikao kufanya maamuzi na kukidhi matakwa ya sheria ya mabadiliko ya katiba.

"Kamati za Bunge Maalum zinaendelea na uchambuzi wa Rasimu ya Katiba, lakini ni kweli kwamba uchambuzi huu wa sasa hauwezi kutuletea katiba bora inayokusudiwa na Rais Jakaya Kikwete... muda wa siku 16 kujadili sura 15 zenye ibara 240 ikiwa ni wastani wa ibara 16 kwa siku moja kazi haitafanyika kwa weledi," alisema.

Mjumbe huyo alitoa maoni yaliyoungwa na wenzake, akisema kuwa ni vyema Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania litakaloketi Novemba mwaka huu kufanya marekebisho kwenye katiba ya sasa ya mwaka 1977 kwa kuweka vipengele vya kuwapo kwa tume huru ya uchaguzi, haki ya kuhoji matokeo ya urais na kuwapo kwa mgombea binafsi.

Aliongeza kuwa, kuendelea kuharakisha mchakato wa kutengeneza Katiba kwa namna inayoendelea sasa hakutaleta katiba bora kwani haitakuwa na ridhaa ya makundi mengi kwenye jamii.

UGUMU KWENYE KAMATI
Ladislaus alibainisha kuwa kwa kadri anavyoona, hivi sasa kamati za Bunge Maalum la Katiba zimekuwa zikifanya kazi alimradi tu kufika mwisho na ionekane kwamba kazi ya kupata katiba mpya imefanyika, jambo analoamini kuwa ni dhambi kubwa kwani kufanya hivyo ni kuhadaa mamilioni ya Watanzania kuwa watapatiwa katiba bora wakati hilo halitawezekana bila pande zote zinazovutana kufikia maridhiano.

"Kwa kuwa Katiba ni moyo wa nchi, tusifanye kazi kwa kulipua alimradi tuwapendeze wachache walioweka maslahi binafsi mbele.Tukifanya hivyo tutakuwa tunaliweka taifa rehani ... na baadaye taifa litaachwa liharibike mikononi mwetu sisi vijana," alisema. Akielezea kuhusu haja ya kuwapo kwa mazungumzo baina ya CCM na Ukawa, Ladislaus alisema:

"Mazunguzo siku zote ni 'give and take' yaani kulegeza msimamo katika baadhi ya hoja badala ya kila upande kushupaa kwa kile unachokiamini, tukiwa na nia ya dhati ya kuzungumza, tukashauriana, tukaridhiana na kukubaliana jinsi ya kutekeleza yale tulioafikiana, basi Taifa litapata Katiba bora hivyo kuondoka katika mkwamo wa sasa na kuondoa mgawanyiko," alisema.

Ukawa huundwa na wajumbe kutoka vyama vikuu vya upinzani nchini vya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Chama cha Wananchi (CUF) na NCCR-Mageuzi.

Wajumbe wa Ukawa walisusia vikao vya Bunge Maalum la Katiba tangu April 16, 2014, ikiwa zimebaki siku 10 Bunge hilo kuhairishwa na wameweka msimamo wa kutorejea tena Bungeni hadi litakapojikita kwenye kujadili Rasimu ya wananchi iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Imeandikwa na Salome Kitomari, Editha Majura na Godfrey Mushi, Dodoma
CHANZO: NIPASHE

Early Favorites for 2014's Fighter of the Year Early Favorites for 2014's Fighter of the Year Ble

Early Favorites for 2014's Fighter of the Year           Early Favorites for  2014's Fighter of the Year
Ble
Broner Promising to KO Taylor Broner Promising to KO Taylor
BoxingNews24.com
Porter Must Impress to Stay in Floyd Sweepstakes Porter Must Impress to Stay in Floyd Sweepstakes
BleacherReport.com
Goossen Files $10M Lawsuit Against Ward Goossen Files $10M Lawsuit Against Ward
BoxingScene.com
Brook Ready to Take Advantage of Spotlight Brook Ready to Take Advantage of Spotlight
BleacherReport.com
Watch: Porter Trains Blindfolded for Brook Fight Watch: Porter Trains Blindfolded for Brook Fight
BadLeftHook.com
Santa Cruz Headlines Mayweather Undercard Santa Cruz Headlines Mayweather Undercard
FightNews.com
Instagram: Shawn Porter Eats Special K for Breakfast Instagram: Shawn Porter Eats Special K for Breakfast
Instagram.com
Boxer Punches Ball 100 Yards Away Boxer Punches Ball 100 Yards Away
BleacherReport.com
Porter: I Know I Can Beat Kell Brook Porter: I Know I Can Beat Kell Brook
BoxingNews24.com
Gonzalez, Arce Close In on Historic Deal Gonzalez, Arce Close In on Historic Deal
ESPN.com
Report: Golovkin vs. Rubio Set for October Bout Report: Golovkin vs. Rubio Set for October Bout
TheSweetScience.com
Is Porter vs. Thurman the Next Big Mega Fight? Is Porter vs. Thurman the Next Big Mega Fight?
BoxingNews24.com
Boxing Stars Failing to Make Most of 2014 Boxing Stars Failing to Make Most of 2014
BleacherReport.com

Boxing Visit BleacherReport.com for more Coverage »