Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au namba +255767869133.
Watu wakikatiza kwenye lango la kuingilia katika Hospital ya Temeke, sehemu ambayo anayedaiwa kuwa mgonjwa wa Ebola amelazwa
Hofu ya ugonjwa wa ebola imeingia jijini Dar es Salam baada ya
msichana anayedhaniwa kuwa na ugonjwa huo kutua nchini akitokea Benin,
Afrika Magharibi na kulazwa katika Hospitali ya Temeke.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Amani Malima
alithibitisha kuwapo msichana huyo mwenye umri wa miaka 14 aliyeingia
nchini jana kuonekana akiwa na dalili hizo.
“Huko alikotoka alihisiwa kuwa na dalili hizo,
alipofika hapa madaktari walipomhoji alisema ana maumivu makali ya
viungo, miguu na mikono,” alisema.
Dk Malima alisema baada ya kupata maelezo hayo,
walichukua vipimo vyote vya damu na majibu yake yatatoka leo kujua kama
ana ugonjwa huo au la.
“Tumegundua kwamba ana malaria lakini vipimo vya
ebola majibu ni kesho (leo), hivyo tunaangalia namna ya kumtibu na kama
atakuwa hana ugonjwa huo tutamruhusu,” alisema Dk Malima.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
No comments:
Post a Comment