TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, June 16, 2016
Watanzania watakiwa kutumia fursa za soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO, Tarehe 16.06.2016
WAFANYABIASHARA wa Tanzania wametakiwa kutumia fursa za biashara zinazopatikana katika soko la nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuuza bidhaa zao ndani ya Jumuiya hiyo.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
“Wafanyabiashara wanatakiwa kuchangamkia fursa ya biashara katika soko la pamoja kwa kuwa ni haki yao na ni utekelezaji wa malengo ya Mkataba wa uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kifungu cha tano ambapo ilianzishwa itifaki ya umoja wa forodha ” ,alisema Bi. Mindi
Wafanyabiashara hao pamoja na wasafirishaji wanaotaka kufanya biashara katika soko la Jumuiya hiyo watatakiwa kuonesha cheti cha uasilia wa bidhaa wakati wakiingia nchi wananchama wa Jumuiya hasa kwa wafanyabiashara wadogo wenye bidhaa zisizozidi dola za kimarekani 2000, ambapo hawalazimiki kuwa na wakala wa forodha.
CAF YAPITISHA MAJINA YA KESSY NA WENZAKE, SASA KUCHEZESHA SHIRIKISJ
kipa Benno David Kakolanya, Hassan Hamisi Ramadhan ‘Kessy’, Vincent Andrew Chikupe na Juma Hassan Mahadhi kucheza Kombe la Shirikisho.
Wachezaji hao wameongezwa kwenye kikosi hicho baada ya kusajiliwa Ikiwa ni lengo lao la kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho ambacho kimeingia kwenye hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho na wanatarajiwa kuanza kukipiga kwenye mechi ya kwanza ya kundi A dhidi ya Mo Bejala itakayopigwa nchini Afrika Kusini.
Yanga kwa sasa wameweka kambi nchini Uturuki pamoja na nyota hao wanne wakiwa tayari wameshaingia kwenye mipango ya Kocha Mkuu Mholanzi Hans Van De Pluijm akisaidiwa na Juma Mwambusi.
MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAKULIMA (AFP) AZUNGUMZA NA WANDISHI WA HABARI JUU YA HUJUMA ALIYOFANYIWA

Baadhi ya wandishi wa Habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima (AFP) Saidi Sudi hayo pichani katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo Mjini Zanzibar. Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.
Na Mwandishi wetu –Habari Maelezo Zanzibar Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima ( A.F.P ) Said Suod Said amemshauri Msajili ya vyama vya siasa nchini kwenda kisiwani Pemba kufuatilia hujuma zinazoendea kufanyika kisiwani huko ili kuweza kuzipatia ufumbuzi . Hayo ameyasema huko katika ukumbi wa Sanaa Rahaleo wakati akizungumza na Waandishi wa habari baada ya kufanyiwa hujuma katika shamba lakeliliopo Mgelema Wilaya ya Chakechake. Alisema kwamba kuna baadhi ya watu wanafanya vitendo vya hujuma vinanyopelekea vinaashiria uvunjifu wa amani na wananchi kuogopa kuendelea kutoa huduma kisiwani humo. Alieleza kuwa baadhi ya hujuma hizo ni pamoja na kuchomewa moto kwa baadhi ya nyumba na kuharibu mashamba ya wananchi kukatiwa vipando ikiwemo mikarafuu, minazi na mashina ya muhogo hali ambayo inarejesha nyuma maendeleo na kutokukuwa uchumi wa nchi.“Vitendo hivyo vimekithiri watu kisiwani Pemba wamezidi siasa wanaifanya ushindani, watu wanashindana kwa kura sasa wao wanafanya hujuma mimi shamba langu wamenikatia mikarafuu 151 ikiwemo 14 tayari kuzaa, minazi 16 pamoja na mashina 250 yenye thamani ya sh. Milioni 200 inaniuma sana.” Alieleza Mwenyekiti huo. Alifahamisha kuwa siasa sio ugomvi kilichobakia ni kuleta maendelo ya nchi kwani uchaguzi umemalizika serikali tayari ipo madarakani hivyo wananchi wanatakiwa kushirikiana kwa pamoja ili kuweza kudumisha amani na kukuza uchumi wa nchi. Aidha amemuomba Rais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuzidisha ulinzi kisiwani Pemba kutokana na hujuma zinaendela kufanyika siku hadi siku kisiwani humo ili amani isije ikatoweka nchini. Amewataka Wazanzibar kuendelea kuwa wastahamilivu kutokana na hujuma zinaendelea kufanywa kisiwani huko kwani nchi inafuata sheria hivyo serikali inawajali wananchi wake na waendelee kudumisha amani.
Mkurugenzi Kinondoni amewataka walipa kodi na ushuru kupewa stakabadhi za kielektroniki
Na Jacquiline Mrisho - MAELEZOMkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni amewataka walipa kodi na ushuru katika Manispaa hiyo kudai stakabadhi za kielektroniki baada ya kufanya malipo ili kuziba mianya ya upotevu wa mapato.
Rai hiyo imetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Aron Kagurumjuli alipokuwa akiongea na mwandishi wa habari hii juu ya njia wanazozitumia katika ukusanyaji wa ushuru wa Manispaa hiyo.
“Napenda kuwasisitiza wananchi kuwa unapofanya malipo yoyote ya Manispaa lazima uhakikishe unapewa stakabadhi ya kielekroniki na iwapo hutopewa, unaruhusiwa kutoa taarifa kwa kupiga simu au kutuma ujumbe mfupi kwenda 0767643460 na utapatiwa maelekezo ya nini cha kufanya”,alisema Kagurumjuli.
Kagurumjuli ameongeza kuwa Ofisa yeyote atakayekaidi kutoa stakabadhi hizo atachukuliwa hatua kali za kisheria kwani kukwepa kulipa mapato ni kurudisha nyuma uchumi wa nchi.
Subscribe to:
Posts (Atom)






