TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, June 27, 2016

MCHEZAJI BORA WA UMMISETA MUSA SAID KUONDOKA JUMATANO JUNI 28, 2016 KWENDA NCHINI UFARANSA.


 Na Devotha Kihwelo.  MCHEZAJI bora wa mashindano ya UMMISETA yaliyofanyika mwaka jana mkoani Mwanza, Said Musa Jumatano ya Juni 28, 2016 kuelekea Ufaransa katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca - Cola ambayo imeandaliwa na kampuni ya kinywaji cha Coca - Cola . Akizungumza jijini Dar es Salaam katibu mkuu wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Mohamed Kiganja alisema udhamini wa kampuni ya Coca - Cola imetambua umuhimu wa michezo hivyo kukubali kudhamini michezo kupitia shule za sekondari ili kukuza vipaji vya wanamichezo chipukizi ambao wanamalengo makubwa katika kuitumikia nchini yao kupitia michezo. “Kwetu sisi imekuwa faraja kwa kuibua kipaji kichanga ambacho kitakuwa ni mfano wa kuigwa kama ilivyo kwa Samatta ambaye amekuwa kioo kwa jamii ya wanamichezo na hivyo kuomba makampuni mengine kujitokeza kwa ajili ya kusaidiana na Coca - Cola”, alisema. Kiganja alimtaka Musa kuzingatia nidhamu kipindi chote atakachokuwepo kwenye kambi ili kujijengea heshima katika kukuza kipaji chake kwa kipindi chote ambacho atakuwa chini ya walimu wageni ambao hajawahi kukutana nao na hiyo italeta heshima nchini. Kwa upande wa Meneja msaidizi wa chapa ya Coca – Cola, Mariam Sezinga, alisema wamefurahi kupata nafasi ya kudhamini mashindano hayo kwa kuwa ndiyo mara yao ya kwanza na imefanikiwa kufikia malengo ya kupata mchezaji ambaye atakuwa muwakilishi wa Tanzania katika kambi ya Kimataifa ya Copa Coca - Cola iliyopo jijini Paris nchini Ufaransa. Alisema Musa ataondoka kwa kupitia Nairobi kwa kuwa kozi inaanza kesho na kumalizika Julai 4, hivyo aliwataka wanafunzi wengine kujituma ili kufikia malengo kama aliyofikia Mussa. “Sisi kama kampuni imekuwa ni faraja kwani tutakuwa tumeitangaza nchini kwa kupitia Mussa na hii itakuwa ni muendelezo katika michezo inayoendelea,”alisema. Mussa ni mwanafunzi wa shule ya sekondari Kibasila ambaye alizaliwa Agosti 11, 2000 huku akiwa ni mchezaji tegemeo katika timu ya shule na Mkoa wa Temeke ambapo walitumia jina hilo kwa kupitia michezo

TASAF YAADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA.



Mfuko huo wa Maendeleo ya Jamii unaotekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini , unatoa huduma kwa Zaidi ya Kaya Milioni Moja na Lakini Moja nchini kote jukumu iliyopewa na serikali katika jitihada zake za kupambana na Umaskini nchini..
Imearifiwa katika kikao hicho kuwa mafanikio makubwa yameanza kujitokeza kwa walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambapo wengi wao wameanza kujiwekea misingi ya kupunguza umaskini kwa kuwa na uwezo wa kusomesha watoto,kupata huduma za afya,kuwa na uhakika wa lishe na kuongeza uchumi wao.
Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini pia umeanza kusisimua hamasa ya walengwa wa Mpango huo kuboresha maisha yao kwa kiwango cha kuanza kuboresha makazi yao kwa kujinunulia mabati na kuezeka nyumba,kuanzisha miradi midogo midogo kama ufugaji wa kuku wa kienyeji,mbuzi nahata nguruwe.

TAASISI YA NITETEE YAIOMBA SERIKALI KUTOA RUZUKU KWA TAASISI ZINAZOFANYA KAZI VIZURI


Twanga Pepeta kufanya shoo kabambe Sikukuu ya Eid Mosi Giraffe Hotel

ZOEZI LA UHAKIKI WA VYAMA VYA SIASA LAANZA LEO

MPALULEBLOGS:
Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Uhakiki wa vyama vya Siasa , Bw. Sisty Nyahoza (kulia) akihakiki daftari lenye orodha ya wanachama wa Chama cha National League for Democratic (NLD) wakati wa zoezi la kuhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa chama hicho Oscar Emmanuel Makaidi na Katibu Mkuu wa NLD Tozzy Ephraim Matwanga.
Bw. Ibrahim Mkwawa, Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Uperembe “Monitoring” (katikati) akikagua nyaraka mbalimbali za Chama cha Sauti ya Umma (SAU) wakati wa uhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa lililoanza leo Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mhasibu Bi. Severa Assey kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.

WAZIRI NAPE NNAUYE AZINDUA STUDIO YA REDIO YA JAMII KATIKA CHUO KIKUU HURIA TANZANIA OUT), JIJINI DAR ES SALAAM LEO


Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akikata utepe wakati wa Uzinduzi wa Redio ya Jamii ya ‘’Community Media Network of Tanzania (COMNET)’’ 27 Juni, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kushoto) akijadiliana jambo na Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa toka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Bi. Zulmira Rodrigues wakati wa Uzinduzi wa ‘’Community Media Network of Tanzania (COMNET)’’ 27 Juni, 2016 Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (kulia) akiwa ndani ya Studio ya ‘’Community Media Network of Tanzania (COMNET)’’ akijibu baadhi ya maswali toka kwa Waandishi wa Habari mara baada ya kuizindua rasmi 27 Juni, 2016 Jijini Dar es Salaam.

MKUU WA MKOA MJINI MAGHARIBI AKANUSHA TAARIFA YA WANYAMA KUCHINJWA MAISARA-ZANZIBAR




Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohammed Mahamoud amekanusha uvumi wa baadhi ya wananchi kuwa wanyama walioshindwa kugombolewa ndani ya muda uliowekwa, kuchinjwa na kuuzwa kwa beinafuu Maisara.

Mkuu huyo alisema taarifa hizo hazina ukweli ukweli ni kwamba wanyama hao wataendelea kutunzwa na Serikali kwa kipindi kinachokubalika na kwa wale ambao watakaoshindwa kuwakombowa wanyama wao watataifishwa na kuwa mali ya Serikali.

Ameyaeleza hayo wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Afisini kwake Vuga Mjini Zanzibari wakati akitowa taarifa maalumu kwa wananchi wa Mkoa Mjini Magharibi kuhusu Uthibiti wa wanyama kwenye maeneo yasio ruhusiwa.

Hata hivyo amewataka wafugaji kutokubali kutowa fedha kwa wahusika na ukamataji wa wanyama bila ya kupitia taasisi husika (Manispaa), kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria na kuwataka wananchi kutoa taarifa kwa Masheha, Polisi au Manisipaa iwapo kutajitokeza hali hio ili kuzuia vitendo vya rushwa.

Aidha ameeleza katika utekelezaji wa zoezihilo kumejitokeza changamoto zikiwemo malalamiko kwa baadhi ya waumini wa dini ambao wanyama wao wanawatumia kwa ajili ya shughuli za ibada wamekamatwa.

Vilevile kumejitokeza kwa baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaohusisha zoezi hilo na mambo ya kisiasa kwa kuwashajihisha wananchi kuvunja sheria kwa kupingana na utekelezaji wa zoezi hilo.


Alisisitiza kuwa zoezi hilo ni endelevu na Serikali ya Mkoa wa Mjini Magharibi haitokuwa na muhali katika utekelezaji wa kazi zao na atakaekwenda kinyume na agizo hilo hatuwa za kisheria zitachukuliwa zidi yake.

Alifahamisha Utekelezaji wa sheria hizo umekuja kutokana na kukithiri kwa uvunjifu wa nidhamu kwa baadhi ya wafugaji katika maeneo mengi ya Mkoa wa Mjini Magharibi jambao ambalo linasababisha uchafunzi wa mazingira, ongezeko la ajali, kukuthiri kwa wizi, kuanza kwa migogoro baina ya wafugaji na wakulima, uharibifu wa miiundombinu pamoja na uhalifu wa kutumia mapanga. 

KITUO CHA HUDUMA NA MTOTO EAGT LUMALA MPYA CHA JIJINI MWANZA CHAKABIDHI MSAADA KWA WATOTO WENYE UHITAJI

MPALULEBLOGS:
Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma na Mtoto EAGT Lumala Mpya, Jorum Samwel (kulia mwenye suti), akitoa ufafanuzi juu ya msaada wa vitanda, magodoro na vyakula uliotolewa na Kituo hicho ambacho kiko chini ya Kanisa la EAGT Lumala Mpya Jijini Mwanza.

Na BMG

Kanisa la EAGT Lumala Mpya lililopo Sabasaba katika Manispaa ya Ilemela mkaoni Mwanza, limekabidhi misaada ya vitu mbalimbali ikiwemo vitanda, magodoro na vyakula kwa watoto wanaotoka katika familia duni ambao wanaolelewa na kanisa hilo.

Akikabidhi msaada huo hii leo, Askofu wa kanisa hilo Dkt.Daniel Moses Kulola, amesema watoto 18 waliokabidhiwa msaada huo ni sehemu ya watoto 264 wanaolelewa na kanisa hilo kupitia Kituo cha Huduma ya Mtoto iliyoanzishwa kanisani hapo tangu mwaka 2010.

Askofu Dkt.Kulola amesema hiyo si mara ya kwanza kwa kanisa hilo kutoa msaada wa vitu hivyo na kueleza kuwa limekuwa likifanya hivyo mara kwa mara ikiwemo kuwalea watoto hao kwenye maadili na afya njema na kuwaandaa kuwa watumishi wema katika jamii kwa baadae.

Nae Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma na Mtoto EAGT Lumala Mpya, Jorum Samwel, amesema msaada huo umetolewa baada ya uongozi wa Kanisa kuzitembelea familia hizo na kujionea hali duni za maisha wanayoishi ambapo baadhi yao hulazimika kulala chini baada ya nyumba zao kuathiriwa na mafuriko ya mvua yaliyotokea mwishoni mwa mwaka jana.

Wazazi, walezi na watoto walionufanika na msaada huo, wameushukuru uongozi wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya kupitia Kituo cha Huduma ya Mtoto, ambapo wametanabaisha kwamba msaada huo utawasaidia kuondokana adha ya kulala chini iliyokuwa ikiwakabiri.

Msaada huo wa vitanda, magodoro, mashuka, mahindi na mchele umegharimu zaidi ya shilingi milioni tisa ambazo zilitolewa na wahisani kutoka nje ya nchi ambapo wazazi na walezi wametakiwa kutambua kwamba jukumu la kuwalea watoto katika maadili mema ni la jamii nzima badala ya kuwaachia viongozi wa dini na taasisi za kijamii pekee.
Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lumala Mpya, Dkt.Daniel Moses Kulola, akitoa ufafanuzi juu ya msaada wa vitanda, magodoro na vyakula uliotolewa na Kituo cha Huduma ya Mtoto ambacho kiko chini ya Kanisa hilo.

NSSF YAOTA ELIMU KUHUSU MAFAO KWA WAFANYAKAZI WA TAZARA

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limetoa Elimu ya Pensheni kwa wâfânyakazi wa TÂZARA.lengo la semina hiyo ni kuwaelimisha wânâchama kuhusu kanuni mpya ya kukokotoa pensheni ya Uzeeni.

Akizungumza na wafanyakazi hao Ofisa Mwandamizi wa Mafao wa NSSF, Christina Kamuzora alisema kuwa kanuni hiyo imekwishaanza kutumika na kuwahakikishia kwamba malipo yao ya pensheni yatatolewa kwa uharaka zaidi kwa kuwa huduma zimeboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Ofisa Mwandamizi wa Mafao wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Christina Kamuzora akizungumza na wafanyakazi wa TAZARA (hawapo pichani), wakati wa utoaji wa elimu kwa wafanyakazi hao.

Wafanyakazi wa TAZARA wakimsikiliza Ofisa Mwandamizi wa Mafao wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Christina Kamuzora (hayupo pichani)

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU KUKUTANA NA WADAU PAMOJA NA WANANCHI 28 JUNI, 2016




OfisiyaTaifayaTakwimu

Taarifa kwa UmmaKatika kuazimisha “WIKI YA UTUMISHI WA UMMA” yenye kauli mbiu “Uongozi wa Umma kwa ukuaji Jumuishi: kuelekea katika Afrika tunayoitaka”, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inawajulisha wananchi na wadau wote kuwa imetenga siku ya Jumanne tarehe 28 Juni, mwaka huu, kuwa siku maalumu ya kukutana na wananchi ili kutoa elimu na kusikiliza hoja na maoni kuhusu utoaji wa takwimu rasmi nchini.

Muda ni kuanzia saa 3.00 Asubuhi hadi saa 9.00 Alasiri katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Makao Makuu.

KARIBUNI WOTE

ImetolewanaMkurugenzi Mkuu,
OfisiyaTaifayaTakwimu.









WAZIRI MKUU KUMWAKILISHA RAIS MAGUFULI MKUTANO MAALUM WA SADC


BALOZI WA JAMHURI YA KOREA NCHINI AKUTANA NA RAIS DK.SHEIN

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII KUSHIRIKI MAONESHO YA 40 YA BIASHARA YA KIMATAIFA SABASABA.


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII



Wizara ya Maliasili na Utalii itashiriki katikaMaonesho ya40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam(SABASABA)kuanzia tarehe 28 Juni hadi tarehe 8 Julai, 2016 katika viwanja vya Mwalimu Julius.K.Nyerere, Dar es Salaam.

Wizara itakuwa na washiriki kumi na sita (16) ambao ni Idara pamoja na Taasisi zake mbalimbali. Idara zitakazoshiriki ni Utalii, Wanyamapori, Mambo ya Kale na Misitu na Nyuki.

Kwa upande wa Taasisi ni Bodi ya Utalii Tanzania (TTB), Chuo cha Taifa cha Utalii, Makumbusho ya Taifa, Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro,Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI) na Vyuo vya Wanyamapori (Mweka, Pasiansi na Likuyu Semaganga).

Taasisi nyingine ni Vyuo vya Misitu na Nyuki (Olmotonyi, FITI Moshi na Chuo cha Nyuki Tabora), Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Wakala wa Mbegu za Miti, Taasisi ya Utafiti wa Misitu na Wadau wa Wizara ya Maliasili na Utalii.

Washiriki wote hao watakuwa kwenye banda moja la MALIASILI, Wizara inawakaribisha wananchi wote kwenye banda hilowaweze kujionea na kuelimika namambombalimbali yanayohusu Utalii, Ufugaji wa Nyuki, Uhifadhi wa Misitu, Malikale na Wanyamapori.

Aidha, Wizara itatoa punguzo kwa watanzania kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Mikumikwa gharama nafuu. Safari ya kwenda na kurudi kwa watoto itakua Tsh. 10,000 na watu wazima Tsh. 20,000. Safari ya kulala itakuwa Tsh. 50,000.

Pia katika maonesho hayo itakuwepo fursa ya kuwaona wanyamapori hai mbalimbali kama vile Chui, Nyoka, Ndege wa aina mbalimbali pamoja na SIMBA.

Kaulimbiu ya Maonesho hayo mwaka huu inasema“Tunaunganisha Uzalishaji wa Masoko” 







Mashine za tiketi za kieletroniki kuanza kutumika Uwanja wa Taifa hivi karibuni.

MPALULEBLOGS:
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Alex Nkenyenge akisisitiza jambo wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya uwekaji wa mashine za tiketi zakieletroniki katika Uwanja wa Taifa leo Juni 27,2016.
Mhandisi kutoka kampuni ya B.C.E.G ya China Bw. Xiong (kushoto) akifafanua jambo kwa Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Alex Nkenyenge(kulia) kuhusu mashine za tiketi za kieletroniki zinazotarajiwa kutumika kuingia katika Uwanja wa Taifa leo Juni 27,2016.
Mtaalamu wa Mashine za tiketi za kieletroniki kutoka kampuni ya Selcom Bw. Adrew Emmanuel (kushoto) akimuelekeza jinsi ya kutumia moja ya mashine hizo Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Michezo kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Alex Nkenyenge alipotembelea kuangalia maendeleo ya uwekaji wa mashine hizo uwanjani hapo Leo Juni 27,2016.
Mtaalamu kutoka kampuni ya Selcom Bw. Adrew Emmanuel akirekebisha moja ya mashine za tiketi za kieletroniki zinazotarajiwa kuanza kutumika kuingia katika Uwanja wa Taifa hivi karibuni.



Baadhi ya wananchi wakijaribu kutumia mashine ya tiketi za kieletroniki zinazotarajiwa kuanza kutumika kuingia katika Uwanja wa Taifa hivi karibuni.Picha zote na Raymond Mushumbusi WHUSM

MKUTANO WA MASHAURIANO YA KITALAM JUU YA KUANZISHA VITUO BORA VYA UVUVI WAFANYIKA ZANZIBAR

Na Mwashungi Tahir- Maelezo Zanzibar

WAZIRI wa Kilimo, Maliaasili Mifugo na Uvuvi Hamad Rshid Muhammed, amesema ipo haja kwa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika AU kuungana kwa pamoja katika kuangalia soko la ndani katika masuala ya uvuvi ili kukuza uchumi wa nchi hizo.

Akifungua mkutano wa siku mbili wa Nchi wanachama wa Umoja wa Arika AU, wa kujadili namna ya uzalishaji wa samaki, taaluma bora ya uvuvi na namna ya kuwawezesha wavuvi, uliofanyika katika ukumbi wa Zanzibar Beach Resort Mazizini, Hamad alisema soko la Afrika limekuwa likishuka kutokana na kutokuwa na wataalamu wa kutosha katika sekta hiyo.

Alisema mara nyingi nchi hizo zimekuwa zikijadili suala la kilimo kutokana na kuonekana ndio muhimu kwa jamii, lakini sasa ipo haja kuzungumzia suala la bahari kwa umuhimu wake hasa katika kukuza kipato cha wananchi na taifa kwa ujumla.

Aidha, aliwataka Waafrika kutumia fursa zilizopo katika nchi zao katika kukuza uchumi wa nchi pamoja na kuwapatia wadau husika elimu itakayowajengea uwezo wa kujua nyenzo ziliopo nchini ili waweze kufaidika nazo pamoja kuwashawishi kutumia masoko ya ndani kwanza kabla ya kutumia masoko ya nje.


Meza kuu ikisikiliza utaratibu wa Mkuta kutoka kwa Masta Solomon hayupo (pichani). Mkurugenzi kutoka Umoja wa Africa- Ofisi ya rasilimali wanyama Simplice Noula akitoa tarifa ya ofisi yake katika Mkutano huo uliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini Mjini Zanzibar.
Waziri wa Kilimo, Maliaasili Mifugo na Uvuvi Zanzibar Hamad Rshid Muhammed akifungua Mkutano wa siku mbili wa mashauriano ya kitaalam juu ya kuanzisha vituo bora vya uvuvi na ufugaji samaki Africa, uliofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mazizini Mjini Zanzibar.

Waganga wa tiba asili watakiwa kujisajili

Na: Lilian Lundo – MAELEZO – Dodoma —————————- Waganga wa tiba asili ambao wamekuwa wakitoa huduma ya tiba pasipo kujisajili wametakiwa kujisajili Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala ili waweze kutambulika kisheria. Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Hamis Kigwangalla ameyasema hayo leo, Bungeni Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge Viti Maalum Mhe. Zainabu Mussa Bakar juu ya udanganyifu unaofanywa na waganga wa tiba asili wa kutoa dawa feki kwa wagonjwa. “Waganga wa tiba asili wapo kisheria, ni kweli wapo wanaotoa dawa feki, na wengi wao ni wale ambao hawajasajiliwa, hivyo tumewaagiza kujisajili ili tuweze kuwatumbua na dawa zao ziweze kuhakikiwa na kusajiliwa kwa ajili ya matumizi ya binadamu,” alifanunua Mhe. Kigwangalla. Mhe. Kigwangalla amesema kuwa, mganga yoyote atakaye kiuka agizo hilo la kujisajili basi hatua kali zitachukuliwa dhidi yake. Aidha, amesema Wizara iko makini na ufuatiliaji wa dawa feki nchini kwani wanapopata fununu ya uwepo wa dawa feki hutuma kikosi kuchunguza na ikibainika kuwa dawa ni feki basi hatua kali huchukuliwa kwa muhusika. Aliendelea kwa kusema kuwa, ili kudhibiti uingizwaji wa dawa feki nchini Wizara hiyo hufanya uhakiki wa muda mrefu kuchunguza iwapo dawa inayopendekeza kuingia nchini siyo feki na inafaa kwa matumizi ya binadamu, ikiwa dawa haina madhara yoyote basi inasajiliwa kwa ajili ya kuingia sokoni. Vilevile Mhe. Kigwangalla amesema kuwa, Wizara imewaagiza waganga wa tiba asili kufunga dawa zao kwa kutumia vifungashio maalum vya madawa ambavyo vitasaidia dawa hizo kuendelea kuwa salama kwa mtumiaji kwa kipindi kilichopangwa kutumika.

WATUMIAJI WA UMEME WA JUA WA MOBISOL WAFIKIA 50,000.



Sunday, June 26, 2016

BREAKING NEWZZZ: Rais Magufuli afanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya na afanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Mikoa


 Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. 
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa. Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma. Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine. 
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara. Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa. Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi. 
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu. Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine. 
Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri. Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali. Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)

ARUSHA
1.      Arusha            -           Mrisho Mashaka Gambo
2.      Arumeru        -           Alexander Pastory Mnyeti
3.      Ngorongoro   -           Rashid Mfaume Taka
4.      Longido          -           Daniel Geofrey Chongolo
5.      Monduli         -           Idd Hassan Kimanta
6.      Karatu             -           Therezia Jonathan Mahongo
DAR ES SALAAM
1.      Kinondoni      -           Ally Hapi
2.      Ilala                 -           Sophia Mjema
3.      Temeke         -           Felix Jackson Lyaviva
4.      Kigamboni     -           Hashim Shaibu Mgandilwa
5.      Ubungo          -           Hamphrey Polepole