TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, December 6, 2011

KILIMANJARO STARS USO KWA USO NA UGANDA YATINGA NUSU FAINALI KWA KUINYUKA MALAWI 1-0

Timu ya Soka ya Kilimanjaro Stars, muda huu imefanikiwa kutinga hatua ya Fainali ya Michuano ya Tusker Challenge Cup kwenye Uwanja wa Taifa baada ya Nurdin Bakari kuifungia timu yetu ya Tanzania goli katika dakika ya 36 ya mchezo kipindi cha kwanza kwa shuti kali , lilikwenda moja kwa moja na kumshinda mlinda mlango wa Timu ya Malawi.

kwa ujumla mchezo ulikuwa mkali na wa kusisimua, zaidi niipongeze timu ya Kilimanjaro Stars kwa kuonyesha kandanda safi ambalo watanzania wengi hawakutarajia kupata ushindi kama huo, pamoja na ushindi huo pia pongezi nyingi ni kwa mlinda mlango wa Kilimanjaro Juma kaseja kutokana na kuonyesha umahiri mkubwa katika kulinda lango.

pamoja na mabadiliko ya hapa na pale lakini hadi mwisho KILIMANJARO STARS 1-0  MALAWI, ambapo sasa kwenye Nusu Fainali timu ya Rwanda itakutana na Timu ya Sudan, wakati Kilimanjaro Stars wenyeji watakutana na Timu ya Uganda.

No comments:

Post a Comment