TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 9, 2011

WATANZANIA WATAKIWA KUWA MAKINI NA MCHAKATO WA KUPATA KATIBA MPYA.

Na Lydia Churi- MAELEZO
Bagamoyo –PWANI.
WATANZANIA wametakiwa kutowapa nafasi watu wanaopotosha mchakato wa kupata Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bali washiriki mchakato huo kwa amani na utulivu.
Akizungumza na Vijana wa Chama cha Mapinduzi wa wilaya ya Bagamoyo leo Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel  Nchimbi  amesema kuwa Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya  Kikwete ana nia njema ya kuhakikisha kuwa watanzania wanapata katiba mpya baada ya kutimiza miaka 50 ya uhuru wa nchi yao.
Amesema taarifa zinazotolewa na serikali juu ya kuanza kwa mchakato wa katiba mpya ni za dhati na serikali ina nia njema katika hili hivyo wananchi hawana budi kuwapuuza wale wanaopotosha taarifa hizo.
Waziri  Nchimbi  amesema hayo wakati wa  uzinduzi wa  Mnara wa kumbukumbu ya mkutano wa kwanza wa TANU kitaifa uliofanywa na Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika mwaka 1954.
 Amewaasa  vijana kuwa Mnara huo usibaki kuwa kumbukumbu tu bali  wayafanyie  kazi yote yaliyofanywa na waliowatangulia.
Amewataka vijana kudumisha amani na utulivu uliopo nchini kwa faida ya vizazi vijavyo na kusherehekea miaka 50 ya uhuru wa Tanzania bara kwa kutathmini kazi zilizofanywa na waanzilishi ili waweze kuwarithisha watoto wao baadaye.
Naye Katibu mkuu wa UVCCM Taifa, Martin Shigella akizungumza wakati wa uzinduzi huo amewataka  vijana wa CCM kuwa na moyo wa kujitolea ili waweze kuliletea taifa  maendeleo.

No comments:

Post a Comment