TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, December 9, 2011

KWA MARA YA PILI MATOKEO YA UCHAGUZI CONGO DRC, YAAHIRISHWA TENA!

kongo 1


Tume huru ya uchaguzi katika Jamhuri ya Demokrasia ya Congo imeahirisha kwa mara ya pili kutangaza matokeo ya uchaguzi wa urais ambapo mkuu wa tume ya uchaguzi amesema kuwa yatatangazwa leo Ijumaa.
Tayari asilimia 90 ya kura zimehesabiwa na rais Joseph Kabila anaongoza kwa asilimia 49 huku mpinzani wake mkuu Etienne Tshisekedi akimfuata kwa asilimia 33, huku Polisi wa kupambana na fujo mjini Kinshasa walipambana na wafuasi wa upinzani ambao wanadai uchaguzi ilikuwa na udanganyifu.
Kulingana na kiongozi wa tume ya uchaguzi Daniel Ngoy Mulunda, wana kibarua kigumu kuhakikisha kuwa matokeo yote yamethibitishwa kabla ya kutangazwa ambapo Tume ya uchaguzi pamoja na magavana wa mikoa wametoa wito kwa watu kutulia lakini mwandishi wa BBC amesema bado kuna shaka kuhusu matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo.
Kulitokea shambulio katika mojawapo wa vituo vya kuhesabu kura katika eneo la Fizi mashariki mwa nchi ambapo Kituo cha radio kinachofadhiliwa na Umoja wa Mataifa, Okapi, kilitangaza kuwa matokeo ya mojawapo ya vituo thelathini katika mji wa pili kwa ukubwa Lubumbashi yamepotea. Inadaiwa kuwa fujo za baada ya uchaguzi ndio zilizosababisha kupotea kwa matokeo hayo.

No comments:

Post a Comment