TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 25, 2012

Airtel yatoa vitabu Kilimanjaro

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Siha,Bw.Rashid Kitambulo akizungumza na kuishukuru kampuni ya Airtel kwa msaada mkubwa wa vitabu ilioutoa kwa shule nne za sekondari zailizopo wilayani hapo, mwisho kushoto ni Mwalimu mkuu wa sekondari ya Oshara Elieta Kaaya akifatiwa na wawakilishi wa Airtel Pascal Bikomagu na Jane matinde (kulia) ni Afisa Elimu Taaluma wa sekondari Wilaya ya Siha,Bw. Mussa Shaban Ally.hafla hiyo ya makabidhiano iliyofanyika shule ya sekondari Oshara jana.
Airtel yatoa msaada wa vitabu shule 4 za secondari wilaya ya SIHA - Kilimanjaro Chini ya mpango wake wa Airtel Shule Yetu kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imetoa vitabu vya ziada na kiada kwa shule 4 za sekondari zilizoko wilaya ya Siha ili kusaidia maendeleo ya elimu wilayani hapo. Hafla hiyo fupi imefanyika katika shule ya sekondari Oshara ambapo shule zilizonufaika na msaada huo ni za sekondari ya Oshara,Kilingi,Magadini na Namwai zote za wilayani humo ambapo wawakilishi wa shule hizo walikabidhiwa msaada huo na Mkurugenzi wa Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Siha bw, Rashid Kitambulo ambaye alikabidhiwa vitabu hivyo na Afisa Uhusiano wa kampuni ya airtel bi, Jane Matinde. kila shule imepewa msaada wa vitabu vyenye thamani ya shilling milio moja. Akiongea katika hafla ya makabithiano iliyofanyika katika shule ya sekondari Oshara Afisa Uhusiano wa Airtel Tanzania Jane Matinde alisema" Airtel kwa kupitia programme ya shule yetu imeweza kuwafikia wanafunzi wengi na shule nyingi nchini Tanzania na leo tunafurahi kuwa sehemu ya maendeleo ya shule hizi 4 za sekondari wilayani Siha na kuweza kuchangia vitabu zitakavyotumika katika kufundishia na kuwa nyenzo muhimu kwa walimu na wanafunzi wa shule hizi” “Tutaendelea kushirikiana na Serikali chini ya Wizara ya Elimu katika kuinuia na kuboresha kiwango cha elimu nchini kwani tunatambua elimu ndio ufunguo wa maisha na vijana ndio nguvukazi ya kesho” Aliongeza Matinde. Mgeni rasmi katika halfa hiyo Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Siha bwana Kitambulio Rashidi alisema tunayo fuhara kuona Airtel inajitoa katika kusaidia kuinua kiwango cha elimu nchini, moja kati mikakati ya elimu halmashauri yetu iliyojiwekea ni kuhakikisha kwamba kila nyumba moja ya mkazi wa siha anatoka graduate na ili kufikia malengo yake kuna mahitaji ya vitabu vya kufindishia, tunashukuru sana Airtel kwa kutusaidia katika kutimiza malengo tuliojiwekea Bw Rashidi pia alichukua fulsa hiyou kuwaasa wanafunzi kuvitumia vizuri vitabu hivyo ili vilete matokeo vizuri kwa wanafunzi na kufikia lengo halmshauri hiyo iliyojiwekea Kwa upande wake Afisa Elimu Taaluma wa sekondari wilaya ya Siha Mussa Shaabani Ally wameishukuru Airtel kwa kuwawezesha vitendea kazi na kuongeza kuwa wilaya hiyo mpya bado inakabiliwa na changamoto nyingi katika elimu hivyo kuiomba kampuni hiyo kuendelea kuisaidia katika mambo mengine. Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imekuwa ikitoa misaada mbalimbali kama vile Vitabu vya shule ya sekondari, wiki iliyopita Airtel ilitoa msaada wa kutoa computer 4 kwa shule ya sekondari mlangarini iliyoko wilaya ya Arumeru mkoani na pia kuchangia katika sekta ya afya ambapo Airtel iligawa baskeli kumi kwa vituo vya afya wilayani misungwi Mkoani Mwanza. Hii ikiwa nikatika kurudisha faida inayoipata na kuchangia katika huduma kwa jamii.

No comments:

Post a Comment