TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 25, 2012

WACHOMA MAHINDI WAPEWA MAJIKO KUJIKWAMUA KIUCHUMI JIJINI ARUSHA


NA GLADNESS MUSHI- ARUSHA
Kikundi cha akinamama wapatao 50 kinaojishughulisha na biashara ya kuchoma mahindi katika jiji la Arusha kinatarajia kuongeza kipato kupitia biashara hiyo baada ya wanachama wake kupatiwa majiko yaliyosanifiwa kwa tenknolojia ya kisasa.
Upatikanaji wa majiko hayo yaliyotengenezwa kwa teknolojia ya aina yake unaelezwa kuiongezea dhamani biashara hiyo ya uchomaji mahindi ambayo akinamama wengi na vijana wamekuwa wakiifanya.
Kwa msaada mkubwa wa mtandao wa vijana nchini,kikundi kinachofahamika kama Wamama Wachoma Mahindi Arusha kimeweza kufadhiliwa na kupata majiko sita yenye dhamani ya shilingi milioni mbili ambapo mwenyekiti wa kikundi hicho Bi Sophia Juma anasema yatasaidia kuongeza ufanisi katika biashara hiyo.
Mwenyekiti wa mtandao wa vijana nchini YDN,Bw.Elipokea Urio amesema upatikanaji wa majiko hayo ni sehemu ya mikopo midogomidogo ambayo imekuwa ikitolewa na halmashauri ya jiji la Arusha katika kuinua vipato cha vya wafanyabiashara wadogo na wakati.
Naye Fundi aliyesanifu majiko hayo Bw.John Werema amesema kitaalamu aina hiyo ya majiko ni rafiki wa mazingira kutokana na muundo wake
Biashara ya uchomaji wa mahindi licha ya kutengeneza ajira kwa baadhi ya kinamama na vijana imekuwa ikielezwa kuchangia uchafuzi wa mazingira katika baadhi ya maeneo nchini lakini sasa aina hii ya majiko inaelezwa kuwa tiba sahihi katika kukabiliana na hali hiyo.

No comments:

Post a Comment