TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 25, 2012

SIMBA YAPATA MTEREMKO TANGA- YAIFUNGA COASTAL UNION 2-1

Mchezaji wa timu ya Simba akikokota mpira baada ya kumtoka beki wa timu ya Coastal Union ya Tanga Felix Stanley katika mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom mzunguko wa pili unaoendelea kwenye uwanja wa Taifa jioni hii,Mpira umekwisha Simba imeshinda goli 2-1goli la kwanza limefungwa na mchezaji Haruna Moshi "Boban" katika kipindi cha kwanza na goli la pili likafungwa na mchezaji Gelvas Kago akipokea pasi nzuri ya Haruna Moshi. Timu ya Coastal Union ilifanikiwa kupata goli katika kipindi cha pili kwa njia ya penati lililofungwa na mchezaji Hamis Shengo, mpaka mpira unakwisha simba 2 na Coastal Union 1.
Mashabiki wa timu ya Simba wakishangilia mara baada ya timu yao kupata goli la kuongoza dhidi ya Coastal Union katika mchezo huo.

Baadhi ya Maafisa Kilimo wa Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga na wakulima wakikagua shamba katika kijiji cha Kaoze.
NA :Ramadhani Juma, Afisa habari wilaya ya Sumbawanga 
VIKUNDI vya wakulima katika Halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga Mkoani Rukwa vimeanza kufaidika na miradi ya kilimo kupitia Mashamba Darasa inayodaiwa kuwaongezea mbinu za kisasa za kilimo bora hali inayotarajiwa kuwaongezea mavuno na kipato ikiwa ni juhudi za kujikwamua kutoka katika lindi la umasikini.
Baadhi ya wanachama wa kikundi cha CHEMKA kilichopo katika kijiji cha Kaoze kilichopo bonde la ziwa Rukwa walisema wamenufaika sana na elimu ya mradi wa shamba darasa uliotekelezwa katika kijiji hicho na kwamba wamekuwa wakipoteza mazao mengi kwa kulima kilimo cha kiasili.
Walisema kuwa, kwa kipindi kirefu wamekuwa wakivuna magunia matatu mpaka matano kwa hekari moja walipokuwa wakilima kilimo cha asili lakini kwa kilimo bora cha kisasa wanategemea kupata magunia 25 mpaka 30 kwa hekari moja hivyo wanategemea kujiongezea kipato na kujikwamua katika umasikini.
Kwa mujibu wa Afisa Kilimo wa wilaya hiyo Shaaban Bahari, Halmashauri hiyo ina jumla ya mashamba Darasa 151 katika vijiji mbalimbali wilayani humo na kwamba hali hiyo inatarajiwa kuwafaidisha wakulima.
“Tunategemea miradu hii itawasaidia wakulima wetu kujiongezea mbinu mbalimbali za kilimo cha kisasa ikiwemo matumizi ya mbolea, kupanda kwa kuzingatia nafasi, pamoja na kutumia mbegu bora” alisema Juma.
Miradi hiyo ya mashamba darasa inatekelezwa na wilaya hiyo katika vijiji na Kata mbalimbali kwa lengo la kuwaongezea ujuzi wakulima wilayani humo, ikiwa ni pamoja na matumizi ya mbolea pamoja na mbinu nyingine za kilimo cha kisasa.

President Jakaya Kikwete is received by the Minister for Agriculture, Food Security and Cooperatives Professor Jumanne Maghembe as he arrives at the Davos Sheraton ahead of the four day World Economic Forum held annually in the mountainous health resort. The forum, that goes under the theme: " The Great Transformation: Shaping New Models", Ais being attended by mong others President Kikwete is also scheduled to hold a number of private meetings and bilateral talks with prominent world leaders and entrepreneurs, besides attending interactive sessions on different issues.
President Jakaya Kikwete holding a preparatory meeting with his delegations soon after arrival at the Davos Sheraton ahead of the start of the four day World Economic Forum held annually in the mountainous health resort. The forum, that goes under the theme: " The Great Transformation: Shaping New Models", Ais being attended by mong others President Kikwete is also scheduled to hold a number of private meetings and bilateral talks with prominent world leaders and entrepreneurs, besides attending interactive sessions on different issues. (PHOTOS BY STATE HOUSE)

No comments:

Post a Comment