TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, August 20, 2013

PEPSI YATINGISHA JIJI LA MWANZA- MICHUANO YA MAYOR'S CUP GUMZO

 Mkurugenzi Mkuu wa Pepsi Mwanza, Nico Coetzer, akifuatilia kwa makini Fainal ya Michuano hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Pepsi Mwanza, Nico Coetzer, akifuatilia kwa makini Fainal ya Michuano hiyo huku akijipongeza na moja ya Kinywaji cha Kampuni
 Baadhi ya Wasanii Chipukizi wa jiji la Mwanza, wakitoa Burudani wakati wa Fainali hizo.
 Wakazi na Mashabiki wa JIJI la Mwanza, wakishangaa Jambo, wakati wa Fainali hizo
 Zawadi ya Mshindi wa Kwanza(BAJAJI) ikiwa mbele ya Viongozi(Wageni Rasmi) wakati wa Fainali hizo, Kulia ni Mkurugenzi wa May Way Entertainment, Waandaaji wa Michuano hiyo, Poul Mganga,
 Meneja Masoko wa Kampuni ya Vinywaji Baridi, PEPSI TANZANIA-MWANZA, Sameer Joqlekar, (kushoto) na Mkurugenzi wa May Way Entertainment, Poul Mganga, wakibadilishana jambo wakati Fainali hizo Zikiendelea Uwanja wa Nyamagana.
 Mkurugenzi wa May Way Entertainment, Poul Mganga, Muda mfupi baada ya kukabidhi Zawadi ya Mshindi wa Kwanza kwa Maafisa Utamaduni na wakuu wa Halmashauri ya Nyamagana, kama zawadi ya Fainali ya Michuano hiyo iliyofanyika  Uwanja wa Nyamagana.
 Baadhi ya Mameya wa Nyamagana, Kagera, Mbeya, Ilala, Arusha, Muda Mfupi kabla ya Kukabidhi Zawadi za Washindi
 Zawadi za Washindi wa Fainali ya Michuano hiyo zikiwa Mezani wakati Mchezo wa Fainali Ukiendelea.
 Mmoja wa Waratibu kutoka Halmashauri ya jiji, Joseph Mlinzi(kushoto) na Mkurugenzi wa May Way Entertainment, Poul Mganga, kulia ni  MC wa Fainali hizo.
 Mgeni Rasmi wa Fainali ya Michuano ya PEPSI Mayor's Cup, Stanlaus Mabula, akiinua juu kitita cha Fedha, ambazo ni Zawadi za Washindi wa Michuano hiyo.
 Mgeni Rasmi wa Fainali ya Michuano ya PEPSI Mayor's Cup, Stanlaus Mabula,akihesabu kwa Mafungu zawadi za wachezaji na washindi wa kwanza.
Mchezaji wa Timu ya Polisi(Captain), Ismail Juma, akionyesha juu Kikombe cha Washindi wa tatu baada ya Kutwa Ubingwa wa PEPSI Mayor's Cup katika Uwanja wa Nyamagana
Baadhi ya Wachezaji wa Timu ya Polisi, washindi wa Pili wa Michuano hiyo wakipita kupokea zawadi.
Wakazi wa jiji la Mwanza, wakishuhudia Fainal hizo
Mgeni Rasmi wa Fainali ya Michuano ya PEPSI Mayor's Cup, Stanlaus Mabula,akiwa na Fungu la zawadi za wachezaji na washindi .
Mayor wa Ilala, Jerry Slaa(kati) akielekeza jambo wakati wa kugawa zawadi kwa washindi
Wachezaji wa Timu ya Polisii, washindi wa pili wakivalishwa Medali na mmoja wa wageni waalikwa
Wachezaji wa Timu ya Polisi, washindi wa pili wakivalishwa Medali na mmoja wa wageni waalikwa
Mfungaji Bora wa michuano hiyo, akionyesha kitita cha shilingi laki moja alizokabidhiwa.
Washindi wa tatu timu ya Polisi wakipokea kati ya zawadi ya Furana kutoka kampuni ya DUME.
Mabingwa wa michuano ya PEPSI Mayor's Cup, Timu ya Mkoalani, wakipokea zawadi mbalimbali kutoka kwa wadhamini wa Michuano hiyo, Pepsi, Vodacom na DUME
Timu capt wa Timu yaMkolani, akipokea zawadi mbalimbali ya Fedha Taslim, Kombe kama zawadi za washindi wa Kwanza wa Michuano hiyo



Mabingwa wa Michuano ya PEPSI Mayor's Cup, timu ya ISAMILO, wakipokea zawadi  na Vikombe
Nyota wa Muziki Kizazi kipya, Kala Jeremihar, akipagawisha mashabiki waliofurika katika Uwanja wa Nyamagana kushuhudia Fainali hzo.
Baadhi ya wachezaji wa Isamilo muda mfupi baada ya kukabidhiwa zawadi, wakionyesha furaha yao.
Mayor wa Nyamagana, Stanlaus Mabula, akizungumza na Vyombo vya habari muda mfupi baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa Fainali hizo.
Askari Polisi wakiwa katika hekaheka za kutuliza purukushani kutoka kwa mashabiki waliofurika uwanjani hapo

Baadhi ya wadau wa Soka, akiwemo Mh. Mbunge jimbo la Lorya, Akairo Lameck(kulia), wengine ni Mameya wa majiji
Wageni mbalimbali wakijiandaa kugawa zawadi
Mashabiki wakifuatilia kila jambo uwanjani hapo


Mkurugenzi Mkuu wa PEPSI Nico Coetzer, akipunga mkono kwa  Mashabiki muda mfupi kabla ya kukabidhi zawadi
Msemaji wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Joseph Mlinzi, akifafanua jambo
Mwakilishi wa Vodacom Mwanza, akifafanua jambo, Vodacom walikuwa ni kati ya wadhamini wa Michuano hiyo.
Mwakilishi wa DUME Condom, akifafanua jambo, Dume ilikuwa ni kati ya wadhamini

Hapa anampongeza kabla ya kumkabidhi zawadi
Meya wa Manspaa ya ILALA, Jerry Slaa, akikabidhi zawadi kwa Captain wa timu ya Polisi, washindi wa Tatu zawadi ya Kombe
Fainali za Michuano ya PEPSI Mayor's Cup, imemalizika jijini Mwanza huku ikiwa imeacha Gumzo kwa wakazi wa jiji hilo pia ikiwa ni Elimu tosha kwa wapenda soka kutokana na Jinsi ilivyoweza kuandaliwa vizuri  na Kampuni ya May Way Entertainment ya jijini Dar es Salaam.
Katika michuano 

ikiwa ni katika jitihada za  kukuza michezo miongoni mwa vijana na maendeleo ya Jiji la Mwanza kwa kujenga mahusiano mazuri kati ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza na wananchi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali hapa nchini, Meya wa Jiji la Mwanza Mstahiki Stanslaus Mabula, akiongea mara tu baada ya fainali hizo jijini Mwanza  alisema kuwa , “waliamua kuanzisha michuano hiyo rasmi kama mashindano ya 2013 MWANZA PEPSI MAYOR CUP na timu zilizoshinda zimepatiwa zawadi bila ubabaishaji wa aina yoyote,  zawadi nono ambazo haijawahi kutolewa kwenye mashindano kama hayo hiyo ikiwa ni chachu kubwa ya mashindano hayo ya kipekee”. “Hili ni tukio la kipekee la kila mwaka ili kuwainua vijana”. Alisema Meya.


Mashindano ya mpira wa miguu na netball kombe la Meya wa Jiji la Mwanza Mstahiki Stanlaus Mabula, yamelindima kuanzia Jumamosi tarehe 15 Mwezi June katika uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. na kuendelea hadi Jumapili ya tarehe 16 June katika viwanja vya Nyamagana, Nyegezi Kona na Mabatini Polisi kila mwisho wa wiki kwa mzunguko wa kwanza,  robo fainali na fainali zilimalizika katika uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.


Akiongea jijini Mwanza pia Mratibu wa mashindano hayo na Mkurugenzi wa MyWay Entertainment Paul Mganga, alisema, “Tumeamua kuanzisha mashindano haya ya 2013 PEPSI MAYOR CUP kukishirikiana na Halmashauri ya Jiji la Mwanza ili kuwakutanisha pamoja vijana mbalimbali Jijini hapa kupitia michezo na kuwawezesha kuwa na vikundi vya ujasiliamali ili kuondokana na umaskini hali kadhalika vishawishi vya mienendo mibaya kwa kuanzisha miradi nakujiunga na saccoss za taasisi mbalimbali.


Mganga alisema, “Mashindano hayo yalihusisha timu 18 kutoka kata 12 za wilaya ya Nyamagana na timu 6 kutoka Polisi Jamii, Mafundi Gereji, Machinga, Jiji, wanahabari na waendesha Bodaboda zote za Jijini Mwanza. Mashindano ya 2013 PEPSI MAYOR CUP yalijumuisha timu za mpira wa miguu na netball za Jijini Mwanza”.


Vilevile ametoa wito wa dhati kwa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, mashirika na wadau mbalimbali wa michezo na wananchi wa Jiji la Mwanza kwa ujumla kuzidi kujitokeza kwa wingi na kuonyesha ushirikiano wa karibu ili katika kufanikisha mashindano hayo kuwa yenye tija na endelevu.


"Tumejipanga vizuri katika kufanikisha mashindano haya makubwa ya 2013 MWANZA PEPSI MAYOR CUP kila mwaka chini ya udhamini mnono wa kampuni ya soda ya PEPSI, tukishirikiana kwa ukaribu na Halmashauri ya Jiji la Mwanza" alisema Mganga


MyWay Entertainment ndio waandaaji wa mashindano hayo kwa udhamini mnono wa PEPSI, Kilimanjaro Premium Beer, Vodacom, Barmedas TV, Dume Condoms na Mwanza City FM pamoja na Kampuni ya Miss Demokrasia Tanzania ambao ni wadhamini kupitia Tovuti ya Mtandao wa .www.missdemokrasia.blogspot.com, pamoja na Blogs ya . www.shaabanmpalule.blogspot.com

-END-

PEPSI MAYOR'S GUMZO JIJINI MWANZA- PEPSI YAPONGEZWA NA WAKAZI WA MKOA HUO

Balozi wa PEPSI TANZANIA- Juma Kaseja, Muda mfupi baada ya kuwasili jijini Mwanza kushuhudia Fainali hizo za Kwanza za Kombe la Pepsi Mayor's Cup. wengine ni wafanyakazi wa kampuni hiyo. 
(Picha Zote kwa Hissani ya Miss Demokrasia Tanzania).
 Mfungaji Bora wa Michuano ya Pepsi Mayor's Cup, Godfrey Gerald, akionyesha Zawadi ya Tuzo ya Dhahabu.
 Vijana wakazi wa jiji la Mwanza wakifuatilia kwa Makini Semina ya Mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa DUME- kuhusiana na Matumizi bora ya kutumia Kinga(DUME Kondom) wakati wa Tendo la Ndoa(Ngono Salama).
 Wachezaji wa Timu za Mpira wa Miguu(Soka) Timu zilizoshiriki michuano hiyo, wakifuatilia kwa Makini Semina ya Mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa DUME- kuhusiana na Matumizi bora ya kutumia Kinga(DUME Kondom) wakati wa Tendo la Ndoa(Ngono Salama).
 Baadhi ya Wachezaji wa Timu katika Michuano hiyo, wakijiandikisha majina yao kabla ya kuingia uwanjani
 Wachezaji wa Timu za Mpira wa Miguu(Soka) Timu zilizoshiriki michuano hiyo, wakifuatilia kwa Makini Semina ya Mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa DUME- kuhusiana na Matumizi bora ya kutumia Kinga(DUME Kondom) wakati wa Tendo la Ndoa(Ngono Salama).
 Baadhi ya Timu Shiriki
 Wachezaji wa Timu za Mpira wa Miguu(Soka) Polisi, Timu zilizoshiriki michuano hiyo, wakifuatilia kwa Makini Semina ya Mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa DUME- kuhusiana na Matumizi bora ya kutumia Kinga(DUME Kondom) wakati wa Tendo la Ndoa(Ngono Salama).
 Wachezaji wa Timu za Mpira wa Miguu(Soka) Timu zilizoshiriki michuano hiyo, wakifuatilia kwa Makini Semina ya Mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa DUME- kuhusiana na Matumizi bora ya kutumia Kinga(DUME Kondom) wakati wa Tendo la Ndoa(Ngono Salama).
 Mayor wa Nyamagana Mwanza, Stanlaus Mabula wa Pili Kulia, akionyesha Moja ya Zawadi za Wadhamini wa Fainali hizo
  Wachezaji wa Timu za Mpira wa Miguu(Soka) Timu zilizoshiriki michuano hiyo, wakifuatilia kwa Makini Semina ya Mafunzo kutoka kwa wakufunzi wa DUME- kuhusiana na Matumizi bora ya kutumia Kinga(DUME Kondom) wakati wa Tendo la Ndoa(Ngono Salama).
 Wapenzi na Mashabiki wa Timu ya Bingwa wa Fainali hizo, ISAMILO, wakiwasili kwenye Uwanja huo

MFALME WA NYIMBO ZA ASILI TANZANIA, COSTA SIBOKA APAGAWISHA WATALII JIJINI DAR ES SALAAM.

 Mfalme Siboka akiongoza kucheza ngoma katika Hafla hiyo.
 Kundi jipya la Ngoma za asili la Mfalme Costa Siboka(MFALME GROUP)
 Costa Siboka, akijaribu kuonyesha kwa Vitendo, wakati mmoja wa Watalii wa Kigeni aliposhindwa kijizuia na kuingia kucheza ngoma ya Twisile ya kabila la wanyakyusa.
Mfalme wa nyimbo za Asili Tanzania, Costa Siboka, akipagawisha Wazungu waliofurika katika Ukumbi wa Golden Jubilee, wakati wa Onyesho la Kutafuta Warembo wa Miss Ilala Tanzania 2013
.(Picha kwa Hissani ya Miss Demokrasia Tanzania).

Matukio katika Picha na taswira yetu kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2015

 Halii ni hatari sana na ni chanzo cha ajali za barabarani, Baadhi ya wafanyabiashara wakitoka kufanya biashara za Mitumba katika Vijiji vya Mkoa wa Shinyanga
 Pamoja na Ahadi nyingi kutoka kwa viongozi wetu, ususani wakati wa kuomba kura wakati wa Uchaguzi, tatizo kubwa linazidi kuwa Maji  kwenye maeneo mengi ya Vijiji, Vijana wakichota maji kwa ajili ya matumizi ya kila siku katika vijiji vya mkoa wa Tabora.
 Ajali nyingi usababishwa na ukaidi ama uzembe wa Madereva, pichani baadhi ya wafanya biashara wa Vijiji vya Mkoa wa Shinyanga wakitoka katika biashara zao za Mitumba Gulioni(MNADA)
 Baada ya Kumalizika Ujenzi wa Barabara ya Mkoa Shinyanga kwenda Mwanza, Hali si shwari kwa Watumiaji wa Barabara hiyo ususani Madereva wa Magari Makubwa yakiwemo Mabasi ya Abiria, Tatizo la Uchakachuaji ni chanzo kinachosadikiwa kuifanya Barabara hiyo kutokuwa bora na ya Ufanisi.
 Wakati Mwingine Magari ya Abiria mabasi upata ajali kutokana na kwenda Safari zao kwa Mashindano, kama walivyoonekana Madereva wa Barabara itokayo Singida kwenda Tabora.
 Wakati Tanzania ikielekea Uchaguzi Mkuu wa Viongozi  2015, Vijana nwengi wameendelea kukumbwa na Tatizo la Ajira, pamoja na ahadi nyingi kutoka kwa Viongozi Maisha Bora kwa Kila Mtanzania.
 Tatizo la Vijana wengi kutoka Vijijini kukimbia mijini linazidi kuongezeka, hiyo ikitokana na uwepo wa Maisha magumu Vijijini, ambapo wameamua kwenda Mijini ili kufanya Biashara na kuwaacha sasa Watoto wadogo wakiendelea kujikongoja na aina mbali mbali za Biashara, kitendo kinachozidi kudidimiza Elimu ya Tanzania( kwa watoto kujiingiza katika soko la Biashara na kukimbia Masomo Darasani).
 Maisha ya Kina mama wakazi wa vijiji inazidi kuwa tete, ambapo sasa kina mama wamejitokeza kwa wingi kuingia katika soko la kujiajiri na hivyo kusahau hali ya kuendeleza kilimo bora, Maisha ambayo yamesababishwa na udanganyifu wa Viongozi wao wakati wa kuomba kura ili wachaguliwe.
  Maisha ya Kina mama wakazi wa vijiji inazidi kuwa tete, ambapo sasa kina mama wanazidi kuangaikia maji, Maisha ambayo yamesababishwa na udanganyifu wa Viongozi wao wakati wa kuomba kura ili wachaguliwe.
 Maslahi ya Wakulima wa Pamba katika Mkoa wa Shinyanga inazidi kulalamikiwa , ambapo serikali inatakiwa kuingilia kati na kuboresha hali hiyo.ambapo wanaofaidika ni wale wafanyabiashara kubwa ya Pamba kuliko wale wadogo.
Ajali nyingi zinazidi kutokea kutokana na Madereva wengi kutotimia ama kufuata masharti ya barabarani, huku tatizo la usafiri pia likizidi kuvikumba vijiji mbalimbali nchini Tanzania ususani kutoka katika Mikoa kwenda kwenye Vijiji. kama walivyokutwa wakazi hawa wa Mkoa wa Shinyanga.
(Picha Zote kwa Hissani ya Miss Demokrasia Tanzania).

Thursday, August 15, 2013

WAKAZI WA JIJI LA MWANZA WAFURIKA KUSIKILIZA MKUTANO WA CHADEMA KATIKA UWANJA WA FURAHISHA


Huu ni mkutano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, katika uwanja wa FURAHISHA, kirumba Mwanza, katika kuzungumzia na kukusanya maoni ya katiba Mpya zoezi linaloendelea kwenye maeneo mbalimbali ya majimbo ya Tanzania. 
(Picha zote kwa Hissani ya Miss Demokrasia Tanzania)