TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Friday, November 20, 2015
EAGT Dodoma walitaka Tamasha la Shukrani
Stanslaus Mabula alitaka Tamasha la Kushukuru
Na Mwandishi Wetu
MBUNGE wa Nyamagana Stanslaus Mabula ameiomba Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Kushukuru linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwewnye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, lihamie jijini Mwanza kwa lengo la kufikisha shukrani kwa Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi, Alex Msama wanayafanyia kazi mapendekezo ya Mabula ili kufanikisha tamasha hilo adhimu lenye nia ya kushukuru Mungu baada ya uchaguzi Mkuu.
MBUNGE wa Nyamagana Stanslaus Mabula ameiomba Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Kushukuru linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwewnye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, lihamie jijini Mwanza kwa lengo la kufikisha shukrani kwa Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25.Friday, November 13, 2015
WANACCM WALIOCHUKUA FOMU KUWANIA USPIKA WA BUNGE
Idadi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaoomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Uspika na Unaibu Spika katika Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) linalotarajiwa kuanza wiki ijayo, inazidi kuongezeka na hapa ni majina 21 ya ambao wameshachukua fomu hizo, kadiri ya taarifa ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Oganaizesheni, Muhammed Seif Khatib.STARS KAMILI KUWAVAA MBWEHA WA JANGWANI
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Charles Boniface Mkwasa amesema kikosi chake kipo tayari kwa mchezo wa kesho dhidi ya Algeria kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Akiongea katika mkutano na waandishi wa habari leo, Mkwasa amesema wamejiandaa kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo huo, wanajua Algeria ni miongoni mwa timu bora Afrika, lakini hilo halitawazuia kuibuka na ushindi.
KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI,VIJANA,UTAMADUNI NA MICHEZO AFANYA ZIARA BASATA,TBC NA TSN.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel(wa kwanza kushoto) akiangalia mitambo ya kurushia matangazo ya Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) wakati alipofanya ziara ya kikazi katika minara ya shirika hilo leo hii Kisarawe.Profesa Elisante amefanya ziara katika Taasisi tatu zilizo chini ya Wizara hiyo ambazo ni Baraza la Sanaa Tanzabia (BASATA),Tanzania Standard Newspapers(TSN) na Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) lengo likiwa ni kufahamiana na wafanyakazi,kuwahimiza kufanya kazi kwa bidii na kujua changamoto zinazowakabili ikiwa ni kutimiza kauli mbiu ya HAPA KAZI TU ya awamu ya Tano.Anaefuatia ni mkurugenzi mkuu wa shirika hilo Bw.Clement Mshana.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel akiangalia tofauti ya santuri ya zamani na flashi ya kisasa zinavyozidiana ukubwa kwa umbo alipotembelea maktaba mojawapo katika ofisi za shirika la utangazaji Tanzania (TBC) alipofanya ziara kuongea na menejimenti ya shirika ilo leo jijini Dar es Salaam.Santuri zilitumika kipinda shirika hilo likiitwa Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD).
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (waliosimama watatu kulia) akiwa katika mojawapo ya studio za kurushia matangazo ya shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) wwakati alipotembelea shirika ilo leo kuongea na menejimenti yake pamoja na kuona utendaji wake.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel (aliyekaa mwenye miwani) akipata maelekezo jinsi gazeti linavyotengenezwa kutoka kwa mtumishi wa Standard News Papers(TSN) leo jijini Dar es Salaam alipofanya ziara ya kikazi na kuangalia utendaji wa kazi.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof Elisante Ole Gabriel(wa pili kulia) akiangalia moja ya kazi za vijana wanojifunza kutengeneza batiki na kuweka chapa alipotembelea ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA) leo hii jijini Dar es Salaam.
Thursday, November 12, 2015
MAKABIDHIANO YA TAARIFA RASMI IKULU.
MAKABIDHIANO YA TAARIFA RASMI IKULU.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, leo katika Ikulu ya Dar es Salaam amepokea taarifa rasmi ya makabidhiano ya Ofisi kutoka kwa Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete.
Makabidhiano hayo yamefanyika leo mchana na kushuhudiwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na Maafisa wa Ofisi Binafsi ya Rais.
Wednesday, November 11, 2015
LIGI KUU ZANZIBAR YAANZA ‘KICHAKANI’, MAFUNZO WACHEZEA KICHAPO CHA JKU
Na Salum Vuai, ZANZIBAR
KUFUATIA uwanja wa Amaan kuzuiwa kutumika kwa mechi za Ligi Kuu ya soka Zanzibar bila kuelezwa sababu za msingi, ligi hiyo iliyochelewa imelazimika kuanza jana katika uwanja wa kijiji cha Bweleo umbali wa takriban maili 15 kutoka mjini Zanzibar.
Kwa kuwa uwanja huo si rasmi na hauna uzio wala huduma muhimu ikiwemo vyoo, waandaaji wa ligi hiyo, kamati ya muda ya ZFA wamejikuta wakipata hasara kwani hakuna kiingilio cha fedha kilichowekwa kwa watazamaji.
Na katika mchezo wa ufunguzi jana, JKU makamu bingwa msimu uliopita, waliilaza Mafunzo mabao 2-1.
Kamisaa wa mchezo Ramadhani Ibada Kibo, akiwaongoza waamuzi wa mpambano huo kurudi uwanjani kuanza kipindi cha pili, baada ya kupumzika katika kichaka pembezoni mwa uwanja.
Mafunzo ndio mabingwa watetezi wa ligi hiyo na wawakilishi wa Zanzibar kweli Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani, wakati JKU watashiriki Kombe la Shirikisho.
TOTO AFRICANS WAAMUA ‘KUTEMBEZA BAKULI’ KWA WANACHAMA WAKE
Na Philipo Chimi, MWANZA
KLABU Toto Africans ya Mwanza imeandaa mkutano maalum kwa wanachama wake kwa ajili ya kufanya harambee kuchangia timu hiyo iweze kushiriki vyema Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Mwenyekiti wa klabu hiyo, Godwine Aiko amesema kwamba wameandaa mkutano huo kufuatia hali mbaya ya kiuchumi inayoikabili timu.
Amesema timu inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinahitaji utatuzi wa haraka ili kunusuru mwendo wake mbovu katika Ligi Kuu.
“Tumeandaa mkutano huo ambao utafanyika siku ya Novemba 22 kwa ajili ya kufanya mipango kuona namna gani timu inapata fedha,” amesema na kuongeza.
Ratiba ya Kombe la Challenge 2015 kama ilivyotolewa na CECAFA
MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Juma Ramadhani Mgunda ameteuliwa kuwa Msaidizi namba moja wa Alhaj Abdallah Athumani Seif 'King Kibaden' katika kikosi cha timu ya Tanzania Bara, 'Kilimanjaro Stars' kitakachoshiriki michuano ya CECAFA Chellenge baadaye mwezi huu mjini Addis Ababa, Ethiopia.
JESHI LA POLISI LAANZA KUTOA ELIMU KWA ABIRIA NA MADEREVA ILI KUKABILIANA NA AJALI KATIKA KIPINDI CHA MWISHO WA MWAKA
Subscribe to:
Posts (Atom)













