Muonekano wa basi la Penguin mara baada ya kupata ajali ya kugongana na land cruser.(habari/picha na Eddy Blog Team)
 Toyota land cruser mara baada ya kugongana na basi la penguin.
 Muonekano wa basi hilo.
Abiria walionusurika kwenya basi hilo wakitazama basi hilo mara baada ya ajali licha ya mvua kunyesha lakini walibaki kuduwaa. 
Zaidi ya abiria 20 waliokuwa wakisafiri na basi la Penguin lenye namba za usajili T 947 BVQ
 kutoka Njombe kuelekea wilayani Makete mkoani Njombe wamenusurika kifo 
baada ya basi hilo kugongana na toyota landcruser pick up yenye namba za
 usajili T 999 ARP
Ajali
 hiyo imetokea jana Februari 22 majira ya saa tisa alasiri katika kijiji
 cha Mang'oto wilayani hapo na kupelekea baadhi ya abiria hao kupata 
majeraha madogo madogo na wengine wakitoka salama
Kwa
 mujibu wa mwandishi wa eddy blog ambaye ni miongoni mwa walionusurika 
kwenye ajali hiyo amesema imetokea kwenye kona iliyokuwa katika eneo 
hilo na kushuhudia abiria hao wakitoka kwenye basi hilo wakiwa 
hawaaamini kilichotokea kufuatia wengi wao kulala kwenye basi huku 
safari ikiendelea kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha
Mmoja
 wa manusura wa ajali hiyo ambaye alikuwa akienda kumuuguza baba yake 
anayeendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Ikonda Consolatha 
ambaye pia hakupenda jina lake liandikwe mtandaoni amesema alikuwa 
amelela lakini ghalfa aliamka kutoka usingizini bada ya kusikia kishindo
 kikubwa huku akisikia abiria wenzake wakipiga kelele
Kwa
 mujibu wa maelezo ya abiria hao wamesema chanzo cha ajali hiyo ni 
mwendo kasi wa magari yote mawili pamoja na mmoja wao kupita eneo ambalo
 si lake (kuibia barabara) na hivyo kutokana na hayo ilikuwa ni vigumu 
kukwepa ajali hiyo isitokee hata kama dereva aliishuhudia toka mbali
Dereva wa Toyota
 landcuser iliyokuwa imetoka kupeleka mafuta kwenye minara ya simu 
wilayani Makete ambaye amezungumza na mwandishi wetu eneo la tukio 
amesema yeye alikuwa mwendo wa kawaida na alikuwa akipita upande wake 
lakini alifatwa na basi hilo na kudai kuwa ukweli wa chanzo cha ajali 
hiyo utafahamika pale askari wa usalama barabarani watakapofika eneo la 
tukio na kufanya vipimo vyao
Abiria
 wengi walitawanyika eneo hilo kutokana na mvua iliyokuwa ikinyesha huku
 magari yanayotoka na kwenda Njombe na Makete yakishindwa kupita 
kutokana na ajali hiyo kuziba barabara
Hadi
 mwandishi wetu anaondoka eneo la tukio majira ya saa 10 jioni askari 
walikuwa hawajafika eneo la tukio, lakini alikutana na gari lao njiani 
eneo la tandala likielekea eneo la tukio
Habari za uhakika baada ya polisi kufika na kufanya vipimo vyao utaipata hapa hapa kesho Jumatatu






No comments:
Post a Comment