TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 15, 2014

HABARI ZILIZOTAWALA SIKU YA TAREHE 13 HIZI HAPA JIKUMBUSHE.

VITUKO VYATAWALA MAZISHI YA MSANII MABOVU IRINGA , MLEVI AFANYA VURUGU KUBWA

Wasanii  wakielezea kifo cha mabovu , Juu ni Msanii Mabovu enzi za uhai  wake
Waombolezaji  wakiwa na jeneza la msanii Mabovu kutoka msikiti wa Mwangata kwenda makaburi ya Mlolo Iringa
Wasanii wakiwa  wamelipiga chata kaburi la mabovu mara baada ya mazishi yake
Baadhi ya  wasanii wa kundi la Weusi ambao  wamefika  Iringa kumzika msanii Mabovu leo
Makini akichangisha rambi rambi
Msanii JOh Makini akiwa na michango ya msiba wa mwenzao Mabovu leo
Mwakilishi  wa  wasanii wa kundi la Weusi Joh Makini kushoto  akimpa pore baba wa msanii Mabovu mzee Upete kulia baada ya kumaliza kuzika nyumbani kwake Mwangata wengine ni baadhi ya  wasanii  walioshiriki mazishi hayo leo
Mwakilishi wa kundi la weusi kwanza Joh Makini akizungumza na mtandao huu wa matukiodaima leo
Picha na habari na kikosi cha matukiodaima.co.tz Vituko vyatawala msiba wa msanii Ahmed Zubery Upete a. k. a Geez Mabovu Iringa mlevi (pichani aliyekaa chini)atembeza kichapo kwa wafiwa kisa ataka aruhusiwe kuufukua mwili wa marehemu ili auage Mara ya mwisho asisitiza kuwa marehemu amekua nae na ana siri nzito ya kifo chake.
Tukio hilo limetokea muda mfupi baada ya mwili wa marehemu kuwasili makaburi ya Mlolo nje kidogo ya mji wa Iringa kwa mazishi.
Chapombe huyo ambae alifika makaburini hapo kwa kuchelewa alivamia eneo hilo la mazishi kwa kuanza kutoa lugha za matusi ya nguoni kwa wafiwa kwa madai wamewezaje kumzika marehemu huyo bila ya yeye kufika eneo hilo.
Kutokana na lugha hizo za matusi iliwalazimu Vijana waombolezaji kumtoa kwa nguvu eneo hilo na kwenda nae pembeni kidogo kumsihi asifanye vurugu kabla ya chapombe huyo kuanza kurusha Ngumi kwa wasanii.
Akizungumza  mara  baada ya mazishi hayo  mmoja  kati ya  wadau  wa  tasinia ya muziki nchini na promota mkubwa wa mziki nyanda za  juu  kusini Edwin Bashir ambae ni  mtangazaji  wa  kituo cha  Radio Ebony  Fm alisema  kuwa  mbali ya umoja ambao  wasanii  wameuonyesha katika msiba huo kwa  kuja kushiriki mazishi  ila bado angeshauri  wasanii kwa  wakati mwingine  kujenga ushirikiano wa  kumjulia hali mwenzao pindi anapoumwa.
” Sisemi  kwa  ubaya  ila kiukweli  msanii  Geez Mabovu  ameumwa sana karibu mwaka mzima anasumbuliwa na ugonjwa  wake ila hakuna  msanii ambae amefika  kumjulia hali  ila  leo wengi  wamesafiri  kuja kumzika….. inapendeza  kusaidiana  wakati wa ugonjwa badala ya  kusubiri mwenzenu afe “
Bashir  alisema  kuwa msanii  huyo ni  miongoni mwa  wasanii  wa mwanzo zaidi  kuutangaza mkoa wa Iriga katika tasnia ya  muziki na kuwa hata kabla ya vituo vya radio  kuanzishwa mkoani Iringa alikuwa akiutangaza mkoa na kusikika katika  radio  mbali mbali za nje ya Iringa.
Alisema  kuwa msanii  huyo toka amemaliza  elimu  yake kamwe  hajapata kufanya  shughuli  nyingine  nje ya mziki na kuwa  wakati  wote  alikuwa akijishughulisha na muziki  zaidi .
Hata  hivyo  alisema chanzo cha Mabovu kuhama mkoa wa Iringa na kuhamishia makazi yake  jijini Dar es Salaam ni  kuzidi  kuutangaza muziki  zaidi na mkoa wake wa Iringa malengo ambayo alipata  kufanikiwa kwa  kiasi  kikubwa .
” Utaona   jinsi ambavyo  msiba  wake  leo  ulivyowavuta  watu  wegi  wapenzi na wadau wa muziki  kutoka mikoa mbali mbali ya nje ya Iringa ambao kimsingi  baadhi yao  imekuwa ni mara yao ya kwanza kufika Iringa ….pamoja na kufarijika kwa  umati wa  watu  waliofika kumzika  ila  moyo umeniuma sana hasa  ukizingatia kuwa   kifo  chake hakikuwa na  ghafla bali  amekufa kwa mateso makubwa kwa  kuugua  karibu mwaka  mzima  sasa hivyo kwa  umoja  huo ningetegemea wangefika enzi za uhai  wake kumuuguza mwenzao”
Kwa  upande wake mwakilishi  kwa  kundi   la Weusi Bw  Joh Makini alisema  kuwa  kifo cha Mabovu  kimeacha  pengo kubwa katika tasnia  ya  muziki hasa muziki wa hiphop Tanzania,
 Alisema  kuwa  Mabovu  amepata  kuishinae Kinondoni  Jijini Dar es Salaam  mtaa mmoja  ila  pia amepata  kushirikiana  kazi mbali mbali  za kimzuki .
Hivyo  alisema  kuwa  ushirikiano  huo  ndio  ambao umewasukuma  kufika mkoani Iringa  kushiriki mazishi  hayo baada ya  pengo kubwa ambalo  wamelipata .
 
Akizungumza  kwa niaba ya  wasanii wazawa na mkoa wa Iringa msanii Squza,alisema  kuwa  Iringa  imempoteza  msanii mkongwe na  kuwa kifo  chake  kitaenziwa na  wasanii wa mkoa wa Iringa  pia  ambao  wapo nje ya mkoa huo kwa kuangalia jambo la kufanya  katika kuwanyanyua  wasanii chipukizi wa mkoa huo.
Alisema  kuwa  wapo  wasanii maarufu  wengi  kutoka mkoa wa Iringa ambao  wana majina makubwa kama  Rehema Chalamila (RAY C} akina  MiKe T  na  wengine  wengi na kuwa  kama  njia ya  kumuenzi  Mabovu  watahakikisha wanaunganisha  nguvu kwa kushirikiana na vyombo  vya habari  kuona Iringa inampata mwakilishi mwingine wa Mabovu kutoka kwa  wasanii Chipukizi .
Msanii Mabovu  alifariki  dunia jana  majira ya saa 2 usiku  nyumbani kwa wazazi  wake eneo la Mwangata mjini Iringa ambako alikuwa akiugulia na amezikwa  leo katika makaburi ya Mlolo nje  kidogo na mji wa Iringa

Tigo kusaidia mpango wa kujenga na kutoa vifaa kwa maabara ya shule za sekondari wilayani Mtwara

unnamed
Mkuu wa wilaya ya Mtwara mjini Bw. Wilman Ndile (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu harambee inayojulikana kama Tigo Mtwara Benefit Gala kwaajili ya ujenzi wa maabara katika wilaya ya Mtwara, kulia kwake niMeneja wa Tigo kanda ya kusini, Bw.Daniel Mainoya na kushoto kwake mkurugenzi wa kampuni ya Proactive Solution, Nestory Phoye.
 ………………………………………………………………………………
Tigo Tanzania leo imetangaza kwamba itasaidia kujenga na kuchangia vifaa katika maabara ya shule za sekondari ambazo zimekwisha jengwa wilayani Mtwara. Mamlaka ya wilaya yanaandaa harambee kubwa siku ya Ijumaa wiki hii kwa ajili kufanikisha jambo hili. Akizungumza wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari leo katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Meneja wa Kanda ya Mtwara kutoka Tigo Daniel Mainoya alisema kwamba kampuni yake inaamini katika kuwapatia watoto mazingira bora yakusomea, ili kuweza kuwajengea uwezo wa kuwa wananchi wanaowajibika na kuzalisha ipasavyo. “Hii ni muhimu sana hasa hasa katika kujifunza masomo ya sayansi. Ni muhimu kwa watoto wetu kupewa vifaa vinavyotakiwa ili kuweza kupata uelewa si wa kinadharia tu bali wakiuzoefu wa namna ya kujifunza masomo ya sayansi kama Baiolojia, Kemia na Fizikia,” alisema Mainoya. Wilaya ya Mtwara, ni moja kati ya wilaya sita zilizoko katika halmashauri ya mkoa wa Mtwara, yenye jumla ya shule za sekondari 42 zinazoendeshwa chini ya serikali. Kati ya hizi asilimia 18 tu ya shule hizi ndo zenye maabara ya kujifunza Fizikia, Kemia na Baiolojia, kutokana na maelezo ya Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Wilman Kapenjama. Akielezea kwamba hali kuwa ni “mbaya,” Kapenjama aliwaambia waandishi wa habari kwamba kukosekana kwa maabara hizo ni kilema kikubwa kwa wanafunzi wanaoazimia kuja kufanya kazi katika tasnia ya sayansi kama madaktari, maenjenia na kadhalika. Kutokana na maelezo ya DC alama ya wastani ya ufaulu kwa wilaya ya Mtwara katika masomo ya sayansi kwenye shule za sekondari kwa sasa ni asilimia 35. “Ni kwa sababu hii tuntoa rai kwa wadau wote kutoka katika sekta binafsi na ya umma kuja kutuunga mkono katika kuchangisha fedha kujenga maabara mapya na kuwapatia vifaa kwa maabara chache ambazo tayari zilishajengwa ili kuweza kuwawezesha watoto wetu kufurahia masomo ya sayansi na wakati huo huo kuweza kutimiza ndoto zao ya kuwa wanasayansi bora duniani,” alisema Harambee hiyo inayojulikana kama Tigo Mtwara Benefit Gala, itafanyika Ijumaa hii na itajumuisha kampuni na watu binafsi, pia kutakuwa kuna mnada wa bidhaa na vitu mbali mbali kama michoro ya Kiafrika, Yakimakonde na mnada wa safari za kitalii nchini, yote haya ni kwa ajili yakuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa maabara 43 katika sekondari mbali mbali hapa wilayani, alisema Kapenjama.

PINDA AAGANA NA MWAKILISHI MKAZI WA UNIDO NCHINI

unnamedWaziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa UNIDO nchini  aliyemaliza muda wake, Bw. Emmanuel Kalenzi ambaye alikwenda ofisini kwa Waziri Mkuu kuaga Novemba 13, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu unnamed1 Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimkabidhi zawadi ya kinyago Mwakilishi Mkazi wa UNIDO  nchini aliyemaliza muda wake, Bw. Emmanuel Kalenzi ambaye alikwenda ofisini kwa Waziri Mkuu kuaga Novemba 13, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
==============================================================

TANZANIA KUJENGA KITUO KIKUBWA CHA SEKTA YA NYUKI DODOMA

index
Mahmoud Ahmad Arusha
Tanzania  inatarajia kujenga kituo Kikubwa   cha sekta ya nyuki ambacho kitatoa mafunzo  juu  ya namna bora ya kufuga nyuki kisasa
 
Mtendaji Mkuu wa baraza la Taifa la uwezeshaji wananchi Kiuchumi Dakta  Anaclet Kashuliza  ameeleza hayo  wakati wa kongamano la kwanza  la ufugaji nyuki barani Afrika.
 
Kituo hicho kinatarajiwa kujengwa MKoani Dodoma kwa msaada wa Kampuni moja kutoka Marekeni mbali na kituo hicho kuhusika na utoaji  mafunzo pia kitahusika na  uchakataji  wa asali
 
Dakta Kashuliza amesema kuwa kituo hicho  kitahusika na utunzani wa  kumbukumbu  ya vitu vya  asali  vya ufugaji nyuki hapa Tanzania na kinatarajia kuanza katika kipindi cha miezi minne ijaayo
 
Dakta Kashuliza  aidha amesema mbali na kujengwa kwa kituo hicho kikubwa barani afrika pia  Tanzania inatarajia kujenga viwanda vidogo vidogo, vya kati na viwanda vikubwa kwa ajili ya kusindika asali na nta
 
Viwanda hivyo  vitatumika kwa ajili ya watalii kutoka nje  watakaopata fursa ya kutembelea viwanda hivyo pamoja na kituo kikubwa  cha  Dodoma kujionea  juu ya hali ya raslimali asali ilivyo.
 
Wakati huo huo Serikali Mkoa wa  Singida imesema kuwa ipo tayari  kuyaondoa  makundi yote  ya watu waliovamia maeneo ya wahadzabe wakiwemo wakulima na wafugaji na hivyo kuwawezesha kumiliki maeneo hayo kama zilivyo jamii nyingine nchini.
 
Kauli hiyo imetolewa leo na mkuu wa mkoa wa Singida,Vicent  Parseko  Kone
 
Hatua hii inalenga kuwapa haki yao  ya msingi ya kumiliki ardhi jamii hiyo ya wahadzabe kama  jamii nyingine ya watanzania hapa nchini
 
Amewaambia washiriki wa kongamano la ufugaji nyuki barani afrika kuwa   asilimia 77 ya eneo linalokaliwa na jamii ya wahadzabe tayari limevamiwa na wafugaji pamoja na wakulima  jambo ambalo linatishia maisha ya jamii hiyo ya wahadzabe ambao  maisha yao yote hutegemea sekta ya nyuki 
 
Amesema katika mkakati huo wa kuwaondoa wavamizi wote pia  Serikali imefanikiwa kupeleka huduma mbambali za kijamii zikiwemo za maji, miundo mbinu ya barabara, elimu na afya.
 
Mkuu huyo wa Mkoa pia amesema Serikali Mkoani humo imefanikiwa kuyapima maeneo yote wanamoishi wahadzabe ili kuwawezesha kupata hati miliki
 
Pia amesema Serikali imesambaza mizinga  zaidi ya 150 katika jamii hiyo ili kuiwezesha kuendeleza zaidi ufugaji wa nyuki katika jamii hiyo pamoja na kuipatia  mtama kwa ajili ya kuwawesha kuendelezaa kilimo katika vijiji vyao
 
Mkoa huo hivi sasa una  watu wapatao 1,300 wa jamii ya  wahadzabe ambapo  300 wanaishi katika wilaya ya Mkalama katika Kijiji cha Munguli
 
Wakizungumza katika kongamano hilo mmoja wa jamii hiyo ya wahadzabe amesema jamii hiyo inayo haki ya kumiliki  ardhi kama jamii nyingine ya kitanzania
 
Aidha ameitaka serikali kukomesha vitendo  vya  baadhi ya jamii kuvamia maeneo yao kwa  kutumia nguvu  za kiuchumi walizonazo
 
Hivyo ameitaka   serikali kuhakikisha  jamii   ya wafugaji na wakulima kufuata taratibu pale wanapoingia katika  baadhi ya maeneo
 
Amekiri kuwa  kwa asilimia kubwa jamii ya wahadzabe walikuwa  hawajui haki haki zao pamoja na matumizi ya ardhi
Continue reading →
==============================================================

Ugungaji wa Semina ya wakuu wa Mikoa na Wilaya Bara na Visiwani

1Wakuu wa Mikoa Bara na Visiwani wakiwa katika ugungaji wa semina yao ya siku taku iliyozungumzia Mahusiano na Mwingiliano katika siasa na Utendaji kwa Wakuu wa Mikoa,Wilaya,Makatibu Tawala wa Mikoa ya Zanzibar na Baadhi ya Tanzania bara iliyofungwa na Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara  Maalum za SMZ Mhe,Haji Omar Kheri katika Ukumbi wa Sea Cliff  Kama nje ya Mji wa Unguja,(Na Mpiga Picha Maalum) 2 Baadhi ya Wakuu wa Mikoa Bara na Visiwani wakimsikiliza Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara  Maalum za SMZ Mhe,Haji Omar Kheri akitoa hutuba yake ya ufungaji wa Semina ya siku tatu kuhusu Mahusiano na Mwingiliano katika siasa na Utendaji kwa Wakuu wa Mikoa,Wilaya,Makatibu Tawala wa Mikoa ya Zanzibar na Baadhi ya Tanzania bara ufungaji huo ilifanyika  jana Ukumbi wa Sea Cliff Kama nje ya Mji wa Unguja,(Na Mpiga Picha Maalum) 3 Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara  Maalum za SMZ Mhe,Haji Omar Kheri akitoa hutuba yake ya ufungaji wa Semina ya siku tatu kwa Wakuu wa Mikoa,Wilaya,Makatibu Tawala wa Mikoa ya Zanzibar na Baadhi ya Tanzania Bara  iliyohusu Mahusiano na Mwingiliano katika siasa na Utendaji  katika  Ukumbi wa Sea Cliff Kama nje ya Mji wa Unguja,(Na Mpiga Picha Maalum) 4Wakuu wa Wilaya za Unguja na Pemba wakimsikiliza Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara  Maalum za SMZ Mhe,Haji Omar Kheri alipokuwa akitoa hutuba yake ya ufungaji wa Semina ya siku tatu kwa Wakuu wa Mikoa,Wilaya,Makatibu Tawala wa Mikoa ya Zanzibar na Baadhi ya Tanzania Bara  iliyohusu Mahusiano na Mwingiliano katika siasa na Utendaji  katika  Ukumbi wa Sea Cliff Kama nje ya Mji wa Unguja jana,(Na Mpiga Picha Maalum) 6 Picha ya pamoja iliyowahusisha washiriki wa Semina ya siku tatu ya kwa Wakuu wa Mikoa,Wilaya,Makatibu Tawala wa Mikoa ya Zanzibar na Baadhi ya Tanzania Barabaada ya kufungwa na Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara  Maalum za SMZ Mhe,Haji Omar Kheri katikat, (Na Mpiga Picha Maalum) 8Picha ya pamoja iliyowahusisha washiriki wa Semina ya siku tatu ya kwa Maafisa Tawala Mikoa na Wilaya za Mikoa ya Zanzibar na Baadhi ya Tanzania Bara  baada ya kufungwa na Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara  Maalum za SMZ Mhe,Haji Omar Kheri katikati, (Na Mpiga Picha Maalum)
==========================================================

WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KUPIMA UGONJWA WA KISUKARI

index
Na Beatrice Lyimo- Maelezo
Serikali imetoa wito kwa kila mwananchi nchini kuhakikisha kwamba anapima afya yake  mara kwa  mara  kwa kuwa ugonjwa wa kisukari unaweza usionyeshe dalili yoyote mapema ili kuweza kukabiliana  na kupunguza athari za ugonjwa huo
Aidha Serikali imesisitiza kuwa endapo mtu atatambulika  kuwa ana ugonjwa huo, atumie huduma za afya kulingana na ushauri wa atakaopewa na wataalam wa afya.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Stephen Kebwe leo alipokuwa anatoa tamko kuhusu Siku ya Kisukari Duniani itakayoadhimishwa Novemba 14, mwaka huu duniani kote yenye kauli mbiu “Ulaji unaofaa, huanza na mlo wa asubuhi”.
Siku ya kisukari duniani ilianzishwa baada ya kuona ugonjwa wa kisukari unaongezeka sana duniani kote na Tanzania kama nchi nyingine duniani huadhimisha siku hii kwa kushirikiana na Chama cha Ugonjwa wa Kisukari  Tanzania kutoa elimu ya umuhimu wa kuzuia na kujikinga na madhara mbalimbali yatokanayo na ugonjwa huu, alisema Naimu Waziri.
“Ugonjwa wa Kisukari ni hali ambayo hutokea wakati sukari katika damu inapokuwa nyingi kupita kiwango cha kawaida kwa muda mrefu” aliongeza Dkt Kebwe.
Amebainisha kuwa asilimia 80 ya wagonjwa wa kisukari ulimwenguni wanaishi katika nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania, na tafiti zinaonyseha kuwa mwaka 2007 kulikuwa na wagonjwa 246 milioni duniani,mwaka 2012 wagonjwa milioni 371, mwaka 2013 wagonjwa milioni 382ulimwenguni kote  na mwaka 2013 kulikuwa na wagonjwa milioni 19.8 barani Afrika.
 
Aidha nchini Tanzania kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka 2012 na kuhusisha wilaya 50 ulionyesha kuwa asilimia 9.1 ya Watanzania wenye umri wa miaka 25 na kuendelea wana ugonjwa wa kisukari.
 Dk. Kebwe  aliongeza  kuwa takwimu za   watoto wenye kisukari mwaka huu ni kati ya asilimia 15 mpaka 20 ya wagonjwa wa kisukari ambao wanatibiwa kwenye kliniki za  hapa nchini.
“Lakini wapo wengine hawajitokezi kwenye kliniki kwa sababu mbalimbali zikiwemo imani potofu, gharama pamoja na umbali wa huduma za afya zilizopo” aliongeza Naibu Waziri huyo.
Aidha Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inaendelea na utekelezaji wa Sera ya Afya(2007) inayolenga kutoa huduma kwa magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kisukari kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani ya Nchi na wa kimataifa.
Tanzania inaungana na mataifa yote duniani kutekeleza azimio la Umoja wa Mataifa la mwaka 2011 la kuhakikisha magonjwa yasio ya kuambukiza yanapungua kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2025.
================================================================

BODI YA FILAMU TANZANIA YAZITAKA KAMPUNI ZA FILAMU KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI ZA FILAMU.

1
Katibu Bodi ya Filamu Tanzania, Bi. Joyce Fissoo akiongea na wahusijka wa Kampuni ya Kajala Entertainment wakati alipofanya nao mkutano leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapa Sheria na Kanuni zilizokiukwa katika filamu ya Mbwa Mwitu.
2q
3
4
Mkurugenzi wa Kampuni ya Kajala Entertainment, Kajala Masanja akiweka sahihi ya kukubali kufanya marekebisho katika filamu yake pamoja na malipo ya faini mbele ya Katibu wa Bodi ya Filamu Tanzania wakati aliitikia wito wa Ofisi ya Bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuelezwa juu ya Sheria na Kanuni zilizokiukwa katika filamu yake ya Mbwa Mwitu.
5
Meneja ambaye pia ni Mratibu wa Kampuni ya Kajala Entertainment, Bi. Leah Mwendamseke akiweka sahihi katika fomu maalum ya kukubali kufanya marekebisho katika filamu iliyokaguliwa na Bodi hiyo mbele ya Katibu wa Bodi ya Filamu Tanzania wakati aliitikia wito wa Ofisi ya Bodi hiyo leo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuelezwa juu ya Sheria na Kanuni zilizokiukwa katika filamu ya Mbwa Mwitu.
6
Katibu Bodi ya Filamu Tanzania, Bi. Joyce Fissoo akiagana na Mkurugenzi wa Kampuni ya Kajala Entertainment wakati alipofanya naye mkutano leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapa Sheria na Kanuni zilizokiukwa katika filamu ya Mbwa Mwitu.
(PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA, MAELEZO-DSM)
Na Benedict Liwenga, Maelezo-DSM.
BODI ya Filamu Tanzania imezitaka Kampuni za filamu nchini kufuata Sheria na Kanuni mbalimbali wakati wa kutengeneza filamu ili kuepusha ukiukwaji wa Sheria na Kununi.
Rai hiyo imetolewa leo na Katibu wa Bodi hiyo, Bi Joyce Fissoo wakati alipofanya mkutano na Kampuni ya Kajala Entertainment ambapo mnamo Septemba 22, mwaka huu ilikagua Filamu fupi ya kampuni hiyo iliyopewa jina la Mbwa Mwitu yenye dakika 12 na kubaini baadhi ya makosa.
Akiongea wakati wa mkutano na wadau wa kampuni hiyo, Bi Fissoo alisema kuwa Bodi iliielekeza Kajala Entertainment kuifanyia marekebisho filamu hiyo katika dakika ya 7 ambapo ilionekana wanawake wakidhalilishwa na kubakwa kinyama na pia katika dakika ya 11 ambapo ilionyesha wizi na uvamizi.
Alisema kuwa, wahusika walielekezwa kufanya marekebisho hayo kwa kuondoa vipande husika na baada ya kufanya marekebisho hayo waliwasilisha Bodi ya Filamu nakala ya filamu iliyokuwa imefanyiwa marekebisho yenye dakika 12 na kupewa kibali namba 4261 ya tarehe 24 Septemba, 2014.
Bi Fisso aliongeza kuwa, mnamo tarehe 25 Septemba, 2014 katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, filamu hiyo fupi ilionyeshwa bila ya kuzingatia marekebisho yaliyokuwa yameelekezwa kwa mujibu wa Sheria kwa kuzingatia kifungu cha Sheria cha 19 (2) (a).
“Baada ya ukiukwaji wa Sheria katika kifungu cha 19 (2) (a) na kile cha 24 (i), (m) na (n) vya Kanuni za Sheria ya Filamu husika, wahusika waliitwa mara mbili kufika Bodi ya Filamu lakini hawakufanya hivyo, lakini baada ya kumbushio na kalipio wahusika baadaye walifika Ofisi za Bodi katika kikao cha tarehe 13 Novemba mwaka huu”, alisema Bi. Fissoo.
Alieleza kwamba, wahusika walikiri kuwa walipata ujumbe wa wito wao wa kuitwa na Bodi hiyo ambapo Mratibu wa masuala yote ya Kampuni ya Kajala Entertainment, Bi. Leah Mwendamseke aliieleza Bodi kuwa anaomba asamehewe kwa kuwa walikuwa na shughuli nyingine mbalimbali.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Kajala Massanja aliiomba radhi Bodi ya Filamu Tanzania huku akisema kuwa mara nyingi yeye huwa amekuwa akiwaachia wsaidizi wake kutekeleza majukumu ya kampuni yake ingawa yeye kama mmiliki wa kampuni hiyo anawajibika moja kwa moja.
Aidha, Bodi iliitaka Kajala Entertainment kueleza sababu ya kukiuka maelekezo ya Bodi ambayo yalikuwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni zake licha ya mtunzi na mwandishi wa musuada na muongozaji wa filamu hiyo, Bi. Leah Mwendamseke alijitetea kuwa alifanya utafiti na kukutanana vijana mbalimbali waliowahi kujihusisha na vitendo vya uhalifu.
Hata hivyo, Leah Mwendamseke alishindwa kuoanisha uhalisia wa matokeo ya utafiti wake na ujenzi wa visa vya hadithi ya filamu ambayo inaweza kupeleka ujumbe chanya kwa jamii, huku wahusika wakieleza kwamba lengo lao kubwa lilikuwa ni kuelimisha jamii kuhusu maovu yanayotokea na namna ya kuyaepuka ambapo mtunzi huyo aliahidi kurekebisha vipengelee husika katika filamu hiyo ili kuwa na filamu bora.
Kwa upande wake Mwakilishi toka Ofisi ya Makao Makuu ya Polisi Tanzania, Sylivester Mganga aliushauri uongozi wa Kajala Entertainment kufuata maelekezo na kuzijua Sheria mbalimbali zinazohusu mambo ya filamu kwa kuvishirikisha vyombo vya ulinzi na usalama kabla ya kujichukulia maamuzi ya kutengeneza filamu zenye kutishia amani ya nchi.
Bodi ya Filamu Tanzania imetoa onyo kali kwa wahusika kwa kutengeenza filamu zenye kuonyesha ama kukuza uhalifu na udhalilishaji bila kuainisha mkondo wa Sheria licha ya msamaha kutokana na kosa hilo ambapo Bodi hiyo imeitaka kampuni hiyo ilipe faini ya shilingi milioni moja kwa mujibu wa kifungu cha 47 (2) (a) cha Kanuni za Sheria ya Filamu ambayo wahusika waliridhia adhabu hiyo.
========================================================

WASIRA AKERWA NA MAKUNDI YA KUDUMU NDANI YA CHAMA

wasira ipp(1)
Na Mahmoud Ahmad, Arusha
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais ,(Uhusiano na Uratibu ) , Stephen Wasira amesema kuwa yupo tayari kuvunja makundi ya kudumu yanayoongozwa na Mbunge wa zamani wa Arusha Mjini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Felix Mrema pamoja na Batilda Burian aliyekuwa mgombe wa ubunge na kushindwa  kwa chama hicho kwenye chaguzi mbali mbali.
Aidha amesema kuwa Arusha inashindwa kwenye chaguzi mbalimbali kutokana na makundi yaliyopo ndani ya chama hicho na si kwasababu ya vyama vya upinzani kuwa na nguvu ya kuiangusha CCM.
Wasira aliyasema hayo jana Jijini hapa kwenye kikao cha Halmashauri ya Wilaya kilichofanyika jana ndani ya ukumbi wa CCM Mkoa na kuhudhuriwa na wajumbe mbalimbali wa chama hicho chenye lengo la kupitisha majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za wenyeviti wa mitaa.
Alisema makundi ya Batilda na Mrema ni lazima yamalizwe na kama mlezi yupo tayari kuyaita makundi hayo ili kumaliza tofauti zilizopo ndani ya chama na kutoa rai kwa wagombea wengine kuwa kama wameshindwa wakubali kushindwa na kumpa ushirikiano mgombe aliyepitishwa kwa wakati huo ila si vyema kuweka makundi ndani ya chama.
“Nakerwa sana na kushindwa kwetu kwenye chaguzi ambao sisi wenyewe ndio tunaofanya tushindwe na kwanini tunaendelea kushindwa kwenye chaguzi mbalimbali sisi tukishinda au kushindwa tunapongezana  hili ni tatizo hata kama tumeshindwa tunapongezana  haiwezekani  lazima tufike mahali tuvunje makundi na kuchagua kiongozi/mgombea aliyemteule na si kuongozi asiyetakiwa na wananchi”.
Hata kamati za Siasa Mkoa wa Arusha nazo pia zimegawanyika  waandika maazimio na kamati nyinge zinakaa na kuyakataa hapana tunachane na makundi  na pia tunapoelekea kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa  lazima tuchague kiongozi mteule na si kumchagua mjomba wala shangazi yako maana akishindwa tunashindwa wote kama chama na si wewe uliyetaka awepo.
Alihoji suala la wananchi wa Kijiji cha Nanja kilichopo Wilayani Monduli kuandamana hadi Ofisi za Mkoa kutoa malalamiko yao kuwa mgombea waliyemtaka si yule aliyepitishwa na kutoa tahadhari kwa wananachama na viongozi kuwa kwanini wanataka kuwa wabinafsi na kuhoji kwanini  mteule asipitishwe badala yake apitishwe mgombea asiyetakiwa na wananchi wa eneo husika/.
Aliongeza asijidanganye mtu Rais ajaye atatoka ndani ya chama cha Mapinduzi (CCM) kwani hata maandiko yanasema kuwa wagombea ni wengi lakini wateule ni wachache  .
Pia Wassira aliwasihi wanachama wa CCM pamoja na wananchi kwa ujumla kujitokeza kupiga kura ya maoni kwaajili ya katiba mpya pamoja na kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura ili kuweza kutimiza wajibu wao.
Naye Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, onesmo ole Nangole awali akikaribisha Wassira ambaye ni mlezi wa chama hicho Mkoani hapa alisema kuwa kinachokiangusha CCM kwenye chaguzi mbalimbali Mkoani hapa ni makundi ndani ya chama na kuyataja makundi hayo kuwa yanaongozwa na Batilda pamoja na Mrema huku akimsihi Wassira kuwaita kwa pamoja na kuwafungia ndani ili waweze kujadili kiini cha makundi hayo na kuyavunja kabisa.
Nangole alihoji ni kwanini wanaangusha wenyewe kwa wenyewe ndani ya chama na kutoa rai kwa wanaccm kuachana na majungu na kuacha watu kuamua nani wanayemtaka badala yake wasipeleke wateule mizigo kwenye chaguzi halafu mwisho wa siku chama kinashindwa kwenye chaguzi mbalimbali.uchaguzi unapofika tuweke nia ya kushindwa na kupongezena
===========================================================

Tigo, Original Komedi,na Wasanii kibao kutikisa jiji la Mwanza kwenye tamasha la Welcome Pack jumamosi hii.

1 Meneja wa Bidhaa wa Tigo Bw. Edwin Mgoa akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) wakati wa kutangaza tamasha kubwa la Tigo welcome pack litakalofanyika uwanja wa ccm Kirumba jijini Mwanza Jumamosi ya wiki hii, tamasha hili litaweza kuwapa wananchi fursa ya kupata maelezo ya kina kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na kampuni ya Tigo.
5Kwaya Master Mwana FA akiongea na waandishi wa habari(hawapo pichani) kuhusu tamasha kubwa la Tigo welcome pack jijini Mwanza jumamosi wiki hii.
6 Kikundi maarufu cha wachekeshaji cha Orijino Komedi kinatarajiwa kuwatumbuiza wananchi wa kanda ya ziwa katika tamasha maalum linaloandaliwa na Tigo jijini Mwanza Jumamosi ijayo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kampeni ya Welcome Pack inayowapa wananchi fursa ya kupata maelezo ya kina kuhusu huduma mbalimbali zitolewazo na kampuni hiyo ya simu.
Meneja Bidhaa wa Tigo Bw.Edwin Mgoa alisema kwamba kampeni hiyo ya Welcome Pack inayoendelea kwa muda wa mwezi mmoja na zaidi sasa imekwisha fanyika kwa mafanikio makubwa katika mikoa mingine ikiwemo Kagera, Kilimanjaro, Arusha, Iringa, Dodoma na Mbeya ambapo imewapa fursa maelefu ya wananchi kupata huduma za Tigo kwa karibu ikiwemo kifurushi cha Welcome Pack.
Kifurushi cha Welcome Pack, kwa mujibu wa Mgoa, kinampa mteja anaenunua laini mpya ya Tigo dakika 20 za muda wa maongezi, MB 175 za intanet, kutuma ujumbe mfupi wa SMS bila kikomo, na kiasi cha shilingi 500 kama salio la Tigo Pesa kwa kila mteja atakaye nunua laini ya Tigo kwa kiasi cha shilingi 1000 tu.
“Tumeandaa matamasha haya kwa ajili ya kusherehekea huduma hii mpya mahususi kwa wateja wetu. Na kwa safari hii, Tigo imeamua kwenda kutikisa jiji la Mwanza na kikundi cha The Orijino Komedi na wasanii wengine wa Bongo fleva. Kwa hiyo tunapenda kuwasihi wateja wetu wote wa kanda hiyo ya ziwa kuchukua fursa hii kuja kujaribu hii huduma yetu mpya pamoja na kupata burudani isiyo na kifani kutoka kwa wasanii bora kabisa kutoka nchini Tanzania,” alisema Mgoa.
Mmoja wa wanakikundi kutoka Orijino Komedi, Lucas Mhavile almaarufu kama Joti alisema kwamba yeye binafsi pamoja na kikundi chake kizima wanafuraha kubwa sana kushiriki katika msafara wa tamasha la Tigo Welcome Pack na wapo tayari kwenda Mwanza kuwapatia zaidi ya burudani mashabiki wao.
“Napenda kutoa rai kwa watu wote wa Mwanza kujitokeza kwa wingi katika uwanja wa CCM Kiruma siku ya Jumamosi kuanzia saa 6 mchana. Tamasha la Tigo Welcome Pack si jambo la kukosa! Njoo upate burudani, ucheze na ufurahi. Lakini usisahau pia kujipatia kifurushi cha Welcome Pack kutoka Tigo na uanze kuwasiliana na marafiki na familia yako kupitia ofa kabambe kabisa kutoka Tigo,” alisema Joti.
Akifafanua kuhusu kifurushi cha Welcome Pack, Mgoa alisema kwamba kifurushi hicho kinakuja na dakika 20 za muda wa maongezi, MB 175 za intanet, kutuma ujumbe mfupi wa SMS bila kikomo, na kiasi cha shilingi 500 kama salio la Tigo Pesa kwa kila mteja atakaye nunua laini ya Tigo kwa kiasi cha shilingi 1000 tu.
“Hii itawawezesha wateja wetu kuwasiliana zaidi na kwa gharama nafuu ambayo haijawahi kutokea,” alisema Mgoa.
Kampeni ya Welcome Pack itakuwepo kwa muda wa miezi mitatu, ambapo misafara zaidi ya 70 ikiwemo basi la Tigo la Kidijitali lenye malengo la kuwaelimisha wateja kuhusu huduma za Tigo za kidijitali litatembelea miji 70 na vijiji zaidi ya 100 ndani ya mikoa 10 tofauti ikiwemo Mbeya, Iringa, Dodoma, Arusha, Kilimanjaro, Kagera, Mwanza, Shinyanga, Kigoma na Mtwara.
Wasanii maarufu wa Bongo fleva watakaotoa burudani ni pamoja na Profesa J, Joh Makini, Shah, Mheshimiwa Temba na Chege, Madee na Izzo Business. Tunapenda kuchukua fursa hii kuwakaribisheni nyote,” alimalizia kwa kusema Mgoa.

No comments:

Post a Comment