TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 15, 2014

HABARI ZILIZOTAWALA SIKU YA TAREHE 14/11/2014 HIZI HAPA JIKUMBUSHE

BONDIA THOMAS MASHALI ASAINI KUZIPIGA NA ABDALLAH PAZI JANUAR MOSI 2015 FRENDS CORNER

Bondia Thomasi Mashali kushoto akitia saini ya kupigana na Abbdallah Pazi kulia baada ya makubaliano na promota Kassim Texas katikati mpambano utakaofanyika january mosi katika ukumbi wa frends corner manzese Dar es salaam
Bondia Abbdallah Pazi kulia akitia saini ya kupigana na Thomasi Mashali kushoto baada ya makubaliano na promota Kassim Texas katikati mpambano utakaofanyika january mosi katika ukumbi wa frends corner manzese Dar es salaam
Bondia Thomasi Mashali kushoto akitunishiana misuli na Abdallah Pazi baada ya makubaliano juzi  ya mpambano wao kufanyika January Mosi 2015 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaa
Promota Kassim Texas katikati akiwainuwa mikono juu mabondia Thomas Mashali kushoto na Abdallah Pazi kuashilia makubaliano ya mpambano wao utakaofanyika january mosi katika ukumbi wa frends corner manzese 
Bondia Thomasi Mashali kushoto akitunishiana misuli na Abdallah Pazi baada ya makubaliano juzi  ya mpambano wao kufanyika January Mosi 2015 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaa Picha na SUPER D BLOG
===============================================================

WAZIRI WA AFYA NA USTAWI WA JAMII AFUNGUA KONGAMANO LA NHIF NA WAANDISHI WA HABARI MJINI DODOMA

1Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Mh. Dr. Seif Rashid akifungua Kongamano la Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na wahariri pamoja na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali linalofanyika kwenye hoteli ya New Dodoma  mkoani Dodoma jana, Kongamano hilo la siku mbili linaendelea leo na linajadili mafanikio mbalimbali na changamoto zinazokabili mfuko huo katika mikoa mbalimbali na Halmashauri ambazo unatoa huduma zake. Kongamano hilo linamalizika leo 2Naibu Katibu wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Dr. Deo Mtasiwa  akizungumza katika kongamano hilo wakati akimkaribisha waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Seif Rashid ili kuzungumza na washiriki wa kongamano hilo. 3Kamimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Khamis Mdee  akitoa maelezo kuhusu shughuli mbalimbali kwa mwaka mzima. 4Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa masoko na Utafiti NHIF,Raphael Mwamoto, Kaimu Mkurugenzi Tiba na Ushauri wa NHIF, Dk Mkwabi Fikirini na Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii CHF Athman Rehani wakiwa katika mkutano huo. 5Hance John Mwankenja Afisa Mwandamizi , Matekelezo NHIF pamoja na maafisa wengine wa mfuko huo wakiwa katika kongamano hilo. 006Mkuu wa Wilaya ya Igunga Mh. Elibariki Kingu akitoa mada katika kongamano hilo. 6Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya Jamii CHF Bw. Athman Rehani akitoa mada katika Kongamano hilo. 7Mkuu wa Wilaya ya Igunga na Mkuu wa Wilaya ya Chamwino Fatma Said Ally wakiwa katika kongamano hilo. 9Baadhi ya wahariri na waandishi wa habari wakifuatilia mada mbalimbali katika kongamano hilo. 10Grace Kingalame wa TBC wa pili na wadau wengine wakiwa katika kongamano hilo. 11Hosea Cheyo wa TBC Mbeya kushoto na Tom Chilala wa Star TV wakifuatilia mada. 12Wanahabari mbalimbali wakifuatilia kongamano hilo. 13 14 15 Baadhi ya maofisa wa NHIF wakiandika mambo muhimu katika kongamano hilo.
=====================================================================

SKYLIGHT BAND NI MOTO WA KUOTEA MBALI, WAZIDI KUWAPA RAHA MASHABIKI WAO KWA BURUDANI NZURI

Pichani Kutoka kushoto ni Bella Kombo akiongoza mashambulizi ya jukwaa akipewa sapoti na Digna Mbepera(katikati) na kwa mbaliiiii ni Aneth kushaba.
Kama kawaida yetu inapofika mwishoni mwa juma yaani Ijumaa huwa inakuwa ni siku ya furaha na kubadilishana mawazo, kupunguza stress za kazini…..paleee Thai Village Masaki.Kwenye Jukwaa Bendi yako matata na inayotikisa Tanzania na Jiji la Dar Skylight Band wanakuwa wanakupa burudani ya nguvu na iliyoenda shule.Karibu leo kuanzia saa 3 kamili usiku upate zile Afropop, Zouk, Lingala,Sebene, Reggae, Naija Flava na zingine kibao!
Aneth Kushaba AK 47 akizipiga vocal za kutoshaaaa ili kuwapa burudani wapenzi wa Skylight Band ndani ya Thai Village Ijumaa iliyopita.
Bella Kombo akitia madaha yake na swagga kibao ndani ya Thai Village.
Digna Mbepera (Mtoto Mzuri) akiimba kwa hisia kali kuwapa ladha wapenzi wa Skylight band ndani ya Thai Village
Anaitwa Hashimu Donode mkali wao akizipiga zile vocal kaliiii na tamuuu kuwapa raha mashabiki wake ndani ya Thai Village

UNESCO, SAMSUNG KUJENGA KIJIJI CHA DIGITALI OLOLOSOKWAN

DSC_0062Mwakilishi mkazi shirika la UNESCO nchini Bi. Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania, Bw. Mike Seo wakibadilishana nyaraka za makubaliano hayo yaliyofanyika ofisi za UNESCO.
Na Mwandishi wetu
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limetiliana saini mkataba na kampuni ya elektroniki ya Samsung ya ujenzi wa kijiji cha digitali cha Ololosokwan, Loliondo.
Makubaliano hayo yalitiwa saini hivi karibuni kati ya Mwakilishi mkazi Unesco nchini Bi. Zulmira Rodrigues na Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania, Bw. Mike Seo katika hafla iliyofanyika ofisi za UNESCO.
Kijiji hicho kitakuwa na shule yenye Tehama ikiwa na maunganisho ya intaneti, kiliniki ya kisasa ikiwa na kituo cha teknolojia ya mawasiliano yenye kuwezesha utabibu (telemedicine) na jenereta linalotumia nguvu za jua kwa ajili ya kijiji hicho.
Utiaji saini huo ulioshuhudiwa na Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, bi. Leah Kihimbi kutoka wizara ya habari, vijana, utamaduni na michezo na Dkt. N. Iriya kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO) Dar es Salaam na wafanyakazi wa UNESCO.
Katika hafla hiyo Bi. Rodrigues amesema kwamba mradi huo utawezesha UNESCO kuwapatia vijana wa Kimasai elimu kutokana na ukweli kuwa kwa utamaduni na kazi zao za ufugaji wamekuwa wakipata shida ya kupata elimu.
DSC_0002Baadhi ya wafanyakazi wa UNESCO na Samsung wakifuatilia kwa umakini hafla hiyo fupi ya kutiliana saini makubaliano baina ya Samsung Tanzania na UNESCO.
“Kupitia kijiji hiki vijana wataendelea na masomo hata kama wanachunga mifugo yao”, alisema Bi. Rodrigues.
Naye Mkurugenzi wa Samsung Electronics nchini Tanzania miongoni mwa manufaa makubwa yatakayopatikana katika mradi huo wa kijiji cha digitali huko Loliondo ni kuweza kupata nishati rahisi na iliyo rafiki kwa mazingira.
Alisema kwamba Afrika imekuwa mstari wa mbele katika uanzishaji wa vijiji vya digitali. Aidha kwa kitendo hicho Afrika inaonesha dunia ni kwa namna teknolojia inaweza kutumika kuleta mabadikliko chanya yanayotakiwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi waliopo vijijini.
Bi Leah Kihimbi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya habari,vijana, utamaduni na michezo, alisema kupitia vijiji vya digitali itawezekana kutekeleza program ya elimu kwa watu wanaoishi Loliondo huku tamaduni zao zikihifadhiwa.
Kijiji hicho cha Loliondo kitakuwa cha nne katika vijiji vya kidigitali barani Afrika. Inatarajiwa kwamba kijiji kingine kitajengwa mjini Zanzibar kwa ushirikiano wa UNESCO na Samsung Electronics mwaka 2015.
Untitled 1 
Pichani ni muonekano wa mchoro wa kijiji hicho utakavyokua.

Nyalandu amteua RC Singida Mwenyekiti wa Kikos kzi alichouunda jana.

images 
Waziri wa Maliasili na utalii Lazaro Nyalandu amemteua Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Paseko Kone kuwa Mwenyekiti wa Kikosi kazi kitachofuatilia uundwaji wa chama cha wafuga nyuki hapa nchini.
Nyalandu alimteua Mkuu wa Mkoa huo kwa kuwa amekuwa mstari wa mbele katika kuwasaidia wafugaji wa nyuki katika mkoa wake wa Singida bila kuchoka.
Waziri Nyalandu alitoa uamuzi huo wakati akifuga kongamano la ufugaji nyuki la Afrika lililomalizika Jijini Arusha jana.
Wajumbe Wengine walioteuliwa katika kikosi kazi hicho ni Juma Shaban Mgoo ambaye atakuwa katibu wa Kikosi kazi hicho na pia ni  Mtendaji Mkuu,wakala wa Huduma za Misitu Tanzania na ambaye alikuwa mkamu mwenyekiti wa Kongamano atakuwa mjumbe katika Kikosi kazi hicho,wengine ni Ester Mkwizu Mjumbe.
Wajumbe wengine ni mwakilishi wa wafugaji nyuki ,mwakilishi wa wasomi na watafiti ili kikosi kazi kiwe na mchanganyiko wa pande zote.
Walioteuliwa wote watapaa barua jumatatu kwa ajili ya kuthibitisha uteuzi wao,ambapo waziri nyalandu alieleza kuwa kuwa uteuzi huo wa wajumbe wanaounda kikosi kazi cha kushughulikia uundwaji wa chama cha wafuga nyuki ni agizo lililotolewa na Waziri Mkuu wakati wa ufuguzi wa Kongamano la nyuki kuwa ipo haja ya kuundwa kwa chama cha wafugaji nyuki ili kiweze kuwaunganisha wafugaji wote ndani ya nchi na kuwa na mtandao mmoja wenye nguvu na sauti.
Katika hotuba yake alieleza jinsi Tanzania ilivyojithatitia kuhakikisha inainua ufugaji nyuki na sekta ya nyuki ili kuwapita nchi ya Ethiopia ambayo ndiyo kinara cha nyuki cha Ufugaji nyuki Afrika.
Akasema kongamano hili ni la kwanza kufanyika katika ardhi ya Tanzania  na limesaidia sana katikakuwafumbua macho watanzania hasa wafugaji nyuki hasa katika masuala muhimu yaliyosisitizwa katika mada zilizojadiliwa kwenye kongamano hilo yatasaidia kukuza sekta ya ufungaji nyuki hapa nchini.
Kongamano hilo lililojumuisha washiriki wapatao 550 kutoka katika mataifa ya Ghana,Ethiopia,Zimbabwe, Afrika kusini,Camerun,Sudani,Kenya,Uganda na Rwanda.
Washiriki wengine walitoka katika nchi ya Kanada,Marekani,Pakstan,Namibia,Misri, Zambia,Ubelgiji,Uturuki na mengine.limekuwa la kufana sana,mada 88 zilikuwepo,mada 45 zilijadiliwa,katiyake mada 26 zilihusu tafiti za nyuki,mada 17 zilijadiliwa kwa wafugaji nyuki.
Awali akimkaribisha waziri Nyalandu Mwenyekiti wa Kongamano hilo SelestinKisimba alieleza kuwa katika kongamano hilo wameondoka na mapendekezo sita mambyo wataenda kuyafanyia kazi mara moja ili kuinua sekta ya nyuki.
Baadhi ya Mapendekzo hayo ni kuwa ufugaji nyuki lazima uweb endevu kwa manufa ya wafugaji wote,,umuhimu wa ufugaji nyuki na maendeleo,tatizo la ukosefu wa mitaji,uendelezaji wa rasilimali zilizopo , kuongeza uzalishaji wa thamani ya asali,ambapo mapendekezo hayo yatasaidia kuboresha ufugaji nyuki.
Washiriki wamepata nafasi ya kutembelea maeneo ya ufugaji nyuki katika mikoa ya Singida,Dodoma na Ngorogoro Mkoani Arusha kuweza kujifunza na kuona hali halisi ya mazingira yalivyo hasa katika maeneo yanayofugwa nyuki.

No comments:

Post a Comment