TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, November 9, 2014

MWANZA WAIKUBALI WINDHOEK WAFURAHIA MPANGO WA MABIBO BIA KUJENGA KIWANDA

 Wadau wa Windhoek ndani ya Villa Park Resort 
katika promosheni hiyo.
 Hapa shughuli imepamba moto waalikwa wakimsikiliza Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr.James Rugemalira.
 
Dotto Mwaibale
WAKAZI wa jiji la Mwanza na mikoa jirani ya Kanda ya Ziwa, wamefurahishwa na uwekezaji unaotarajiwa kufanywa na Kampuni ya Bia ya Mabibo (MBL) kwa ajili ya kujenga kiwanda cha bia za Windhoek.
Wakizungumza katika promosheni iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza juzi katika  ukumbi wa Villa Park Resort, wanachi hao walionesha kuguswa na uwekezaji huo na kushauri kijengwe kiwanda hicho jijini Mwanza.
Walisema kujengwa kwa kiwanda hicho kutachochea kasi ya maendeleo  ya kiuchumi na kuongeza ajira kwa vijana wa Kanda ya Ziwa.
Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr James Rugemalira alisema lengo la kufika Mwanza ni kupata mawazo mapya na ushauri wa nini kifanyike katika uwekezaji huo jijini humo.
“Tumeamua tuje Mwanza na kuomba ushirikiano wenu na rai yangu ni kupata maoni yenu ili tukipata fursa tuwe na viwanda vidogo vidogo,lakini si sawa na Tanzania Breweries (TBL),maana hatuwezi kushindana nao,” alisema Rugemalira.
Alisema ushindani wa haki ni lazima kila mtu apate haki ya kushinda,na wataka waweke misingi hiyo kwanza katika mikoa ya Mwanza, Kagera, Mbeya na Mtwara kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo.
Aliwataka wananchi wa kanda ya ziwa kuwaonesha  na kuwaunga mkono ili wazalishe kinywaji cha windhoek Mwanza badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi kama ilivyo sasa,ambapo kinywaji hicho kinagizwa kutoka nchini Namibia.
“Mtu anaweza kunipa ushauri au akaniamuru atakavyo ili nijitambue na ni vema kukubaliana na ushindani  bila hivyo hatuwezi kupata maendeleo na malengo ya kampuni yetu ni kushirikiana na serikali kukabiliana na uhaba wa ajira kwa Watanzania kwa kujenga viwanda hivyo ”alisema Rugemalira.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Mabibo Bia (MBL), Kanda ya Ziwa, Godfrey Mwangungulu alisema Bia ya Windhoek imewahi kushinda medali za juu saba  kwa ubora Barani Afrika tangu ianze kuzalishwa mwaka 1920.
 
“Bia ya Windhoek ilishinda tuzo hizo mfufulizo kuanzia mwaka 2007, 2008, 2009,2010,2011,2012  na 2013. 

No comments:

Post a Comment