TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, November 15, 2014

Rais Kikwete atoka Hospitalini Baada ya KUPATA NAFUU

 unnamed.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete  akisindikizwa na Daktari Bingwa
Edward Schaeffer kutoka
Hospitali ya Johns Hopkins alipokuwa amelazwa baada ya kufanyiwa
upasuaji wa kuondoa tezi dume mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya
kupata nafuu.Kulia nia Mke wa Rais Mama Salma Kikwete. Hali ya Rais Kikwete imezidi kuimarika baada ya kutoka wodini na kuwa mapumzikoni akiuguza kidonda kilichotokana na upasuaji aliofanyiwa, kabla ya kwenda kuondolewa nyuzi siku chache zijazo. Huku akiendelea kufanya mazoezi kila siku, Rais Kikwete pia ameendelea kupokea salamu za Watanzania kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kila pembe ya dunia pamoja na salamu za kumtakia nafuu mapema kutoka kwa viongozi mbalimbali wakiwemo mabalozi na wawakilishi wa nchi za nje. Naye amekuwa akizijibu kwa kadri anavyoweza.
1Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Daktari Edward Schaeffer
muda mfupi baada ya kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya Johns
Hopkins huko Baltimore, Maryland nchini Marekani ambapo alifanyiwa
upasuaji wa kuondoa tezi dume mwishoni mwa wiki iliyopita. Hali ya
Rais Kikwete imezidi kuimarika baada ya kutoka wodini na kuwa mapummzikoni akiuguza kidonda kabla ya kwenda kuondolewa nyuzi siku chache zijazo. Huku akiendelea kufanya mazoezi kila siku, Rais Kikwete pia ameendelea kupokea salamu za Watanzania kwa njia ya ujumbe mfupi (SMS) kutoka kila pembe ya dunia pamoja na salamu za kumtakia nafuu mapema kutoka kwa viongozi mbalimbali wakiwemo mabalozi na wawakilishi wa nchi za nje. Naye amekuwa akizijibu kwa kadri anavyoweza  (Picha naFreddy Maro)

No comments:

Post a Comment