TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Thursday, November 13, 2014

MTOTO ANYONGWA BILA HURUMA ENEO LA MAJOHE DAR ES SALAAM

 Mtoto Nuru kabla yakufikwa na umauti pichani alipo kuwa na miaka 3.Mtoto huyo anadaiwa kunyongwa  Alhamisi iliyopita na kuzikwa katika Makaburi ya Majohe kwa Muslim   (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA BILALI) Mmiliki wa Blog ya UJIJIRAHAA.
 Nguo ya Mmtoto huyo alio kua ameivaa kabla ya kunyongwa kinyama .
 Hii ni Mipira ya kuvaa mikononi iliyotumika kuubeba Mwili huo.
 Mama wa marehemu Nuru  Mohamedi , ambaye ni Sauda Ally.  akiwa amelala kutokana na kuishiwa nguvu mwilini kwa kufikwa na tukio hilo.  wakati  akiongea  na mwandishi wa habari.
 Mama wa marehemu Nuru  Mohamedi , ambaye ni Sauda Ally (wakwanza kushoto). akiongea kwa shida  na mwandishi wa habari, Nyumbani kwa Mama  huyo leo Dar es Salaa eneo la Majohe.




 Familia ya mtoto Nuru Mohamed (7) pichani  juu,  wakitoka nje baada ya kumuonyesha mpiga picha wa Gazeti la  sehemu iliyopo ndani ya pagala alipouawa mtoto huyo kwa kuwekewa matofari juu ya  mtu asiyejulikana Alhamisi jioni eneo la Majohe Kichangani, Ukonga, Dar es Salaam.
Pagala la Nyumba hilo lipo barabarani.

WAZIRI MUHONGO AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS WA MCC

8
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akisistiza jambo katika kikao baina ya Makamu wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan (wa pili kushoto) na ujumbe wake akiwemo Balozi wa Marekani nchini Mark Childress(wa kwanza kushoto). Wengine wa kwanza ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava na watendaji wa Wizara,na wa taasisi za Wizara wakifuatilia kikao hicho.
9Makamu wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan ( wa kwanza kushoto ) akimweleza jambo Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (wa kwanza kulia) anayesikiliza katikati ni Balozi wa Marekani nchini, Mark Childress mara baada ya kikao hicho.
11Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospter Muhongo katikati) katika picha ya pamoja ofisini kwake na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan (kushoto) na Balozi wa Marekani nchini , Mark Childress (Kulia)..
……………………………………………………………………
Na Asteria Muhozya, Dar es Salaam Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amekutana na Makamu wa Rais wa Mfuko wa Changamoto za Millenia (MCC) Kamran Khan na Ujumbe wake akiwemo Balozi wa Marekani nchini Mark Childress, katika kikao kilicholenga kujadili maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa MCC Awamu ya pili na masuala ya kuendeleza sekta ya nishati nchini. Kikao hicho kimezihusisha pia taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na Madini ikiwemo, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania (TGDC) pamoja na taasisi nyingine za Serikali ikiwemo Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (EWURA). Katika kikao hicho, Profesa Sospeter Muhongo amezitaka taasisi hizo kutekeleza miradi hiyo kwa kasi zikizingatia suala la uwajibikaji, ubunifu, uwazi na kuongeza kuwa, miradi hiyo itatekelezwa bila kuwepo na mazingira ya rushwa , huku akisisitiza ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi katika uendelezaji wa miradi hiyo. Kwa upande wake Makamu wa Rais wa MCC, Kamran Khan ameahidi kutoa ushirikiano kwa Wizara katika kutekeleza miradi hiyo ambayo inalenga kuhakikisha kuwa Tanzania inakuwa na umeme wa uhakika na wa kutosha. Kwa upande wake Balozi wa Marekani nchini Mark Childress amesisitiza suala la kuzingatia muda katika utekelezaji wa miradi hiyo na kuongeza kuwa, hakuna sababu itakayokwamisha miradi hiyo.

Rangers vs Majimaji Karume kesho

Mwandishi Wetu
index
KIKOSI cha timu ya Friends Rangers, kesho kinajitupa kwenye Uwanja wa Karume kuvaa na timu ya MAjimaji ya Songea, katika mchezo wa

Ligi Daraja la kwanza.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa timu hiyo Asha Kigundula, alisema kuwa
wanatarajia kuona upinzani mkali kutoka katika timu hiyo ambayo  mpaka sasa ndiyo inaongoza
ligi, wakati wao wakishika nafasi ya pili.
Kigundula alisema kuwa kikosi chao tayari kipo kambini kikijiandaa na mchezo huo, huku
kocha wao Ally YUsuph ‘Tigana’ akijipanga kuhakikisha pointi tatu zinabaki nyumbani.
PIa Kigundula amewataka wapenzi kujitokeza kwa wingi kuipa ushirikiano timu yao ambayo
inapambana kuhakikisha inapanda daraja msimu ujao.
“Kikubwa tukipata ushirikiano kwa wapenzi ambao wamekuwawakijitokeza kutushangilia mwanzo
mwisho tunaomba mjitokeze kutushangilia tufanye vizuri”alisemaKIgundula
Rangers ina pointi 16, baada ya kucheza mechi 8 huku wanaoongozawakiwa Majimaji
wakitofautiana kwa pointi mbili, endapo Rangers itashinda itakuwa ikiongoza kwa tofauti ya pointimoja.
Ikiwa imeshinda mechi nne na kutoka sare mechi nne , huku ikiwa inakimbizana na Majimaji ambayo nayo ina pointi 15.

NHC yavutia uwekezaji kongamano la uwekezaji JNICC

Naibu
Waziri wa Fedha, Adam Kighoma Malima akifungua kongamano la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) lililolenga kukuza na kuvutia uwekezaji kutoka kwa makampuni na
taasisi mbalimbali kubwa za kimataifa katika sekta za Uendelezaji
Miliki, Kilimo na Usafirishaji. (Picha Zote za Kitengo cha Mawasiliano
kwa Umma na Huduma kwa Jamii cha Shirika la Nyumba la Taifa)
Meneja waUendelezaji Biashara wa NHC, William Genya akijadiliana jambo na washiriki wa kongamano hilo

Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu akitoa
mada kwenye kongamano la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo, lililolenga kukuza na
kuvutia uwekezaji kutoka kwa makampuni na taasisi mbalimbali kubwa za
kimataifa katika sekta za Uendelezaji Miliki, Kilimo na Usafirishaji.
 
 
Mkurugenzi wa Ukusanyaji Mapato wa Ofisi ya Rais, Usimamizi na Utekelezaji wa Miradi (PDB), Bw. Lawrence Mafuru ambao ndio wandaaji wa kongamano hilo akizungumza  kwenye
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo,
kongamano hilo limelenga kukuza na kuvutia uwekezaji kutoka kwa
makampuni na taasisi mbalimbali kubwa za kimataifa katika sekta za
Uendelezaji Miliki, Kilimo na Usafirishaji.
Baadhi
ya washiriki waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.
 Baadhi
ya washiriki waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.

 Baadhi
ya washiriki waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, DkShaban Mwinjaka, Naibu
Waziri wa Fedha, Adam Kighoma Malima na Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison
Mwakyembe wakifuatilia mada katika kongamano la uwekezaji lililoandaliwa
na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo.

Naibu
Waziri wa Fedha, Adam Kighoma Malima na Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison
Mwakyembe wakifuatilia mada katika kongamano la uwekezaji lililoandaliwa
na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo.
Mkurugenzi
Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Bi Julieth Kairuki akitoa mada kwenye
kongamano la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa
(Big Results Now) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa
cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo, lililolenga kukuza na kuvutia uwekezaji
kutoka kwa makampuni na taasisi mbalimbali kubwa za kimataifa katika
sekta za Uendelezaji Miliki, Kilimo na Usafirishaji.
Mtendaji
Mkuu wa Investment Capital Group (ICG), Shose Sinare na baadhi ya
washiriki wengine waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.
Mkurugenzi wa Ukusanyaji Mapato wa Ofisi ya Rais, Usimamizi na Utekelezaji wa Miradi (PDB), Bw. Lawrence Mafuru na washiriki
wengine waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji lililoandaliwa
na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika
Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo.
 Baadhi
ya washiriki waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.
 
 
 
 Naibu Waziri wa Fedha, Adam Kighoma Malima akizungumza na waandishi wa habari, wakati wa kongamano hilo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akizungumza na waandishi wa habari kwenye kongamano hilo.

Baadhi ya washiriki waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.

Baadhi ya washiriki waliokuwapo katika kongamano hilo la uwekezaji
lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na
kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere
(JNICC) leo.
Maafisa NHC  Clara Lumbanga, Fatima Rajabu na Bulla Boma wakifuatilia mada katika
kongamano hilo la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo Makubwa
Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano cha
Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo.
 
 Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Kyando Mchechu akitoa
mada kwenye kongamano la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo, lililolenga kukuza na
kuvutia uwekezaji kutoka kwa makampuni na taasisi mbalimbali kubwa za
kimataifa katika sekta za Uendelezaji Miliki, Kilimo na Usafirishaji.
 
Mkurugenzi
Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa NHC, David Shambwe akifuatilia
kwa makini kongamano la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika Kituo cha Mikutano
cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo, lililolenga kukuza na
kuvutia uwekezaji kutoka kwa makampuni na taasisi mbalimbali kubwa za
kimataifa katika sekta za Uendelezaji Miliki, Kilimo na Usafirishaji.
 
 Maafisa
wa NHC  nje ya kongamano la uwekezaji lililoandaliwa na Mpango wa
Matokeo Makubwa Sasa (Big Results Now) na kufanyika katika Kituo cha
Mikutano cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere (JNICC) leo, lililolenga
kukuza na kuvutia uwekezaji kutoka kwa makampuni na taasisi mbalimbali
kubwa za kimataifa katika sekta za Uendelezaji Miliki, Kilimo na
Usafirishaji.
 Mkurugenzi
Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu akiwa katika
majadiliano ya kina na baadhi ya washirikia walioonyesha nia ya
kuwekeza katika miradi ya NHC.
Afisa Uendelezaji Biashara NHC, Fatima Adadi Rajabu akijadiliana jambo na Mtendaji Mkuu wa Investment Capital Group (ICG), Shose Sinare
 
Afisa Masoko wa NHC, Mariam Ndabagenga akijadiliana jambo na washiriki wa kongamano hilo 
Mkurugenzi Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wa NHC, David Shambwe akijadiliana jambo mmoja wa washiriki wa kongamano hilo

Taasisi ya Starkey Hearing Foundation yakabidhi madarasa matatu shule ya msingi ya Loiborsoit

1Mwanzilishi wa Taasisi ya Starkey Hearing Foundation, Bill Austin pamoja na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wakifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa majengo matatu ya shule ya Msingi ya Loiborsoit yaliyojengwa na mwanzilishi huyo kwa ajili ya jamii ya Kimasai katika sherehe zilizofanyika eneo hilo wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara jana.David na steven
2 3Mwanzilishi wa Taasisi ya Starkey Hearing Foundation, Bill Austin akipima sikio kwa mmoja wa watoto waliohudhuria kliniki iliyokwenda sambamba na ufunguzi rasmi wa majengo matatu ya shule ya Msingi ya Loiborsoit yaliyojengwa na mwanzilishi huyo kwa ajili ya jamii ya Kimasai katika sherehe zilizofanyika eneo hilo wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara jana.
4Mwanzilishi wa Taasisi ya Starkey Hearing Foundation, Bill Austin pamoja na Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wakifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa majengo matatu ya shule ya Msingi ya Loiborsoit yaliyojengwa na mwanzilishi huyo kwa ajili ya jamii ya Kimasai katika sherehe zilizofanyika eneo hilo wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara jana.
5Mwanzilishi wa Taasisi ya Starkey Hearing Foundation, Bill Austin pamoja na mkewe, Tani wakipokelewa na wanakikiji wa Loiborsoit kwenye ufunguzi rasmi wa majengo matatu ya shule ya Msingi ya Loiborsoit yaliyojengwa na mwanzilishi huyo kwa ajili ya jamii ya Kimasai katika sherehe zilizofanyika eneo hilo wilayani Simanjiro mkoa wa Manyara jana.Kulia ni David Furnish mmoja wa wageni maarufu aliyehudhuria hafla hiyo.Yohana shinini
7Wanafunzi wa darasa la kwanza wa Shule ya Msingi Loborsoit iliyopo Simanjiro wakiwa darasani huku timu ya Taasisi ya Starkey Hearing Foundation wakiwa nyuma yao wakati wa kukabidhiwa majengo hayo katika sherehe iliyofanyika Wilayani Simanjirojana..
9 11a
unnamed1Wakiwa katika picha ya pamoja  unnamed2Wakurugenzi wa Kampuni ya Montage Nesto Mapunda na Teddy Mapunda wakiwa katika picha ya pamoja  unnamed3Mkurugenzi wa Kampuni ya Montage Teddy Mapunda akishuka kwenye helkopeta iliyowachukua wakuu wa taasisi ya Starkey Hearing Foundation

MWILI WA MAREHEMU ROBERT LENGEJU WAAGWA JIJINI DAR ES SALAAM KUZIKWA KESHO KIPERA MOROGORO.

Hili ndilo sanuku lililouhifadhi mwili wa Mwandishi/Mchambuzi wa Jukwaa Maalumu la MWALE WA DEMOKRASIA katika Gazeti la Raia Tanzania (Gazeti dada
la Raia Mwema),
kila Alhamisi. Mwili wa shujaa huyo wa Demokrasia uliswaliwa katika Kanisa Katoliki M
Watu mbalimbali walihudhuria katika misa hiyo ya kumsindikiza Lengeju katika safari yake ya mwisho kabla ya maziko yatakayo fanyika kesho (Novemba 13,2014) Kijijini kwako Kipera, Kata na Tarafa ya Mlali, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro. Na Mroki Mroki-Father Kidevu Blog.
 Ndugu wa marehemu Robert Lengeju wakitoa heshima za mwisho kwa mwili wa mdogo wao.
Heshima za mwisho ziliendelea kutolewa na ndugu jamaa na marafiki.
Godfrey Dililunga kutoka kampuni ya Raia Mwema wachapaji wa gazeti la Raia Mwema na Raia Tanzania akitoa heshima za mwandishi huyo wa Makala za Mwale wa Demokrasia katika gazeti lao.
Mhariri wa Raia Mwema, Ezekiel Kamwaga akitoa heshima kwa mwili wa marehemu.
Waombolezaji wakipita kutoka heshima za mwisho.
Mkuu wa Mkoa wa Mstaafu, Isdore Shirima nae alikuwepo kutoa heshima za mwisho kwa Lengeju.
Waombolezaji
wanakwaya wakiimba katika misa hiyo.
wanafamilia wakiwa Kanisani katika misa.
Wanafamilia, ndugu jamaa na marafiki wakiwa katika misa hiyo leo.
 Kaka wa Marehemu Charles Lengeju akiwa amebeba msalaba wa marehemu.
Gari lililobeba mwili wa marehemu Robert Lengeju likiwa tayari kwa safari ya Kipera Mkoani Morogoro.

KAMPUNI YA MABIBO BIA NA JESHI LA POLISI WAFANYA SEMINA SHIRIKISHI MKOANI MOROGORO

Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi, Ramadhan Abdul Mambea (kulia), naye akichangia jambo kwenye semina hiyo.
 Kaimu Meneja Mkuu wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Eustadius Mutabingwa (kulia), naye alichangia uzoefu wake katika semina hiyo.
 Mkurugenzi wa Maghala na Usalama wa Kampuni ya Mabibo Bia (MBL), Boniface Katanyebile naye alikuwa katika semina hiyo akifuatilia kila jambo lililokuwa likijadiliwa.
 Wadau wakiwa katika semina hiyo.
 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Bia ya Mabibo (MBL), Respicius Didace akitoa historia fupi ya kampuni ya Mabibo na mambo mbalimbali ya kisheria kuhusu utii wa sheria bila shuruti.
 Ofisa Mnadhimu wa Jeshi la Polisi, SSP Gemin Mushy (kushoto) na Mshauri wa Kampuni ya Mabibo, Kamala Stephen wakifuatilia mada katika semina hiyo.
………………………………………………………………………..
 
Dotto Mwaibale
 
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imesema ni kosa kisheria kwa mtu kukutwa akiuza bidhaa au vinywaji vilivyosamehewa kodi na serikali vinavyouzwa majeshini.
 
Hayo yalisemwa na  Ofisa Mwandamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mkunga Tuwaha wakati akitoa mada kwenye semina shirikishi kati ya Jeshi la Polisi na Kampuni ya Bia ya Mabibo iliyofanyika Top Life Hoteli mjini Morogoro leo asubuhi iliyohusu kujadili mambo mbalimbali ya jeshi hilo na utii wa sheria bila shuruti.
 
“Vinywaji na bidhaa zingine zenye msamaha wa kodi hasa katika majeshi yetu ni vema zikatumika kwa ajili ya askari na familia zao na si mtu mwingine” alisema Tuwaha.
Semina hiyo ilishirikisha askari wa jeshi hilo ambao ni mameneja wa kantini kutoka  mikoa ya Njombe, Tanga, Dodoma, Morogoro, Tanga na Dar es Salaam na kudhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Mabibo. (Imeandaliwa na mtandao wa 
www.habari za jamii.com-simu namba 0712727062)

WANASHERIA MWANZA WAIFAGILIA WINDHOEK WASEMA NI BORA KWA AFYA

Wanasheria wa jiji la Mwanza wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Mwanasheria Mtalemwa (wa pili kushoto), akiwa na wanasheria wenzake  wakifurahia Windhoek.
Kikao na hafla vikiendelea.
…………………………………………………………………………….
 
Dotto Mwaibale
 
BAADHI ya Wanasheria wa jiji la Mwanza wamesema unywaji wa bia ya Windhoek utasaidia kujenga afya za wanywaji kwani imetengenezwa kwa ubora wa juu ukilinganisha na bia zingine.
 
Wanasheria hao waliyabainisha hayo jijini Mwanza katika hafla fupi iliyoandaliwa na Kampuni ya Bia ya Mabibo kwa ajili ya kujua changamoto mbalimbali kutokana na soko la bia za Windhoek na Windhoek Draught na kupata maoni ya wadau wa vinywaji hivyo  iliyofanyika jijini humo mwishoni mwa wiki.
 
Mmoja wa wanasheria hao,   alisema kwa muda mrefu na familia yake amekuwa akitumia Windhoek na ajawahi kupata shida yoyote  kwani inachangamsha akili tofauti na bia zingine.
 
Bia hii haiwezi kumfanya mtumiaji ajisikie vibaya hata akinywa kiasi kikubwa na ndio maana mimi na wenzangu tunatumia bia hizi za windhoek.
 
“Iwapo tutajenga tabia ya kunywa bia hii hakika utafanya kazi zetu kwa uhakika hata tukiwa makazini kwani haitoi harufu mdomo na kulewesha ni vizuri  tukaiunga mkono Kampuni ya Mabibo Bia ” alisema Mwanasheria huyo.
 
Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr James Rugemalira aliwaomba wanamwanza kuiunga mkono Kampuni ya Mabibo Bia kwa kununua vinywaji vyake kwani mpango wa kampuni hiyo ni kujenga kiwanda ambapo kitakuza uchumi wa mkoa wa Mwanza na kutoa ajira kwa vijana.
 
“Hatuwezi kukamilisha ndoto zetu za kujenga kiwanda bila ya nyinyi kutuunga na kupata mrejesho mzuri wa mauzo ya bidhaa zetu tuungeni mkono kwa kununua Windhoek Lager na Windhoek Draught zenye namba ya MB66 ubavuni ambazo ndizo halali katika soko la Tanzania na si vinginevyo” alisema Fr James. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Washiriki wa Kongamano la Ufugaji nyuki Afrika washauri kutumia mizinga ya udongo

unnamed
Mshiriki katika kongamano akiendelea kujifunza namna ya ufugaji nyuki kutoka Halmashauri ya Mpanda Mkoani Katavi wakati wa kongamano la Ufugaji nyuki la Afrika jijini Arusha ambapo banda la Halmashauri ya Mpanda lawa kivutio kwa washiriki hasa asali safi ya nyuki wadogo na wakubwa iliyotokea kupendwa na kuwavutia washiriki wengikwenye kongamano.
(Picha Na Kibada Kibada -Arusha.)
………………………………………………………………………………………………..
Kibada Kibada-Arusha.
Washiriki wa Kongamano  la Ufugaji nyuki Afrika linaloendelea kwenye ukumbi  wa mikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha wameshauri kuona  uwezekano wa kutumia mizinga iliyotengenezwa kwa udongo  ambayo ni rafiki wa mazingira ili kuepeusha uharibifu wa mazingira unaoweza kujitokeza kutokana na matumizi ya mizinga inayotengenezwa kwa kutumia miti.
  mama wengi nchini Zambia wanaofuga nyuki kwa kutumia mizinga iliyotengenezwa kwa udongo katika kuhifadhi mazingira.
Akichangia katika kongamano hilo Afisa nyuki kutoka Tanzania ambaye ni mmoja wa washiriki kwenye kongamano hilo MR Rupia alieleza uzoefu wake alioupata kutoka nchini Zambia alipotembelea kujifunza masuala ya ufungaji nyuki  ambapo akina mama wengi nchini Zambia wanaofuga nyuki wanatumia  mizinga iliyotengenezwa kwa udongo katika kuhifadhi mazingira na  robo tatu ya wananchi wa Zambia wanaojishughulisha na ufugaji nyuki ni akina mama na watumia ufugaji nyuki wa mizinga iliyotengenezwa kwa udogo ili kuokoa mazingira na katika hilo  wamefanikiwa kuhifadhi mazingira.
Rupia akaeleza kuwa wanaumekatika nchi ya Zambia  ni wachache sana wanaojishughulisha na ufugaji nyuki kwa kuwa teknolojia inayotumika imekuwa rafiki zaidi kwa wanawake katika uhifadhi wa mazingira ndiyo maana wanawake wengi wanajihusisha na ufugaji nyuki kwa kutumia mizinga iliyotengenezwa kwa udogo kwa kuwa inasaidia kutochangia  uharibifu wa mazingira.
Akashauri hapa nchini Tanzania elimu na  hamasa ianze  kutolewa kwa wafugaji nyuki ili kufuga nyuki kwa kutumia mizinga iliyotengenezwa kwa udogo kwani itasaidia sana katika uhifadhi wa mazingira kwa kuwa itakuwa inatumia udongo kuliko kukata miti na kutengeneza mizinga  ya miti.
A wali wawasilishaji wa mada katika kongamano hilo waliwasilisha  mada mbalimbali baadhi ya mada    iliyohusu kupanua wigo wa mazao ya nyuki Tanzania iliyowasilishwa na Linus Gedi kutoka Tanzania,kuelewa ufugaji nyuki katika misitu na kuzingatia mfumo endelevu wa matumizi ya ardhi iliyowasilishwa na Janeth Lowore kutoka Uingereza,Athari za mabadiliko ya tabia nchi katika ufugaji nyuki, kwa kuzingatia utafiti uliofanyika Mkoa wa Kigoma iliyowasilishwa na Seif Salum kutoka Tanzania,
Mada nyingine ni mabadiliko ya Tabia nchi na tofauti zinazojitokeza katika ufugaji nyuki katika wilaya ya Kiteto Mkoani Arusha  na hatua za kukabiliana na athari hizo,muhtasari wa Hali ya Misitu na udhibiti wa moto wa nyika nchini Tanzania iliyowasilishwa na Gerald Otieno kutoka Tanzania pamoja na ile iliyohusu Sababu za zinazochangia ushiriki hafifu wa wanawake na Vijana katika Tasinia ya ufugaji nyuki kwa kuzingatiastadi iliyofanyika mkoani kigoma iiliyowasilishwa na Dkt Angela Mwakatobe kutoka Tanzania ambayo ilionekana kuwa na ushawishi mkubwa kwa washiriki.,
Kongamano hilo la wafuga nyuki la Afrika   lilifunguliwa na waziri Mkuu Mizengo Pinda  kwa kuwashauri wafugaji nyuki watumie nafasi hiyo  kupata uzoefu kutoka kwa wafugaji tofauti ndani na nje ya nchi hasa wa Bara la Afrika katika.Kauli mbiu ya Kongamano hilo ni kufuga nyuki kuzingatia hifadhi ya mazingira na kukuza uchumi, lengo kuboresha sekta ya ufugaji nyuki Afrika na nchi zinazoendelea kwa ustawi wa wananchi hasa waishio Vijijini.

ZAIDI YA WANARIADHA ELFU KUMI NA TANO KUSHIRIKI UHURUMARATHON 2014

unnamed
Mratibu wa mbio za uhurumarathon 2014 Innocent Melleck katikati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam juu ya maandalizi yam bio hizo kwa mwaka huu ambapo zitafanyika 07/12/2014 na kuongozwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete huku Zaidi ya wanariadha elfu kumi na tano kukadiriwa kushiriki kwa mara ya kwanza.Kulia kwake ni Katibu mkuu wa shirikisho la riadha nchini Selemani Nyambui na kushoto ni mjumbe wa chama cha riadha mkowa wa Dar Es Salaam Tullo Chambo
………………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
 
ZAIDI ya wanariadha 15,000 kutoka ndani na nje wanatarajiwa kuthibitisha kushiriki katika mbio za Uhuru Marathon ambazo zinatarajiwa kufanyika Desemba 7 kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es Salaam.
 
Akizungumza jana jijini, Mratibu wa mbio hizo, Innocent Melleck, alisema kuwa maandalizi yako katika hatua za mwisho huku akimtaja Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, anatarajiwa kuongoa mbio hizo.
 
Melleck pia jana alikabidhi ada ya Sh. Milioni mbili kwa Chama cha Raidha Tanzania (RT) na Sh. Milioni moja kwa wenyeji Chama cha Raidha Mkoa wa Dar es Salaam (DAAA), ili kupata kibali cha kuendesha mbio hizo.
 
Mratibu huyo alisema kuwa fomu kwa ajili ya kushiriki mbio hizo zimeanza kutolewa jana na jijini zinapatikana katika maduka yote ya TSN, huku pia zikitolewa kwenye mikoa ya Arusha, Moshi mkoani Kilimanjaro na Leaders.
 
“Tunawashukuru wadau wote walioshiriki katika kujiandaa kushiriki mbio hizo hasa klabu za jogging ambazo zinahamasisha wanariadha kushiriki mbio hizo zenye kuhamasisha Amani, ushirikiano na mshikamano,” alisema Melleck.
 
Katibu Mkuu wa RT, Suleiman Nyambui, alisema kuwa chama kimeialika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani, nchi za Afrika Mashariki na mataifa mengine ambayo yako tayari kushiriki mbio hizo zitakazofanyika sambamba na sherehe za Uhuru wa Tanzania.
 
Nyambui alisema kuwa wanariadha wamejiandaa kuonyesha vipaji vyao na wanaamini yataendelea kukuza vipaji vyao kulitangaza jina la Tanzania.
 
Naye Mjumbe wa DAAA, Tullo Chambo, alisema kwamba chama kimeshiriki kuanzia hatua ya awali na wanawahakikishia wadau kuwa mbio za mwaka huu zitakuwa na mafanikio.
 
Chambo alisema kuwa wanazipongeza klabu na makundi yote yanayoendelea kujiandaa kushiriki mbio hizo na kila kitu kitafanyika kwa kufuata taratibu za kiufundi.
 
Melleck alitoa rai kwa makampuni na mashirika pia watu binafsi kujitokeza kwa wingi ili kuweza kudhamini mbio hizi kwani bado nafasi ipo kwa wale wote wenye nia ya kudhamini kwa mwaka huu
 
Mbio za Uhurumarathon kwa mwaka huu zinadhaminiwa na Kampuni ya Bia nchini TBL kupitia kinywaji chake Grandmalt,Maji ya Uhui,Azam Tv,Tbc 1,Mwananchi Communications Ltd,Magazeti ya Uhuru,Jambo Leo,Michuzi media,CxC  Africa,Kitwe General Traders,Samsung,Cokacola,Tindwa Mediacal Service,Gazeti la TABIBU,Konyagi,na TSN SUPERMARKETS.

VACANCY ANNOUNCEMENT

imagesP
ost Title: Research Director
Background The Ministry of Health and Social Welfare and the Drug Control Commission (DCC) in collaboration with the Centers for Disease Control and Prevention, Muhimbiili National Hospital, Mwananyamala Municipal Hospital and Temeke Municipal Hospital is implementing a program aim
ed at increasing coverage of people who use drugs (PWUDs) into medically assisted treatment (MAT) of opioid dependence with an ultimate goal of minimizing HIV infection among PWUDs. The program intends to achieve this goal through execution of innovative Key Population Implementation Science (KPIS) on Optimized Methadone Delivery with Take away Doses of Methadone. The initiative will be implemented with the financial support from the USA President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR) through the Centers for Disease Control and Prevention with technical assistance from a USA based PANGAEA Global AIDS Foundation.
The Ministry now invites applicants who are qualified, self motivated, dynamic, results oriented performer and committed individuals to fill the position of a Research Director. The incumbent will be part of the key population implementation science team of investigators.
Continue reading →

TAARIFA MBALIMBALI ZA KIMICHEZO KUTOKA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TFF

index17
KAMATI YA SHERIA YAPITISHA USAJILI SDL
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji imepitisha usajili wa Ligi Daraja la Pili (SDL) huku ikikata majina mawili ya wachezaji katika klabu za Abajalo ya Dar es Salaam na Magereza ya Iringa.
 Klabu hizo mbili zilisajili wachezaji 31 badala ya 30 ambapo ni kinyume na Kanuni ya 61(2) ya Ligi Daraja la Pili inayoruhusu klabu kusajili wachezaji wasiozidi 30 na wasiopungua 18.
 Wachezaji ambao Kamati ya Sheria iliyokutana jana (Novemba 11 mwaka huu) imewaondoa ni wale waliokuwa wameorodheshwa namba 31 katika usajili wa klabu hizo. Wachezaji hao ni Andrew Mathew Kazembe (Abajalo) na Joshua Omari (Magereza).
 Michuano ya Ligi Daraja la Pili inayoshirikisha timu 24 katika makundi manne ya timu sita kwa mtindo wa nyumbani na ugenini itaanza kutimua vumbi Novemba 22 mwaka huu.
 Wachezaji waliopitishwa katika kila klabu na idadi yao kwenye mabano ni Abajalo (30), Arusha FC (18), Bulyanhulu (28), Kariakoo (30), Kiluvya United (23), Magereza (30), Mbao (27), Milambo (29), Mji Mkuu (29) na Mkamba Rangers (30).
 Wengine ni Mpanda United (29), Mshikamano (28), Mvuvumwa (18), Njombe Mji (25), Pamba (24), Rwamkoma JKT (25), Singida United (26), Town Small Boys (22), Transit Camp (28), Ujenzi Rukwa (30), Volcano (25) na Wenda (20).
 Klabu zote zinakumbushwa kulipia na kuchukua leseni za wachezaji wao kabla ya ligi kuanza, kwani kwa mujibu wa kanuni hakuna mchezaji atakayeruhusiwa kucheza mechi ya ligi bila kuonyesha leseni yake. 
 WATANO WAUNDA JOPO KUHAKIKI UMRI COPA
Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeunda jopo la watu watano kuhakiki umri wa wachezaji watakaoshiriki hatua ya ngazi ya Taifa ya michuano ya Copa Coca-Cola 2014.
 Michuano hiyo ya ngazi ya Taifa itafanyika Dar es Salaam kuanzia Desemba 13 hadi 20 mwaka huu. Uhakiki wa umri utafanyika Desemba 11 na 12 mwaka huu wakati timu zote zinatakiwa kuwasili Shule ya Filbert Bayi mkoani Pwani kuanzia Desemba 10 mwaka huu.
 Jopo hilo la uhakiki linaongozwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Henry Tandau. Wengine katika jopo hilo ni Ally Mayay, Charles Boniface Mkwasa, Dk. Jonas Tiboroha na Richard Yomba.
 Timu 16 zitakazocheza michuano hiyo inayoshirikisha watoto wenye umri chini ya miaka 15 ni Arusha, Dodoma, Geita, Katavi, Kigoma, Kinondoni, Kusini Pemba, Kusini Unguja, Lindi, Mbeya, Mjini Magharibi, Morogoro, Mwanza, Ruvuma, Simiyu na Tanga.
 Vyama vya mpira wa miguu vya mikoa vinakumbushwa kutuma TFF fomu za usajili ambazo zinatakiwa kuambatanishwa vyeti vya kuzaliwa vya wachezaji husika.

TANESCO YASHINDWA KUWAUNGANISHIA UMEME WANANCHI WILAYANI MERU KWA MUDA MREFU

index
Mahmoud Ahmad Meru
Wananchi wa kata ya Seela\Sing’isi wilayani Arumeru mkoani Arusha wamelilalamikia shirika la ugavi wa umeme(TANESCO)kushindwa kuwaunganishia huduma ya umeme kwa muda mrefu sasa licha ya kulilipa shirika hilo fedha za kuunganishiwa umeme hali inayowaleta usumbufu wa mara kwa mara kuifuatilia huduma hiyo.
Kadhia hiyo imeibuliwa na mtandau huu  wakti lilipokuwa wilayani Meru baada ya wananchi kuelezea Kero mbalimbali wanazokumbana nazo katika kujiletea maendeleo yao na taifa kwa ujumla huku wakiliomba shirika hilo kutekeleza maombi yao ya kupatiwa huduma hiyo.
Wakionyesha Nakala za Mikataba yao na barua za Malalamiko walizopeleka kwa Meneja wa wilaya na mkoa wa shirika hilo la ugavi huku majibu yakinifu wakishindwa kuyapata na lini watapata huduma hiyo.
Mmoja ya wananchi hao aliyezungumza na mwandishi wa habari hii Khamis Juma alisema kuwa wana muda sasa karibu miezi mitano hawajapata huduma walioomba huku akifuatilia maeneo mbalimbali kujua wamekwamia wapi bila ya kupata majibu na teyari alikwisha lipia fedha za mkataba wa kuunganishiwa umeme.
Juma alionyesha barua ya Mkataba huo yenye kumb;USA\SL2 ya tarehe 136\2014 na kulipiwa siku hiyo hiyo na hadi leo takribani miezi mitano hajaungiwa umeme huku akifuatilia na kupewa majibu ya njoo kesho kutoka kwa watendaji wa shirika hilo la ugavi.
Suala la kuunganishiwa umeme kwenye baadhi ya kata wilayani humo limekuwa likiangaliwa kwa watu wenye nacho ambao wamekuwa wakitoa chochote kwa watendaji hao hali inayowafanya wasio naocho kukosa huduma hiyo kwa wakati.
Gazeti hili lilipomtafuta Meneja wa wilaya na mkoa kwa njia ya simu zaoa za mkononi  hawakuweza kupokea hata walipotumiwa ujumbe wa sms na mwandishi kujitambulisha bado hakukuwa na majibu.
Kwa upande wake dc wa wilaya hiyo Nyerembe Munasa Alisema kuwa Atalifuatilia suala hilo ili wananchi hao waweze kupata huduma yao ya msingi kwa ni haki yao na shirika linatakiwa kuwapa kwa wakati.

Serikali kudhibiti ukimwi kifikia maambukizi sifuri

 5Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho akimpongeza kijana Yohana Haule mwenye umri wa miaka 23 kwa kuchora nembo na kupata tuzo ya kimataifa ya AIDS.
3Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho akizungumza na wadau mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Serikali na wadau wa Ukimwi kupitia utekelezaji wa programu za ukimwi jana jijini Dar es Salaam.
2Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Florens Turuka akifungua Mkutano wa Serikali na wadau wa Ukimwi kupitia utekelezaji wa programu za ukimwi jana jijini Dar es Salaam.
1Mwenyekiti wa wadau wa Maendeleo kwenye sekta ya ukimwi Dkt. Michelle Roland akiwasilisha mada wakati wa Mkutano wa Serikali na wadau wa Ukimwi kupitia utekelezaji wa programu za ukimwi jana jijini Dar es Salaam.
6Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Florens Turuka aliyekaa katikati kwenye picha ya pamoja na Wadau mbalimbali walioshiriki Mkutano wa Serikali na wadau wa Ukimwi kupitia utekelezaji wa programu za ukimwi.
……………………………………………………………….
Na: Genofeva Matemu – Maelezo
Serikali imepanga mikakati na kusimamia juhudi zinazofanywa na kuendelezwa na wadau wa ukimwi kuhakikisha kuwa maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi yanapungua hadi kufikia sifuri ifikapo mwaka 2025.
Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti mtendaji kutoka Tume ya kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dkt. Fatma H. Mrisho wakati wa mkutano wa serikali na wadau wa ukimwi kupitia utekelezaji wa programu za ukimwi jana jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa mkutano huo Dkt. Mrisho amesema kuwa maambukizi ya ukimwi yamepungua ukilinganisha na miaka 10 iliyopita kwani idadi imepungua kutoka waathirika laki moja na elfu themanini hadi kufikia waathirika elfu sabini na mbili kwa sasa.
Akitoa mfano Dkt. Mrisho amesema kuwa Mkoa wa Njombe, Shinyanga, Dar es Salaam, Mbeya na Rukwa ni mikoa ambayo inaonyesha kuwa na idadi kubwa ya waathirika wa ukimwi hivyo kuwataka wadau wa ukimwi kutoka mikoa hiyo kutoa elimu ya kutosha kwa jamii ili kupunguza maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi pamoja na magojwa ya zinaa.
Akifungua mkutano huo, Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Dkt. Florens Turuka amesema kuwa serikali imedhamiria kuanzisha mfuko utakaokua unashughulikia masuala ya ukimwi wakati wa bajeti ya mwaka 2015/2016 wenye lengo la kuondoa maambukizi mapya ya ukimwi nchini.
Aidha Dkt. Turuka ameitaka jamii kutowanyanyapaa waathirika wa ukimwi bali wawapende na kuwapa moyo ili waendelee kuwa na afya bora kwani serikali inawapigania na kuhakikisha kuwa wanatumia dawa za kuongeza maisha ili kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Mkutano wa serikali na wadau wa ukimwi kupitia utekelezaji wa programu za ukimwi ulianzishwa mwaka 2003 ukifuatiwa na ule wa mwaka 2006 na kuendelezwa kila baada ya miaka miwili ambapo mkutano wa mwaka huu ni wa sita na umebeba kauli mbiu inayosema “Kwa yale mafanikio ambayo tumeyapata mpaka sasa tunayaendeleza”.

SHIWATA YALIA KUMPOTEZA AMIGOLAS

Amigolas_1001
Na Mwandshi Wetu
MTANDAO wa Wasanii Tanzania (SHIWATA)unaungana na watanzania kuomboleza kifo cha mwanamuziki maarufu Hamisi Kayumbu ‘Amigolas’ aliyefariki Jumapili na kuzikwa Jumatatu iliyopita katika makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Taalib alisema jana Dar es Salaam kuwa marehemu Amigolas atakumbukwa kwa mengi aliyoyafanya akiwa mwanachama wa mtandao huo alishiriki kutafuta eneo la makazi ya wasanii ya kijiji cha Mwanzega na shamba la wasanii lililopo Ngarambe wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani.
Alisema alikuwa kiongozi wa mstari wa mbele pale  alipowahamamisha wanamuziki wenzake kujiunga SHIWATA kutoka bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’akiwemo Luiza Mbutu,marehemu Abuu Semhando na wengine.
Marehemu Amigolas alifariki kwa ugonjwa wa moyo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (M.N.H) alipokuwa amelazwa kwa siku tano kabla mauti kumkuta Jumamosi saa tano usiku.
Mkurugenzi wa African Stars ‘Twanga Pepeta’, Asha Baraka aliyekuwa mwajiri wake kabla ya kuhamia bendi ya JKT Ruvu alisema marehemu alikuwa mwanamuzi aliyejituma na kufanya kazi kwa juhudi zote kutoka ajiunge na bendi hiyo mwaka 1997.
Hivi karibuni SHIWATA imepoteza wanachama wake maarufu waliofariki akiwemo Abuu Semhando,Amina Ngaluma na Muhidin Gurumo.
Marehemu Amigolas alizikwa na umati mkubwa wa waombolezaji kwenye makaburi ya Kisutu Jumatatu saa 10 jioni. Ameacha wajane wawili na watoto wanne. Mungu ilaze roho marehemu mahali pema peponi. Amen.

AFRICA’S REGIONAL NETWORK FOR YOUTH POLICIES EXPERTS LAUNCHED AT THE FIRST GLOBAL FORUM ON YOUTH POLICIES ON BAKU, AZERBAIJAN.

Invest in Youth Logo 
Africa made history during the closing session of the just concluded First Global Forum on Youth Policies, held in Baku, Azerbaijan by announcing the birth of African Network of Youth Policy Experts (AfriNYPE) to advance the cause of youth policies in the region.
The network was announced at the closing plenary session attended by over 700 invited delegates constituting of experts, researchers, professors, government representatives across the world, and the United Nations Secretary-General’s Envoy on Youth, Mr. Ahmad Alhendawi.
A member of the Steering Committee, Adeola Austin Oyinlade, Human rights lawyer and Youth rights/policy expert from Nigeria described the unveiling as ‘good news from Africa’.
According to Mr. Oyinlade who is also a resource person to the African Union (Youth Division) on the implementation of African Youth Charter, the network’s objectives include establishing a comprehensive research and studies unit, in order to collect reliable data and analyse the current situation of youth policies in order to advise key African Stakeholders on concrete and practical mechanisms, for a more inclusive development and implementation of these policies, while improving legal enabling environment of youth participation in decision making.
Ms. Karima Rhanem, a civil society and youth policy expert from Morocco told the gathering that prior to the global forum, young African delegates to the forum engaged in intensive dialogue, through social media and desk research review to do situation analysis of youth policies in the region, mappings and SWOT analysis, which subsequently produced a concrete strategic document that led to the emergence of AfriNYPE.
According to Ms. Rhanem, AfriNYPE is a collective initiative of experts on youth policies in Africa who shared understanding of the urgent need for concrete development and implementations of youth policies in an African context.
interview with MAG TV 
Seleman Kitenge interviewed with MAG TV.
Yvonne Akoth, a gender equality expert from Kenya and a panelist during the Forum mentioned the need for young African voices to be heard in public policy and youth policy development processes, in preparation for the Post2015 Development Goals.
This would be one of the objectives of AfriNYPE, ‘a network that would build the capacity of young people, by enabling them to understand the importance of policy implementation in addressing issues affecting their overall development’ said by Ms. Akoth.
On the strategy to achieve its objective, Abiola Hamid, a youth leader and Youth expert from Nigeria said the network will develop a common and workable understanding of youth policies with theoretical and practical key indicators. He added that the network intends to create a database and fact files as reference point for youth policy research in Africa, and carry out assessments and evaluations of African youth policies, implementations and impacts on the lives of African youths.
interview with UN RadioSeleman Kitenge interviewed with UN Radio in Baku Azerbaijan.
On what he wants to do differently, Mr. Seleman Kitenge, Communication Personnel and Under Secretary General For Media-GIMUN from Tanzania responded, “I want to see young people have enough understanding of all matters related to policy, as well as being able to have a platform to voice out their views and being part of the problem solving, not being seen as a problems’.
On membership of the Network, Michael Zinkanell from Austria who is working with youth empowerment projects in Uganda said “our members consist of youth policy experts, who are directly working with youth empowerment and/or youth policies, targeting the youth in Africa.
All members should commonly value a democratic, fair and gender-balanced approach on how to improve young African’s life through policy development and implementation, regardless of ethnicity, religion, sexuality, or political orientation’.
Adding further, LombeTembo, an economist and a member of the Youth Governance and Accountability Task Team under Restless Development UK from Zambia said the Network membership base is made up of ‘African youth activists, researchers, policy experts and members of civil society organisations who attended the just ended First Global Forum on Youth Policies’. According to Ms. Tembo, ‘we are looking to widen our membership base and will be reaching out to African youth and youth -led organisations within Africa, as well as African youths in the Diaspora’.
meeting with Envoy2Seleman Kitenge(second left) and his counterparts in a special meeting with the UN Secretary General’s Envoy on Youth Ahmad Elhandawi.
During the AfriNYPE steering committee meeting with the United Nations Secretary-General’s Envoy on Youth, Ahmad Alhendawi charged the young network to take it from ideas to actions.
While also speaking to the United Nations News Centre, Mr. Alhendawi said “we have seen young Africans come together to establish a network for researchers on youth policies. We have seen countries pledging support and commitment and resources to support the global initiative on youth policies. I’ve seen people debating issues around youth policies.”
Since the forum ended in Baku, delegates have returned to their various countries to renew their commitment, engagement and advocacy on youth policy matters. The First Global Forum on Youth Policies was hosted by the Government of Azerbaijan in Baku on 28-30th October, 2014 and was co-organised by the office of the UN Youth Envoy, Council of Europe, UNDP, and UNESCO with technical support of Youthpolicy.org
with minister of sportSeleman Kitenge with the Minister of Youth and Sport of Azerbaijan,H.E Azad Rahimov.

KINUKAMORI WAOMBA DOLA 30,000 KUTENGENEZA AJIRA KWA WATU 300

DSC_0218Mkurugenzi Mtendaji wa EWP na Mkurugenzi wa Kinukamori Enterprises, Bw. Alpha Phares Moshi (wa pili kushoto) akimkaribisha Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la maendeleo UNDP, Alvaro Rodriguez alipowasili kwenye Taasisi isiyo ya kiserikali inayo shughulika na uhifadhi wa mazingira eneo la Kinukamori, Marangu mkoani Kilimanjaro wakati wa ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali inayofadhiliwa na UNDP huku akiwa amembatana na Mratibu wa Kitaifa miradi ya COMPACT mkoani Kilimanjaro, Victoria Nderumaki (wa tatu kulia) pamoja na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu (wa pili kushoto).
Na mwandishi wetu, Moshi
Taasisi isiyo ya kiserikali inayo shughulika na uhifadhi wa mazingira eneo la Kinukamori, Marangu mkoani Kilimanjaro Executive Wilderness Program (EWP) inatafuta dola za marekani 30,000 kwa ajili ya kuendesha program tatu zenye kutengeneza ajira, ujasirimali, utunzaji wa mazingira na mvuto kwa watalii wanaokwenda kupanda mlima Kilimanjaro.
Kauli hiyo wameitoa kwa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la maendeleo UNDP, Alvaro Rodriguez wakati alipofanya ziara mkoani Kilimanjaro kuangalia miradi inayofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).
Uongozi wa EWP and Kinukamori Enterprises katika taarifa yao kwa Mratibu huyo, iliyosomwa na Mshauri wao wa fedha Grace Shayo wamesema pamoja na nia yao ya kuhakikisha maporomoko ya Kinukamori yanaendelea, kwanza kama taasisi na pili kama mradi wa kuhifadhi mazingira ya Mlima Kilimanjaro ambao ni sehemu ya urithi wa dunia, wakishirikiana na KINAPA wamefikiria miradi kadhaa ambayo ikienda kwa pamoja itaendeleza eneo hilo.
Wamesema fedha hizo zitatumika kutoa elimu ya ujasirimali kwa vijana 300 wanaoishi katika jamii ya Marangu ambao hutoa huduma mbalimbali kwa wenyeji na pia wageni wakiwemo watalii.
Kundi hilo linalotakiwa kupewa mafunzo ni pamoja na wapagazi 50, waendesha pikipiki 100, wachuuzi 100 na walima mboga 50.
DSC_0221Mshauri wa fedha wa EWP na Kinukamori Enterprises, Grace Shayo akisalimiana na Mratibu miradi ya UNDP Kitaifa, Nehemia Mususuri aliyembata na Bw. Alvaro Rodriguez. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa EWP na Mkurugenzi wa Kinukamori Enterprises, Bw. Alpha Phares Moshi.
Pia fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuanzisha na kutoa huduma ya chakula kwa wanaopanda mlima Kilimanjaro kwa lengo la kupunguza uchafu katika mlima huo na wakati huo huo kuongeza ajira kwa vijana.
Aidha fedha hizo zitatumika kuanzisha kituo cha mazoezi kwa ajili ya wageni wanaotaka kupanda mlima Kilimanjaro kujizoesha na hali ya eneo hilo kabla ya kupanda mlima.
Grace alisema shughuli zote hizo zimelenga vijana kuwa na maeneo ya kudumu yenye ajira endelevu.
Pamoja na kutoa ombi la kusaidiwa kupata fedha hizo, wameshukuru pia kwa misaada iliyotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kwa kupitia COMPACT.Wamesema kama si misaada hiyo eneo hilo ambalo lina historia ya kuharibiwa kwa mazingira yake lisingekuwa linavutia na kutoa ajira kama ilivyo sasa.
Eneo hilo limeboreka mazingira baada ya kuanzishwa kwa taasisi hiyo ya EWP kazi iliyofanywa na Bw. Alpha Phares Moshi ambaye kwa sasa ndiye Mkurugenzi Mtendaji wa EWP na Mkurugenzi wa Kinukamori Enterprises ambapo kwa kushirikiana na KINAPA na COMPACT vijana walipewa elimu iliyowezesha kutengenezwa kwa mradi wa kuhifadhi mazingira ya mto Una wenye maporomoko ya Kinukamori.
DSC_0231Bw. Alvaro Rodriguez akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye mradi huo.
Vijana hao ambao ndio wanaoishi katika mteremko wa mlima Kilimanjaro walianza shughuli hizo mwaka 1997 na kuanza kufikiria kuyatengeneza maporomoko ya Kinukamori kama chanzo cha kivutio katika juhudi za kuhifadhi mto Una.
Walisema kwa kuzingatia madhumuni ya kuanzishwa kwa mradi huo vijana na wanawake walianza kurejesha hali ya mazingira kwa kuyaweka bora na kudhibiti uharibifu wa ikolojia.
Kutokana na juhudi hizo miti zaidi ya 5000 mingi ikiwa ya asili ilipandwa kandoni mwa mto na sasa miti hiyo inatumika kutoa mafunzo na kurejesha hali ya upatikanaji wa maji ya kutosha kwa ajili ya wananchi wa Marangu.
Aidha wanyama na ndege waliokuwa wametoweka kutokana na uharibifu wa mazingira uliokuwepo kwanza wameshaanza kurejea eneo hilo.
Pamoja na mafanikio hayo EWP wanakabiliwa na changamoto kubwa hasa ukubwa wa eneo la shughuli zao ambalo ni ndogo na sasa wanataka kusaidiwa kufika hadi maeneo ya chemchem ya Soko iliyopo Kahe.
DSC_0262Mshauri wa fedha wa EWP na Kinukamori Enterprises, Grace Shayo akisoma taarifa ya taasisi yao kwa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la maendeleo UNDP, Alvaro Rodriguez.
Aidha wamesema wanakabiliwa na tatizo la fedha na hasa kushawishi vijana kujikita zaidi katika masuala ya uhifadhi wa mazingira na utalii wa kitamaduni.
Naye Mwakilishi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa pamoja na kuwapongeza EWP kwa kufanikisha kurejesha mazingira katika hali ya kawaida katika eneo hilo amesema kwamba wataendelea kushirikiana nao kuhakikisha kwamba shughuli za hapo zinahifadhi mazingira na kutoa ajira kwa vijana.
Alisema duniani nzima kwa sasa inakabiliwa na tatizo la ajira kwa vijana ambao kutokana na kukosekana kwa ajira wanatopea katika ulevi na hivyo kuhatarisha nguvu kazi hiyo muhimu.
Alisema hata Tanzania pamoja na kuanza kufikiria kuwa na uchumi wa gesi, hatua hiyo itachukua muda lakini kuna haja ya vijana wanaomaliza shule wakawajibika katika miradi mbalimbali ya uhifadhi na maendeleo ya kiuchumi.
DSC_0271Mshauri wa fedha wa EWP na Kinukamori Enterprises, Grace Shayo akikabidhi taarifa ya taasisi hiyo kwa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la maendeleo UNDP, Alvaro Rodriguez aliyetembelea mradi wao na kujionea maendeleo yao.
Mwakilishi huyo pamoja na kutotoa ahadi katika ombi la taasisi hiyo amesema kwamba wataangalia nini cha kufanya kwani alifika eneo hilo kujifunza na kuona maendeleo kwani ana miezi miwili tu toka ameingia nchini kuwakilisha mashirika ya Umoja wa Mataifa.
Alisema amefurahishwa na maendeleo yaliyopo na hasa kwa kuzingatia kwamba kulikuwa na tatizo la raslimali kufanya shughuli hiyo.
Alisema anatambua changamoto zilizopo cha ongezeko la watu, tatizo la ajira kwa vijana na mabadiliko ya tabia nchi na kwamba wataendelea kushirikiana na taasisi hiyo kuona kwamba changamoto hizo zinakabiliwa na kufutwa.
DSC_0228Bango linaloonyesha tarehe ya kuzinduliwa kwa mradio huo wa COMPACT unaofadhiliwa na UNDP.
DSC_0455Baadhi ya sheria zilizowekwa kwenye maporomoko ya maji ya Kinukamori yaliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro.
DSC_0238Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania Hoyce Temu akiwa amefuatana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la maendeleo UNDP, Alvaro Rodriguez kutembelea mazingira ya taasisi hiyo pamoja na vivutio vya kitalii vilivyomo kwenye Maporomoko ya maji ya Kinukamori yaliyopo Marangu mkoani Kilimanjaro.
DSC_0276Pichani juu na chini ni mtoa maelezo kwa watalii (Guide) wa EWP na Kinukamori Enterprises, Pascal Cosma akitoa maelezo ya sehemu ya utamaduni wa Kabila la Kichaga kwa Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la maendeleo UNDP, Alvaro Rodriguez aliyembatana na ujumbe wake kutembelea miradi mbalimbali inayofadhiliwa na UNDP.
DSC_0280
DSC_0285
DSC_0283 
Sanamu la aliyekuwa Chifu wa kabila la Wachaga Chifu Thomas Marealle lilipo kwenye taasisi hiyo.
DSC_0293
Pichani juu na chini ni mtoa maelezo kwa watalii (Guide) wa EWP na Kinukamori Enterprises, Pascal Cosma akiendelea kutoa maelezo ya tamaduni mbalimbali za kabila la wachaga ikiwemo na sanamu mbalimbali zilizowekwa kwenye taasisi hiyo.
DSC_0295

No comments:

Post a Comment