TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, November 15, 2013

MAZITO YAMKUTA MBUNGE LEMA ,JK ARUDISHA ZAWADI YA DHAHABU,VIWANJA VIBOVU SABA VYASIMAMISHWA LIGI KUU

Posted: 13 Nov 2013 12:10 AM PST
  • ALIKUWA KWENYE MATIBABU AFRIKA KUSINI
  • NCCR- MAGEUZI KUZUNGUMZIA MSIBA 
Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dkt. Sengondo Mvungi, amefariki dunia jana alasiri nchini Afrika Kusini, katika Hospitali ya Milpark, Johannesburg.

Dkt. Mvungi ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi na Mhadhiri Mwandamizi wa Sheria Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UB), alipelekwa nchini humo baada ya kuvamiwa na kujeruhiwa usiku wa kuamkia Novemba 3 mwwaka huu akiwa nyumbani kwake, Kimbamba Msakuzi.
Chama cha NCCR-Mageuzi, kimethibitisha juu ya kifo hicho na kuongeza kuwa, taarifa kamili zitatolewa leo Makao Makuu ya chama yaliyopo Ilala, kuanzia saa tatu asubuhi.
Mtoa habari hizo ndani ya chama ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema marehemu Dkt. Mvungi alikuwa kiongozi mkubwa ndani ya chama na ametumia fursa hiyo kukifanya chama hicho kiwe na wanachama wengi.
Dkt. Mvungi baada ya kujeruhiwa kwa mapanga, alikimbizwa katika Hospitali ya Rufaa Tumbi, iliyopo Kibaha, mkoani Pwani na baadaye kuhamishiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Kitengo cha Wagonjwa Wanaohitaji Uangalizi Maalumu (ICU).
Kutokana na hali yake kutoimarika vizuri akiwa hospitalini hapo, Novemba 7 mwaka huu, Dkt. Mvungi alisafirishwa kwa ndege ya kukodi ya Shirika la Ndege la Flightlink, kwenda Afrika Kusini kwa matibabu zaidi hadi mauti yalipomkuta wakati madaktari wakiendelea kuokoa maisha yake.
Msemaji wa Kitengo cha Taasisi ya Mifupa (MOI), Bw. Jumaa Almas, alisema walilazimika kumsafirisha Dkt. Mvungi kutokana na afya yake kutoimarika vizuri.
Dkt. Mvungi alipata majeraha makubwa kichwani ambapio katika msafara wake, aliongozana na Daktari Bingwa wa Upasuaji Ubongo na Mishipa ya Fahamu Dkt. Clement Mugisha na Muuguzi, Bi. Juliana Moshi.
Juzi Jeshi la Polisi nchini kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi, alisema watu tisa ambao walihusika kumpiga, kumjeruhi na kuiba vitu mbalimbali vya marehemu Dkt. Mvungi, tayari wamekamatwa.
Dkt. Nchimbi alisema watu hao walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya Dar es Salaam kwa nyakati tofauti ambapo awali walikamatwa sita na juzi kufikia tisa.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, ambaye alikuwepo katika mkutano huo, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Msigwa Mpopela (30), Shabago Magozi na Hamadi Ally, jina maarufu 'Hatibu'.
Wengine ni Zakaria Raphael (dereva wa bodaboda), Mmanda Saluwa, Juma Hamisi, Longisho Semeriko (muuza ugolo), Paul Jeirosi na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Kilimimazoka, ambao wote ni wakazi wa Dar es Salaam
"Watuhumiwa hawa walikutwa na mapanga, kigoda ambavyo vimethibitika kuwa vilitumika katika tukio hilo, pia walikutwa na simu ya mkononi mali ya Dkt. Mvungi," alisema.
Kamishna Kova alisema, katika mahojiano ya awali na watuhumiwa, walikiri kuhusika na tukio hilo na ushahidi umekamilika kwa asilimia 80.
"Watuhumiwa wote wamekiri kosa hivyo tunakamilisha upelelezi ili wafikishwe mahakamani mara moja," alisema.
Marehemu Dkt. Mvungi, aliwahi kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2005 kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi



Posted: 13 Nov 2013 12:16 AM PST

  •  ACHAFULIWA MTANDAONI, AITUHUMU UVCCM TAIFA
Queen Lema, Arusha na Mariam Mziwanda, Dar
  Katika hali isiyo ya kawaida, Mbunge wa Arusha Mjini, Bw. Godbless Lema, ameutuhumu uongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Taifa kwa mada ya kusambaza picha zinazoonesha akiingiliwa kinyume na maumbile katika mitandao ya kijamii.

  Mbali ya uongozi huo, Bw. Lema pia alimtuhumu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Bw. Sadifa Juma Khamis, kwa kushiriki kumchafua hivyo amemtaka Spika wa Bunge, Bi. Anne Makinda, achukue hatua na kudai ushahidi wa jambo hilo upo hadharani.
  Bw. Lema aliyasema hayo Mjini Arusha jana alipokutana na waandishi wa habari ili kuzungumzia jambo hilo na kusisitiza kuwa, suala hilo limemsikitisha sana. “Ushahidi wa namba za simu zilizohusika kusambaza picha hizo upo, Khamis (Mwakilishi Jimbo la Donge, Zanzibar), anahusika na udhalilishaji uliofanywa na vijana wa UVCCM Taifa,” alisema Bw. Lema.
  Alisema picha hizo zimesambazwa katika mitandao ya kijamii na watumiaji wa simu za mkononi zikiwa na ujumbe unaodai Lema akilawitiwa na wanaume wenzake.Aliongeza kuwa, Oktoba 29 mwaka huu, mkewe aliyemtaja kwa jina la Bi. Neema Lema, alipata picha hizo zilizotumwa moja kwa moja katika simu yake zikiwa na ujumbe usemao “Hiyo ndiyo kazi anayoifanya mume wako”.
   Bw. Lema alisema, suala hilo halikuishia hapo kwani picha hizo zilitumwa kwa mama mkwe wake na kusababisha familia ya mke wake na wazazi wake kukosa amani “Mke wangu alitumiwa picha hizi katika mtandao wa WhatsApp na baadaye ilisambazwa zaidi hadi kwa wapigakura wangu jimboni na kudai ndiyo kazi inayofanywa na Mbunge wao,” alisema.
  Aliongeza kuwa, uchafu huo ulikuwa ukifanyika wakati akiwa bungeni Dodoma ambapo Bw. Khamis, alionekana akisambaza picha hizo kutoka kwenye kompyuta yake (mpakato), kuwapa wabunge jambo ambalo lilichangia amani ya bunge kuharibika siku hiyo.
 “Wakati picha hizi zikisambazwa, nilijulishwa suala hili na wabunge wanawake wa CCM, ilibidi niende kwa Spika ambaye alikiri picha hizo zimesababisha akose morali ya kuendesha vikao. “Pia nilizungumza na uongozi wa Bunge nikilalamikia kudhalilishwa kwa kutengenezewa picha zinazoonesha nikiingiliwa na wanaume wenzangu... Spika aliahidi kulishughulikia,” alisema Bw. Lema.
  Bw. Lema alisema, kutokana na picha hizo, bado hazimnyimi kinga ya kuendelea kusema ukweli juu ya jambo lolote badala yake ataendelea kupambana ili kuwatetea wanyonge.“Kamwe siwezi kuwatafuta waliotengeneza picha hizi na kuzisambaza kwenye mitandao na simu za watu bali atawasaidia viongozi wa UVCCM kuzisambaza kwenye Makanisa, Misikiti, mikutano ya hadhara ili kuwaonesha wananchi ukatili dhidi yake unavyozidi kushika kasi asiwe na sauti ndani ya nchi,” alisema.
  Wakati huo huo, Mke wa Mbunge huyo, Bi. Neema, alisema hicho ni kitu kidogo sana dhidi ya mumewe na waliofanya vitendo hivyo walilenga kuvunja ndo yake lakini haitatokea. Sadifa azungumza
  Akijibu tuhuma hizo akiwa njiani kwenda nchini Ethiopia, Bw. Khamis alisema jumuiya hiyo au yeye mwenyewe hawezi kutumia cheo chake kufanya vitendo hivyo.
  “Mimi na Mheshimiwa Lema wote ni wabunge, tofauti yetu ipo katika vyama na majimbo...tomefahamiana bungeni na wala simjui kwa undani, tuhuma dhidi yangu si za kweli kwani siwezi kufanya kitendo hicho ambacho si cha kibinadamu hata kama tuna tofauti za kisiasa.
 “Mimi ni Muislamu na dini yangu hairuhusu kufanya hivyo, binafsi sijui kutumia kompyuta na Mheshimiwa Lema analijua hilo...hivi sasa Ofisi ya Bunge imeanza kutoa mafunzo kwa wabunge wasiojua kutumia kompyuta, nami najifunza,” alisema.
  Alisema simu anazomiliki ni mbili, moja ni Nokia ya tochi na nyingine ya kichina yenye laini tatu na hajui kama simu hizo zina mitandao na hajawahi kujaribu.Bw. Khamis aliongeza kuwa, hulka yake hayupo karibu na makundi yanayoweza kumuingiza au kumshawishi afanye vitendo hivyo hivyo yupo tayari kukutana na Bw. Lema kwa amani ili wazungumze na kuwasaka waliofanya vitendo hivyo ambavyo si vya kistaarabu.
“Mheshimiwa Lema akinitafuta nitampa ushirikiano, ninachokijua mimi, mwenzangu ananitafutia umaarufu kwa sababu pamoja na vyeo nilivyonavyo bado sifahamiki sana.
  “Natumia cheo changu ndani ya UVCCM kuijenga jumuiya na CCM... kwanza namuomba radhi kwa sababu tayari ana imani potofu dhidi yangu, pili namshauri afanye utafiti,” alisema.
Alisema imani yake ni kwamba, tofauti zao kisiasa haziwezi kumshawishi afanye vitendo hivyo kwani ipo siku Bw. Lema anaweza kurudi CCM na kufanya naye kazi pamoja.
  Aliongeza kuwa, umefika wakati wa Bw. Lema kukumbuka kuwa, tofauti za kisiasa zilizopo ndani ya chama chao pia zinaweza kutumika kumchafua katika mitandao

Posted: 13 Nov 2013 12:25 AM PST

 Rais Jakaya Kikwete, amerudisha zawadi ya dhahabu safi gramu 227 aliyopewa na Kampuni ya Nyamigogo Grand Vezir Holdings ya mkoani Geita na kutaka itumike kuwasaidia watoto yatima, anaripoti Mwandishi Wetu
. Zawadi hiyo alikabidhiwa juzi katika sherehe ya uzinduzi wa Mgodi wa Uchenjuaj iDhahabu wa kampuni hiyo uliopo nje kidogo ya Mji mdogo wa Kharuma ambako ndiko Makao Makuu ya Wilaya Mpya  ya Nyang’hwale,mkoani humo.
  Dhahabu hiyo ina thamani ya sh. milioni 16 kwa bei ya sasa katika soko la dhahabu duniani ambapo baada ya kukabidhiwa, Rais Kikwete aliuliza; “Sasa nifanye nini na zawadi hii, naomba kuirudisha hii dhahabu muiuze popote, fedha ambayo itapatikana tutawapa watoto yatima,” alisema.
  Akizungumza na wananchi katika mgodi huo, Rais Kikwete aliupongeza uongozi wa mgodi na kusema umeongeza thamani ya dhahabu na ya maisha ya wananchi katika eneo hilo.Aliushauri uongozi wa mgodi huo, kufanya jitihada za kuboresha teknolojia inayotumika. “Mgodi huu ni mradi wa maana sana kwani umeongeza thamani ya dhahabu na kuboresha maisha ya wananchi katika eneo hili, ubunifu huu unastahili pongezi.
  “Lazima tuboreshe teknolojia, ile inayotumika katika mgodi huu ni ya zamani kidogo, hii ni sawa na hadithi ya mtu mwenye chongo katika jamii ya vipofu watupu, yeye anaonekana kama mfalme,” alisema Rais Kikwete.
  Mgodi wa Nyamigogo ni wa marudio kwa maana ya kuzalisha dhahabu kutokana na mchanga ambao awali ulifukuliwa ili kutoa dhahabu na ulianzishwa mwaka 2011 ambapo hadi sasa, sh. bilioni 1.6 zimewekezwa katika uendelezaji wa mgodi huo.
  Katika risala ya uongozi wa mgodi huo, ilisema mgodi huo unazalisha kati ya gramu 500 na 600 kwa mwezi na umeajiri watu 45 wakiwemo wanawake 10.Tangu kuanzishwa kwake, umekuwa unaunga mkono shughuli za jamii inayouzunguka kwa kujenga zahanati na madarasa ya shule katika vijiji viwili.
  Rais Kikwete amezindua mgodi huo kama sehemu ya kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo akiwa katika ziara yake rasmi ya kikazi mkoani humo ambao ni miongoni mwa mikoa minne aliyoianzisha mwaka 2012.
  Ziara hiyo imemalizika jana kwa kupokea ripoti ya maendeleo ya Wilaya ya Nyang’hwale na kuhutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Mji Mdogo wa Kharuma

Posted: 13 Nov 2013 12:29 AM PST
 Frank Monyo na Daniel Samson
  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Zuberi Samatabe, amewahimiza walimu wa shule za msingi kuwajengea wanafunzi utamaduni wa kujisomea vitabu ili kuongeza uelewa katika masomo yao.
Aliyasema hayo katika uzinduzi wa tovuti ya kufuatilia mgawo wa vitabu vya chenji ya Rada uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Lengo la tovuti hiyo ya www. pesptz.org ni kutoa taarifa kwa wadau wa elimu pamoja na wanafunzi juu ya vitabu vinavyosambazwa katika shule za msingi kwa kutumia chenji hiyo.
Alisema, Serikali ya Uingereza iliamuru fedha zilizotumika vibaya katika manunuzi ya Rada zirudishwe kwa Watanzania na zitumike katika manunuzi ya vitabu na madawati kwa shule za msingi.
"Fedha za chenji ya Rada sh. bilioni 72 zilizorudishwa ziliingizwa katika mpango wa manunuzi ya vitabu na madawati katika shule za msingi na asilimia 75 zimetumika katika manunuzi ya vitabu vya wanafunzi na vya mwongozo wa walimu kufundishia," alisema Samatabe.
  Kwa upande wake Meneja Takwimu wa Kampuni ya Data vision International, William Kihula alisema Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI kupitia Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Uingereza (DFID) iliwapa jukumu la kutengeneza tovuti kufuatilia mgao wa vitabu vya chenji ya Rada, ili kuwezesha ushirikishwaji wa wadau wa elimu na wananchi katika kufuatilia usambazaji wa vitabu shuleni.
  Alisema hatua hii itawezesha serikali kuendelea kutembelea katika maeneo yake na kuwa na uendeshaji wa uwazi ndio maana wamejenga mfumo huu katika namna ambayo itaweza kutumika na wizara hata baada ya mradi huo wa mgawo wa vitabu vya chenji ya rada kuisha.
"Tovuti hiyo ndio pekee inayoweka mtandaoni majina yote ya shule za hapa nchini wilaya na mikoa iliyopo hii itatoa mwanga wa kuanzia katika ufuatiliaji wa maendeleo ya mwanafunzi mmoja mmoja," alisema Kihula.
  Aliongeza kuwa, kuwepo kwa jitihada za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuanza kutumia mfumo mpya wa kupima ufaulu wa wanafunzi kwa kuhusisha "Continous Assessment" kwa kuanza na shule za sekondari.
  "Katika hili Datavision tupo kwenye hatua za mwisho za kutengeneza mfumo wa teknolojia itakayowezesha kupatikana na kutunza taarifa za maendeleo ya mwanafunzi shuleni kwa wakati," alisema Kihula.
Posted: 13 Nov 2013 12:32 AM PST

 Penina Malundo na Maua Mashu
  Wafanyakazi wakiwemo vibarua zaidi ya 200 wa Kampuni ya STRABAG inayojenga barabara ya mabasi yaendayo kasi jijini Dar es Salaam wamegoma.

Mgomo huo ulianza jana jijini humo kwa madai ya kutaka kulipwa stahiki zao za zamani kabla ya kampuni hiyo kuingia mkataba na kampuni nyingine.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana na waandishi wa habari, wafanyakazi wa kampuni hiyo walisema kuwa, wameingia katika kampuni hiyo kwa sheria zote na wengi wao wameweza kufanya kazi zaidi ya mwaka mmoja, hivyo wanapaswa kulipwa madai yao kabla ya kuvunja mkataba na Kampuni ya STRABAG.
Walisema kuwa, mgogoro mkubwa uliibuka kati ya vibarua hao na kampuni iliyoingia mkataba na Strabag ijulikanayo kama Laba Constractors juu ya malipo watakayolipwa kuwa madogo tofauti na malipo ya Kampuni ya Strabag.
"Jumamosi tulikaa kikao na viongozi wa Laba Constractors wakatueleza kuwa kuanzia siku ya Jumatatu (juzi), malipo yetu yatakuwa chini yao, kwani wameingia mkataba na Kampuni ya Strabag kwa ajili ya kulipa wafanyakazi wake na vibarua, jambo la kushangaza sisi hatujapata taarifa yoyote kutoka kwa Strabag juu ya mkataba huo walioingia na Kampuni ya Laba Constractors," alisema mmoja wa vibarua hao ambaye hakutaka kutaja jina lake.
Alisema kuwa, Kampuni ya Strabag ingefanya utaratibu maalumu wa kumaliza madai yote ya msingi kwa vibarua wake na hapo ndipo wangeweza kuanza kuingia mkataba na kampuni nyingine.
"Mpaka sasa hatujui hatma yetu, sisi tumekaa hapa toka saa 12 asubuhi na tutaendelea kukaa mpaka kieleweke hadi tupatiwe haki yetu, malipo yetu tupewe ndiyo kampuni nyingine ianze upya na sisi, kwani tumeshakaa zaidi ya mwaka mmoja, kisheria sisi tayari ni wafanyakazi halali," alisema.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi katika Kampuni ya STRABAG (TAMICO), Abdullah Rukusa alisema kuwa, Kampuni ya Strabag ilikuwa inawalipa vibarua hao malipo ya sh. 12,500 kwa siku huku malipo ya posho yakiwa sh. 4,800 kwa saa za ziada.
Alisema kuwa, Kampuni ya Laba Contractors inataka kuwalipa vibarua hao kiasi cha sh.10,000 kwa siku hali itakayofanya kampuni hiyo kuwanyonya wafanyakazi hao pindi wanapoanza kazi saa 12 asubuhi hadi saa 12 jioni.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Laba Contractors, Emanuel Mshana alisema kuwa, mkataba kati yao na Kampuni ya Strabag ulisainiwa Jumamosi iliyopita na kazi rasmi ilianza kufanyika juzi huku tayari akidai wamekutana na wafanyakazi hao kwa mazungumzo.
Alisema kuwa, vibarua 95 waliopewa na Kampuni ya Strabag kati yao 45 ndio walioanza kufanya kazi nao juzi na kampuni yao kuongeza vibarua 28 kwa siku, kwa ajili ya kufanya kazi.
Juhudi za kumtafuta Mkurugenzi wa Kampuni ya Strabag ziligonga mwamba baada ya kugoma kuzungumza na waandishi wa habari huku geti likizuiliwa na mawe makubwa ya barabaran
Posted: 13 Nov 2013 12:39 AM PST

 Na Grace Ndossa
   Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba (NHC), Nehemia Mchechu ametunukiwa tuzo ya uongozi bora pamoja na cheti kwa kutambua mchango wake mkubwa katika jamii na ndani ya shirika hilo.

  Tuzo hiyo ilikabidhiwa jana jijini Dar es Salaam na Rais wa Rotary Klabu ya Mzizima, Ambrose Nshala ambapo alieleza kuwa Mkurugenzi huyo amekuwa kiongozi bora na amethubutu kufanya kazi kwa ujasiri na kuonesha ndoto za kufika mbali.
  Alisema kuwa, Mkurugenzi huyo ni kijana mdogo, lakini ameonesha uthubutu wake katika kufanya kazi na mageuzi ndani ya shirika, hali ambayo imeonesha hatua kubwa kiuchumi na kazi anazofanya zitalifikisha mbali shirika.
  Alisema kuwa, Rotary klabu inathamini mchango wake na kutambua kazi aliyofanya kwa jamii kwani ni kubwa hivyo wametoa tuzo hiyo na cheti kwa ajili ya kuongeza hamasa kwa viongozi wengine kuiga mfano wa mkurugenzi huyo ili nchi iweze kupata maendeleo.
  Kwa upande wake, Mchechu alisema kuwa, tuzo hiyo itasaidia kuongeza hamasa zaidi katika kufanya kazi ili nchi iweze kupata maendeleo.
  Alisema kuwa, sera za Tanzania ni nzuri ila tatizo liko kwenye utekelezaji kwani viongozi wengi wanathamini maneno kuliko vitendo, hivyo ndiyo vinavyofanya mambo mengi kukwama.
  Pia alisema, sera nyingi hapa nchini nyingi huishia kwenye karatasi na nchi nyingi huiga sera za Tanzania katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ndiyo maana zimepiga hatua
Posted: 13 Nov 2013 12:36 AM PST

 Na Mwandishi Wetu
  Imeelezwa kuwa kuanzishwa kwa kampuni huru za minara ya mawasiliano ya simu, kunaweza kupunguza gharama za uendeshaji kwa kampuni za simu za mkononi nchini, hivyo kuweza kusaidia kuleta ahueni kwa watumiaji wa simu hizo.

Kabla ya hapo kampuni zote za simu za mkononi nchini kila moja ililazimika kujenga mnara wake ambao unahitaji kiasi kikubwa cha uwekezaji ikiwa ni pamoja na matumizi ya jenereta, ulinzi na gharama nyingine za uendeshaji.
Hayo yalibainishwa jana na Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Helios Towers, Michael Magambo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
"Hapo ndipo kampuni huru za minara zinapoingia. Humiliki, husimamia na huendesha minara, inayoweza kutumiwa na kampuni nyingi za simu kwa wakati mmoja na pia hata matangazo ya Tv, redio na mawakala wa hali ya hewa," alisema.
  Alisema, matumizi ya mnara mmoja huondoa mzigo wa gharama za uwekezaji wa miondominu pamoja na shughuli nyingine kwenye eneo la mnara.
  Pia alisema, kampuni za simu zinapata nafasi ya kuelekeza nguvu zaidi katika eneo wanaloliweza zaidi kutoa huduma za sauti na 'data' kwa Watanzania.
 "Wengi hawaufahamu mchango wetu katika kupanua huduma za simu Tanzania na Afrika kwa ujumla. Helios Towers ni kampuni kubwa ya minara huru nchini, ikiwa imejenga zaidi ya minara 1,000 ya Tigo Tanzania mwaka 2010, kisha ikajenga minara mingine 250 na inatarajia kuongeza mingine 150 ifikapo Desemba mwaka huu," alisema Magambo.
  Aidha, alisema kwa miaka miwili iliyopita, maeneo ya Helios yanayotumiwa kwa pamoja na kampuni za simu ni asilimia 53 kwa sasa na ni asilimia 60 ya maeneo mapya kwa nchi nzima huku ikisubiri uthibitisho wa serikali wa kuchukua minara ya Vodacom Tanzania.
"Tumekuwa tukisikia wakosoaji wakidai kwamba, kampuni kama Helios hayana ushindani kwa kuwa yamekamata soko kubwa.
  "Hii si kweli. Uhakika ni kwamba Helios imekuwa chachu ya kuwapo kwa ushindani kwenye soko la huduma za simu, ikiruhusu wageni kuingia kwenye soko na kuwapa nafasi watoa huduma kupeleka vijijini bila wasiwasi.
  "Mwishowe ni walaji ndio hufaidika zaidi kwa kupunguziwa bei za simu na kuchagua mtandao wanaoutaka. Ukweli ni kwamba tunafungua zaidi soko," aliongeza Magambo.
  Hata hivyo, katika kupunguza changamoto za kupeleka huduma maeneo ya vijijini yasiyo na huduma za simu, awali Serikali ilitoa gari lijulikanalo kama Universal Communication Action Fund (UCAF) linalosaidia kupunguza gharama na kuwahamasisha watoa huduma kwenda kwenye soko la vijijini.
  Hatua hiyo ilitokana na Sheria ya Upatikanaji wa Mawasiliano ya mwaka 2006 yenye lengo la kukuza maendeleo ya kijamii na uchumi mijini na vijijini kupitia TEKNOHAMA.Mbali na hayo Kampuni ya Helios iko mbioni kuweka mitambo 27 chini ya UCAF
Posted: 13 Nov 2013 12:42 AM PST

 Na Mwandishi Wetu
  Kampuni ya Simu za Mkononi ya Airtel Tanzania imeamua kupambana na changamoto zinazoikabili sekta ya elimu nchini kwa kuzisaidia shule mbalimbali za sekondari kupata miundombinu ya kufundishia na vifaa vya kujifunzia.

  Pia kampuni hiyo kupitia mradi wake wa Shule Yetu imewanufaisha wanafunzi wa Shule ya Sekondari Chalinze iliyopo mkoani Pwani baada ya kukabidhi vitabu vya masomo ya sayansi vyenye thamani ya sh. milioni tano kwa shule hiyo.
  Akizungumza wakati wa kukabidhi vitabu hivyo, Meneja Masoko wa Airtel Kanda ya Kusini na Mkoa wa Morogoro, Aminata Keita alisema vitabu hivyo vitatumika katika kuongeza kiwango cha uelewa na kukuza ufaulu kwa wanafunzi wa shule hiyo ambao walikuwa na tatizo la uhaba wa vitabu.
  "Vitabu hivi...vitatumika kukuza ufaulu kwa wanafunzi maana wanafunzi wataweza kujisomea kwa urahisi na kufuatilia masomo kwa ukaribu zaidi," alisema Aminata.
  Aliongeza kuwa, msaada huo wa vitabu ni sehemu ya mpango mkakati wa kuzisaidia shule za kata zinazolalamikiwa kufanya vibaya katika mitihani yao ya kitaifa.
  "Tumetoa vitabu vya masomo ya sayansi tukijua kabisa wanafunzi wengi hushindwa masomo hayo kwa sababu mbalimbali, ikiwemo upungufu wa zana za kujifunzia ila nina imani mradi huu wa Shule Yetu utaziwezesha shule za kata kufanya vizuri kwenye mitihani ya kitaifa," alisema Aminata.
  Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo, Emmanuel Kahabi alisema, upatikanaji wa vitabu utarahisisha kazi ya ufundishaji kwa wanafunzi na pia wanafunzi wataweza kuelewa kiurahisi maana zana za kufundishia zinapatikana
Posted: 13 Nov 2013 12:49 AM PST

Neema Ndugulile
  Timu ya Mbeya City imepigwa faini ya sh. 500,000 na Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) na kupewa onyo kali kwa timu yake ya U20 kutocheza mechi ya utangulizi walipocheza na Yanga.

  Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambaye pia ni Kaimu Katibu Mkuu wa shirikisho hilo, Boniface Wambura alisema pia Mbeya City wanatakiwa kulipa gharama za uharibifu, baada ya mashabiki wao kuvunja kioo cha basi la Yanga, baada ya gharama hizo kuthibitishwa na bodi hiyo.
  "Pia Mbeya City imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa mashabiki wake kushambulia basi la wachezaji wa Tanzania Prisons, baada ya mechi dhidi yao na kulipa gharama za uharibifu baada ya kuthibitishwa na Bodi ya Ligi," alisema Wambura.
  Alisema Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 kutokana na vurugu za mashabiki wake ilipocheza na Azam kwenye Uwanja wa Mkwakwani ambapo mwamuzi msaidizi, Hassan Zani alishambuliwa kwa mawe na kujeruhiwa mkononi na kichwani, tukio lililosababisha mchezo kusimama kwa dakika tatu.
  Wambura alisema beki wa Coastal Union, Hamad Khamis amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kumpiga kichwa kwa makusudi Kipre Tchetche wa Azam. "Kitendo hicho kilisababisha refa amtoe nje kwa kadi nyekundu, hivyo atakosa mechi tatu zinazofuata za timu yake.
  "Nayo Simba wamepigwa faini ya sh. 500,000 kutokana na vurugu za mashabiki wake wakati wa mechi dhidi ya Kagera Sugar," alisema Wambura.
  Alisema adhabu zote zimetolewa kwa mujibu wa kanuni. Pia Bodi ya Ligi imeahirisha kufanya uamuzi wa mechi kati ya Stand United na Kanembwa JKT iliyochezwa Uwanja wa Kambarage, ili kukusanya taarifa zaidi. Mechi hiyo haikumalizika. Bodi ya Ligi itakutana tena Jumapili.
Posted: 13 Nov 2013 12:46 AM PST
Na Fatuma Rashid
  Bodi  ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board), imefungia viwanja saba vilivyokuwa vikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL), hadi vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi za mpira wa miguu.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Boniface Wambura alisema uamuzi huo umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika juzi ambapo pamoja na mambo mengine, kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL katika mzunguko wa kwanza.
  Alisema viwanja vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza, ili viruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa yake yamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji) na Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo (dressing rooms) havina hadhi.
  Wambura alisema Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea-pitch ni mbovu), Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha (sehemu ya kuchezea ni mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishia kutumika kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea (pitch ni mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu).
  Wambura ambaye ni Kaimu Katibu Mkuu wa TFF, alisema klabu ambazo timu zake zinatumia viwanja hivyo zimeshataarifiwa rasmi juu ya uamuzi huo, ambapo ama vinatakiwa kuwasiliana na wamiliki wa viwanja hivyo, ili wafanye marekebisho au kutafuta viwanja vingine vya kuchezea mechi zao.
  Wakati huo huo, timu za Taifa za Future Taifa Stars na Taifa Stars zinacheza leo. Mechi hiyo ya kirafiki itafanyika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni.
  Mechi hiyo ni maalumu kwa Benchi la Ufundi la Taifa Stars linaloongozwa na Kim Poulsen, kuangalia wachezaji kumi kutoka Future Taifa Stars watakaoongezwa katika Taifa Stars, tayari kwa mechi ya kirafiki ya kimataifa itakayochezwa Novemba 19, mwaka huu jijini Arusha.
  Watazamaji 300 tu wataruhusiwa kushuhudia mechi hiyo kwa kiingilio cha sh. 5,000. Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imeingia kambini jana. Miongoni mwa wachezaji wanaotarajia kuripoti ni kipa Ivo Mapunda wa Gor Mahia.
Posted: 13 Nov 2013 12:57 AM PST

Na Fatuma Rashid
  Kocha mpya wa timu ya Azam Fc anatarajiwa kutua katika kikosi hicho mapema, kabla ya wachezaji wa timu hiyo kurudi kambini.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Msemaji wa timu hiyo, Jaffer Iddi alisema wachezaji wote wamepewa likizo ya wiki mbili, hivyo uongozi upo katika mchakato wa kutafuta kocha atakayerithi mikoba ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mwingereza Stewart John Hall.
Msemaji huyo alisema kocha mpya atakapowasili, ndipo atakapojua ni mchezaji gani atataka aanze naye na yupi amalize naye, kwani yeye ndiye atakuwa akiufahamu uwezo wa wachezaji kuanzia mazoezini hadi katika mechi.
Akizungumzia katika mechi ya mwisho ya mzunguko wa kwanza ya michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mbeya City, Iddi alisema ilikuwa nzuri kuliko nyingine kwani wote walikuwa wazuri na walipigana kutafuta nafasi nzuri katika kumalizia mzunguko huo.
  Alisema timu yake kwa sasa ipo mapumziko na itarudi kambini baada ya wiki mbili, ili kujipanga zaidi kwa mzunguko wa pili wa ligi hiyo na michuano ya kimataifa.
  Aliongeza kuwa, katika mzunguko wa pili anaimani timu yake itakuwa vizuri zaidi kutokana na kuona pamoja na kupima uwezo wa kila timu shiriki za Ligi Kuu, ambazo uwezo wake wameshauona, hivyo anaona timu itajifunza kutokana na walichokiona katika mzunguko wa kwanza.
  Kocha Hall aliwaaga wachezaji na benchi la ufundi, mara tu baada ya mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza dhidi ya Mbeya City uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3 kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi, Dar es Salaam.  

NITAMNG’OA SPIKA MAKINDA-MBUNGE, CHADEMA: HATUHUSIKI MADAI YA ZITTO,

Posted: 12 Nov 2013 12:15 AM PST

  •  ASEMA CCM HAIWEZI KUONDOA HOJA YAKE BUNGENI
  • ASISITIZA MSIMAMO WAKE KWA WAPIGA KURA JIMBONI

Na Suleiman Abeid, Nzega
   Mbunge wa Nzega mkoani Tabora ,Dkt.Hamisi Kig wangalla,amesema bado ana dhamira ya kuwasilisha hoja ya kumng’ oa madarakani Spika  wa B unge, Bi.Anne Makinda .Alisema uvumi ulioenea kuwa hoja yake imeondolewa kwa agizo la Chama Cha Mapinduzi (CCM), hauna ukweli
.  Dkt. Kigwangalla aliyasema hayo mwishoni mwa wiki katika mkutano wa hadhara ulioshirikisha wakazi wa jimbo hilo na vitongoji vyake uliofanyika katika Uwanja wa Parking.Katika mkutano huo, Dkt. Kigwangalla aliulizwa swali na mkazi wa jimbo hilo kama kweli ana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda, anayetokana na chama chake.
“Mheshimiwa mbunge,naomba utu thibitishie kama una uwezo wa kumng’oa Spika wa Bunge (Makinda), kama ulivyotangaza dhamira ya kuwasilisha hoja binafsi bungeni ili bunge liweze kumng’oa.
“Kwa jinsit unavyofahamu utaratibu ndani ya CCM, huna ubavu wa kufanya hivyo , inaonesha ulikuwa ukijifurahisha tu,”alihoji mwananchi huyo.
Mwananchi huyo aliongeza kuwa, kwa kawaida CCM ina utaratibu wa kuzuia hatua mbalimbali zinazotaka kuchukuliwa na wanachama wake hivyo alimshauri Dkt.Kigwangalla, aacha ne na hoja hiyo kwani hana ubavu wa kumng’oa Bi.Makinda.
Akijibu swali hilo,Dkt. Kigwangalla alisema,si kweli kwamba CCM ina utaratibu wa kuondoa kinyemela hoja ambazo haikubaliani nazo ambapo suala la kutaka kumng’oa Bi. Makinda lipo ndani ya uwezo wake na kufafanua kuwa, hoja hiyo haijaondo lewa na hivi sasa ipo katika hatua za mwisho ili iweze kufikish wa bungeni.
“Kwa hili la kumng’oa Spika wa Bunge,niwaeleze wazi kuwa si kweli linawezaku nishinda... hoja imewasilishwa na Bi.Makin da atang’oka kama nikiamua kuendelea nayo kwa sababu tayari hoja nimeiwasilisha na nimekidhi mashart iyote.
“Hivi tunavyoongea, hoja yangu tayari imetoka hatua ya kwanz a na kukidhi vigezo vyote sasa inaenda hatua y a pili ambayo Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge,itaamua ho ja yangu iingizwe bungeni au isiingizwe,”alisema .
Aliongeza kuwa, baada ya hapo utafuata mcha kato wa mwisho ambao ni hoja hiyo kufikishwa bungeni na yeye kuiwasilisha rasmi mbele ya Bunge ili kufanyiwa uamuzi na wabunge wote kwa kupiga kura na kama atashinda au kushindwa,hilo ni jambo lingine.
Dkt.Kigwangalla alisema uamuzi wa kuondoka au kutoondoka kwa Spika, kutategemea uamuzi wa wabunge wenzake na kusisitiza kuwa , CCM haiwezi kuzuia hoja hiyo bila ya kupatiwa uamuzi na wabunge wote.
Akijibu swali ambalo lilihusiana na fedha za ushuru wa huduma zilizotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Resolute, ulioko wilayani humo, Dkt. Kigwangalla alisema fedha hizo sh. Bilioni 2.340,zililipwa na mgodi huo na sasa zimehifadhiwa katika ak aunti maalumu ili baadaye zitumike kama mtaji wa kuanzishia Ben ki ya Maendeleo ya Wananchi wa Nzega .
“Fedha hizi tulizipigania kwa kiasi kikubwa hadi kuandam ana lakini tulifanikiwa kuzipata, niwathibitishie zipo sa lama katika akaunti maalumu tuliyoianzisha ili baadaye ziweze kuanzisha Benki yetu ya Maendeleo ambayo itaweza kutupa mikopo ya kuendesha shughuli zetu,”a lisema .
Alisema lengo lake ni kuhakikisha fedha hizo zinatumika vizuri ili kuwasaidia wananchi wa Nzega kubadilisha maisha yao ambapo watu watahamasishwa kujiunga katika ushirikaau SACCOS ili waweze kupewa mikopo pia zitatumika kununulia mitambo ya kutengeneza barabara na uchimbaji visima vya maji.
Gazeti moja linalotoka kila siku (si Majira), liliandika habari inayosema Dkt. Kigwangalla anadai Bi. Makinda amekiuka kanuni kwa kuidhinisha malipo ya sh. 430,000 kama posho kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, tofauti na wajumbe wa kamati nyingine ambao malipo yao ni sh. 180,000 kwa siku.
Hoja hiyo ilipingwa vikali na baadhi ya wabunge akiwemo Mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Aden Rage (CCM) na Mbunge wa Kigoma Kusini, Bw. David Kafulila (NCCR-Mageuzi) ambao walidai hawaoni sababu ya kumuondoa Bi. Makinda madarakani.
Bw. Kafulila alisema hilo ni suala la wana-CCM, kwani Bi. Makinda aking’olewa madarakani, mtu ambaye ataziba pengo lake hawezi kutoka upinzani. Hoja hiyo ya Dkt. Kigwangalla iliibua mjadala kwa baadhi ya wabunge na wengine kukataa kusaini karatasi ambayo walipelekewa ili kuunga mkono.
Mbunge wa Ludewa, mkoani Njombe, Bw. Deo Filikunjombe, alisema hoja ya Dkt. Kigwangalla imejengwa katika msingi hafifu isiyozingatia masilahi mapana ya nchi na mtazamo finyu
Posted: 12 Nov 2013 12:36 AM PST
  • SASA WAFIKIA TISA, WAKUTWA NA MAPANGA,SIMU YAKE
 Rehema Maigala na Isaya Ng wijo
Jeshi la Polisi nchini, linawashikilia watuhumiwa tisa wanaosh ukiwa kumvamia, kumjeruhi na kuiba vitu mbalimbali vya Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu yaC hama cha NCCR-Mageuzi, Dkt.Sengondo Mvungi.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Sa laam jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Emmanuel Nchimbi,alis ema kukamatwa kwa watuhumiwa hao, kumechangiwa na ushirikiano uliotolewa na familia ya Dkt. Mvungi.
Alisema watuhumiwa hao wamekamatwa jijini Dar es Sa laam kwa nyakati tofauti ambapo awali walikamatwa sita lakini majina yao yalifichwa ili kutovuruga upelelezi.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova,ambaye alikuwepo katika mkutano huo, waliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Msigwa Mpopela (30) ,Shabago Magozi na Hamadi Ally, jina maarufu‘Hatibu’.
Wengine ni Zakaria Raphael (dereva wa bodaboda), Mmanda Saluwa,Juma Hamisi,Longisho Semeriko(muuza ugolo), Paul Jeirosina mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Kilimimazoka,am bao wote ni wakazi wa Dar es Salaam.
“Watuhumiwa hawa walikutwa na mapanga, kigoda ambavyo vim ethibitika kuwa vilitumika katika tukio hilo, pia wa likutwa na simu ya m kononi mali ya Dkt. Mvungi,”alisema.
Kamishna Kova alisema, katika mahojiano ya awali na watuhumiwa, walikiri kuhusika na tukio hilo na ushahidi umekamilika kwa asilimia 80.
“Watuhumiwa wote wamekiri kosa hivyo tunakamilisha upelelezi ili wafi kishwe mahakamani mara moja,”alisema .
Dkt. Mvungi alivamiwa, kujeruhiwa na watu wanaodhaniwa kuwa majambazi usiku wa kuamkia Novemba 3 mwaka huu , nyumbani kwake Kibamba, Dar es Salaam.
Hivi sasa,Dkt. Mvungi anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Milpark, nchini Afrika Kusini na hali yake inaendelea kuimarika .
Akizungumzia suala la kuwakamata wahamiaji haramu, Dkt.Nchimbi alisema mpango walionao ni kuweka Ofisa mmoja wa Polisi kila Tarafa nchini aweze kusaidiana na Polisi Jamii pa moja na wananchi kuwabaini watu hao.
Posted: 12 Nov 2013 12:52 AM PST
 Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Ofisi ya Katibu Mkuu wa chama hicho imepokea barua iliyoandikwa na Naibu Katibu Mkuu, Bw. Zitto Kabwe, anaripoti Rose Itono.

Barua hiyo, inamtaka Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt
 Wilbrod Slaa athibitishe madai ya ripoti inayosema“Taarifa ya Siri ya CHADEMA”iliyosamba zwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
Taarifa hiyo inadai kuchunguza mwenendo wa Bw.Kabwe tangu mwaka2008-2010 na kubaini amepokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuivuruga CHADEMA.
Akizungumza na Majira jana, Ofisa Habari wa CHADE MA,Tumaini Makene,alisema barua aliyoiandika Bw. Ka bwe itafanyiwa kazi kwa mujibu wa taratibu, kanuni za katiba ya chama.
“Chama chetu kinaongozwa na vikao hivyo barua yake itafanyiwa kazi...CHADEMA haiendeshwi na taarifa za magazetini au mitandaoni,”alisema Bw. Makene.
Aliongeza kuwa,si mara ya kwanza makundi yasiyojulikana kusambaza taarifa za kutaka kumchafua Bw. Kabwe kupitia mitandao hiyo ambapo Ofisi ya Habari,ilishughulikia suala hilo na kuhakikisha taarifa hizo zinaondolewa .
“Hivi sasa ni mara ya pili, Bw. Kabwe anali fahamu hilo hivyo CHADEMA hakihusiki, lakini kitashughulikia s uala hili kupitia vikao ili kupata majibu sahihi,” alisisitiza Bw.Makene.
Katika taarifa yake aliyoitoa juzi kwa vyombo vya habari, Bw.Kabwe alisema taarifa hizo zimesambazwa katika mitandao ya kijamii hivyo alimtaka Dkt.Slaa, athibitishe ki nachoitwa“Taarifa ya Siri ya CHADEMA”,kama ni taa rifa ya chama au kuikanusha ili kumpa fursa ya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya waandishi wa taarifa hiyo.
Hata hivyo, Bw. Kabwe ambaye pia ni Mbunge wa Kig oma Kaskazini,aliziita taarifa hizo za kutunga zilizojaa uongo wa kiwango cha kutisha hali ambayo imemfedhehesha, kumsikitisha na kumkasirisha.
Alisema taarifa hizo ziliibuliwa katika kipindi ambach o alikuwa safarini kutetea haki zaWatanzania na Afrika amb ao utajiri wao wa rasilimali unafaidiwa na watu wachache waliohifadhi fedha katika akaunti nje ya nchi.

Posted: 12 Nov 2013 02:46 AM PST

   Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba, amestaafu rasmi kazi kwa mujibu wa sheria baada ya kufikisha umriwamiaka 60.Katika utumishi wake ndani ya Jeshi la Polisi, amefanya kazi katika nyadhifa mbalimbali zikiwemo chumba cha kupokea mashtaka kuanzia mwaka (1976-1977).

  Nafasi nyingine ni Mwendesha Mashtaka Wilaya ya Kibondo na Kasulu, mkoani Kigoma (1977- 1984), Mkufunzi wa Chuo cha Polisi Dar es Salaam, (1984-1987), Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Magomeni, Kinondoni na Naibu Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (1987-1993),
  Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Msemaji wa jeshi hilo, SSP Advera Senso, ilisema Manumba pia aliwahi kuwa Mkuu wa Upelelezi mkoani Arusha (1993- 1995), Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Polisi Moshi (1995-1996) na Mkuu wa Kitengo cha Fraud Makao Makuu ya Upelelezi (1996-1997).
  Nafasi nyingine Mkuu wa Kitengo cha Usalama wa Nchi, Intelijensia na Dawa ya Kulevya Makao Makuu ya Upelelezi (1997- 2001) na Msaidizi wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (2001-2006).
 Alisema kuanzia 2006 hadi anastaafu, alikuwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI).Mkuu wa jeshi hilo nchini, IGP Said Mwema, amemshukuru Manumba kwa kulitumikia Taifa katika nyadhifa mbalimbali ndani ya jeshi hilo kwa weledi na uaminifu mkubwa wakati wote wa utumishi wake.
  Alimtaka aendelee kuwa msaada kwa jeshi hilo, kutoa ushirikiano wa namna yoyote unaoweza kupunguza uhalifu nchini kwa sababu suala la usalama ni taaluma kama zilivyo taaluma zingine na taaluma hiyo wanayo watu wachache.
  SSP Senso alisema, wakati taratibu za uteuzi wa DCI mpya zikiendelea, Mkuu wa Ufuatiliaji na Tathmini CID Makao Makuu, Kamishna Isaya Mungulu, atakua akikaimu nafasi hiyo.
Posted: 12 Nov 2013 03:00 AM PST


Na Elizabeth Joseph, Dodoma
  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimepanga kuiburuza mahakamani Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kosa la kubomoa nyumba za wananchi bila fidia.

Uamuzi huo ulitolewa juzi na Mkurugenzi wa Organizesheni na Mafunzo Taifa (CHADEMA), Benson Kigaila wakati akihutubia wananchi katika mikutano wa hadhara uliyofanywa katika Kata ya Mkonze na Kikuyu Kusini mkoani humo ambapo alisema kuwa hivi karibuni wakazi wa maeneo hayo walitangaziwa kubomolewa nyumba zao na CDA kwa madai kuwa wameyavamia.
Kigaila aliwataka wananchi wanaoishi katika maeneo hayo kujiorodhesha majina yao ili kupitia chama hicho waweze kutafuta wakili kwa ajili ya kuweka pingamizi la kusitisha ubomoaji huo.
Kigaila alisema kuwa CDA ilitakiwa kufanya kazi ya kustawisha mji na kuondoka lakini cha kushangaza hadi leo bado iko Dodoma na kuwanyanyasa wananchi kwa kuwauzia viwanja kwa bei ya kiasi kisichopungua milioni 5 pindi wanapohitaji viwanja na wakati mwingine kufukuzwa katika ardhi ambazo wamezikuta toka enzi za mababu zao jambo ambalo ni kuwanyima haki ya kumiliki ardhi yao.
  Hivyo ili kutetea haki ya wananchi chama hicho kimeona ni vyema kuungana na wananchi katika kuishtaki Mamlaka hiyo ili kujua suluhu ya wakazi wa mkoa huu .
  Aliongeza kuwa hata chama kilichopo madarakani (CCM) kimekuwa kikifumbia macho kero za wananchi wa mkoa huu kuhusiana na Mamlaka hiyo kwani taarifa juu ya CDA inajulikana lakini kimekuwa kikipiga danadana katika kutoa uamuzi wa kuiondoa mamlaka hiyo ili wazawa waweze kujua suluhisho la maisha yao katika kumiliki ardhi ambayo walifukuzwa bila kulipwa fidia.
  Aidha, aliwataka wananchi kwa pamoja kupinga suala la CDA kuvunja maeneo yao bila fidia na kuungana na chama hicho katika kutetea haki yao ili waweze kuishi kwa amani katika ardhi ya nchi yao pamoja na kuwataka wananchi kuondoa ukereketwa wa vyama ili kufanikisha suala hilo.
  Mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mussa Ndalu katika Kata ya Mkonze alisema kuwa Chama kilichopo madarakani ndio kinaoongoza kwa kuwagawanya Watanzania kwa kuyafumbia macho malalamiko ya wananchi juu ya umiliki wa ardhi ya nchi yao huku wageni wakipewa kipaumbele katika suala hilo.
Posted: 12 Nov 2013 03:05 AM PST


  •   AL AHLY BINGWA AFRIKA
MANCHESTER, Uingereza
  Mholanzi Robin van Persie juzi aliizamisha klabu yake ya zamani, Arsenal akiifungia bao pekee la ushindi Manchester United na kuirejeshea matumaini ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England.

 Van Persie alifunga bao tamu kwa kichwa akiunganisha kona iliyochongwa kitaalamu na Wayne Rooney dakika ya 27 Uwanja wa Old Trafford.
Kikosi cha Man United kilikuwa; De Gea, Smalling, Vidic/Cleverley dk45, Evans, Evra, Valencia, Jones, Carrick, Kagawa/Giggs dk78, Rooney na Van Persie/ Fellaini dk85.
Arsenal; Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta/Gnabry dk82, Flamini/Wilshere dk61, Ramsey, Ozil, Cazorla/Bendtner dk78 na Giroud.
CAIRO, Misri
TIMU ya Al Ahly ya Misri, imenyakua taji la Klabu bingwa Afrika baada ya kuicharaza Orlando Pirates ya Afrika Kusini mabao 2-0 katika mechi ya fainali ya pili iliyopigwa juzi katika Uwanja wa Arab Contractors jijini Cairo. Al Ahly, wamejinyakulia kombe hilo kwa mara ya saba.
Hata hivyo, kulikuwa na ripoti za vurugu kuzuka kati ya mamia ya wafuasi wa Al Ahly na polisi nchini Misri, kabla ya mechi kuanza.
Baada ya vurugu kusitishwa mchezaji mkongwe, Mohamed Aboutrika ndiye aliyefunga bao la kwanza dakika ya 54. Dakika ya 78, Ahmed Abdul Zaher aliipatia Al Ahly bao la pili.
Hata hivyo, mabingwa hao wa Misri walipata pigo baada ya beki wake, Sherif Abdel Fadil kutolewa na mwamuzi kwa kadi nyekundu kutokana na kumfanyia dhihaki mchezaji wa Orlando Pirates, Daine Klate.
Pirates, ambao ni mabingwa wa mwaka 1995, walicheza kwa nguvu zote, lakini walikosa nguvu baada ya Al Ahly kupata bao la pili katika mechi hiyo iliyokuwa na mashabiki lukuki.
Hata hivyo, mabingwa hao wa Afrika Kusini walikosa nafasi nyingi za kufunga katika mechi hiyo.
Baada Al Ahly kunyakua kombe hilo walizawadiwa kitita cha dola milioni 1.5 za Marekani, Pia watawakilisha Afrika katika Kombe la Dunia la Klabu Bingwa Duniani litakalofanyika nchini Morocco mwezi ujao.
Kabla ya mechi hiyo mamia ya mashabiki wa Ahly walikabiliana na polisi ambao walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya mashabiki waliokuwa wakitupa mawe huku wakilazimisha kuingia uwanjani kwa nguvu.
Ni mechi ya kwanza kubwa, ambako mashabiki waliruhusiwa kuingia uwanjani tangu mashabiki wa Al Ahly, walipouawa katika mechi iliyokumbwa na vurugu mwaka jana.

ZIARA YA RAIS KIKWETE WILAYANI MBOGWE, BARABARA YAPANDISHWA DARAJA

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiweka jiwe la msingi kuashiria uzinduzi rasmi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Uyovu yenye urefu wakilometa 45 inayojengwa kwa kiwango cha lami mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (aliyeshika mkasi) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Uyovu yenye urefu wa kilometa 45 inayojengwa kwa kiwango cha lami mkoani Geita. Kulia kwa Rais ni Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na kushoto kwa Rais ni Mbunge wa Bukombe Mhe. Kulikoyela Kahigi kutoka CHADEMA. Wengine ni baadhi ya Mawaziri na Viongozi wa Kitaifa na kutoka mkoa wa Geita waliokuwepo katika sherehe hizo.
 Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (aliyeshika kipazasauti) akitoa taarifa kwa wananchi wa Iboya waliousimamisha msafara wa Rais Kikwete alipokuwa kwenye ziara ya kikazi katika Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Kiongozi wa Kikundi cha Mchelemchele kilichotumbuiza wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Uyovu inayojengwa kwa kiwango cha lami mkoani Geita.
Kikundi cha Mchelemchele kutoka Mwanza kikitumbuiza wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Uyovu inayojengwa kwa kiwango cha lami mkoani Geita.
===============================================================
 
ZIARA YA RAIS KIKWETE WILAYANI MBOGWE, BARABARA YAPANDISHWA DARAJA
Wananchi wa wilaya ya Mbogwe mkoani Geita wamenufaika kwa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kusikilizwa ombi lao ambapo barabara inayounganisha maeneo ya Masumbwe na Makao Makuu ya wilaya hiyo imepandishwa daraja na kuwa barabara ya mkoa. Awali barabara hiyo ilikuwa ikihudumuwa na wilaya lakini ikipatiwa matengenezo ambayo hayakidhi ongezeko la magari yanayotumia barabara hiyo kwa sasa.

Mheshimiwa Rais akiwa njiani kutokea mji wa Masumbwe kupitia makao makuu ya wilaya mpya ya Mbogwe kabla ya kuingia Geita alisimamishwa mara kadhaa na wananchi wanaoishi katika vijiji inakopita barabara hiyo ambao walitumia fursa hiyo kuwasilisha kero zao na hususan suala la barabara ambayo ilielezewa kutokidhi mahitaji halisi kwa wakazi hao na maeneo jirani.

Akijibu maombi ya wananchi hao, Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alielezea kuwa barabara hiyo inayolalamikiwa kwa hivi sasa iko chini ya usimamizi wa wilaya husika. Hata hivyo, kwa kuzingatia umuhimu wa barabara husika na uchanga wa wilaya hiyo mpya, alikipokea kilio cha wananchi hao na kukubali barabara hiyo ipandishwe  daraja na kuwa ya mkoa.

“Nitatumia mamlaka niliyopewa chini ya Sheriaya Mfuko wa Barabara Namba 13 ya mwaka 2007  kuipandisha barabara hii ambayo inaanzia Masumbwe kupitia Mbogwe,  Nyikanga hadi Butengo Lumasa yenye urefu wa kilometa 81 kwamba itakuwa ya mkoa na hivyo kuwa chini ya usimamizi wa Tanroads” alisemaWaziri Magufuli.

Aidha, katika hatua nyingine Mheshimiwa Magufuli  alibainisha kuwa katika mipango ya mwaka ujao wa fedha wa 2014/2015, wizara yake itaanza kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara inayotokea mji wa Katoro hadi Ushirombo yenye urefu wa kilometa 56 ili kuijenga kwa kiwango cha lami.

Naye Mbunge wa Mbogwe Mheshimiwa Augusto Manyanda Masele kwa upande wake alielezea kufurahishwa kwake na hatua hiyo na hasa katika kipindi hiki ambacho wilaya hiyo mpya inahitaji kuimarisha miundombinu mbalimbali kwa lengo la kuharakisha maendeleo katika eneo hilo.

“Hii imekuwa ni faraja kubwa kwa wana Mbogwe kwani suala la usafiri limekuwa ni kero ya muda mrefu, tunashukuru sana kwa kutembelewa na ugeni huu wa Kitaifa hapa mkoa ni kwetu” alisisitiza Mheshimiwa Masele.

Monday, November 11, 2013

JK ampa rungu Magufuli-Bwanga – Biharamulo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (aliyeshika mkasi) akikata utepe kuzindua rasmi ujenzi wa barabara ya Bwanga – Biharamulo. Kushoto kwa Rais ni Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John P. Magufuli na kulia kwa Rais ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Alhaj Eng. Mussa Iyombe. Wengine katika picha ni baadhi ya Mawaziri, Wabunge na Viongozi wa Mikoa ya Geita na Kagera walioshiriki katika sherehe hizo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimwagilia mti alioupanda katika eneo la Buziku mkoani Geita wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Biharamulo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Waziri wa Ujenzi Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Biharamulo.
Lori aina ya Scania la Kampuni ya MAP CO Ltd. likiwa na usajili namba T 895 AFH/T 226 AGB kama  lilivyokutwa eneo la Manyoni mkoani Singida likiwa limekatika katikati kutokana na kuelemewa na uzito wa mzigo lililoubeba
Umati wa wananchi waliojitokeza kumlaki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alipowasili eneo la Buziku mkoani Geita tayari kwa uzinduzi wa ujenzi wa barabara ya Bwanga – Biharamulo. (Picha kwa Hissani ya Miss Demokrasia  Tanzania)

 
========================================================================
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtaka Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Magufuli kuhakikisha kuwa Sheria ya Usalama Barabarani inasimamiwa vizuri ili kuhakikisha kuwa barabara zinazojengwa nchini zinadumu kwa muda uliokusudiwa.

Akizungumza katika eneo la Buziku mkoani Geita wakati akizindua ujenzi wa barabara ya Bwanga hadi Biharamulo yenye urefu wa kilometa 67, Rais Kikwete alisema kuwa wizara ya Ujenzi ni lazima ihakikishe inasimamia sheria zilizopo na hasa hii ya kutoruhusu magari yenye uzito uliozidi viwango vilivyoainishwa katika Sheria Namba 30 ya Mwaka 1973.

Akisistiza umuhimu wa kutunza barabara Rais Kikwete alibainisha kuwa “adui wakuu watatu wanao sababisha barabara kuharibika mapema ni; magari yanayobeba mizigo zaidi ya uzito uliowekwa kisheria, ujenzi duni usiozingatia viwango na kuachwa kwa maji kuzagaa barabarani”.

Wakati huo huo Rais Kikwete alielezea kufurahishwa kwa kuanza ujenzi wa mradi huo kwani wapo baadhi ya watu waliokuwa waliokuwa wakieneza taarifa kuwa sehemu hiyo ya barabara haiwezi kujengwa lakini sasa wameumbuka.

Awali akitoa maelezo ya mradi huo Mtendaji Mkuu wa Tanroads Injinia Patrick Mfugale alielezea kuwa mradi mradi wa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami umegharimu Shilingi bilioni 55 fedha zote zikiwa zimetolewa na Serikali ya Tanzania. “Mradi huu utajengwa kwa muda wa miezi 27 na hivyo kukamilika mwezi Februari mwaka 2015” alisema Injinia Mfugale.

Naye Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Magufuli alimhakikishia Rais Kikwete kuwa wizara yake itahakikisha kuwa inamsimamia mjenzi wa mradi huo ambaye ni Kampuni ya Sinohydro Ltd. ya kutoka Jamhuri ya Watu wa China ili aukamilishe kwa muda na viwango vilivyokusudiwa na bila ya visingizio vya nyongeza ya gharama.

Akimpongeza Rais kwa kutekeleza ahadi yake, Waziri Magufuli alibainisha kuwa wananchi wa mikoa  ya Geita na Kagera wamefurahishwa sana kuona kuwa hatimaye barabara hiyo muhimu inajengwa kwani hiyo ndiyo sehemu pekee iliyokuwa imebaki ikiwa haina lami kwa barabara inayounganisha mikoa hiyo ya ziwa.