TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, November 9, 2014

TAASISI YA STARKEY HEARING FOUNDATION YASAIDIA WASIOWEZA KUSIKIA MJINI MOSHI

TAASISI ya Starkey Hearing Foundatioin ikitoa huduma ya kliniki kwa kuwawekea vifaa vya kuongeza usikivu masikioni kwa watu zaidi ya 1000 wenye matatizo ya kusikia katika Mkoa wa Kilimanjaro shughuli iliyoanza jana kwenye viwanja vya Shree Hindu Mandal vilivyopo kando ya barabara ya Mawenzi mjini Moshi .
unnamedMwanzilishi wa taasisi hiyo, Bill Austin na mkewe Tani wamekuwa wakiongoza zoezi hilo toka lilipoanza majira ya saa mbili asubuhimjini Moshi jana.
unnamed1 unnamed2ESTHER Urassa ambaye naye ana tatizo la kusikia akipewa huduma hiyo kabla ya kuwasaidia wenzie.
unnamed3 unnamed4Lina John ambaye ni kipofu akipima kiwango cha sauti kwenye kidevu chake ili kama mtoto Ronald anaweza kusikia mara baada ya kuwekewa kifaa cha kuongeza usikivu:

HII NDIO BARABARA ILIYOKARABATIWA KWA MILIONI 90 UKONGA MAZIZINI- MOSHI BAR

 Hii ndio ile barabara ya Ukonga Mazizini- Moshi Bar ambayo inadaiwa kugharimu kiasi cha shilingi Milioni 90 kuikarabati kwa kiwango cha changarawe kwa umbali wa kilometa tatu. Picha hizi ni madimbwi ya mwanzo tu ya hizo kilometa tatu.(Picha na Father Kidevu Blog).
Meya Jerry Silaa wa Ilala ambaye ni Diwani wa Gongo la Mboto alipotembelea aliwaambia wananchi kuwa fedha za ujenzi huo ni kutoka mfuko wao ni . PICHA ZA CHINI NI SIKU MEYA SILAA ALIPOTEMBELEA UJENZI WAKE. 
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala Jerry Silaa Jana amefanya ziara fundi ya ukaguzi wa
ujenzi wa barabara ya ukonga Moshibarkilometa 3 kiwango cha changalawe awamu yakwanza. Ikiwa ni
utekelezaji wa miradi yadharura kulingana na uharibifu wa miundo mbinuulitokea baada
ya Mvua kubwa. Mradi huoambao unaghalimu kiasi cha shilingi millioni 90.Pesa za
Ujenzi huohizo zinatoka Halmashauri ya Manispaa ya Ilala.Pia Barabara hiyo
itawekwa Lami kwa awamu ya pili ndani ya mwaka huu kwa kilomita tatu.
Greda likirekebisha Barabara ya Ukonga-mazizini kulekea moshi bar
Mwonekano wa Bara barabara hiyo

MWANZA WAIKUBALI WINDHOEK WAFURAHIA MPANGO WA MABIBO BIA KUJENGA KIWANDA

 Wadau wa Windhoek ndani ya Villa Park Resort 
katika promosheni hiyo.
 Hapa shughuli imepamba moto waalikwa wakimsikiliza Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr.James Rugemalira.
 
Dotto Mwaibale
WAKAZI wa jiji la Mwanza na mikoa jirani ya Kanda ya Ziwa, wamefurahishwa na uwekezaji unaotarajiwa kufanywa na Kampuni ya Bia ya Mabibo (MBL) kwa ajili ya kujenga kiwanda cha bia za Windhoek.
Wakizungumza katika promosheni iliyoandaliwa na kampuni hiyo jijini Mwanza juzi katika  ukumbi wa Villa Park Resort, wanachi hao walionesha kuguswa na uwekezaji huo na kushauri kijengwe kiwanda hicho jijini Mwanza.
Walisema kujengwa kwa kiwanda hicho kutachochea kasi ya maendeleo  ya kiuchumi na kuongeza ajira kwa vijana wa Kanda ya Ziwa.
Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr James Rugemalira alisema lengo la kufika Mwanza ni kupata mawazo mapya na ushauri wa nini kifanyike katika uwekezaji huo jijini humo.
“Tumeamua tuje Mwanza na kuomba ushirikiano wenu na rai yangu ni kupata maoni yenu ili tukipata fursa tuwe na viwanda vidogo vidogo,lakini si sawa na Tanzania Breweries (TBL),maana hatuwezi kushindana nao,” alisema Rugemalira.
Alisema ushindani wa haki ni lazima kila mtu apate haki ya kushinda,na wataka waweke misingi hiyo kwanza katika mikoa ya Mwanza, Kagera, Mbeya na Mtwara kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo.
Aliwataka wananchi wa kanda ya ziwa kuwaonesha  na kuwaunga mkono ili wazalishe kinywaji cha windhoek Mwanza badala ya kuagiza kutoka nje ya nchi kama ilivyo sasa,ambapo kinywaji hicho kinagizwa kutoka nchini Namibia.
“Mtu anaweza kunipa ushauri au akaniamuru atakavyo ili nijitambue na ni vema kukubaliana na ushindani  bila hivyo hatuwezi kupata maendeleo na malengo ya kampuni yetu ni kushirikiana na serikali kukabiliana na uhaba wa ajira kwa Watanzania kwa kujenga viwanda hivyo ”alisema Rugemalira.
Meneja Masoko wa Kampuni ya Mabibo Bia (MBL), Kanda ya Ziwa, Godfrey Mwangungulu alisema Bia ya Windhoek imewahi kushinda medali za juu saba  kwa ubora Barani Afrika tangu ianze kuzalishwa mwaka 1920.
 
“Bia ya Windhoek ilishinda tuzo hizo mfufulizo kuanzia mwaka 2007, 2008, 2009,2010,2011,2012  na 2013. 

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MKUTANO WA MAADHIMISHO YA MIAKA 20 YA MAHAKAMA YA MAUAJI YA KIMBARI YA RWANDA ICTR JIJINI ARUSHA.

unnamedMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia kwenye Maadhimisho ya miaka 20 ya Mahakama ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), ulioanza leo Novemba 8, 2014 kwenye Ukumbi wa AICC Jijini Arusha. Picha na OMR
unnamed1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia kwenye Maadhimisho ya miaka 20 ya Mahakama ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), ulioanza leo Novemba 8, 2014 kwenye Ukumbi wa AICC Jijini Arusha. Picha na OMR
unnamed2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitazama baadhi ya picha za kumbukumbu za Mahakama ya Kimbari zilizo katika ukumbi huo wakati akiondoka baada ya kufungua rasmi Mkutano wa Maadhimisho ya miaka 20 ya Mahakama ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda ICTR, ulioanza leo Novemba 8, 2014 kwenye Ukumbi wa AICC Jijini Arusha. Picha na OMR
unnamed3 Baadhi ya washiriki waliohudhuria mkutano huo wakimsikiliza makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia. Picha na OMR unnamed4 Baadhi ya washiriki waliohudhuria mkutano huo wakimsikiliza makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia. Picha na OMR unnamed5 Baadhi ya washiriki waliohudhuria mkutano huo wakimsikiliza makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia. Picha na OMR unnamed7Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya washiriki wa mkutano huo wa maadhimisho ya miaka 20 ya Mahakama ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR), ulioanza leo Novemba 8, 2014 kwenye Ukumbi wa AICC Jijini Arusha. Picha na OMR

Lilian Kamazima Miss Tanzania 2014 baada ya Sitti Mtemvu kujiuzuru na kuvua taji

2Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania akizungumza na waandishi wa habari wakati akitangaza kujiuzuru kwa Sitti Mtemvu  aliyekua Miss Tanzania 2014 baada ya kuzuka Sintofahamu kuhusu Umri wake, Lundenga amesema Sitti Mtemvu aliandika barua ya kujivua taji na kuiwasilisha kwa kamati ya Miss Tanzania Novemba 5 2014 ambapo kamati hiyo imeridhia kujiuzuru kwake na kumvua taji , Hivyo taji hili na majukumu ya Miss Tanzania sasa yatachukuliwa na mshindi wa pili Lilian Kamazima aliyekaa kushoto katika picha   ambaye taratibu za Miss Tanzania zinamruhusu kuchukua jukumu hilo, Hashim Lundenga ametangaza uamuzi huo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye hoteli ya JB Belmonte jijini Dar es salaam 3Miss Tanzania 2014  Lilian Kamazima  akizungumza na waandishi wa habari kuelezea furaha yake baada ya kamati ya Miss Tanzania kumvisha taji hilo kutokana na kujiuzuru kwa Sitti Mtemvu aliyekuwa Miss Tanzania, Kulia ni Hashim Lundega Mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania. 1Hashim Lundega Mkurugenzi wa kamati ya Miss Tanzania akionyesha barua iliyowasilishwa kwa kamati hiyo na Bi. Sitti Mtemvu mara baada ya kujiuzuru Umiss Tanzania na kujivua taji hilo.

DR. SHEIN YUPO PEMBA


4Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein na Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar akisalimina na Viongozi mbali mbali alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Karume Pemba leo. (Picha na Ramadhan Othman Ikulu) unnamed

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA IJITIMAI YA KIMATAIFA MJINI MOROGORO

unnamed3Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati akifungua rasmi semina ya mafunzo ya Kiislamu (IJITIMAI) iliyofunguliwa  Novemba 7, 2014 kwenye Msikiti wa Jabalhira, mjini Morogorogo. 
Picha na OMR 
unnamed4Sehemu ya waumini wa dini ya kiislam waliohudhuria hafla hiyo ya ufunguzi wa IJITIMAI, wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akihutubia. Picha na OMR
unnamed6Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waumini wa dini ya kiislamu wakati akiondoka baada ya kufungua rasmi IJITIMAI hiyo katika msikiti wa Jabalhira, mjini Morogorogo. Picha na OMR

Sitti Mtemvu amejivua taji la Miss Tanzania 2014

Barua ya aliyekuwa Miss Tanzania 2014 Sitti Abbas Mtemvu aliyowaandikia Lino International Agency kuhusu uamuzi wake wa kujivua taji hilo.
Barua ya aliyekuwa 
Miss Tanzania 2014, 
Sitti 
Abbas Mtemvu, 

aliyowaandikia Lino International Agency
 kuhusu uamuzi wake 
wa
 kujivua taji hilo.
Hatimaye aliyekuwa mrembo wa Tanzania 2014 (Redd’s Miss Tanzania 2014), Sitti Abbas Mtemvu, ametangaza kujivua taji hilo. Taarifa News imebaini.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga, amesema Sitti amechukua hatua hiyo kutokana kuzongwa na madai ambayo amesema si ya kweli.
Lundenga amesema waandaaji wa Miss Tanzania wamekubaliana na uamuzi huo kumvua taji Sitti ambaye ni mtoto wa mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu.
Badala yake taji limeenda kwa Lilian Kamazima aliyekuwa mshindi wa pili katika mashindano hayo yaliyozua tafran mbaya zaidi tangu kuanza kwa Miss Tanzania.
Taarifa zinaeleza kuwa mrembo huyo aliitumia barua kamati ya uandaaji wa Miss Tanzania iliyoeleza uamuzi wake wa kuvua taji hilo.
Baada ya kukabidhiwa taji la Redd’s Miss Tanzania 2014 Oktoba 11, siku chache baadaye Sitti alikumbwa na kashfa ya kudanganya umri baada ya kuonekana kuna utofauti wa umri kati ya leseni na pasipoti yake.

SUNDERLAND DOES IT AGAIN AT WTM-TANZANIA STAND

unnamed unnamed1
By  Ayoub  mzee
Today was the final day of WTM 2014 at ExCeL London. Sunderland AFC continued  to strengthen its links with  Tanzania in particular, following the signing of a ground-breaking business partnership, which sees the country become the ‘Official Destination Partner’ of Sunderland AFC.
 
Once  again  Sunderland  officials  were  present  at  the  Tanzania’s  stand  at  the  world  travel  market  not  only  to give  support   to  Tanzania  Tourist  board  as  tourism is a key factor in the upward growth of the Tanzanian economy and the partnership aims to use the global reach of the Barclays Premier League to promote the country as a tourist destination. Premier League football is watched in over 200 countries, with accumulative audience of a phenomenal 4.7 billion, making it the most watched sporting league in the world but   also  free  tickets  were  offered  through  a  rafle   to  watch  a match  between Sunderland   and  Chelsea. Present  was  the  Tanzania  high  commissioner  H.E  Peter  kallaghe and  other  dignitaries .

Mwimbaji wa zamani wa Twanga Pepeta, Hamis Kayumbu 'Amigolas' AFARIKI DUNIA.

Mwimbaji wa zamani wa Twanga Pepeta, Hamis Kayumbu 'Amigolas' enzi za uhai wake.
MWANAMUZIKI wa  zamani wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’, Khamis Kayumbu ‘Amigolas’  amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa siku kadhaa.
Amigo alilazwa Muhimbili kwa matatizo ya moyo ambapo taratibu za kufanyiwa upasuaji zilikuwa zikiandaliwa lakini mauti yakamkuta kabla ya lolote kufanyika.

Mwimbaji huyu ambaye hadi anafariki, alikuwa mtumishi wa bendi ya Ruvu Stars inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
Amigo alikuwa mmoja wa wanamuziki waasisi wa Twanga Pepeta, akaitumikia kwa uaminifu mkubwa kwa miaka mingi kabla ya mwanzoni mwa mwaka huu yeye na wenzake kadhaa kuanzisha Super Stars Band ambayo baadae ikachukuliwa na JKT na kuwa Ruvu Stars Band.
 Akiwa Twanga Amigo akajijengea umaarufu wa aina yake na kuwa kama moja ya nembo ya bendi, katika utumishi wake uliotukuka ndani bendi hiyo, akafanikiwa kutunga wimbo mmoja 'AMINATA'  ambao ulikamata chati kwa miaka mingi tangu ulivyorekodiwa mwaka 2003.
Kufariki kwa Amigo ni pengo kubwa kwa Ruvu Stars hasa kutokana na ukweli kuwa yeye ndiye alikuwa
‘injinia’ wa mipango yote kuanzia Super Stars hadi Ruvu.
Kabla ya Twanga Pepeta, Amigo aliitumikia pia bendi ya Bicco Stars chini ya Kinguti System.

Msiba uko nyumbani kwa mama mzazi wa marehemu Mburahati jijini Dar es Salaam jirani kabisa na Shule ya Msingi Mianzini na taratibu za mazishi zinasubiri ndugu na jamaa kutoka Tabora na Kigom

LEO KATIKA UKUMBA WA MANYARA MSHIKE MSHIKE WA NGUMI MANZESE DAR ES SALAAM.

BONDIA Samsoni Maisha wa kyela Mbeya amewasili jijini Dar es salaam na kutamba kunyakuwa ubingwa wa TPBO kwa kumpiga Ibrahimu Tamba wakati wa mpambano utakaofanyika novemba 9 mwaka huu katika ukumbi wa Manyara Park Manzese Dar es salaam
mpambano huo wa raundi kumi kugombania ubingwa wa taifa unaotambuliwa na TPBO utatanguliwa na mpambano mwingine wa ubingwa kati ya julius Kisarawe na
Moro Best mpambano wa raundi kumi pia mwandaaji wa mpambano huo Jafari Ndame amesema maandalizi yote yapo tayali hivyo wanasubili siku tu kukamilisha mpango mzima
Aliongeza kuwa siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi ambapo Karim Ramadhani atapambana na Stevin Kobelo na Robinson Msimbe atamenyana na Fadhili Boika na mipambano mingene mikali zaidi siku hiyo kutakuwa na michezo ya utangulizi zaidi ya nane yenye raundi sita sita katika mpambano huo siku hiyo kutakuwa na ulinzi wa kutosha kabisa kutokana na kujipanga vizuri katika swala hilo kingilio ni shilingi, 5000; kwa kila mtu mchezo huu utapambwa na burudani mbalimbali siku hiyo pia kutakuwa zikiuzwa DVD mpya za masumbwi ambazo zinaonesha mafunzo mbalimbali ya mchezo wa ngumi yanavyoanza hatua kwa hatua mpaka kujua kitu kamili katika mchezo huo pia kunakuwa na mapambano ya mabondia mabigwa wa dunia wa mchezo huo kama Floyd Maywether, Manny Paquaio,mike Tyson, Mohamed Alli pamoja na mabambano ya ngumi ya ndani

MKUTANO MKUU WA PILI WA CHAMA CHA USHIRIKA CHA AKIBA NA MIKOPO TCRA

 Meneja Wa Chama Cha Ushirika wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw.Damai J Mapunda Akitoa Muongozo Jinsi gani Mkutano Utakavyo Endeshwa  
Mwenyekiti Wa Chama Cha Ushirika cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Erasmo A.Mbilinyi Akiwasilisha taarifa aliyo iandaa kwa kipindi Cha November 2013 Hadi September 2014 Katika Mkutano Huo
 Makamu Mwenyekiti Mpya Bi.Mabel Masas Ambapo Chama Cha TCRA SACOSS kiliweza kufanya Uchaguzi Katika Kuendeleza Kuimarisha Chama Na Kisheria Za Chama
Bw.Damian.F.Mashauri Mkaaguzi wa COASCO Ambaye aliwakilisha kwaniaba ya wakaguzi wengine Wanaofanya kazi za Ukaguzi katika Vyama Vya Usharika Hapo akitoa Taarifa ya Ukaguzi katika Mkutano waTCRA SACOS
Dk. Raymond Mfungahema ambaye aliwakilisha ripoti ya upande wa wajumbe wakamati ya
usimamizi waSACOSS ya TCRA
Washarika wakiendelea kufuatilia kwa umakini Mkutano huo
 Miongoni Mwa Wanachama Cha  Ushirika cha TCRA  walio weza kuhudhuriaMkutano wa Pili  
 Bw.Charlse Thomas Mjumbe wa Bodi Akisisitiza jambo katika mkutano huo
 Bw.Abduh Husein Akitoa mchango wake wa mawazo katika Mkutano huo
 Wanachama wakiwa katika mkutano 
 Bw.Francis MAYILA. akiwa ni Mwana Kamati Ya Usimamizi akichangia Maada Iliyokuwa ikiendelea Katika Mkutano huo
Masai John Masai  Akiomba Kura  Ya kuchaguliwa Katika Nafasi ya Kuwa Mjumbe Wa Bodi na Hatimaye kuweza Kunyakuwa Nafasi hiyo Baada ya Wanachama Kumpigia Kura 
Afisa Ushirika Kinondoni Philipo Emannuel Akitoa nasaha katika mkutano huo uliofanyika Katika Ukumbi wa TCRA
Omary Mkamba  Afisa Usharika Ambaye Ndiye Aliyekuwa Akiendesha Maada zote zilizo kuwa Zikiendelea Katika Mkutano Huo