TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, March 16, 2015

Mkutano Mkuu wa TASWA umepangwa kufanyika Julai 25 na 26 mwaka huu mkoani Morogoro

imagesKAMATI YA Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) ilikutana Dar es Salaam jana na kujadili masuala mbalimbali.     
A; MAFUNZO
Kikao kilikubaliana watafutwe wataalamu wa kuendesha mafunzo kwa kada mbalimbali za waandishi wa habari za michezo nchini ili kuongeza ufanisi katika namna ya kuripoti habari za michezo michezo mbalimbali.
Kundi la kwanza litakuwa la waandishi chipukizi ambao wapo chini ya miaka mitano katika taaluma, ambapo mafunzo yao yatafanyika Machi 25 mwaka huu Dar es Salaam yakishirikisha waandishi wa habari chipukizi 30 na wa kada ya kati 10.
Tayari TASWA imepata mdhamini wa mafunzo hayo na kinachofanyika hivi sasa ni uteuzi wa washiriki, ambapo wahariri wa habari za michezo watahusishwa kupendekeza washiriki kutoka katika vyombo vyao.
Wakufunzi wa semina hiyo watakuwa waandishi wa habari wakongwe, walimu wa uandishi wa habari na wataalamu wa michezo mbalimbali nchini. Jumatano Machi 18 TASWA itatangaza mdhamini wa mafunzo ya Dar es Salaam pamoja na majina ya washiriki.
 Awamu ya pili pia itafanyika Dar es Salaamwaandamizi ikihusisha waandishi wa habari za michezo wa kada ya kati 30 na waandishi wa habari waandamizi 10 na itafanyika mwanzoni mwa Mei mwaka huu.
Awamu ya tatu itahusisha waandishi wa habari za michezo waandamizi na wahariri wa habari za michezo na jumla yao itakuwa 40 na  itafanyika mkoani Mtwara Mei 29, 30 na 31 mwaka huu. TASWA ipo hatua za mwisho za mazungumzo na wadhamini wa mafunzo hayo ya Mtwara.
     B; MKUTANO MKUU
Mkutano Mkuu wa TASWA umepangwa kufanyika Julai 25 na 26 mwaka huu mkoani Morogoro, ambapo pamoja na mambo mengine utajadili Rasimu ya Katiba mpya ya chama hicho.
 
Kamati ya Utendaji ya TASWA imeteua kamati maalum ya kushughulikia katiba hiyo, ambapo hivi sasa Katibu Mkuu anawasiliana na wajumbe walioteuliwa katika kamati hiyo na baada ya wote kupewa barua na kukubali uteuzi atatangaza majina hayo.
 
C: Kamati ya Faraja
 
Kikao kilikubaliana kuwa iundwe Kamati ya Faraja kwa ajili ya kuwafariji wanachama wake kutokana na matukio mbalimbali yanayowakuta ikiwemo ugonjwa.
Uamuzi huo umechukuliwa kwa nia ya kuhakikisha waandishi wa habari za michezo wanakuwa wamoja kwa shida na raha kwa vile wamekuwa kama ndugu.
Kwa kuanzia TASWA inawaomba wadau wote kushirikiana na kamati hiyo ambayo jukumu lake la kwanza itakuwa kumsaidia mwandishi mkongwe nchini, Masoud Sanani, ambaye waandishi wengi kwa namna mbalimbali wamepita mikononi mwake.
Sanan hivi sasa ni mgonjwa kwa zaidi ya mwaka mmoja na yupo kwao Zanzibar, ambapo juzi niliwasiliana naye na amesema afya yake inazidi kuimarika siku hadi siku.
Kutokana na hali hiyo TASWA kwa kushirikiana na kamati hiyo imepanga kwenda kumjulia hali Jumapili Machi 22 mwaka huu.Tunaomba wadau waipe ushirikiano kamati yetu.
Walioteuliwa katika kamati hiyo na nafasi zao kwenye mabano ni Angela Msangi (Mwenyekiti), Majuto Omary (Katibu), Zena Chande (Mhazini),  Asha Kigundula, Isakwisa Mwaifuge  na Elias Kambili (Wajumbe).
 
D;MEDIA DAY
Maandalizi kuhusiana na bonanza kwa wanahabari yanaendelea na matumaini ni kuwa litafanyika Aprili 25 mwaka huu jijini Dar es Salaam kama ilivyopangwa.
 
E;MSIBA WA KOCHA MARSH
TASWA imepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha aliyepata kuwa Kocha Msaidizi wa timu ya Taifa ‘Taifa Stars’, Sylivestre Marsh, hivyo inatoa pole kwa familia na wanamichezo wote hapa nchini katika kuomboleza kifo cha kocha huyo.
 Marsh atakumbukwa na waandishi wa habari za michezo kutokana na ukaribu wake na alikuwa na ushirikiano wa kutosha pale alipoombwa kufanya hivyo.

MASHINDANO YA NSSF MEDIA CUP 2015 YAFUNGULIWA

NHIF KUPIMA AFYA NA KUKUSANYA DAMU KWA USHIRIKIANO WA MPANGO WA TAIFA WA DAMU SALAMA KATIKA MIKOA SITA

MOTO WATEKETEZA HOSTELI ZA MABIBO

Taarifa zilizo tufikia muda huu kuwa moja ya bweni la hostel ya mabibo inateketea kwa moto, hadi sasa hakuna mtu aliye dhurika na moto huo na jitihada za kuuzima moto huo zinaendelea.
chanzo cha moto huo mpaka sasa haujafahamika.
baadhi ya wanafunzi wakiwa katika pirika za kuokoa baadhi ya vitu vilivyomo ndani ya jengo hilo.
Muonekano wa moto huo 

Je,wakati umefika kwa vyama vya upinzani kuchukua madaraka?.



Thursday, March 12, 2015

ANGALIA MAISHA YA MTU MWENYE KUWA NA HURUMA: JE NA WEWE UNAWEZA KUWA NA MOYO KAMA HUO?



The creative nature of man to build something useful and harmless for us to use is simply awesome.



Mwarobaini wa utoroshwaji wa madini ya tanzanite nchini kupatikana

1
Kamishna wa Madini Nchini Mhandisi Paul Masanja amesema kuwa Serikali imejipanga kuimarisha ulinzi ndani ya machimbo ya tanzanite ya Mirerani yaliyopo katika wilaya ya Simanjiro, mkoani Manyara Mhandisi Masanja aliyasema hayo mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kwenye kikao chake na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini wanaosimamia sekta za madini kilichofanyika jijini Arusha jana. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ipo mkoani Arusha kwa ajili ya kutembelea miradi mbalimbali ya umeme pamoja na kuzungumza na watendaji. Aidha kamati hiyo, ilikutana na watendaji kutoka Shirika la Umeme Nchini (TANESCO), Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA) na Wakala wa Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kwa ajili ya kupokea taarifa mbalimbali za utekelezaji wa miradi na kutoa maazimio na mapendekezo mbalimbambali. Mhandisi Masanja alisema kuwa Serikali ilijenga uzio wenye urefu wa kilomita 10 kwa gharama ya shilingi milioni 300 na kuongeza kuwa bado serikali ina mpango wa kujenga vibanda kwa ajili ya walinzi ili kupunguza wachimbaji haramu kuingia ndani ya maeneo ya uchimbaji wa madini hayo na kutoroka na tanzanite. Alisema pamoja na kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya mgodi, Serikali imepanga kujenga kituo kikubwa kwa ajili ya biashara ya madini aina ya vito kitakachojulikana kwa jina la “Madini House” ambapo kutafanyika biashara ya madini hali itakayopunguza utoroshwaji wa madini yanayopelekwa nje ya nchi. Aliongeza kuwa uanzishwaji wa kamati ya usalama kwa kushirikiana na mkuu wa wilaya, kituo cha polisi umechangia kuimarishwa kwa ulinzi katika eneo la mgodi na kusisitiza kuwa bado serikali inabuni njia nyinyine zaidi za kisasa kwa ajili ya kudhibiti utoroshwaji wa madini ya tanzanite nje ya nchi. Akielezea changamoto katika eneo ya Mirerani Mhandisi Masanja alisema kumekuwepo na migogoro ya wachimbaji wenyewe kwa wenyewe kugombea ardhi na kutokuzingatia sheria na kanuni za uchimbaji madini hali inayopelekea ajali za mara kwa mara mgodini. “ Kule kwenye eneo la mgodi kuna uchimbaji hatari unaofanyika chini kwa chini ambapo wamejiwekea utaratibu wa kuwa, mchimbaji anapokutana na mwenzake kwenye mkondo wa madini chini ya ardhi, anatakiwa kurudi nyuma hatua kumi lakini bado kumekuwepo na changamoto ya wachimbaji kuvamia maeneo wanayohisi madini yapo bila kuzingatia kanuni za uchimbaji madini,” alisisitiza Mhandisi Masanja Aliongeza kuwa changamoto nyingine ni pamoja na maeneo ya uchimbaji kuwa madogo na kuongeza kuwa ili kukabiliana na changamoto ya migogoro aliwashauri wachimbaji wadogo kuunda umoja kwa kuunganisha maeneo yao na kuomba leseni ya pamoja hali itakayowaongezea kipato huku ikipunguza migogoro isiyo ya lazima. “ Kwa mfano iwapo wachimbaji wataungana ya kuomba leseni ya pamoja na kuchimba madini, kila mchimbaji ana uhakika wa kupata faida ya shilingi milioni 500 kwa mwaka,” alisema Mahandisi Masanja Wakichangia kwa nyakati tofauti wajumbe kutoka Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini waliitaka Serikali kuongeza juhudi zaidi katika usimamizi wa sekta ya madini ikiwa ni pamoja na suala la ulinzi kwenye migodi hususan katika eneo la Mirerani Akichangia hoja katika kikao hicho mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini ambaye ni Mbunge wa Singida (Viti Maalum) Martha Mlata alisema kuwa mbali na kuimarisha ulinzi katika eneo la Mirerani kwa kuweka uzio na vibanda kwa ajili ya walinzi, vitambulisho kwa ajili ya wachimbaji wa mgodini vinatakiwa kutengenezwa vikiwa na majina ya makampuni yanayochimba madini. Alisema kufanya hivyo, kutapunguza wimbi la wachimbaji haramu na wahamiaji wanaoingia katika maeneo hayo na kutoroka na madini hayo. Mlata alisisitiza kuwa makampuni yanayoshindwa kulipa kodi kwa kisingizio cha kupata hasara yasivumiliwe kamwe , ikiwezekana yanyang’anywe leseni za madini. Naye Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Richard Ndassa alisema kuwa muarobaini wa utoroshwaji wa madini ya tanzanite unaweza kupatikana kwa kujenga ukuta mkubwa imara na kuitaka Serikali kuwa na mikakati zaidi kwa ajili ya kuimarisha ulinzi katika eneo la Mirerani. Ndassa alisema kuwa suala la usimamizi wa sekta ya madini halihitaji siasa, na kuwataka wajumbe wa kamati hiyo kuwa wazalendo badala ya kuweka siasa zaidi kwenye usimamizi wa sekta ya madini. “Madini ya tanzanite yanapatikana Tanzania pekee duniani, hivyo ni vyema kuhakikisha madini haya yanalindwa kwa nguvu zote pamoja na usimamizi wake bila kuongozwa na siasa,” alisema Ndassa

Wizara ya vipatia vijiji 10 umeme jua katika Wilaya za Kongwa

1
Jumla ya Vijiji 10 katika Wilaya za Kongwa, Mlele na Uyui vimeunganishiwa umeme kupitia Mradi wa makontena ya kuzalisha umeme kutokana na jua. Mradi huo unatekelezwa na Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, ambapo upo katika hatua ya majaribio na unalenga kuvipatia umeme vijiji vilivyo mbali na mfumo wa gridi ya Taifa. Wizara ya Nishati na Madini wiki hii, ilisaini makubaliano ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya Mradi na Kampuni ya Elektro-Merl ya nchini Austria ambayo ndiyo ilileta na kufunga makontena 14 ya umeme wa jua pamoja na mfumo wa usambazaji umeme kwa nyumba zilizoko katika vijiji husika. Akizungumza mara baada ya kusaini makubaliano hayo, Mwakilishi kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Styden Rwebangira alisema wananchi waliounganishiwa umeme huo wa jua, watapata huduma hiyo bure kwa kipindi cha miaka miwili ya mwanzo ambayo ni ya matazamio. Alisema kuwa, baada ya miaka miwili, kuanzia tarehe waliyosaini makubaliano, wananchi wa vijiji husika wataanza kuchangia fedha kidogo kwa ajili ya ununuzi wa vifaa mbalimbali kama betri na paneli vinavyotumika katika mradi huo, ambavyo vina ukomo wa kutumika. “Vifaa hivi vina gharama kubwa sana, hivyo inabidi kuwa na utaratibu wa kukusanya fedha za kutosha ili kuweza kununua vifaa vingine pindi vilivyopo vinapofikia ukomo wake wa kutumika. Hivyo kila mwananchi anayetumia huduma hii inabidi achangie gharama,” alisema Mhandisi Rwebangira. Aidha, aliongeza kuwa, ili kuhakikisha mradi unatoa matokeo yaliyotarajiwa, inabidi uendeshwe na mtu au kampuni yenye utaalamu wa masuala ya umeme, mitambo ya umeme jua pamoja na uzoefu na ufahamu wa kutosha kuhusu mitambo ya aina hiyo. “Hivyo, kila baada ya miaka miwili, ukiacha kipindi cha majaribio ambapo mradi utakuwa chini ya Wizara, atachaguliwa mtaalamu au kampuni kupitia njia ya ushindani ambaye atalipwa kwa utaratibu utakaokubaliwa katika mkataba,” alisema Rwebangira. Kwa upande wake, Ofisa wa Wizara aliyefika kushuhudia utiaji saini makubaliano ya kukamilika kwa awamu ya kwanza ya mradi, Paul Kiwele alisema Wizara ilifanya tathmini ya kuchagua vijiji kwa ajili ya majaribio ya mradi huo ambapo vigezo mbalimbali vilitumika. Kiwele alivitaja vigezo hivyo kuwa ni pamoja na Kijiji husika kuwa mbali na gridi ya Taifa, kutokuwa katika mpango wa kufikiwa na miradi ya umeme ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) hivi karibuni. Alitaja vigezo vingine kuwa ni nyumba za Kijiji husika kuwa karibu pamoja na uwepo wa matumizi ya kiwango cha umeme utakaozalishwa. “Aidha, kwa kuwa mradi huu ni wa majaribio, ililengwa kupata mikoa mitatu tofauti ili uzoefu utakaopatikana utumike katika uendelezaji teknolojia hii katika maeneo mengine ya nchi,” alisema. Naye, Mtaalam kutoka Kampuni ya Elektro Merl, Mhandisi Hannes Merl akizungumzia mkataba uliosainiwa na Wizara pamoja na Kampuni yake, Januari mwaka jana kuhusu utekelezaji wa mradi husika, alisema mbali na kufunga makontena 14 ya umeme wa jua pamoja na mfumo wa usambazaji umeme, mkataba pia ulihusisha ufungaji wa waya, taa, swichi na soketi moja kwa kila nyumba iliyofikiwa. Mhandisi Merl alisema kila kontena lina uwezo wa kuzalisha kWp 13.75 ambapo kila nyumba ya makazi na huduma za biashara zimetengewa W 250 na taasisi za kijamii zimetengewa W 500. Aliongeza kuwa, wananchi wanaweza kuunganisha mashine ndogo ndogo za kusaga, kuchomelea, kuranda na kuchana mbao pamoja na nyinginezo kutoka katika makontena hayo hivyo kunufaika na shughuli za kiuchumi. Pia, Mhandisi Merl alisema mradi umetoa jokofu kwa kila zahanati na vituo vya afya vilivyopo katika vijiji vinavyonufaika na mradi huu. Aidha, alisema kuwa mradi umefunga taa za mitaani kwa kila kijiji kitakachonufaika na mradi husika. Kwa upande wao, baadhi ya wananchi katika vijiji vilivyonufaika na mradi huo wa makontena ya umeme wa jua, waliishukuru na kuipongeza Serikali kwa wazo zuri la kuwapelekea wananchi hao umeme wa jua ili nao waweze kunufaika kwa namna mbalimbali kutokana na uwepo wa nishati hiyo muhimu. “Ninaishukuru sana Wizara ya Nishati na Madini kuona matatizo yetu na kusikia kilio chetu. Imekuwa kama ndoto. Umeme huu umeniwezesha kuendesha biashara ya saluni kwa njia ya kisasa kabisa. Situmii tena Mkasi kunyoa wateja wangu kama hapo awali. Sasa ninatumia mashine za kunyolea na ninapata wateja wengi, hivyo kuboresha kipato changu na maisha yangu kwa ujumla,” alisema Lazaro Kutamika, mkazi wa Kijiji cha Lobilo, Wilaya ya Kongwa, mkoani Dodoma. Wizara ya Nishati na Madini imekuwa ikitumia mbinu mbalimbali katika jitihada za kuwafikishia wananchi huduma ya umeme. Kwa kupitia mradi huo wa makontena ya kuzalisha umeme kutokana na jua, Serikali inafanya majaribio ya kuvipatia umeme vijiji vilivyo mbali na mfumo wa gridi ya Taifa kwa kutumia teknolojia husika. Vijiji vilivyonufaika na mradi huo kwa awamu ya kwanza ni pamoja na Lobilo, Leganga, Ngutoto na Silale vya mkoa wa Dodoma. Vingine ni Tura, Loya na Lutende vilivyoko mkoa wa Tabora. Aidha, kwa mkoa wa Katavi, vijiji vilivyonufaika ni Nsenkwa, Mapili na Ilunde.

ZIARA YA WAZIRI WA ARDHI MWANZA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI

11
New Picture (3)

WATU WATATU WAFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA KIFUSI WAKIWA KATIKA SHUGHULI ZA UCHIMBAJI MADINI.

UWT MERU WACHANGA MILIONI 17 KWA AJILI YA UNUNUZI GARI

Mgodi wa Dhahabu Chunya wahesabiwa siku

images
Baraza la Taifa la Hifadhi naUsimamizi wa Mazingira na Wataalam wa Mazingira wameagizwa kutoa elimu ya mazingira kwa wawekezaji wa Mgodi wa Dhahabu wa Sunshine uliyopo Wilaya ya Chunya mkoani Mbeya . Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira, Injinia Binilith Mahenge jana alipotembelea machimbo ya Mgodi huo nakubaini kuwa unaendeshwa bila kuzingatia Kanuni za Mazingira. Katika ziara hiyo Mh. Mahenge alibaini kuwa mgodi huo hauna mtambo wa kutibu maji-taka yake kabla ya kuyatiririsha katika mazingira pia bwawa linalotumika kuhifadhi maji-taka hayo halikidhi viwango vya Kanuni za Mazingira pamoja na kuzibwa kwa mfereji wa asili hivyo kuzuia mkondo wa mvua. Kutokana na hali hiyo, Waziri Mahenge alitoa siku 30 kwa wataalam wake kuwapatia elimu ya Kanuni za Mazingira wawekezaji wa Mgodi wa Sunshine ikiwa ni pamoja na kuwataka wawekezaji hao kutekeleza kanuni hizo ndani ya siku 30 kuanzia jana. Wakati huo huo Mh. Mahenge alitembelea Machimbo ya Dhaabu ya Mek na Mgodi wa Shanta Wilayani Chunya ambapo Wataalam wake Mazingira walibainisha kuwa wawekezaji wa migodi hiyo wametiza kanuni za mazingira. Sanjari na hayo Injiania Mahenge alikutana na Watendaji wa Halmashauri ya Chunya na kukabidhiwa Mapendekezo ya Mradi Maalumu wa kulinusuru Ziwa Rukwa ili lisitoweke kutokana na kilimo holela, uchimbaji wa madini na utirirshwaji wa maji-taka kwenye vyanzo vya Ziwa hilo. Katika makabidhiano ya Mapendekezo hayo Mh. Mahenge aliwaahidi Watendaji wa Halmashauri ya Chunya kuwa atayafanyia kazi Mapendekezo yao lakini pia aliwaomba na wao kuishauri Wilaya waingize Mazingira katika bajeti zao .

Kikao cha Kamati cha wasilisha hesabu za Shirika la Umeme la Tanzania (Tanesco)

1

LEADING TEA PACKING COMPANY PROMISES GREAT TEA

IMG_0207