TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Tuesday, April 30, 2013

RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KUFUNGUA MKUTANO WA KILIMO.

images
Na Hassan Silayo na Lorietha Laurence
…………………………………………………….
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Kikwete anatarajia kufungu
a mkutano wa Kilimo wa Umoja wa Nchi za Kusini mwa Africa, utakaofanyika tarehe 13 hadi 14 Mei mwaka huu .
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Mkutano wa Vyama vya Kilimo vya Kusini mwa Afrika (SACAU), Ishmael Sunga wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu mkutano huo utakao fanyika katika hoteli ya White sands iliyopo jijini Dare s salaam.
Alisema kuwa kipaumbele katika kipindi hiki ni kupambana na changamoto ya kilimo,na usalama wa chakula ili kufanya sekta ya kilimo kukua , kustawi na kufanya kilimo kuwa biashara badala ya kufikiri katika kuondoa umaskini.
“Lengo litakuwa ni kubadilisha mtazamo wa watu kuwa, kilimo ni kwa ajili ya kumfanya mkulima ajikimu mahitaji ya kawaida na kuondoa umaskini, bali ni kumfanya mkulima kupata faida na kutajirika kupitia kilimo katika ngazi zote za kilimo”, alisema Sangu.
Aliongeza kuwa mkutano huo una malengo ya kuwasaidia na kuwaongezea nguvu wakulima pamoja na kutoa taarifa za kilimo kwa wadau wa sekta hiyo kwa niaba ya wakulima wote wanachama wa umoja huo ili kuleta tija katika sekta hiyo muhimu ya kilimo.
Naye Mkurugenzi wa Baraza la Kilimo Tanzania Janet Bitegeko alisema baada ya mkutano huo washiriki watapata fursa ya kutembelea wakulima wa mpunga katika kijiji cha Bagamoyo ili kujionea changamoto na nini wakulima hao wanafanya na kutoa ushauri ili kuweza kuboresha zaidi zao hilo.
Janet aliongeza kuwa umoja huo utatoa taarifa za utekelezaji za mwaka pamoja na kufanya ukaguzi wa hesabu za mwaka za umoja huo.
Mkutano huo utahudhuriwa na washiriki kutoka nchi 14 wakiwemo wakurugenzi na wenyeviti kutoka nchi za kusini mwa afrika, wawakilishi zaidi ya 10 wa muungano wa wakulima pamoja na taasisi za kifedha.
Kauli mbiu ya mkutano huo ni kusaidia kilimo cha biashara na maendeleo ya biashara yanayolenga mkakati maendeleo ya kilimo katika nchi za kusini mwa afrika, ambapo waziri wa kilimo wa Nigeria atatoa kauli.

No comments:

Post a Comment