TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, July 26, 2014

SERIKALI HAINA MPANGO WA KUPUNGUZA MAFAO YA PENSIONI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au  namba +255767869133
 
Chama cha Walimu Tanzania (CWT)
 
Serikali imesema kuwa haina mpango wa kupunguza mafao ya pensheni kwa wanachama wa Mfuko ya Hifadhi ya Jamii na kwamba maamuzi yote yanayohusu mafao yao yanafanyika kwa uwazi.
 
Hivi karibuni Chama cha Walimu Tanzania (CWT) na Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU) walitoa taarifa kupitia vyombo vya habari wakieleza kuwa serikali ina mpango wa kupunguza mafao ya pensheni ya wanachama wa mifuko ya LAPT na PSPF.
 
Tamko hilo la serikali lilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Kamishina wa Wizara ya Kazi na Ajira, Saul Kinemela, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamko lililotolewa na CWT pamoja na THTU na kueleza kuwa tuhuma hizo siyo za kweli kwani wanapotosha umma.
 
Alisema kuwa Wizara ya Kazi na Ajira ndiyo yenye dhamana ya sekta ya hifadhi ya jamii Tanzania na ndiyo maana wameamua kutolea ufafanuzi suala hilo ili jamii iweze kuelewa kwa kina dhidi ya upotoshaji huo.
 
"Wizara Kazi na Ajira inachukua nafasi hii kukanusha vikali taarifa zilizotolewa na CWT na THTU ambazo kwa namna moja au nyingine zinalenga katika upotoshaji," alisema
"Tunaomba wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii na umma kwa ujumla, uelewe wazi kuwa si SSRA wala serikali zimetoa tamko lolote kuhusiana na upunguzaji wa mafao ya pensheni kwa wanachama wa mifuko ya PSPF na LAPF," alisema Kinemela
 
Kinemela alisema kinachoendelea ni majadaliano ya wadau wa sekta ya hifadhi ya jamii yenye lengo la kuboresha mafao ya wastaafu. Hata hivyo, majadiliano hayo hakuna maamuzi wala tamko lolote lililotolewa kuhusiana na upunguzwaji wa mafao ya wanachama.
 
Hata hivyo, alisema CWT na THTU ni moja kati ya wadau wa sekta ya hifadhi ya jamii, wanayo haki kikatiba ya kukutana na kujadiliana masuala mbalimbali  yakiwemo mifuko hiyo ya kijamii na siyo vizuri wakafanya upotoshaji kuhusu jambo hilo muhimu.
 
Alisema serikali inachukua fursa hiyo kuwatoa hofu wastaafu na wanachama wote wa mifuko ya hifadhi ya jamii, hususani wale wa PSPF na LAPF na walimu wote kwa ujumla kuwa maamuzi yoyote kuhusiana na mafao yao yanafanyika kwa uwazi na kuwahusisha wadau wote.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment