TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, July 26, 2014

Jezi ya James Rodriguez yaingiza pato la 345,000 kwa masaa 48 tu.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au Tupigie n amba +255767869133/ +255-713-869133
 

James Rodriguez  

Ni kama ajabu, lakini ndiyo hivyo baada ya jezi yenye namba 10 aliyokabidhiwa staa huyo kuuzwa kama njugu ndani ya saa 48 tu tangu alipotambulishwa rasmi Jumanne iliyopita kuwa ni mchezaji wa Real Madrid.
REAL Madrid imepiga bao. Imetoa pauni 63 milioni kumnasa James Rodriguez na hata kabla hajaanza kucheza mechi yoyote kuleta mataji klabuni hapo, pesa zao zimeanza kurudi.
Ni kama ajabu, lakini ndiyo hivyo baada ya jezi yenye namba 10 aliyokabidhiwa staa huyo kuuzwa kama njugu ndani ya saa 48 tu tangu alipotambulishwa rasmi Jumanne iliyopita kuwa ni mchezaji wa Real Madrid.
Ripoti zinabainisha kwamba Real Madrid hadi sasa tayari imesharudisha kiasi cha pauni 21 milioni baada ya mauzo ya jezi 345,000 za Rodriguez ndani ya saa 48 tu.
Mashabiki wa timu hiyo wameonekana kupagawa na usajili wa Rodriguez, ambaye amepewa jezi iliyokuwa ikivaliwa na Mesut Ozil (kabla hajabadili na kuvaa namba 11) na mwaka jana kutimkia Arsenal.
Kwa mujibu wa gazeti moja la michezo la Hispania, kampuni ya wataalamu wa masoko ya kibiashara michezoni ilifanya hesabu na kugundua kwamba jezi hizo 345,000 zilizouzwa kwa saa 48 ni sawa na mauzo ya jezi 7,188 kwa saa. Hii ni rekodi.
Real Madrid haijawahi kusumbuka juu ya mauzo ya jezi za mastaa wao wanaowasajili kwa pesa nyingi, lakini nyota huyo aliyetamba kwenye Kombe la Dunia nchini Brazil mauzo ya jezi zake zimeweka rekodi.
Kwenye utambulisho wake uliofanyika uwanjani Bernabeu Jumanne iliyopita zaidi ya mashabiki 44,000 walijitokeza kumshangilia mchezaji huyo huku wengine 900 tayari walionekana kuvaa jezi za mchezaji wao huyo mpya.
Kwa mauzo hayo ya siku mbili tu ya jezi za Rodriguez, tayari Real Madrid imebakiza pauni 3 milioni tu kurudisha pesa walizomsajili kiungo Toni Kroos, aliyejiunga na timu hiyo kwa pauni 24 milioni kutoka Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment