TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, November 11, 2015

DK. KIMEI AONGOZA HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA SIHA SANGO






Katika harambee hiyo iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika kanisa hilo mkoani Kilimanjaro, Dk. Kimei aliwapongeza waamini hao kwa kupata moyoa wa kujenga nyumba ya Mungu.

“Mimi sio mwanasiasa pengine nitakua mwanaisasa baadae lakini sio sasa… nimefurahi kualikwa hapa na nimebahatika kukanyaga kanisa hili kabla halijabomolewa.

“… Ni kanisa la zamani limechakaa, mmeliona hili nawapongeza kwa kuamua kujenga jingine jipya,” alisema Dk. Kimei aliyeongozana na baadhi ya watumishi wa benki hiyo.

Mchungaji Kiongozi wa KKKT Usharika wa Siha Sango, Cuthbert Temba aliwataka waamini na watanzania kufanya shughuli za maendeleo kwa nchi baada ya uchaguzi mkuuu kumalizika kwa amani.

“Nawaomba watanzania wote tushirikiane, tufanye kazi za ujenzi wa taifa hili kwa lengo la kujiletea maendeleo ya kiuchumi, uchaguzi umeisha salama sasa tujenge taifa na nyumba ya Mungu,” alisema Mchungaji Temba.

Kanisa la KKKT Usharika wa Siha Sango lilijengwa mwaka 1916 hivyo limechakaa, waamini wa kanisa hilo walikubaliana kujenga kanisa jipya kwenye eneo hilo litakalogharimu sh milioni 200.

No comments:

Post a Comment