TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Friday, November 13, 2015

WANACCM WALIOCHUKUA FOMU KUWANIA USPIKA WA BUNGE

Idadi ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaoomba kuteuliwa kugombea nafasi ya Uspika na Unaibu Spika katika Bunge la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT) linalotarajiwa kuanza wiki ijayo, inazidi kuongezeka na hapa ni majina 21 ya ambao wameshachukua fomu hizo, kadiri ya taarifa ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Oganaizesheni, Muhammed Seif Khatib.
  1. Aliyekuwa Naibu Spika katika Bunge la 10 na Mbunge mteule wa Kongwa, Job Ndugai
  2. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dk Tulia Arkson 
  3. Aliyekuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk Didas Masaburi
  4. Aliyewahi kuwa Spika na Waziri, Samuel Sitta
  5. Mbunge mteule wa Chato, Dk Medard Kalemani
  6. Diwani wa Goba jijini Dar es Salaam, Mwakalika Watson
  7. Julius Pawatila
  8. Agnes Makune
  9. Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Abdullah Ali Hassan Mwinyi
  10. Naibu Waziri, Ritha Mlaki 
  11. Mhitimu wa chuo kikuu mwenye umri wa miaka 28, Veraikunda Urio
  12. Aliyekuwa Mbunge wa Karagwe, Gosbert Blandes 
  13. Aliywania nafasi ya Urais wa JMT kupitia CCM, Dk Kalokola Muzzamil.
  14. Mbunge wa Songea Mjini, Dk Emmanuel Nchimbi
  15. Aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge Philip Marmo
  16. Balozi wa zamani wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu
  17. Mbunge wa zamani wa Afrika Mashariki, George Nangale
  18. Simon Rubugu
  19. Banda Sonoko
  20. Leonce Mulenda
  21. Mbunge mteule wa Kasulu Mjini Daniel Nswanzungwanko
  22. Mbunge mteule wa Ilala Mussa Hassan Zungu

No comments:

Post a Comment