TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, January 12, 2014

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo amaliza ziara yake katika Mkoa wa Pwani.

Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe Bi.Mwanamvua Mrindoko akimweleza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel(mwenyeshati Jeusi) Mpango wa kuendelea kuwawezesha vijana katika halmashauri yake kwa Kutekeleza mipango mbalimbali iliyowekwa ikiwamo kutoa mafunzo kwa vijana na kuongeza bajeti hadi kufikia shilingi milioni 40 kutoka milioni 10 iliyokuwa inatolewa hapo awali kwa mwaka wa fedha 2014-2015,wakati wa Ziara ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo kuangalia shuguhuli mbalimbali za vijana zinazoratibiwa na Wilaya hiyo.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel(mwenyeshati Jeusi) akiongea na vijana wa kikundi cha bodaboda wakati wakati wa Ziara ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo kuangalia shuguhli mbalimbali za vijana leo katika wilaya ya Kisarawe.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel(mwenye suti  Jeusi) akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa kikundi cha bodaboda kutoka katika wilaya ya Kisarawe, wakati wa ziara yake ya kuangalia shuguhuli mbalimbali za vijana zinazoratibiwa na Wilaya hiyo
Afisa Maendeleo ya Jamii ya Vijana Toka Wilaya ya Mkuranga Bi.Safina Msemo akimweleza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel(kushoto) Mafanikio yaliyotokana na Utoaji wa asilimia tano(5%) katika pato la halmashauri kwa ajili ya shughuli za vijana,pia uandaaji  wa kambi ya vijana ya siku 40 watakayoshirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) kwa ajili ya kutoa mafunzo mbalimbali hasa katika sekta ya ujenzi, wakati wa Ziara ya Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Mkoani Pwani.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel akimsisitiza Afisa Maendeleo ya Jamii ya Vijana Toka Wilaya ya Mkuranga Bi.Safina Msemo(kulia) kuendelea kusimamia na kuratibu shughuli zinazotekelezwa na vijana katika Wilaya hiyo ili kuweza kuwasaidia kuleta maendeleo kwa Vijana
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel akisaini kitabu cha wageni alipotembelea kikundi cha MWAMKO FARM GROUP katika wilaya ya Mkuranga.kulia kwake ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkuranga Bi. Joyce Nampesya na Mbele yake ni Mwenyekiti wa Kikundi hicho Bw.Hemed Kassim.
Wanakikundi cha MWAMKO FARM GROUP toka Wilaya ya Mkuranga eneo la Kimanzichana wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel wakati wa ziara yake Mkoani Pwani.
Sehemu ya Miradi wa Kikundi cha MWAMKO FARM GROUP toka Wilaya ya Mkuranga,mbali na Ufyatuaji wa Matofali pia wanajishughulisha na ulimaji wa Miti ya miembe na uuzaji wa maji kwa wanakijiji wa eneo hilo kutokana na Visima viwili wanavyovimiliki.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel akiwa katika picha ya pamoja na wanakikundi cha MWAMKO FARM GROUP na baadhi ya Maafisa toka Wilaya ya Mkuraga.
Mwanakikundi cha NAMPULA CARVINGS Bw.Steven Mwidumbi akimuonesha Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel(mwenye suti NYEUSI) kinyago mfano wa nyani wanaodandia Miti,wakati alipowatembelea leo katika wilaya ya Mkuranga.
(Picha zote na Hassan Silayo-MAELEZO

RAIS KIKWETE AWAANDALIA MABALOZI SHEREHE YA KUUKARIBISHA MWAKA IKULU

sp3
sp4
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wengine akisikiliza hotuba toka kwa Balozi wa DRC nchini Mhe Asumani Mpango ambaye pia ndiye Kiongozi wa Mabalozi nchini akihutubia wakati wa Sherehe ya Kuukaribisha Mwaka Mpya(Sherry Party)  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 10, 2014
sp5
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mabalozi  na wawakilishi wa taasisi za kimataifa wanawake wakati wa Sherehe ya Kuukaribisha Mwaka Mpya(Sherry Party) aliyowaandalia Ikulu jijini Dar es salaam leo January 10, 2014

PINDA AKUTANA NA UONGOZI WA KAMPUNI YA CMHI YA CHINA INAYOJENGA BANDARI YA BAGAMOYO

IMG_0167
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na  viongozi wa Kampuni ya Kichina ya  China  Merchant Holdings International  (CMHI) Ofisini kwake jijini Dar es salaam Januari  10, 2013. Kushoto  kwake  ni  Kiongozi wa Ujumbe huo ,  Hu Jianhua na kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Dr. Mary Nagu. Kampuni hiyo inatarajiwa kujenga bandari mpya ya Bagamoyo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
IMG_0176 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na  Kiongozi wa Ujumbe  kutoka Kampuni ya kichina ya  China Merchant  Holdings International (CMHI), Bw.  Hu Jianhua  kabla ya mazungumzo yao, Ofisini kwa Waziri Mkuu, jijini Dar es salaam Januari 10, 2014. Kampuni hiyo inatarajiwa kujenga kampuni mpya ya Bagamoyo. (picha na Ofisi ya  Waziri Mkuu)

DAWATI LA JINSIA NA WATOTO LAJENGEWA UWEZO.

photo(2) 
Pichani washiriki wa mafunzo ya namna ya kutambua makosa ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto wakimsikiliza mgeni rasmi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Adolfina Chialo, wakati wa kufuata mafunzo ya kutambua makosa ya ukatili wa kijinsia na watoto, yaliyofanyika mkoani Morogoro, mafunzo hayo yaliwakutanisha washiriki kutoka katika kanda tatu za mikoa ya Dodoma, Pwani pamoja na wenyeji mkoa wa Morogoro.( Picha na Demetrius Njimbwi, Jeshi la Polisi )
…………………………………………………………………………
Na Demetrius Njimbwi, Jeshi la Polisi
Mkuu wa Dawati la Jinsia na Watoto Nchini, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Adolfina Chialo, amewataka wananchi kote nchini, kutofumbia macho vitendo vya ukatili na unyanyasaji ambavyo vimekuwa vikitokea katika jamii yetu huku vikiathiri idadi kubwa ya wanawake na watoto.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akifunga semina ya mafunzo kwa askari Polisi ya namana ya kutambua viashiria vya makosa ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji wa watoto, mafunzo yaliyofanyika kwa muda wa siku tano katika mkoa wa Morogoro, huku yakiwakutanisha washiriki kutoka katika kanda tatu za mikoa ya Dodoma, Pwani pamoja na wenyeji wa mafunzo hayo mkoa wa Morogoro.
Hata hivyo, Kamishna Chialo, alisema kuwa, lengo la mafunzo haya kwa askari na maofisa wa Jeshi la Polisi, ni kuwajengea uwezo katika kutoa huduma bora katika kazi za dawati la jinsia na watoto, ikiwa pamoja na kufahamu mbinu mbalimbali za kutambua makosa ya ukatili wa kijinsia huku wakitambua kuwa suala la utoaji wa huduma bora kwa mteja si hiari bali ni lazima.
Naye kwa upande wake mwakilishi wa Kituo cha Sheria ( legal Sector) waliofadhili mafunzo hayo, Bi. Wanyenda, alisema  kuwa, Jeshi la Polisi linamchango mkubwa katika kuwahudumia waathirika wa ukatili wa kijinsia na hivyo kutokana na mafunzo haya yatawasaidia askari katika kupambana na matukio ya ukatili wa kijinsia ambayo kwa kiasi kikubwa yamekuwa yakitendeka katika jamii.
Bi. Wanyenda, aliongeza kuwa, ni vyema askari waliopatiwa mafunzo haya wakaitumia  fursa hii waliyoipata kuweza kutoa elimu kwa askari ambao hawakuweza kushiriki katika mafunzo haya kwa lengo la kuwajengea uwezo na namna ya kutambua viashiria vya makosa ya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji.
Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi kwa niaba ya washiriki wenzake, Mkaguzi msaidizi wa Polisi, Letea Mofuga, alisema kuwa, mafunzo waliyopatiwa yamewasaidia kutambua na kubaini viashiria pamoja na dalili za mtu aliyefanyiwa ukatili na hivyo kuahidi kufanya kazi kwa kuzingatia miongozo waliojifunza.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA SHULE YA SEKONDARI YA KIEMBE SAMAKI ZANZIBAR

01
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza jambo na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kiembe Samaki, Amina Salum Khalfan, wakati alipokuwa akitembelea chumba cha Maabara baada ya kuzindua rasmi Shule hiyo wakati wa hafla fupi iliyofanyika shuleni hapo mjini Zanzibar leo Jan 10, 2014. Picha na OMR
1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na mmoja wa wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Kiembe Samaki, baada ya uzinduzi rasmi wa shule hiyo uliofanyika leo Jan 10, 2014, mjini Zanzibar. Picha na OMR
02
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kiembe Samaki, Amina Salum Khalfan, wakati alipotembelea katika chumba cha Mawasiliano na mafunzo ya Kompyuta cha shule hiyo, baada ya uzinduzi rasmi wa shule hiyo uliofanyika leo Jan 10, 2014, mjini Zanzibar. Picha na OMR 2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikagua moja ya vitabu vya kumbukumbu za Maktaba ya Shule mpya ya Sekondari ya Kiembe Samaki wakati alipotembelea chumba hicho cha Maktaba baada ya kuzindua rasmi Shule hiyo wakati wa hafla fupi iliyofanyika shuleni hapo mjini Zanzibar leo Jan 10, 2014. Kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Amina Salum Khalfan. Picha na OMR 03
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea chumba cha Maabala kati ya vyumba vinne vilivyopo shuleni hapo. Picha na OMR 3
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea chumba cha Maabala kati ya vyumba vinne vilivyopo shuleni hapo. Picha na OMR
04
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akikata utepe kuzindua shule ya Sekondari ya Kiembe Samaki, wakati wa hafla fupi iliyofanyika shuleni hapo mjini Zanzibar leo Jan 10, 2014. Kulia ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Ali Juma Shamhuna. Picha na OMR
4 06
8
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifunua kitambaa kuashiria kuweka jiwe la Msingi la shule ya Sekondari ya Kiembe Samaki, wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa shule hiyo iliyofanyika shuleni hapo mjini Zanzibar leo Jan 10, 2014. Picha na OMR  
Wanafunzi wa shule ya Msingi Kiembe Samaki, wakitoa burudani wakati wa hafla hiyo ya uzinduzi.

MATOKEO YA SENSA YA IDADI YA TEMBO KATIKA MFUMO WA IKOLOJIA WA SELOUS-MIKUMI NA RUAHA-RUNGWA

tembo 
Wizara ya Maliasili na Utalii inapenda kuujulisha umma matokeo ya sensa ya tembo iliyofanyika mwezi Oktoba na Novemba mwaka huu ili kuiwezesha Serikali kutambua hali ya rasilimali ya wanyamapori ndani na nje ya maeneo yaliyohifadhiwa.
Wizara kwa kushirikiana na wataalamu wa ndani na nje ya nchi imefanya sensa katika Maeneo ya Mfumo ikolojia wa Selous – Mikumi na Ruaha – Rungwa pekee kwa kuwa ni maeneo yenye tembo wengi nchini. 
Matokeo ya sensa hii yanaonyesha kwamba Mfumo wa ikolojia wa Selous-Mikumi kwa sasa una tembo wapatao 13,084 na Ruaha–Rungwa una tembo wapatao 20,090. Takwimu hizi zinaonesha kupungua kwa idadi ya tembo na hasa katika mfumo ikolojia wa Selous-Mikumi ikilinganishwa na Sensa za awali.
Takwimu za muda mrefu zinaonesha kwamba mwaka 1976 katika mfumo ikolojia wa Selous–Mikumi kulikuwa na tembo 109,419. Idadi hii ilipungua kufikia 22,208 mwaka 1991 kutokana na wimbi la ujangili uliokuwepo katika kipindi cha mwaka 1984 -1989. Hata hivyo, idadi hiyo iliongezeka na kufikia 70,406 mwaka 2006 baada ya Operesheni Uhai iliyofanyika mwaka 1989 na 1990 na juhudi za kimataifa za uhifadhi ikiwemo kusitisha biashara ya meno ya tembo.
Aidha, idadi ya tembo nchini ilipungua hadi kufikia jumla ya tembo 38,975 mwaka 2009 na kuendelea kupungua hadi kufikia tembo 13,084 hivi sasa.
Hali kama hiyo inaonekana pia katika mfumo wa ikolojia wa Ruaha-Rungwa ambapo sensa ya mwaka 1990 ilionesha kuwa na tembo 11,712 kutokana na wimbi la ujangili. Idadi hii iliongezeka na kufikia 35,461 mwaka 2006. Hata hivyo, idadi hiyo imepungua na kubakia tembo 20,090 hivi sasa.
Kwa matokeo haya inaonesha kuwa katika mfumo ikolojia wa Selous-Mikumi idadi ya tembo imepungua kwa asilimia 66 ikilinganishwa na idadi ya mwaka 2009 ambapo kulikuwa na jumla ya tembo 38,975. na katika Mfumo ikolojia wa Ruaha–Rungwa Tembo wamepungua kwa asilimia 36.5 ikilinganishwa na idadi ya mwaka 2009 ambapo kulikuwa na jumla ya tembo wapatao 31,625.
Kupungua huku kunathibitishwa na idadi ya mizoga ya tembo iliyohesabiwa wakati wa zoezi la sensa. Jumla ya mizoga 6,516 na 3,496 ilihesabiwa katika mifumo ikolojia ya Selous-Mikumi na Ruaha–Rungwa. Katika zoezi hili Wizara ilitumia vigezo vya uwiano wa mizoga na tembo hai waliohesabiwa (carcass ratio) kubaini vyanzo vya vifo hivyo. Katika hali ya kawaida, uwiano wa asilimia 7 – 8 unaashiria vifo vya asili kama vile ugonjwa na uzee. Zaidi ya asilimia hiyo inaashiria vifo visivyo vya asili.
Sensa iliyofanyika mwaka huu imeonesha uwiano wa asilimia 30 kwa mfumo ikolojia wa Selous-Mikumi na asilimia 14.6 kwa Ruaha–Rungwa. Kwa mujibu wa matokeo hayo, idadi kubwa ya vifo vya tembo vimetokana na vifo visivyo vya asili.
Uchambuzi wa kina umebainisha kuwa asilimia 95 na 85 ya mizoga iliyoonekana katika mifumo ikolojia ya Selous-Mikumi na Ruaha–Rungwa ni ya zaidi ya miezi 18 iliyopita.
Hii inaonesha kuwa juhudi za makusudi zilizofanywa na serikali ikiwa ni pamoja na kuimarisha doria na operesheni maalum mbalimbali za hivi karibuni zimesaidia kupunguza wimbi la ujangili kwa kiasi kikubwa.
Aidha, kukamatwa kwa meno ya tembo yenye uzito wa kilogramu 32,987 ndani na nje ya nchi katika kipindi cha 2008 hadi Septemba 2013 ni ishara tosha kuwa ujangili ni mojawapo ya sababu kubwa za kupungua kwa idadi ya tembo nchini.
Sababu nyingine ni kuongezeka kwa mifugo katika maeneo yaliyohifadhiwa na shoroba za wanyamapori. Mathalan, katika Pori Tengefu la Kilombero ambalo ni sehemu ya ikolojia ya Selous – Mikumi, mwaka 2002 lilikuwa na tembo 2,080, katika sensa ya mwaka huu, hukukuwa na tembo hata mmoja. 
Ongezeko la bei katika masoko ya biashara haramu ya meno ya tembo hususan katika nchi za Mashariki ya mbali ni kichocheo na kisababishi kikubwa.
Kufuatia hali hii, Wizara inaimarisha ulinzi wa wanyamapori kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama na taasisi nyingine za kanda na kimataifa pamoja na kuelimisha na kushirikisha wananchi katika masuala mbalimbali ya uhifadhi.
Ili kuimarisha na kuboresha shughuli za uhifadhi, Wizara iko katika hatua za mwisho za kuanzisha mamlaka mpya ya wanyamapori. Vilevile sheria za uhifadhi zinapitiwa ili kuruhusu kuanzishwa kwa mfumo wa kijeshi kwa watumishi wa sekta ya wanyamapori.
Wizara inapenda kuwatambua na kuwashukuru wafadhili wote waliofanikisha sensa hii iliyogharimu kiasi cha dola za kimarekani 160,000ikiwa ni fedha za serikali na wafadhili. Wafadhili hao ni Shirika la Misaada ya Kiufundi la Ujerumani (GIZ) kupitia Frankfurt Zoological Society (FZS) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) kupitia Mradi wa TANAPA wa SPANEST.
Imetolewa na
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Mhe. Lazaro Nyalandu (MB)

Mh. Lowassa akagua miradi ya maji jimboni kwake Monduli

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (katikati) akiongozana na wadau mbali mbali wa maendeleo wakati ziara yake ya kukagua maendeleo ya Mradi wa ujenzi wa bwawa la maji katika kata ya Meserani kijiji cha Nalarami,jimbo la Monduli.Wa tatu kushoto ni Diwani wa kata hiyo,Edward Lenanuu.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisikiliza maelezo kutoka kwa kaimu mhandisi wa maji wa wilaya ya Monduli,Bw. Wasiwasi Mgala (kushoto) wakati alipotembelea Mradi wa ujenzi wa bwawa la maji katika kata ya Meserani kijiji cha Nalarami,jimbo la Monduli.Katikati mwenye shati jekundu ni mwenyekiti wa CCM Monduli,Ruben Kunayi.

DK.Shein Mgeni Rasmi katika Fensi Kibandamaiti

TA1A8509
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wasanii wa asili na vikundi vya ngoma wakati Fensi katika barabara ya Kibandamaiti Wilaya ya Mjini jana,katika shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar,wengine waliokaa Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi,Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Abdalla Mwinyi Khamis na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]TA1A8498 
Wasanii wa fensi ambao hujipaka mafuta machafu (mobile) wakiwa na mishale  wakipita mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein pamoja na Viongozi mbali mbnali na wananchi waliohudhuria kuangalia fensi hiyo iliyoshirikisha kazi za taasisi za Serikali na Binafsi,katika Barabara ya Kibandamaiti Mjini Unguja jana,ikiwa ni shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

TA1A8530
Wasanii wakionesha namna ya tiba za asili kwa njia ya kupandisha mizuka ikiwemo ngoma za pungwa, wakati wa Fensi iliyopita katika barabara ya Kibandamaiti,Wilaya ya Mjini jana,katika shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A8539
Baadhi ya Wananchi wa Mji wa Unguja na Vitongoji vyake wakiangalia Fensi iliyopita  katika Barabara ya Kibandamaiti Mjini Unguja jana,ikiwa ni shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A8541 
TA1A8543
Baadhi ya Wananchi wa Mji wa Unguja na Vitongoji vyake wakiangalia Fensi iliyopita  katika Barabara ya Kibandamaiti Mjini Unguja jana,ikiwa ni shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
 
 Ngoma ya Beni (Mbwa kachoka)  ikipita mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, katika barabara ya Kibandamaiti Mjini Unguja jana,ikiwa ni shamra shamra za miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI

DV7A3218 
WILAYA YA RUNGWE – MAUAJI. 
MNAMO TAREHE 09.01.2014 MAJIRA YA SAA 06:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA ILENGE, KATA YA KYIMO, TARAFA YA UKUKWE WILAYA YA  RUNGWE  MKOA WA MBEYA. MAGRETH D/O IJUMBA, MIAKA 55, KYUSA, MKULIMA, MKAZI WA KIJIJI CHA ILENGE ALIUAWA AKIWA NYUMBANI KWAKE KWA KUPIGWA JIWE KICHWANI NA MTU/WATU WASIOFAHAMIKA KISHA KUTUPWA KATIKA SHAMBA LAKE LA MIGOMBA UMBALI WA MITA 69 KUTOKA NYUMBANI KWAKE. MBINU NI KUVUNJA MLANGO WA NYUMBA YA MHANGA AMBAYE ANAISHI PEKE YAKE KUINGIA NDANI NA KUMUUA KWA KUTUMIA JIWE. AIDHA WATU HAO PIA WALIKWENDA MTAA WA PILI NA WALIMSHAMBULIA KISA W/O EPHRAIM, MIAKA 50, KYUSA, MKULIMA, MKAZI WA KIJIJI CHA ILENGE KWA KUTUMIA JIWE KICHWANI NA AMELAZWA HOSPITALI YA  MISHENI IGOGWE.  CHANZO NI IMANI ZA KISHIRIKINA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED. Z. MSANGI ANATOA WITO JAMII KUACHA KUAMINI IMANI POTOFU ZA KISHIRIKINA KWANI ZINA MADHARA MAKUBWA KATIKA JAMII. AIDHA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MTU/WATU WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MBEYA VIJIJINI – MAUAJI.
MNAMO TAREHE 09.01.2014 MAJIRA YA SAA 16:00HRS HUKO MLIMA NYOKA, KATA YA IGAWILO, TARAFA YA IYUNGA, WILAYA YA MBEYA VIJIJINI, MKOA WA MBEYA, WATU WAWILI 1. CHARLES S/O LIVINGSTONE, MIAKA 32, MSAFWA, MKULIMA, MKAZI WA ITEZI NA 2. TATIZO S/O MBWIGA, MIAKA 27, MSAFWA, MKULIMA, MKAZI WA NSALAGA WALISHAMBULIWA  KWA KUPIGWA NA KUNDI LA WANANCHI WALIOAMUA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI WAKITUMIA SILAHA ZA JADI FIMBO NA MAWE HADI KUFA.  CHANZO NI TUHUMA ZA WIZI WA PIKIPIKI T.693 CBD AINA YA SHANLEY MALI YA KEVEN S/O MSEMWA, MIAKA 24, MUWANJI, MKULIMA, MKAZI WA UYOLE.  MAREHEMU  CHARLES S/O LIVINGSTONE ALIKUWA ANATOKA MAHAKAMA YA  MWANZO UYOLE AKIWA MLALAMIKAJI KATIKA KESI CC 568/2013 KOSA SHAMBULIO AKIWA NI MLALAMIKAJI NA MAREHEMU TATIZO S/O  MBWAGA  ALIKUWA ANAMSINDIKIZA NA WALIPOFIKA ENEO LA UYOLE KATI WALIIBA PIKIPIKI HIYO. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED. Z. MSANGI ANATOA WITO JAMII KUACHA TABIA YA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA. AIDHA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA MTU/WATU WALIOHUSIKA NA TUKIO HILI AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MBEYA VIJIJINI – KUPATIKANA NA BHANGI.
MNAMO TAREHE 09.01.2014 MAJIRA YA SAA 09:00HRS HUKO MBALIZI KATA YA BONDE LA SONGWE, TARAFA YA USONGWE, WILAYA YA MBEYA VIJIJINI, MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIMKAMATA GEOFREY S/O SACKSON, MIAKA 23, MNYIHA, MKULIMA, MKAZI WA MBALIZI AKIWA NA BHANGI KETE 27 SAWA NA UZITO WA GRAM 135. MTUHUMIWA NI MUUZAJI /MTUMIAJI WA BHANGI. TARATIBU ZINAFANYWA ILI AFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED. Z. MSANGI ANATOA WITO JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI. AIDHA ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA AU MWENYE KUONA VIASHIRIA VYOVYOTE VYA MTU/WATU WANAOJIHUSISHA NA UUZAJI NA USAMBAZAJI WA DAWA ZA KULEVYA AZITOE ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
WILAYA YA MBARALI – KUPATIKANA NA NYARA ZA SERIKALI. 
MNAMO TAREHE 09.01.2014 MAJIRA YA SAA 09:00HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA KWATWANGWA NDANI YA HIFADHI YA TAIFA YA RUAHA, TARAFA YA  RUJEWA, WILAYA YA  MBARALI, MKOA WA MBEYA. ASKARI WANYAMAPORI [TANAPA] WAKIMKAMATA  JUMA S/O KALINDI, MIAKA 72, MSUKUMA AKIWA NA NYARA ZA SERIKALI PEMBE MBILI ZA DIGIDIGI NA NYAMA YA  TEMBO. THAMANI BADO KUFAHAMIKA. MTUHUMIWA NI MUWINDAJI HARAMU. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED. Z. MSANGI ANATOA WITO JAMII KUACHANA NA TAMAA ZA MALI KWA KUTUMIA NJIA ZISIZO HALALI NA BADALA YAKE WAFANYE KAZI HALALI ILI WAJIPATIE KIPATO. AIDHA ANATOA WITO KWA JAMII KUENDELEA KUTOA TAARIFA KATIKA MAMLAKA HUSIKA JUU WA MTU/WATU WANAOJIHUSISHA NA UWINDAJI HARAMU ILI WAKAMATWE NA SHERIA ICHUKUE MKONDO WAKE.
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

NHIF & KfW yakabidhi vifaa tiba Mbeya na Tanga

1     
 Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa tiba vitakavyotumika katika vituo vya kutolea huduma vinavyohudumia wanufaika wa mradi wa akina mama wajawazito unaofadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Watu wa Ujerumani (KfW) kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
2 
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid akikabidhi  moja  ya vifaa tiba kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Dk.Noman Sigalla. 3   
 Naibu waziri wa Afya Dk Seif Rashid akimkabidhi moja ya mashine ya
kusaidia watoto wachanga matroni Mary Mlay aliyemwakilisha mkuu wa
mkoa wa Tanga katika hafla hiyo.
4 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Hamis Mdee akitoa maelezo ya Mradi wa KfW unaoendeshwa kwa ushirikiano wa Benki wa Watu wa Ujerumani na NHIF.  5  
Kaimu Mkuu wa Mbeya Dk. Noman Sigalla akitoa salaam za Mkoa kwa wadau wa mradi huo mbele ya Naibu Waziri wa Afya.  6 
 Maofisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (mbele) wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii. 7    
Sehemu ya wadau wa sekta ya afya kutoka Mbeya na Tanga waliohudhuria hafla hiyo.
………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu, Mbeya
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya watu wa Ujerumani (KfW) imeunga mkono mkakati wa Kitaifa wa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano kwa kutoa vifaa tiba katika vituo vya matibabu vinavyohudumia  kundi hilo.
Msaada huo unaohusisha mikoa ya Mbeya na Tanga wenye thamani ya shilingi milioni 989.1 umekabidhiwa leo na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Seif Rashid kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hussein Mwinyi kwa Waganga Wakuu wa mikoa hiyo.
 Akikabidhi msaada huo, Dk. Rashid alisema kuwa msaada huo utaboresha huduma za akina mama wajawazito na kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi lakini pia ni fursa ya vyanzo vya mapato kwa Halmashauri na watoa huduma.
“Sote tunafahamu kuwa matibabu sahihi yanatokana na vipimo sahihi hivyo uwekezaji unaofanywa kwa pamoja na NHIF & KfW kupitia mradi huu kwa lengo la kuviwezesha vituo vya matibabu kupata vifaa tiba utasaidia sana kupunguza tatizo la upatikanaji wa huduma ya vipimo kwa akina mama wajawazito na watoto,” alisema Dk. Rashid.
Kutokana na hali hiyo, Dk. Rashid aliwaagiza Waganga Wakuu ambao wamekabidhiwa vifaa hivyo kuhakikisha vinatumika ipasavyo na kutunzwa kwa faida ya Taifa ili vipumguze vifo vya akina mama hao na watoto.
“Ni vyema walengwa wa mradi huu wakapata huduma bora na si bora huduma, msaada huu uwe na matokeo mazuri kwa walengwa ili mradi uwe na manufaa kwa nchi yetu,” alisema.
Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Hamisi Mdee alisema Mfuko unatarajia mafanikio ya utekelezaji wa mradi huo yatashawishi akina mama wengi zaidi kutumia huduma za uzazi salama katika vituo vya matibabu lakini pia wafadhili kupanua maeneo ya mradi katika mikoa wanayofadhili.
Aidha alizitaka Halmashauri kuwasilisha kwa wakati madai yao baada ya kutoa huduma kwa wanachama pamoja na maombi ya fedha za tele kwa tele ili kuboresha huduma za matibabu katika vituo vyao.
Akizungumzia mafanikio ya mradi, alisema kuwa hadi sasa umefikia walengwa 74,099 ambao ni sawa na asilimia 105 na jumla ya shilingi 644,1118,912 zimelipwa kwa vituo vya matibabu vya mikoa ya Mbeya na Tanga vilivyotoa huduma kwa akina mama hao lakini pia shilingi milioni 400.4 zimetumika kulipia familia za akina hao kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).

Dr. Shein weka Jiwe la Msingi Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitambulishwa  kwa mshauri wa Ujenzi wa kampuni ya Hab Consult Bw.Habib Nuru,Katibu Mkuu Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar Dkt.Khalid Salum,alipofika viwanja vya Kisonge,Michenzani Mjini Unguja, kuweka Jiwe la Msingi  Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A8256 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kuweka jiwe la msingi Ujenzi   wa Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar, katika viwanja vya Kisonge,Michenzani  Mjini Unguja leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A8305 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi   Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisonge,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A8342 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia mkono wananchi waliohudhuria katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi   Mnara wa Kumbu kumbu ya Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisonge,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A8358 
Wananchi na wanachama wa CCM Jimbo la Mpendae wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Mnara wa Kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisongo,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] TA1A8359 
Wananchi naa wanachama wa CCM Jimbo la Mpendae wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Mnara wa Kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisongo,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A8360Wafanyakazi wa ZSSF,wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Mnara wa Kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar katika viwanja vya Kisongo,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
TA1A8398 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake kwa wananchi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Mnara wa Kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar, katika viwanja vya Kisongo,Michenzani Mjini Unguja leo asubuhi,(kulia) Waziri wa Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

IAA and TPDF signs MoU to equip military personnel with Strategic Studies

Photo four
A group photo of members of military and IAA staff members after the signing ceremony early today.
pHOTO oNE
The Command and Staff College (CSC) Commandant Maj General Kyunga signs a document of Memorandum of Understanding (MoU) in Arusha today to allow military personnel with the necessary skills and knowledge in Strategic Studies at IAA
Photo three
The Institute of Accountancy Arusha (IAA) Rector Prof. Prof. Johannes Monyo (2nd from R) exchange a Memorandum of Understanding (MoU) with The Command and Staff College (CSC) Commandant Maj General Ezekiel-Elias Kyunga (1st from L). The MoU signed today in Arusha will equip military personnel with the necessary skills and knowledge in Strategic Studies at IAA.
photo two
IAA Rector Prof. Johannes Monyo signs a document of Memorandum of Understanding (MoU) in Arusha today to allow military personnel with the necessary skills and knowledge in Strategic Studies at IAA.
………………………………………………………………………………..
By Our Reporter
The Institute of Accountancy Arusha (IAA) Rector Prof. Johannes Monyo said ion speech: “Today I have great pleasure to officiate a special ceremony on signing the Memorandum of Understanding between the Institute of Accountancy Arusha (IAA) and Tanzania People’s Defense Forces (TPDF). This is a great event and privilege for both IAA and TPDF. CSC deserves a special mention as the institution that initiated the event”
He added: “It is our understanding that many institutions in Tanzania are not used to working closely with Military personnel. TPDF and Command and Staff College realized that members of military forces are good partners in development. It is true that once good partnership is established the country tends to prosper faster” He also said that the Command and Staff College (CSC) has good working relationship with the Institute of Accountancy Arusha
(IAA) that has lasted for 8 years. In 2006 a special CSC tailored programme was developed and this was the beginning of a close working relationship between the two institutions. In this relationship the academic staff from IAA were invited to facilitate in a number of other related programmes conducted by CSC. But the target of CSC was to have long term programmes and academic partner with a capacity to run the new targeted programmes.
CSC initially, consulted several institutions and universities in the country to establish long term courses in strategic studies but this effort was unsuccessful. It is the flexibility of IAA management and the IAA Governing Council that authorized the commitment of resources in the year 2011 and allowed the development of Strategic Studies programmes at CSC- Monduli.
“Two curricula were developed in the area of Strategic Studies and these included the Ordinary Diploma and Postgraduate Diploma in Strategic Studies. These curricula were developed following NACTE standards. The Ordinary Diploma curricula comprising of NTA levels 5 and 6 were submitted to NACTE for validation and were approved. Furthermore, IAA developed Postgraduate Diploma in Strategic Studies Programme. These programmes are
currently in progress and have a total of 52 participants from EAC and SADC countries” he said
He revealed that both programmes are aimed at equipping Military personnel with the necessary skills and knowledge in Strategic Studies that are needed at their workplace and elsewhere in the world. These programmes which commenced in May 2013 are expected to produce the first graduands by March this year (2014).
Although this is the first collaborative arrangement with a partner from within the country IAA has two other collaborations with partners from foreign countries. IAA signed a MoU with Coventry University of UK way back in 2009 to run four masters degree programmes (MBA – ITM, MBA – LM, MBA – PSM and MSc. FI). These programmes have been running for last four years. In 2013 IAA signed another MoU with Galgotias University of India to run three masters degree programmes namely; Master in Information Security, Master in Software Engineering and Master in Computer Application. These programmes started in November 2013.
In the same vein we are working with TMA to establish a Bachelor Degree in Military Science. This degree is expected to be run
effective 2015 if the accreditation processes will be completed in time. 
Today we are here to officially sign the MoU between IAA and TPDF and inform Tanzanians in particular and the world at large that Military staff are good partners in development.
I would also like to take a moment of personal privilege to acknowledge some of those who helped to make this day and the event surrounding possible. I wish to thank members of IAA Academic staff, members of CSC staff, TPDF headquarters, members of the Governing Council, NACTE, TMA and all others not mentioned above but helped in one way or the other to make this day possible.