TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Sunday, December 14, 2014

KATIBU MTENDAJI BARAZA LA BIASHARA ZANZIBAR AZUNGUMZA NA WANAHABARI KUHUSU MKUTANO WA NANE WA BARAZA HILO

MAMA KIKWETE AWAPA TAHADHARI VIJANA KUTOKUBALI KUDANGANYWA NA KUTUMIWA KUFANYA VURUGU

unnamed9
Na Anna Nkinda – 

Maelezo, Lindi
14/12/2014 Vijana wa wilaya ya Lindi mjini wametahadharishwa kutokubali kudanganywa na kutumiwa kufanya  vurugu ambazo zinaharibu vitu vichache walivyonavyo na  kwa kufanya hivyo wanarudisha nyuma maendeleo yao.
Tahadhari hiyo imetolewa jana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)  kupitia wilaya hiyo  Mama Salma Kikwete wakati akiwanadi wagombea wa chama hicho kwenye mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi wa Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za mitaa uliofanyika katika Kata ya Makonde.
Mama Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema ni vyema vijana wakaelewa historia ya nchi yao na kujua lipi jema na baya kwani kuna baadhi ya wanasiasa wanawashawishi ili wafanye vurugu kwa madai kuwa hakuna maendeleo yoyote yaliyopatikana jambo ambalo siyo kweli.
“Hao wanaowadanganya nyinyi mfanye vurugu na kuharibu vile vichache mlivyonavyo eti kwa kuwa maisha yenu hayajaimarika kwao hawafanyi hivyo, kwao kuna maendeleo na ninyi mnazidi kujirudisha nyuma kimaendeleo. Msikubali  mkoa wetu uwe sehemu ya majaribio na kutumika kwa manufaa yao”.
Kama wangekuwa  wanawapenda na kutaka kuwasaidia ili muendelee wangewajengea hata shule ambazo zingewafanya vijana na watoto wetu wasome, hapo hakuna kipingamizi kwani Elimu ni mkombozi wa maisha na elimu inaleta maendeleo”, alisema Mama Kikwete.
MNEC huyo alisema Serikali makini ni lazima ijali maisha ya watu wake, kwa kutambua hilo Serikali ya CCM imeimarisha miundo mbinu kwa kujenga barabara za lami,  shule ili watoto wasome na kuimarisha huduma za afya ikiwa ni pamoja na kujenga Hospitali na  vituo vya afya na kuhakikisha wahudumu wa afya wanaongezeka.
Alisema, “Maisha bora kwa kila mtanzania siyo Chama kinapita nyumba kwa nyumba kugawa pesa bali ni kwa kuboresha miundombinu, kukiwa na shule watoto watasoma, kukiwa na barabara nzuri wananchi wasafirisha mazao yao, kukiwa na huduma bora za afya wananchi watatibiwa haya yakifanikiwa  maisha ya mtu mmoja mmoja yataimarika”.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Lindi Mjini Muksini Rafii alisema katika uchaguzi huo ndani ya wilaya hiyo wagombea za nafasi za wajumbe 147 na wenyeviti saba wamepita bila kupingwa.
Kwenye mkutano huo mwanachama mmoja aliyejulikana kwa jina la Raphael Mahuna  kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)  ambaye alikuwa ni mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa mtaa wa National Housing kwa tiketi ya chama hicho na mwanachama mmoja  kutoka Chama cha Wananchi (CUF) walijiunga na Chama Cha Mapinduzi.
Mahuna alisema ameamua kwa hiari yake mwenyewe bila ya kulazimishwa kujiunga na CCM kwani alipokuwa anagombea nafasi ya Mwenyekiti wa mtaa wa National Housing alishindwa kufanya kampeni kwa kuwa alikosa  wajumbe wa kumuunga mkono.
Katika uchaguzi wa Serikali za mitaa, vijiji na vitongoji mkoani  Lindi wagombea wa Chama Cha Mapinduzi katika vitongoji 600, vijiji 87 na mitaa nane wamepita  bila kupingwa.

SECURITYGROUP (T) LTD (SGA) WAFANYA USAFI KUADHIMISHA MIAKA 30 YA UTENDAJI KAZI NCHINI

unnamedWafanyakazi wa kampuni ya ulinzi ya ulinzi ya Security Group (T) Ltd (SGA), wakifanya usafi katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, Mbezi Beach, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kudhimisha miaka 30 ya kampuni hiyo tangu kuanza kufanya kazi zake hapa nchini. unnamed1Wafanyakazi wa kampuni ya ulinzi ya ulinzi ya Security Group (T) Ltd (SGA), wakifanya usafi katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, Mbezi Beach, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kudhimisha miaka 30 ya kampuni hiyo tangu kuanza kufanya kazi zake hapa nchini. unnamed2Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya ulinzi ya Security Group (T) Ltd (SGA), Eric Sambu akizungumza na wafanyakazi wa kampuni hiyo muda mfupi kabla ya kuanza kuufanyia usafi ufukwe wa Bahari ya Hindi, eneo la Mbezi Beach, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki kuadhimisha miaka 30 ya utendaji kazi wa kampuni hiyo nchini. unnamed3Meneja Mawasiliano wa kampuni ya ulinzi ya Securty Group (T) Ltd (SGA), Sofia (kushoto) akitoa maelekezo kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati wa zoezi la kufanya usafi katika ufukwe wa Bahari ya Hindi, eneo la Mbezi Beach, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ikiwa ni kuadhimisha miaka 30 ya utendaji kazi wa kampuni hiyo hapa nchini. unnamed4Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya ulinzi ya Security Group (T) Limited (SGA),  Eric Sambu (kulia) akifurahi na wafanyakazi wa kampuni hiyo baada ya kumaliza kusafisha ufukwe wa Bahari ya Hindi, eneo la Mbezi Beach, Dar es Salaam ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 30 ya utendaji kazi wa kampuni hiyo nchini.

Neno La Leo: Kwenda Kupiga Kura Ni Kwenda Kuchagua.

imagesNdugu zangu,
Leo ni siku ya kupiga kura kwenye Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji. Huu ni Uchaguzi Muhimu sana katika nchi. Uchaguzi huu ndio MSINGI wa siasa kubwa za Kitaifa.
Siasa ya nchi inaanzia kwenye Mtaa, Kijiji na Kitongoji. Na hakika, siku ya leo ilipaswa uwe ni uchaguzi pia kwa ngazi ya Manispaa na Halmshauri, kwa maana ya kuwachagua Madiwani.
Inahusu Serikali za Mitaa ( Local Goverment). Nimepata kuandika, kuwa Mahtama Ghandhi alipata kusema, kuwa ukitaka kuujua moyo wa nchi, nenda vijijini.
Katika nchi zetu hizi, uchaguzi wa leo ni kipimo cha Uchaguzi Mkuu ujao. Chama ama kambi itakayofaulu kupata asilimia 80 ya viti vyote vinavyogombaniwa, basi, naweza kuandika hapa, Kuwa ni ndio chama au kambi itakayounda Serikali baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa Oktoba mwakani.
Na kama kwenda kupiga kura ni kwenda kuchagua swali ni je, wapiga kura wanajua wanachokwenda kuchagua? Jibu, yumkini kuna wapiga kura wenye kwenda kuchagua sura na majina ya watu, lakini, kwa wengi waliohamasika au kuhamasishwa kujiandikisha, leo Jumapili wanakwenda kuchagua wanachokijua na kukiamini.
Na siasa ni itikadi, na kwenye itikadi, kama nilivyoandika huko nyuma, kuwa kuna KULIA na KUSHOTO. Ni imani. Hivyo, kuwa na msimamo kisiasa ina maana ya kusimama ama Kulia, au Kushoto. Kushoto ni wenye mrengo wa Kijamaa na Kujitegemea na kujali zaidi maslahi ya walio wengi. Kushoto ni Mrengo wenye kusimamia katika Haki na Usawa kwenye jamii. Kulia ni upande wa Mabwanyenye ama Mabepari. Ni wenye kuamini zaidi katika Mtaji na kukuza mtaji, bila kujali maslahi ya wengi. Na walio kwenye upande huo, wanaamini, kuwa Kutokuwepo kwa Usawa kwenye jamii ni jambo lisiloepukika.
Na kuna Katikati ya kiitikadi, kwamba kuna waliosimama kati. Lakini, aliyesimama kati anapo anapoegemea. Hivyo, kuna waliosimama kati wakiegemea Kushoto na wengine wakiegemea Kulia. Nao waweza kuwa viongozi bora, kama mpiga kura atafanya maamuzi yake.
Leo tunakwenda kuwachagua viongozi wetu kwenye Mitaa yetu, Vijiji na Vitongoji. Na kuna kisa cha mume aliyegombea nafasi ya uongozi. Alikwenda kituo cha kupigia kura na mkewe. Kura zilipohesabiwa aliambulia kura moja, ya kwake mwenyewe. Nyumbani akamuulizia mkewe; ” Hivi mke wangu hata wewe hukunipigia kura?”
Mkewe akajibu: ” Mume wangu, tulikwenda kupiga kura kumchagua Kiongozi Bora, na kama ingelikuwa kumchagua Mume Bora, kura yangu ingeangukia kwako!”
Naam, e twendeni tukapige kura kuwachagua viongozi bora, nao watokane na itikadi bora wenye kuzisimamia.
Ni Neno La Leo.

6TH ANNIVERSARY GROOVEBACK PARTY 2014 YAFANA NA BIA YA WINDHOEK DRAUGHT NDANI YA THE ARCADE HOUSE.

Meneja Biashara wa Bia ya Windhoek Joseph Boniface akielezea kuhusiana na Grooveback Party ambayo wao wamekuwa wadhamini wakuu kwa mwaka 2014 katika kutimiza miaka sita ya Grooveback
 Wa pili kushoto ni Msimamizi  wa Windhoek Salum Kabanda akielezea ni jinsi gani wanavyotoa fursa kwa vijana na kuweza kuitumia hususani kwa wanamuziki ambapo wanaandaa matamasha mbalimbali na kuweza kuwa wadhamini wakuu hivyo kuwapa changamoto vijana kwa kuweza kuandaa michanganuo mbalimbali ya kazi kuifikisha kwao na kuifanyia kazi kwa kuwasaidia.
 
 Wahudumu wa The Arcade wakiwa katika Pouzi wakati wakiwahudumia wateja wao waliofika katika Sherehe ya Miaka Sita ya Grooveback iliyofanyia jana
 Dj JB akiendelea kumwaga Burudani ya nguvu ya ngoma za Zamani na kukuna nyoyo za watu wengi waliofika katika Sherehe hiyo.
 Wapambe wa Windhoek wakiwa wanapata Picha ya pamoja wakati wa Sherehe ya kuadhimisha Miaka sita ya Grooveback
 Dj Nijo ambaye aliingia kwa awamu ya pili na kubadirisha radha ya muziki wa Lingara zile za Kitambo na kukonga nyoyo za wengi
 6th Anniversary Grooveback  Party 2014  Cheers ! na Windhoek Draught
Party ikiwa inaendelea huku Windhoek Draught zikiwa zimezagaa kwa kila Meza!
 Dj Pierra Kutoka Nchini Kenya nae hakuwa nyuma kuendeleza Burudani ya Muziki kwa ajili ya Kusherekea Grooveback Party iliyotimizia Miaka sita
 Ni mwendo wa ku party…..
 Mashabiki wa Grooveback na watumiaji wa Windhoek Draught wakiwa katika Tabasamu la Hatari …
 
 Dj KT kutoka Tanzania akiwa anaangusha bonge la moja Burudani …..
 
 Hakuna kulala full ku party …
 DJ Pinye Mkali kutoka nchini Kenya .. akiangusha Burudani … Hii ilikuwa hatare sana Mashabiki walifurahia Burudani hii ya nguvu.
 Twende Dj Pinye….
 Dj Crusia Toni kutoka Nchini Kenya akiendelea na Burudani ya Nguvu … Party inaendela..

Sumaye kubariki Tamasha la Krismas Mbeya

indexNa Mwandishi Wetu
 
WAZIRI Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi wakati wa Tamasha la Krismas Desemba 25 mwaka huu Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ilieleza kuwa maandalizi kuhusiana na tamasha hilo yanaenda vizuri.
“Tulikubaliana katika kamati tumuombe Waziri Mkuu mstaafu Sumaye aje atupe baraka kwenye tamasha la Krismasi, nafurahi kusema ni mtu wa watu, amekubali kujumuika na wadau wengine siku hiyo. Hili ni jambo la furaha kubwa kwetu.
“Wasanii mbalimbali tunaendelea kuzungumza nao kuhakikisha wanashiriki katika tamasha hilo,”  alisema Msama katika taarifa yake.
Sumaye alikuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Tatu kuanzia mwaka 1995 hadi mwaka 2005, akiwa ndiye Waziri Mkuu aliyekaa muda mrefu katika wadhifa huo kwa historia ya Tanzania. 
Alisema wamepanga kufanya maboresho makubwa katika tamasha hilo na moja ya maboresho hayo ni kuweka kiingilio rahisi zaidi ili kila mmoja aweze kuhudhuria na kupata baraka kutoka kwa waimbaji hao wanaomsifu Mungu.
“Waimbaji wote maafuru wa muziki wa Injili watakuwepo, kwani tumejipanga vizuri mno kuhakiksha kwamba tamasha hili litakuwa gumzo kila mahali.
“Wapendwa wajiandae kushiriki kwa wingi kwani watashiba kiroho kutokana na kuwa na waimbaji wengi wenye hamasa ya kiroho,” anasema. Baada ya onesho la Desemba 25 mkoani Mbeya, siku inayofuata itakuwa Uwanja wa Samora Iringa na Desemba 28 Uwanja wa Majimaji Songea.

Tigo yadhamini maonesho ya Tehema kwa vijana, Viwanja vya Posta Moja

unnamed1Ofisa kutoka mradi wa Data Huru ulio chini ya Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Daudi Fufuji akitoa maelekezo kuhusiana na namna ambavyo mradi huo unafanya kazi, maadhimisho hayo yalidhaminiwa na kampuni ya simu za mkononi ya Tigo .
unnamed3Wanafunzi wa Chuo cha A3 Institute wakionesha manjonjo yao ya upigaji wa picha katika maonesho hayo ya Tehama
unnamed5Chombo maalum ambacho kinatumika kupigia picha kutokea angani hapo kilioneshwa namna kinavyofanya kazi.
unnamed6 unnamed8Baadhi ya mabanda ambayo wadau mbalimbali wa masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama) walihudhuria.
unnamedWadau kutoka Kituo cha Utamaduni cha Ujerumani, Goethe Institute wakiwa kwenye maonesho hayo

PSPF YAPATA TUZO YA KIMATAIFA KWA KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA WAKE

unnamedBalozi wa PSPF Bw.Mrisho Mpoto alionesha tuzo iliyotolewa na Taasisi ya Kimataifa ya kusimamia Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (ISSA) kwa Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwa ajili ya kwa  kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasilino katika utunzaji wa kumbukumbu za wateja na kwa kuwasiliana na wateja wake kwa kutumia simu za mikonono, kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw. Adam Mayingu.

MIKUTANO YA KAMPENI KATIKA KATA ZA JAMHURI NA MAKONDE HUKO LINDI MJINI ZANOGESHWA NA HUTUBA ZA MAMA SALMA KIKWETE

unnamedMke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi Mama Salma Kikwete akishangiliwa na wajumbe wa Halmashauri ya Tawi la Mayani lililoko katika Kata ya Jamhuri wilayani Lindi Mjini wakati alipowasili tawini hapo kwa ajili ya mkutano wa ndani tarehe 13.12.2014. unnamed2Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayewakilisha Wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akizungumza na wajumbe wa Halmashauri ya Tawi la Mayani lililoko katika Kata ya Jamhuri huko Lindi Mjini wakati wa kikao cha kuzungumzia uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 14.12.2014 unnamed3Baadhi ya mamia ya wananchi wa Lindi Mjini waliojumuika na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakifurahia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati wa kilele cha kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 14.12.2014. unnamed4  Wajumbe wa Halmashauri ya Tawi la Tulieni wakimsikiliza kwa makini Mjumbe wa NEC Taifa ya CCN, Mama Salma Kikwete wakati alipofika tawini hapo kwa ajili ya kufanya mkutano nwa ndani na wajumbe hao kuzungumzia uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini n tarehe 14.12.2014. unnamed5Wajumbe wa Halmashauri ya Tawi la Tulieni wakimsikiliza kwa makini Mjumbe wa NEC Taifa ya CCN, Mama Salma Kikwete wakati alipofika tawini hapo kwa ajili ya kufanya mkutano nwa ndani na wajumbe hao kuzungumzia uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini n tarehe 14.12.2014. unnamed6Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa kutoka Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akipokea kadi kutoka kwa mwanachama wa Chama cha Wananchi, CUF, Ndugu Rukia Seleman Ngodo aliyeamua kuachana na chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wakati wa kilele cha kampeni ya uchaguzi wa serikali ya mitaa unatarajiwa kufanyika tarehe 14.12.2014. Kilele hicho kilifanyika katika Kata ya Makonde huko Lindi Mjini. unnamed8  Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na wananchi wa Lindi Mjini wakati wa kilele cha kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji unaotarajiwa kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014. unnamed9 Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi na wananchi wa Lindi Mjini wakati wa kilele cha kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa, vitongoji na vijiji unaotarajiwa kufanyika nchini kote tarehe 14.12.2014.

TANGAZO LA KIFO CHA MAMA MZAZI WA AKINA MWAIBALE

Twitikege Mlagha Mafumu enzi za uhai wake
 
Familia ya  Mwaibale inatangaza kifo cha mama yao mpendwa, Twitikege Mlagha Mafumu kilichotekea leo saa 5 usiku wakati akipelekwa  Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.
 
Mipango ya mazishi inafanywa nyumbani kwa mtoto wake Mwalimu Mary Anyitike, eneo la Bucha Mbagala Kuu jijini Dar es Salaam.
 
Kwa mawasiliano zaidi  wasiliana na ndugu Kulwa Mwaibale kwa simu namba 0712-707630, O758-971351 na Dotto Mwaibale kwa namba ya simu 0712-727062, O786-858550, 0754-362990.
 
Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe.