TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, March 12, 2015
Wednesday, March 11, 2015
MSHINDI PROMOSHENI YA ‘WEKA NA USHINDE’ AONDOKA NA GARI
Mkurugenzi
Mtendaji wa BOA bank Tanzania, Bw. Ammish Owusu-Amoah, akiangalia funguo za
gari hilo kabla ya kumkabidhi, Bw. Said Mohamed Bakari, mshindi wa gari aina ya
Toyota Berevis, baada ya kushinda promosheni ya ‘Weka na Ushinde’ iliyoendeshwa
na benki hiyo, Dar es Salaam leo. Kulia ni Afisa wa Benki hiyo, Bw. Solomon
Haule.
|
Mshindi wa
Gari Bw. Bw. Said Mohamed Bakari akingia ndani ya gari hilo leo baada ya
kukabidhiwa
|
Mkurugenzi
Mtendaji wa BOA bank Tanzania, Bw. Ammish Owusu-Amoah akizungumza na waandishi
wa habari baada ya kukabidhi zawadi ya gari kwa mshindi.
Waandishi wa
habari wakizungumza na mshindi wa promosheni ya gari, Bw. Said Mohamed Bakari
Mwakilishi
wa mshindi wa pili wa Promosheni ya ‘Weka na Ushinde’, Bi. Rhoda Manase
(aliyemwakilisha Bi. Thureiya Zabron) akipoke pikipiki hiyo kutoka kwa Mkurugenzi
Mtendaji wa BOA bank Tanzania, Bw. Ammish Owusu-Amoah Dar es Salaam leo.
“Tumemaliza
salama”, ndivyo wanavyosema Mkurugenzi Mtendaji wa BOA benk Tanzania, Bw. Ammish
Owusu-Amoah na Afisa wa Benki hiyo, Bw. Solomon Haule, baada ya kukabidhi
zawadi kwa washindi leo
|
PINDA AKUTANA NA RAIS WA KAMPUNI YA CONTRACTUS YA POLAND
PINDA AKUTANA NA BALOZI WA KUWAIT NCHINI
Mrembo Miss Tanzania aongoza wakazi wa dar katika zoezi la uchangiaji damu
Mshindi
wa tatu wa Miss Tanzania 2014,Doris Mollel akishiriki zoezi la
uchangiaji damu katika ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Siku ya wanawake
Duniani,iliyofanyika Buguruni Chama jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto
Ofisa Muuguzi kutoka Benki ya Damu Salama,Selina Joseph. Zoezi hilo la
uchangiaji damu liliandaliwa na Mrembo huyo. Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani,mrembo Doris Mollel
ambaye ni Miss Tanzania namba tatu kwa mwaka 2014 ameongoza mamia ya
watanzania katika zoezi la kizalendo la kuhamasisha kuchangia damu kwa
watanzania kwa ajili ya wagonjwa mbalimbali,zoezi ambalo limefanyika
jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Zoezi hilo ambalo lilikuwa
linaongozwa na mpango wa taifa wa damu salama kwa udhamini wa kampuni ya
METL lilikuwa na lengo la kupata damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya Mama na Mtoto kwani matatizo ya damu katika hospitali za Tanzania
yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku,jambo lililompelekea mrembo huyo
kuamua kujitoa kuhamasisha watanzania kujitokeza kwa wingi katika zoezi
hilo.
wa tatu wa Miss Tanzania 2014,Doris Mollel akishiriki zoezi la
uchangiaji damu katika ikiwa ni sehemu ya kusherehekea Siku ya wanawake
Duniani,iliyofanyika Buguruni Chama jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kushoto
Ofisa Muuguzi kutoka Benki ya Damu Salama,Selina Joseph. Zoezi hilo la
uchangiaji damu liliandaliwa na Mrembo huyo. Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani,mrembo Doris Mollel
ambaye ni Miss Tanzania namba tatu kwa mwaka 2014 ameongoza mamia ya
watanzania katika zoezi la kizalendo la kuhamasisha kuchangia damu kwa
watanzania kwa ajili ya wagonjwa mbalimbali,zoezi ambalo limefanyika
jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Zoezi hilo ambalo lilikuwa
linaongozwa na mpango wa taifa wa damu salama kwa udhamini wa kampuni ya
METL lilikuwa na lengo la kupata damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya Mama na Mtoto kwani matatizo ya damu katika hospitali za Tanzania
yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku,jambo lililompelekea mrembo huyo
kuamua kujitoa kuhamasisha watanzania kujitokeza kwa wingi katika zoezi
hilo.
43 WAAPISHWA KUWA MANAIBU WASAJILI WA MAHAKAMA YA TANZANIA LEO JIJINI DAR ES SALAAM.
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila akimwapisha Mhe.
Lenatus Ishengoma (kulia) kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania leo jijini
Dar es salaam. Wanaoshuhudia kiapo hicho ni Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Mohamed
Othman Chande (kushoto) na Mhe. John Kahyoza, Msajili Mahakama Kuu ya Tanzania.
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila akimkabidhi Katiba
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwongozo wa utendaji kazi wa Mahakama
Mhe. Zahara Abdallah Mlacha mara baada ya kumwapisha kuwa Naibu Msajili wa
Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam.
![]() |
| Mhe. Elizabeth Mkwizu akisaini hati ya kiapo cha kuwa Naibu Msajili wa Mahakama mbele ya Jaji Kiongozi Mhe. Shaaban Ali Lila baada ya kuapishwa leo leo jijini Dar es salaam. |
Naibu Msajili
wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Hussein Shaaban Mushi akipokea Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania na Mwongozo wa utendaji kazi wa Mahakama kutoka kwa Jaji Kiongozi Mhe. Shaaban Ali Lila mara baada ya kuapishwa
kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania leo jijini Dar es salaam.
Mhe. Isaya
Khalfan (kulia) akila kiapo cha kuwa Naibu Msajili wa Mahakama ya Tanzania
mbele ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila
(kulia) leo jijini Dar es salaam.
Jaji
Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Shaaban Ali Lila (aliyekaa) akisaini
kiapo cha Mhe. Angela Maria Thei (kulia) aliyeapishwa kuwa Msajili wa Mahakama ya Tanzania katika hafla
fupi iliyofanyika viwanja vya Mahakama ya Rufani leo jijini Dar es salaam.
Anayetazama kiapo hicho ni Msajili wa Mahakama kuu ya Tanzania Mh. John Kahyoza
(katikati).Picha na Aron Msigwa –MAELEZO.
Tuesday, March 10, 2015
Jumuiya ya Bango Sangho watoa huduma za afya bure Kibugumu
Dk
Hamza Mzige kutoka Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe akimpima moja ya
mtoto aliyeletwa kupata huduma katika zoezi hilo lililoendeshwa eneo la
Kibugumu Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa huduma hizo, Dk. Ali Mzige (wa kwanza kulia) akitoa huduma kwa wagonjwa katika zoezi hilo.
Mmoja
wa wahudumu wa afya akitoa huduma kwa baadhi ya watoto waliofikishwa
katika zoezi hilo lililoendeshwa eneo la Kibugumu Kigamboni jijini Dar
es Salaam.
Dk Hamza Mzige kutoka Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe akitoa huduma kwa mmoja wa wateja wake katika zoezi hilo.
BALOZI WA HARAKATI ZA “IMETOSHA!” HENRY MDIMU APELEKA UJUMBE WAKE UWANJA WA TAIFA
Na Henry Mdimu
Tangu
asubuhi leo nilikuwa busy na awareness za uwanja wa Taifa katika mechi
ya watani wa Jadi Yanga na Simba (picha ya pili). Ila jioni hii
nilipoangalia simu yangu nikakuta watu wakinilaumu kutokana na tukio la
mtoto Baraka Cosmas (picha ya kwanza) ambaye usiku wa kuamkia leo
amekatwa mikono yake.
Wanasema nilikuwa nakula Bata Uwanja wa Taifa huku watu wanateketea.
Hasa alikuwa akiongea mtu anaitwa @hmgeleka.
Hasa alikuwa akiongea mtu anaitwa @hmgeleka.
Kwanza
nalaani kitendo hicho cha kikatili na kuzidi kumuomba Rais wangu Mhe
Jakaya Mrisho Kikwete aongee na vyombo vyake vya usalama, wasiliache
hili lipite hivi hivi.
Lakini jingine jamani suala hili sio la mmoja. Kwa sababu nimejitwika ubalozi ndio nilaumiwe kwa hata lililo mbali na mimi?
Vita hii ni ya wote, mimi nina wiki mbili tu tangu nianze kazi hii na bado natafuta mtaji wa kuendesha zoezi langu.
Tafadhali tutende wote tusinyoosheane vidole, huku tukiwa vijiweni, mmenielewa?
#IMETOSHA
Vita hii ni ya wote, mimi nina wiki mbili tu tangu nianze kazi hii na bado natafuta mtaji wa kuendesha zoezi langu.
Tafadhali tutende wote tusinyoosheane vidole, huku tukiwa vijiweni, mmenielewa?
#IMETOSHA

.jpg)
Bango
la harakati za “Imetosha!” likiingizwa uwanjani sambamba na ya FIFA ma
FIFA Fair Play wakati wa mchezo wa ligi kuu wa watani wa jadi Simba na
Yanga Uwanja wa Taifa leo. Chini ni Balozi wa Harakati za Imetosha Henry
Mdimu akiongea machache kuhusu harakati hizo zenye lengo la kuhamasisha
wadau wote kukomesha vitendo vya mauaji na vya kikatili dhidi ya ndugu
zete Albino.
NHIF MOROGORO YAADHIMISHA WIKI YA WANAWAKE KWA KUTEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA MKOANI MOROGORO
Katika
kuadhimisha wiki hiyo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ulitembelea kituo
cha watoto yatima cha Aldee Musleem Chidren Centre cha Morogoro , na
kugawa vitu mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya kituo hicho vikiwemo
vyandarua, vyakula na vifaa vya shule kama anavyoonekana Kiongozi wa
msafara wa wafanyakazi wa NHIF Bi. Rose Ongara akikabidhi zawadi hizo
kwa mmoja wa viongozi wa kituo hicho Bwana Rajabu Shomari.
Baadhi
ya watoto wa kituo hicho wakikabidhiwa zawadi hizo na kiongozi wa
msafara kutoka NHIF Bi Rose Ongara pamoja na wafanyakazi wa Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya mkoani Morogoro.
Bi.Rose Ongara akifurahi na watoto wa kituo hicho wakati akikabidhi zawadi hizo.
KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AMALIZA ZIARA YAKE CHILONWA, KESHO KUENDELEA JIMBO LA MTERA
WEMA SEPETU NDANI YA STUDIO ZA RADIO 5 JIJINI ARUSHA
Wema Sepetu akiwa ndani ya
studio za Radio 5 jana mara baada yan kufanya ziara fupi mjengoni hapo
akielezea pia kuhusu show yake ya black and white party iliyofanyika
jana usiku tarehe 7/3/2015 jijini Arusha kushoto ni mtangazaji mahiri wa
kituo hicho Wilfredy akiwa anafanya kipindi na mwanadada huyo,
Wanaonekana pichani ni team Wema.(Habari Picha na Pamela Mlollel wa
jamiiblog)
Wema Sepetu akiwa anaeleza
furaha yake yakuwepo jiji Arusha ambapo amesema jiji la Arusha ni
miongoni mwa majiji anayoyapenda, Mwanza ikiwa ya kwanza na Arusha ya
pili, Kulia ni msanii Petiman a.k.a Wakuache.
Msafara wa Wema Sepetu ukiingia kwa mbwembwe katika studio za Radio5 zilizopo njiro jijini Arusha.
WANAWAKE WA MSD WASHEREHEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA AINA YAKE.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa (MSD), Bw. Cosmas Mwaifani akifungua sherehe za Siku ya Akina Mama Duniani zilizofanyika.
Bw.
Mwaifani akimkaribisha mgeni rasmi wa sherehe hizo, Bi.Helen Mwakipunda
ambaye ni Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.
Bi. Mwakipunda akizungumza na wafanyakazi wa (MSD) wakati wa sherehe hizo
CMEA ni suluhilisho kwa wanamuziki- January Makamba
Naibu Waziri Sayansi na Teknolojia January Makamba akizungumza wakati wa
uzinduzi wa kampuni ya na kampuni ya Copyrights Management East Africa
Limited (CMEA).
Afisa Mtendaji Mkuu wa CMEA,
Paul Matthysse akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa kampuni hiyo
yenye lengo la kuwakwamua wanamuziki katika umaskini. CMEA pia
itawawezesha pia watayarishaji wa muziki na wasanii wengine pamoja na
vyombo vya habari kupata kufahami takwimu sahihi za nymbo zilizochezwa
kwa siku, wiki, mwezi na kwa mwaka.
…………………………………………………………………………………………..
MAMA SALMA KIKWETE MGENI RASMI KILELE CHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI MKOANI DAR
RAIS DR. SHEIN AFUNGUA WA HOTELI YA PARK HYATT ZANZIBAR
Moruwasa kufanya upanuzi wa bwawa la Mindu
Hussein Makame-MAELEZO MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Manispaa ya Morogoro (MORUWASA) imepanga kuongeza uwezo wa bwala la Mindu mara mbili zaidi ili liweze kukusanya maji mengi zaidi kukidhi mahitaji ya maji ya wakazi wa manispaa ya Morogoro.
Akizungumza na waandishi wa habari waliomtembelea ofisi kwake mjini Morogoro mwisho mwa wiki hii, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka hiyo Mhandisi Nicholaus Angumbwike, alisema pia wamepanga kujenga mtambo mwengine wa kutibu maji ili kuongeza kiasi cha maji kutoka chanzo hicho. Alisema tayari mkandarasi ameshaandaa pendekezo la mradi (proposal) kupitia awamu ya kwanza ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) na kwamba imeshakamilika na ameiwasilisha Wizara ya Maji kwa ajili ya utekelezaji. Mhandisi Angumbwike aliongeza kuwa wanatarajia kwamba utekelezaji wa mradi huo utafanyka katika awamu ya pili ya WSDP iliyoanza Juni mwaka jana iwapo Wizara itawapatia fedha kwa ajili ya kazi hiyo. “Kuna utafiti imeshafanyika kuhusu bwawa la Mindu, kuna uwezekano kwamba uwezo wa bwala la Mindi ukaongezeka mara mbili zaidi yaani uwezo wa kukusanya maji mengi zaidi kuliko ilivyo sasa na tukajenga mtambo mwengine wa kutibu maji ili kuongeza kiasi cha maji yanayotoka chanzo cha bwawa la Mindu” alisema Mhandisi Angumbwike na kuongeza: “Hii kazi imeshafanyika katika mradi wa WSDP awamu ya kwanza, mkandarasi amefanya akaandaa proposal yake na tuna matumaini kwamba ameshakamilisha na amewasilisha Wizara ya Maji, tunatarajia katika hii awamu ya pili kama Wizara ikitufikiria tuweze kutekeleza mradi huo”
Alisema kinachotakiwa kufanyika ni kuongeza tena urefu wa tuta la bwawa hilo kwa urefu wa mita 2 na kujenga mtambo mwingine wa kutibu maji kwani mtambo ulipo una uwezo wa kutibu maji kwa siku lita milioni 27 tu. Aliongeza kuwa gharama za mradi huo wa kuongeza uwezo wa chanzo hicho cha maji cha bwawa la Mindu na mtambo wa kutibu maji, kwa mwaka 2008 ilikuwa ni shilingi Bilioni 35. Alisema mbali na juhudi hizo MORUWASA imekuwa ikitafakari vyanzo vingine vya maji kukidhi mahitaji ya wakazi 315,000 wa manispaa ya Morogoro ikiwemo kufikiria kwenda juu zaidi ya milima ya Uluguru kutafuta vyanzo hivyo. Alisema wanaangalia uwezekano wa kuchimba visima virefu lakini changamoto iliyopo ni kwamba ni shida kupata maeneo ambayo watapata maji baridi kwa sababu maeneo mengi ya Morogoro ukichimba unapata maji ya chumvi. Kwa upande wa uboreshaji wa miundombinu chakavu, Mhandisi Angumbwike alisema wamepokea fedha kiasi cha shilingi Milioni 240 kutoka Wizara ya Maji ambayo itatusaidia kubadilisha kilomita kadhaa ya miundombinu ya maji iliyochakaa ili kuboresha upatikanaji wa maji. Katika kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji vilivyopo, Mhandisi Angumbwike alisema wanashirikia na wadau wengine kama Ofisi ya Bonde la Maji, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, katika kulinda vyanzo hivyo. “Tumekuwa tukifanya kazi pamoja, tunakutana pamoja tunakwenda kwenye miradi (sites) tumeainisha maeneo ambayo yanataka kuyatunza, tumetoa elimu kwa wananchi watambue kwamba jukumu la kutunza vyanzo vya maji ni la kila Mtanzania na wao wakiwemo”alisema na kuongeza: “Wananchi wanatakiwa watambue kwamba jukumu la kutunza vyanzo vya maji ni muhimu kwa manufaa ya Watanzania wote” Kuhusu wizi wa maji, Mkurugenzi huyo alisema wana Operesheni za kukamata watu wanaojiunganishia maji kwa kupita nyumba kwa nyumba ili kuwabaini na kuwakamata watu ambao wanatumia maji bila kuyalipia. “Wapo watu ambao wanataka wapate maji bila kuyalipia, tunafanya operesheni nyumba kwa nyumba na tunapowakamata tunawatoza faini na kuwachukulia hatua lakini shida kubwa ni uunganishaji mwingine ni ngumu kuubaini” alisema Mkurugenzi huyo na kuongeza: “Wapo tuliowakamata kwa ushirikiano na wananchi na tunatoa motisha wa fedha kwa wananchi wanaotupa taarifa hizo. Pia tunacho kikosi maalum kinachopita mitaani na katika hoteli mbalimbali kuchunguza mifumo ya maji ili kubaini watu wanaoiba maji. Tumeshakamata baadhi ya hoteli zimejiunganishia maji, tukawauliza wanasema wamechimba kisima lakini baada ya kupima sampuli ya maji tunakuta kwamba ni maji ya Morowasa” Hivyo aliwataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kuwafichua wezi wa waji au watu wanaojiunganishia maji kiholela ili kudhibiti asimilia 40 ya maji ambayo hayaipatii mapato MORUWASA.
Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) ya mwaka 2006 hadi 2025, inatekelezwa kwa awamu ya miaka mitano mitano ambapo awamu ya Kwanza ilianza mwaka 2007 na kukamilika 2014 na awamu ya Pili ilizunduliwa na Waziri wa Maji Juni mwaka jana tayari kwa utekeleaji.
Subscribe to:
Posts (Atom)





