TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Thursday, January 3, 2013
SHEREHE ZA MIAKA 49 YA MAPINDUZI KUANZA KESHO ZANZIBAR
Na Maelezo Zanzibar
Sherehe za miaka 49 ya Mapinduzi
ya Zanzibar zinaanza rasmi kesho kwa kazi za kufanya usafi wa mazingira
katika Wilaya zote za Unguja na Pemba.
Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na Kamati ya Sherehe na maadhimisho ya kitaifa imeonesha kuwa Miradi ipatayo 62 inatarajiwa kuzinduliwa katika Visiwa vya Unguja na Pemba.
Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na Kamati ya Sherehe na maadhimisho ya kitaifa imeonesha kuwa Miradi ipatayo 62 inatarajiwa kuzinduliwa katika Visiwa vya Unguja na Pemba.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete atafungua Skuli mpya ya Sekondari ya
Mlimani, iliyopo Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja ikiwa ni Shamra shamra
za Sherehe hizo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein naye atazindua miradi
mbalimbali ikiwemo Ufunguzi wa Jengo la Chuo cha Utawala wa Umma huko
Tunguu Wilaya ya Kati Unguja.
Pia atafungua mradi wa
E-Government katika Wilaya ya Magharibi Unguja na kufungua Skuli mpya ya
Sekondari ya Umoja, iliyopo Uzini Wilaya ya Kati Unguja pamoja na
kuzindua Barabara kutoka Mfenesini hadi Bumbwini Wilaya ya Kaskazini B
Unguja.
Hali kadhalika Dkt.Shein
atafungua Mradi wa kuhama kutoka Teknolojia ya Analojia kwenda Dijitali
na Ufunguzi wa Studio ya kurikodia Sanaa na Muziki ambapo kwa upande wa
Pemba atafungua Skuli mpya ya Sekondari ya Shamiani iliyopo Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.
Mbali na Shughuli hizo siku ya
kilele hapo January 12 kwenye Uwanja wa Amani Rais Shein atakagua
Gwaride lililoandaliwa na Vikosi vya ulinzi na usalama na Vikosi vya SMZ
pamoja na kulihutubia Taifa na Usiku kuhudhuria Taarab rasmi huko
katika Ukumbi wa Salama Hoteli ya Bwawani
Naye Makamo wa Kwanza wa Rais
Maalim Seif Shariff Hamad atafanya uzinduzi mbali mbali kwa ufunguzi wa
Skuli na Maabara wakati Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Idd atafanya
Shughuli kama hizo kwa ufunguzi wa Skuli na Majengo mapya ya nyumba za
Wazee zilizopo Sebleni Wilaya ya Mjini Unguja.
Mbali na shughuli hizo baadhi ya
Marais wastaafu,Mawaziri mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar
na Muungano watafanya shughuli za ufunguzi wa Miradi mingine ikiwemo ya
Maji, Skuli na Mradi wa Mnara wa Radio wa Masafa ya Kati uliopo Bungi
Wilaya ya Kati Unguja.
Achomwa Kisu akidai haki yake
Mkazi wa Mji wa Moshi akiwa katika majeraha baada ya kuchomwa kisu na mfanyabiashara wa kuuza nyama ya (Bucha) eneo la Moshi Mjini. tukio hili limetokea siku ya Mwaka Mpya 2013.
Hapa Ndugu zake wakiwa katika Hospitali ya Mawenzi kupata Huduma ambayo hata hivyo iliwachukua Zaidi ya Masaa Mawili bila kupata ama kuonana na wauguzi.
Ndugu akijaribu Kumfariji
Tuesday, January 1, 2013
Manispaa ya Kinondoni kuongeza kasi ya utatuzi wa migogoro ya ardhi
MANISPAA ya Kinondoni
imeahidi kuongeza nguvu katika kushughulikia masula ya migogoro ya
ardhi , huku pia ikiwataka wananchi kutoa ushirikiano wao katika
mapambano dhidi ya watu wote wanaokwenda kinyume na utaratibu uliopo.Akizungumza
na jiji Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Fortunatus
Fwema alisisitiza kuwa katika kukabiliana na migogoro hiyo, uongozi wa
manispaa umekuwa ukichukua hatua za haraka kuhakikisha viongozi na
watendaji wanaojihusisha na migogoro na kashfa za ardhi wanachukuliwa
hatua mara moja.
Alisema katika kuishughulikia
migogoro hiyo, manispaa imekuwa ikiendelea kuyafanyia kazi mapendekezo
ya Kamati ya migogoro ya ardhi iliyoundwa kwa maelekezo ya Rais, hatua
aliyosema kuwa kwa kiasi kikubwa imeweza kuleta mafanikio.
“Hadi sasa migogoro iliyokuwepo
imeshughulikiwa kwa asimilia 95 na kupatiwa ufumbuzi, kwa sasa migogoro
iliyopo ni ile inayotokana na uvamizi wa ardhi unaofanywa na makundi ya
watu kinyjme na sheria ambayo manispaa kwa kushirikiana na Serikali kuu
imeendelea kuipatia ufumbuzi” alisema Fwema.
Aidha alisema kumekuwa na mawazo
potofu ya baadhi ya watu kwamba manispaa hiyo imekuwa ikifanya
upendeleo kwa wakubwa wakati wa uuzaji wa viwanja vyake, madai aliyosema
kuwa si ya kweli na zaidi yamelenga kuichafua manispaa hiyo.
“Madai haya si ya kweli
ikizingatiwa kuwa katika kipindi kinachokaribia miaka 10 manispaa ya
Kinondoni haijawahi kupima viwanja na kuviuza kwa wananchi kutokana na
changamoto mbalimbali hasa zinazohusiana na utwaaji wa ardhi na ukosefu
wa fedha kwa ajili ya kugharamia fidia na upimaji” alisema Fwema.
Alisema manispaa kwa muda mrefu
imekuwa ikihangaika kutafuta fedha za kupimia viwanja kutoka sehemu
mbalimbali zikiwemo taasisi za fedha na madhumuni ni kuvipima viwanja
hivyo ili kukabiliana na ongezeko la ujenzi holela katika maeneo
yasiyopangwa.
Kuhusu utoaji wa vibali vya ujenzi
na kushughulikia maombi ya kubadili matumizi ya ardhi, Fwema alisema
manispaa hiyo kwa kutumia wataalam wake, kabla ya kutoa vibali hivyo
wameweka utaratibu wa kuhakikisha maombi yaliyotolewa, hayakinzani na
matumizi yaliyopo na yaliyoidhinishwa katika mpango wa matumizi ya
ardhi.
“NAFSI NI NYONGE” Tusameheane na maisha yaendelee. karibu 2013 kwa ufanisi zaidi.!
Wapendwa ndugu,jamaa na marafiki
popote pale mlipo,yamebaki masaa kadhaa kuuaga mwaka 2012,ambao kwa
hakika ulikuwa na changamoto nyingi za kimaisha,dhoruba za hapa na pale
wengi zilitukumba,lakini kwa kudra za Mwenyezi Mungu akatushika mkono
akatuinua na maisha yakaendelea.
Binafsi
mpaka dakika hii namshukuru Mungu nikiwa mwenye afya njema
kabisa.Maisha ya sasa Wanadamu wengi wamekuwa dhaifu kwa mambo
mengi,lakini Mungu ndiyo njia sahihi wa kumtumia katika sala zako
kuyashinda majaribu na madhaifu ya Dunia.Yako mengi ambayo naweza
nikayaandika hapa lakini bado yasitoshe pia.Nasema asanteni kwa
ushirikiano wenu mkubwa kwa namna moja ama nyingine,kama kuna mahali
nilikosea,tukakwaruzana kidogo basi “NAFSI NI NYONGE” Tusameheane na
maisha yaendelee.
Tunahamia
mwaka mwingine mpya kabisa 2013,basi na tuendelee na ushirikiano huu
tuliokuwa nao kwa mambo mbalimbali yenye kujenga na kuleta tija katika
maisha yetu,Mwaka 2013 uwe wa kuhakikisha kweli sote pia tumehamia
kwenye mfumo wa kidijitali,tushauriane,tuelemishane tunyooshane njia
iliyo sahihi ili kila mmoja kila wakati abaki nafsini mwake mwenye
furaha daima,Pia tumtangulize Mungu kila wakati kwa kila jambo ili pia
azidi kuzibariki kazi za mikono yetu daima.
Kwa
Blogaz wenzangu,changamoto nyingi tumekumbana nazo 2012,ikiwemo tatizo
kuu la KUKOPY NA KUPASTE.! Na nyinginezo nyingi tuzijuazo zinatusumbua
kwa namna moja ama nyingine,basi ni nyema 2013 iwe ya kuzitafutia
ufumbuzi,kama si kuzimaliza kabisa basi angalau tuendelee kuzipunguza
ili kuzimaliza kabisa,huku suala la kujituma na ubunifu vikiwa ndio ngao
kuu ya mabadiliko miongoni mwetu.Ushirikiano tuliokuwa nao umeonesha
tuna uwezo mkubwa wa kuisadia jamii inayotuzunguka na hata serikali pia
kwa namna moja ama nyingi,basi tusimame kidete kuhakikisha ushirikiano
huu hauteteleki ama haupotei kirahisi,badala yake tuiimarishe zaidi kila
kona .
Natoa
shukurani za dhati kabisa kwa makampuni na wadau mbalimbali
ambayo/ambao kiukweli yametoa mchango mkubwa kuhakikisha tunasonga mbele
na libeneke hili ,si vibaya nikiyataja makampuni hayo kuwa ni Serengeti
Breweries Ltd,Airtel,Bayport,Msama Promotions Ltd,kampuni ya
R&R,Dada Teddy Mapunda,Hoyce Temu,Blogaz wote (bila kinyongo) na
wengine waliotupa hatua ya kusogea kwa namna moja ama nyingine,Mungu
awabariki sana.
Asanteni
Nawatakia heri ya sikukuu ya Mwaka mpya.
MSTAHIKI MEYA JERRY SILAA AKABIDHI ZAWADI ZA MWAKA MPYA KWA KITUO CHA TUSHIKAMANE CHILDREN CARE TRUST FUND
Mstahiki
Meya wa Manispaa ya Ilala Jerry Silaa akikabidhi Mbuzi kwa Mkurugenzi
wa Taasisi ya Tushikamane Children Care Trust Fund Bw. Gratho Messy
Mbele (wa kwanza kulia) na Mkuu wa Shule ya Tushikamane Bi. Euphrosine
Mtundu, kama zawadi kwa watoto yatima wa kituo hicho ambapo panapo
majaliwa hapo kesho atajumuika nao kupata chakula cha mchana.
Anayeshuhudia tukio hilo ni Diwani wa Kata ya Tabata Hajati Mtumwa
Mohamedi (wa pili kushoto)
Mstahiki Meya Jerry Silaa akikabidhi ndoo ya mafuta kwa kituo hicho
chenye lengo la kuhudumia watoto yatima na watoto wanaoishi katika
mazingira magumu na hatarishi kwa kuwapa mahitaji muhimu kama vile
elimu, afya, chakula, malazi, mahitaji ya shule, pamoja na huduma za
kisaikolojia na ulinzi dhidi ya manyanyaso.
Viongozi wa kituo hicho wakimshukuru Mstahiki Meya Jerry Silaa.
Meya
wa Manispaa Mstahiki Jerry Silaa akibadilishana mawazo na baadhi ya
viongozi wa kituo hicho mara baada ya kukabidhi zawadi za vyakula ikiwa
ni mchango wake kwa vijana hao katika kusherehekea mwaka mpya 2012/2013.
Kila
mwaka wakati wa sherehe za mwaka mpya Mstahiki Meya wa Manispaa ya
Ilala yeye binafsi hutoa sadaka kwa wahitaji kwa kumshukuru Mungu kwa
kumuwezesha kumaliza mwaka salama.
Leo
Mstahiki Meya Jerry Silaa ametoa chakula kwa kituo cha Watoto Yatima na
watoto Yatima na watoto Waishio Katika Mazingira Hatarishi cha
Tushikamane Children’s Care Trust Fund ambapo pamanapo majaliwa hapo
kesho atakula chakula pamoja nao.
Asasi
hiyo ya Tushikamane Children’s Care Trust Fund ilianzishwa mwaka 2001
na kupata usajili wa kudumu mwaka huo huo ili iweze kujiendesha kwa
mujibu wa sheria za nchi.
Rais Kikwete azindua matokeo ya sensa ya watu na makazi 2012.
Rais
Jakaya Kikwete akibonyeza kitufe kwenye kompyuta kuzindua matokeo ya
Sensa ya Watu na Makazi mwaka 2012 jana jijini Dar es salaam ambapo
idadi ya watu Tanzania imefikia milioni 44 929 002.Picha na Aron Msigwa
-MAELEZO
Rais Jakaya Kikwete katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali na vyama vya siasa.
Rais
Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja kwenye bango linaloonyesha
idadi ya watu Tanzania na viongozi na watendaji wa Ofisi ya Taifa ya
Takwimu mara baada ya kutangazwa kwa matokeo ya sensa ya watu na makazi
ya mwaka 2012.
Mkurugenzi wa Rahabu Ulcers Clinic, Dk Rahabu Rubago atoa msaada kituo cha yatima Kurasini
OFISA mfawidhi kituo cha kulelea
watoto yatima Kurasini, Ramadhani Yahaya ameiomba serikali kufanya
jitihada za kuwaondoa vijana wanaoendelea kuishi katika kituo hicho,
licha ya kupoteza sifa ya kuishi katika kituo hicho kwa kuwa wamevuka
miaka 18.
Ofisa huyo aliyaeleza hayo jijini Dar es
Salaam jana, wakati Mkurugenzi wa Rahabu Ulcers Clinic, Dk Rahabu Rubago
alipokuwa akitoa zawadi mbalimbali kwa ajili ya kusherehekea mwaka mpya
ikiwemo chakula, vinywaji na vifaa vya shule kwa watoto wa kituo hicho
waliokuwa wamechanganyika na watoto wa kituo cha wasabato.
Ramadhani alisema kituo hicho
kwa sasa kinakumbwa na changamoto kubwa ya kuwa na vijana wengi wenye
umri zaidi ya miaka 18 hivyo wanashindwa kufuata masharti ya kituo hicho
ikiwemo kuwa ndani ya uzio ifikapo saa 12 jioni.
“Changamoto kubwa ni vijana
wenye umri mkubwa kuendelea kuishi katika kituo hiki naiomba serikali
iwatengenezee vijana hawa mazingira ya kuwaondoa katika maeneo haya ili
nao wakawe na maisha yao na kuachana na utegemezi wa hapa” alisema
Ramadhani
Naye Dk Rahabu aliwataka vijana
na watoto hao kutokukata tamaa katika maisha yao huku akiwataka kusoma
kwa bidii ili waweze kukamilisha ndoto zao na malengo waliyojiwekea.
“Mimi niliishi hapa nimekuja
kufurahi nanyi na kuwatia moyo msijione kama mpo peke yenu tupo pamoja
na kutokana na kujibidiisha tumefanikiwa hivyo nanyi nawahasa
mjibidiishe kwa bidii zote ili muweze kufanikiwa na kufikia malengo
yenu,” alisema Dk Rahabu”alisema Rahabu
Naye mwanafunzi anayesoma chuo
cha uhasibu, ambaye anaishi katika kituo hicho, Robert Bernard ameiomba
serikali kutowaondoa vijana waliozidi miaka 18 bila kuwatengenezea
mazingira mazuri ya kwenda kuishi.
“Kuondoka hapa si tatizo
tunachoomba kama serikali inataka kutuondoa hapa kwa kuwa umri wetu
mkubwa hatukaidi bali tunachoomba watuwekee mazingira mazuri huko
wanakotaka twende lakini bila hivyo watakuwa hawajatusaidia” alisema
Bernard.
Wasanii Richard wa Big Brother na Mwanamuziki Dully, usiku wa Mkesha wamekuwa ni miongoni mwa watu waliofanya shangwe katika kusherehekea kuingia mwaka 2013.
Shangwe hizo zimefanyika mara tu baada ya kugonga sekunde ya 60 ya
kuthibitisha kuingia mwaka mpya ambapo walisikika wakipiga kelele na
shangwe huku wakiwaomba mashabiki wao kuingia jukwaa kusakata Ngoma huku
wakizongwa na maelfu ya wanawake na Vijana wa mji wa Moshi kutaka
kucheza na kufurahi nao.
aidha alikuwa ni Richard ambaye muda wote alionekana akigandwa
na wanawake wengi wa kizungu huku yeye akionekana kuwakwepa na
kuendelea kucheza hadi furaha yake ilipokwisha na kwenda kujipumzisha
na kuhusu kugandwa na kuwa na kundi kumbwa la ulinzi Dully "
hawa ni jamaa zangu yaani Mashabiki wangu, ambao siku zote wananipa
sapoti kubwa, hivyo mara baada ya kuingia katika mji wa Moshi
wamenipokea vizuri na ndiyo maana unawaona, na kuhusu kina dada hawa
hilo siwezi kusema kwani wewe mwenyewe unajua mimi mashabiki wangu ni
kina nani, na hata siku moja siwezi kuacha kuwasifia na kutaka kuja
kwangu vile wapendavyo"alisema Dully huku akitoweka na Mmoja wa
Wasichana waliokuwa wakimganda Tangu alipoingia ndani ya CLUB LA-LIGGA.
PICHA ZOTE NI TUKIO AMBALO LIMEFANYIKA WAKATI WA KUUKARIBISHA MWAKA MPYA KWENYE UKUMBI WA KISASA WA -CLUB LA- LIGGA
Subscribe to:
Posts (Atom)
