TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 9, 2013

MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA ZANZIBAR MAALIM SEIF SHARIF HAMAD AFUNGUA SKULI YA MBUYU TENDE ZANZIBAR

 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Ali Juma Shamhuna mara alipowasili katika Kijiji cha Mbuyu Tende Wilaya ya Kaskazini “A”kwa ajili ya kufungua Skuli ya Primary yenye madarasa Manne,ikiwa ni Shamra shamra za Maadhimisho ya Miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akikata Utepe kuashiria kufungua Skuli yenye madarasa manne katika Kijiji cha Mbuyu Tende Wilaya ya Kaskazini “A”,ikiwa ni Shamra shamra za Maadhimisho ya Miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akipanda Mche wa Mnazi baada ya kuupanda katika eneo la Skuli ya Mbuyu Tende Wilaya ya Kaskazini “A”,Baada ya Kuifungua Skuli hiyo ikiwa ni Shamra shamra za Maadhimisho ya Miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Wanafunzi wa Skuli ya Mbuyu Tende Wilaya ya Kaskazini “A”,wakifurahia Baada ya 
kufunguliwa kwa Skuli yao ikiwa ni Shamra shamra za Maadhimisho ya Miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
PICHA NA YUSSUF SIMAI-MAELEZO ZANZIBAR.
……………………………………………………….

                     Na Khadija Khamis –Maelezo Zanzibar                      
 Makamo wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad amewataka Wazazi na Walezi wa Wanafunzi wa Skuli ya Mbuyu Tende kujenga Mashirikiano na Walimu ili  kuweza kuwapatia  haki na fursa sawa wanafunzi wa kike na wakiume Skulini hapo.      
Hayo ameyasema leo huko Skuli ya Msingi Mbuyu Tende Wilaya Kaskazini “A” Unguja wakati wa ufunguzi wa skuli hiyo ikiwa ni mwendelezo wa shamra shamra za kutimiza miaka 49 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 Maalim Seif  amewataka Wazazi wasikubali kuwaozesha watoto wa kike waume mapema kwani hali hiyo ndiyo inayochangia ukosefu wa Walimu wa kike wazawa katika Vijiji  vingi.
 Aidha alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaendelea kuwapatia wananchi wake haki ya elimu bila ya malipo ili kuondosha adui ujinga na kuwaletea maendeleo.
  “Elimu ni msingi wa maisha kwa vijana na ndio inayoleta maendeleo na mwangaza hasa wakati wa sasa na ujinga ni kiza katika maisha ya leo,”alisisitiza Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar.

No comments:

Post a Comment