TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 9, 2013

TUME YA MABADILIKO YA KATIBA YAENDELEA KUKUTANA NA VYAMA VYA SIASA

Mwenyekiti wa Chama cha Kijamii (CCK), Constantine Makitanda akizungumza katika mkutano uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba mara baada ya  Chama hicho kuwasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya leo (Jumanne Januari 8, 2013).
 
Katibu wa Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD),Ndg.  Juma  akizungumza wakati wa mkutano uliofanyika leo (Jumanne Januari 8, 2013) baina ya Chama hicho na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambapo Chama hicho kiliwasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Kulia ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba na Katibu wa Tume,Assaa Rashid.
 
Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD) wakifuatilia mkutano baina yao na Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo( Jumanne Januari 8, 2013), ambapo Uongozi wa Chama hicho uliwasilisha maoni ya Chama hicho kuhusu Katiba Mpya.
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Wakulima (AFP), Rashidi Mohamed akiwasilisha maoni yao kuhusu Katiba kwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam leo (Jumanne, Januari 8 2013).
 
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Mhe. Raza Hamad akizungumza  katika mkutano na Viongozi wa Chama cha Wakulima (AFP) uliofanyika katika viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam wakati Chama hicho kilipowasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya leo (Jumanne Januari 8, 2013).
 
Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Salim Ahmed Salim akizungumza katika mkutano na Viongozi wa Chama cha Kijamii (CCK) uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam wakati Chama hicho kilipowasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya leo (jumanne Januari 8, 2013).
 
Mjumbe Wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Ndg. Ussi Khamis akizungumza katika mkutano na Viongozi wa Chama cha Kijamii (CCK) uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam wakati Chama hicho kilipowasilisha maoni yao kuhusu Katiba Mpya leo (jumanne Januari 8, 2013).

No comments:

Post a Comment