TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 9, 2013

WAZIRI MKUU PINDA AZINDUA KITABU CHA WAPIMBWE

    
*Ataka makabila mengine yatunze historia zao.
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezindua kitabu cha historia ya kabila la Wapimbwe lililoko mkoani Katavi na kutayataka makabila mengine kuandika historia zao ili waweze kutunza kumbukumbu kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Akizindua kitabu hicho hivi karibuni mjini Mpanda, Waziri Mkuu aliwataka watu wa makabila mengine ya mkoa wa Katavi ambayo ni Waruira, Wabende, Wakonongo na Warungwa wafanye tafiti kuhusu mila na tamaduni zao na kisha waandike vitabu vyao.
Kabla ya uzinduzi huo, mtunzi wa kitabu hicho, Bw. Peter Mgawe alisema kitabu hicho kimetokana na utafiti uliofanywa tangu mwaka 2007 ambao ulilenga kukusanya  taarifa na masimulizi mbalimbali kutoka kwa wazee wa Kipimbwe ambao wameishi miaka mingi huku wakiwa na hazina ya mila na tamaduni za kabila hilo ambalo pia ni kabila lake Waziri Mkuu Pinda. 
“Hili ni kabila dogo lisilofahamika na wengi, nimekuwa nikitafuta taarifa na machapisho (literature) mbalimbali kuhusu kabila hili lakini sikuwahi kupata chochote… ndipo nikamshirikisha Mheshimiwa Waziri Mkuu juuya kufanya utafiti na kuandika historia yetu naye akalikubali wazo langu,” alisema Bw. Mgawe ambaye pia ni Mhadhiri wa Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama, Dar es Salaam.
Akizungumza na wakazi waliohudhuria uzinduzi huo, Waziri Mkuu alisema utafiti huo usiishie hapo tu, bali wafanye tafiti nyingine kuhusu mavazi, vyakula, ndege, wanyama waliokuwa wakipendelewa na mababu zao ili kuongeza hazina ya taarifa ya kabila hilo.
“Lengo la kitabu hiki lilikuwa ni kuhifadhi katika maandishi historia ambayo ilikuwa imefichika ndani ya vichwa vya wazee wetu kutoka vijiji mbalimbali vya Mpimbwe… nafurahi kwamba tunao wazee watatu waliokuwa katika warsha ya kwanza kabisa iliyofanyika mwaka 2008. Leo hii wako hapa na wanashuhudia matunda ya kazi yao,” alisema Waziri Mkuu.
Wazee hao ni Mzee Simba Pangani Kalulu (76) kutoka kijiji cha Mamba, Mzee Valeri Kipande (76)  kutoka kijiji cha Lyangalile na Mzee Moses Kasalani (67) kutoka kijiji cha Mirumba. Vijiji vyote hivyo viko wilaya ya Mlele, mkoani Katavi.
Waziri Mkuu amerejea jijini Dar es Salaam leo mchana (Jumanne, Januari 9, 2013) akitokea kijijini kwake Kibaoni, wilayani Mlele, Katavi ambako alifanya ziara ya siku 10 kwenye jimbo lake la Katavi na kisha kuwa na mapumziko ya Krismasi na mwisho wa mwaka.

No comments:

Post a Comment