TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, August 16, 2014

HOFU YA EBOLA DAR, MGENI KUTOKA BENIN ALAZWA TEMEKE

  Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu mchimati@gmail.com au  namba +255767869133.

Watu wakikatiza kwenye lango la kuingilia katika Hospital ya Temeke, sehemu ambayo anayedaiwa kuwa mgonjwa wa Ebola amelazwa  
 Hofu ya ugonjwa wa ebola imeingia jijini Dar es Salam baada ya msichana anayedhaniwa kuwa na ugonjwa huo kutua nchini akitokea Benin, Afrika Magharibi na kulazwa katika Hospitali ya Temeke.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Amani Malima alithibitisha kuwapo msichana huyo mwenye umri wa miaka 14 aliyeingia nchini jana kuonekana akiwa na dalili hizo.
“Huko alikotoka alihisiwa kuwa na dalili hizo, alipofika hapa madaktari walipomhoji alisema ana maumivu makali ya viungo, miguu na mikono,” alisema.
Dk Malima alisema baada ya kupata maelezo hayo, walichukua vipimo vyote vya damu na majibu yake yatatoka leo kujua kama ana ugonjwa huo au la.
“Tumegundua kwamba ana malaria lakini vipimo vya ebola majibu ni kesho (leo), hivyo tunaangalia namna ya kumtibu na kama atakuwa hana ugonjwa huo tutamruhusu,” alisema Dk Malima.
 Chanzo;Mwananchi

No comments:

Post a Comment