TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Monday, February 2, 2015
Bondia wa kulipwa Farncis Cheka atupwa jela miaka mitatu, familia yapanga kukata rufaa
Na Ripota wetu, Morogoro
Bondi wa kulipwa nchini, Francis Cheka ambaye
maarufu kwa jina la SMG, amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela na faini ya
Sh milionai moja kwa kosa la kumpiga meneja waje wa baa, Bahati Kibanda.
Cheka alitiwa hatiani Julai 2 mwaka jana
kwa kumpiga na kumsababishia maumivu makali Kibanda ambaye alikwenda hapo kudai
fedha zake katika baa aliyokuwa anaifanyia kazi
ijulikanayo kwa jina la Vijana Social Hall.
Hakimu Mwanamizi wa mahakama ya mkoa wa
Morogoro Said Msuya alikubaliana na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka
na kuthibitisha shitaka hilo.
Hakimu Msuya alisema kuwa adhabu hiyo ni
fundisho kwa mshitakiwa na watu wengine wanaotumia vibaya nguvu zao kwa watu
wengine na anatakiwa kumlipa mlalamikaji fidia ya Sh milioni moja.
Pamoja na Cheka kupewa nafasi ya
kujitetea, bondia huyo hakutoa maelezo yoyote na kuiachia mahakama hiyo kutoa
adhabu inayostahili kwa bondia huyo aliyejizolea sifa kemkem katika ngumi za
kulipwa nchini.
Hata hivyo, taarifa zilizotufikia wakati
tunakwenda mitamboni, familia ya Cheka inampango wa kukata rufaa kupinga hukumu
hiyo.
Vijana Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali wameishukuru Serikali kutoa elimu ya Ujasiriamali
Katibu
Tawala Mkoa wa Mbeya Bibi Mariam A. Mtunguja (katikati) akizungumza na maafisa
kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya
kutembelea vijana wa Mkoa wa Mbeya na kutoa elimu ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi
za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.
Mwezeshaji
kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa (kushoto)
akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali Bw. Gullamhussein S. Kifu (katikati)
wakati wa ziara ya kutoa mafunzo ya Ujasiriamali kwa vijana wa Wilaya hiyo.
Kulia ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na
anayefuata ni Kaimu Afisa Vijana Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali Bw. Athuman
Mustafa Kinza.
HOTUBA YA RAIS KIKWETE KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 38 YA KUZALIWA KWA CCM
HOTUBA YA MWENYEKITI WA CCM TAIFA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO
KIKWETE, KATIKA SHEREHE ZA KUTIMIZA MIAKA 38 YA CCM, KWENYE UWANJA WA MAJIMAJI,
SONGEA - RUVUMA,
TAREHE 01 FEBRUARI, 2015
Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete akihutubia umati wa wananachi
Ndugu
Philip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM;
Mheshimiwa
Mizengo Peter Pinda, Waziri Mkuu na mjumbe wa Kamati Kuu;
Mheshimiwa
Anne Makinda, Spika wa Bunge na Mjumbe wa Kamati Kuu;
Ndugu
Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa CCM;
Ndugu
Mike Mukula, Makamu Mwenyekiti wa NRM ya Uganda na ujumbe wake;
Waheshimiwa
Wajumbe wa Kamati Kuu;
Mheshimiwa Oddo
Mwisho, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Ruvuma;
Waheshimiwa Wajumbe
wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa;
Wajumbe
wa Sekretarieti ya CCM;
Ndugu Verena
Shumbusho, Katibu wa CCM Mkoa wa Ruvuma;
Wenyeviti
wa Jumuiya za CCM;
Viongozi,
wananchama na wapenzi wa CCM;
CCM
Oyee!
Benki ya CRDB na kampuni ya Bima ya Heritage zanyakua tuzo za BBLA 2014

Naibu Waziri wa Nishati
na Madini, Mhe. Charles Kitwanga, (Kushoto) akimkabidhi tuzo mshindi wa Tuzo za
Bodi yenye Uongozi Bora za 2014 (BBLA) katika sekta ya kibenki, Mwenyekiti wa
Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya CRDB Bw. Martin Mmari (kulia). Benki ya CRDB
iliibuka mshindi katika sekta ya kibenki wakati kampuni ya Heritage Insurance
iliibuka kinara katika sekta ya bima katika tuzo hizo zilizofanyika katika
Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
Naibu Waziri wa Nishati
na Madini, Mhe. Charles Kitwanga, (Kushoto) akimkabidhi tuzo mshindi wa Tuzo za
Bodi yenye Uongozi Bora za 2014 (BBLA) katika sekta ya bima, Mwenyekiti wa Bodi
ya Wakurugenzi ya kampuni ya Heritage Insurance, Bw. Yogesh Manek (kulia).
Heritage Insurance iliibuka mshindi katika sekta ya bima wakati Benki ya CRDB
iliibuka kinara katika sekta ya kibenki katika tuzo hizo zilizofanyika katika
Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.
RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA PILI, ALI HASSAN MWINYI AZINDUA MAADHIMISHO YA WIKI YA SHERIA NCHINI
-Rais Mstaafu wa
awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi (wa pili kushoto) akiongozana na jaji mkuu wa
Tanzania, Mohamed Othaman Chande (watatu kushoto) pamoja na Mkuu wa Mkoa
wa Dar es Salaam, Said
Meck Sadiki (wa kwanza kushoto), Jaji Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu,
na Jaji
Kiongozi wa
Mahakama Kuu, Shabani Ally LILA wakiwa katika matembezi ya
kuadhimisha wiki ya sheria nchini matembezi hayo yalianzia katika Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu na kuishia katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es
salaam February 1, 2015.
Bendi ya polisi ikiongoza
matembezi ya wiki ya sheria nchini.
SIKU YA WAPENDANAO KIGAMBONI ITAKAVYOSHEREHESHWA NA WADADAZZZZZ
Watu mbali mbali mnakaribishwa kufika siku ya wapendanao huko kigamboni ambako kutakuwa na Mashindano ya kumpata mrembo wa siku hiyo kwa wale watakaoingia ukumbini na kisha kuchaguliwa kama Mrembo aliyevalia na kuweza kutokelezea zaidi ya wenzake(Miss Valentine Day) ambaye pamoja na ushindi wake atajipatia Donge Nono la Fedha Taslim kutoka kwa Waandaaji.
Wateja wa Airtel kushinda gari Moja Kila Siku Kupitia huduma ya Airtel Yatosha
Airtel
Tanzania leo imezindua promosheni kabambe ijulikanayo kama Airtel
Yatosha Zaidi kwa wateja wanaotumia vifurushi vya Airtel Yatosha kuweza
kujishindia gari
Aina ya Toyota IST kila siku
Mkurugenzi
wa Mawasiliano wa Kampuni ya Airtel Tanzania, Beatrice Singano, (kulia)
akifafanua jambo wakati wa Uzinduzi huo, kushoto ni Mkuu wa Masoko,Levi
Nyakundi,
Hii ni promosheni ya aina yake ambapo
wateja wetu wanazawadiwa kutokana na matumizi yao ya kawaida ya
vifurushi vya Yatosha. tunatoa wito kwa wale ambao hawajajiunga na
vifurushi vya Airtel yatosha kufanya hivi na kupata nafasi
ya kushinda gari moja kila siku”aliongeza Mallya
FEDHA ZACHANGWA KWA AJILI YA FRANK KIBIKI ANAYETAKIWA KUCHUKUA FPOMI YA UBUNGE JIMBO LA IRINGA
Kibiki mwnye koti,akibadilishana mawazo na mmoja wa wanachama wa tujiwezeshe cha kituo kikuu cha mabasi mjini Iringa
Katibu wa kikundi cha tujiwezeshe chenye wanachama zaidi ya 560, wa
kituo kikuu cha mabasi mjini Iringa Manet Charles akizungumza baada ya kumkabidhi sh 110,000 mwanachama mwenzao Frank Kibiki, ambaye ni
mwanahabari baada ya kutangaza nia wa kuomba kuwania ubunge wa jimbo la Iringa mjini kupitia CCM.
kituo kikuu cha mabasi mjini Iringa Manet Charles akizungumza baada ya kumkabidhi sh 110,000 mwanachama mwenzao Frank Kibiki, ambaye ni
mwanahabari baada ya kutangaza nia wa kuomba kuwania ubunge wa jimbo la Iringa mjini kupitia CCM.
Temeke mabingwa Wa Proin Women Taifa Cup mara baada ya kuifunga Pwani katika fainali
Waziri
wa Habari,Vijana Utamaduni na Michezo, Mh Dkt Femella Mukangara (wa
pili kushoto) akiwasili katika uwanja wa Azam Complex Chamanzi wakati wa
fainali ya Mashindano ya Proin Women Taifa Cup yaliyofikia Tamati leo
kwa kuzikutanisha Timu za Temeke na Pwani.
Waziri
wa habari utamaduni na Michezo, Mh Dkt Fenella Mukangara akimkabidhi
kombe nahodha wa timu ya Temeke mara baada ya kuibuka washindi wa
Mashindano ya Proin Women Taifa Cup ambayo yalichezwa katika Dimba la
Azam huku Proin Promotions na Azam wakidhamini mashindano hayo.
VIJANA WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KYELA WASHAURIWA KUTUMIA UJUZI KUJIAJIRI WENYEWE
Mwezeshaji kutoka Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa wa pili kulia
akizungumza na Kaimu Mkurugenzi wa Wilaya ya Kyela Dr. Festo Dugange
Januari 30,2015 wakati wa ziara ya kuhamasisha vijana wa Kyela. Wa
kwanza kulia ni Afisa Maendeleo ya Vijana Bi. Amina Sanga, wa kwanza
kushoto ni Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele na
wa pili kushoto ni Afisa Vijana Mkoa wa Mbeya Bw. George Mbijima.
Afisa Vijana kutoka Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akiwaelimisha
vijana wa Wilaya ya Kyela kuhusu mwongozo unaosimamia Mfuko wa Maendeleo
ya Vijana wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na
Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyofanyika katika Wilaya ya Kyela Mkoa wa
Mbeya
Sunday, February 1, 2015
KAIMU KATIBU TAWALA MKOA WA MTWARA AFUNGA KIKAO KAZI CHA MAAFISA MA WASILIANO
Wawasilishaji kutokakampuniya PUSH
OBSERVE Wakiwaelezea maafisa mawasiliano huduma wanazotoa ikiwa
ufuatiliaji wa taarifa mbalimbali kwenye vyombo vya habari na mitandao
yakijamii pia utoaji wa taarifa wajumbe kupitia mitandao ya simu (Bulk
messages)
MAMA NA MTOTO MPANGO WA SERIKALI KUPUNGUZA VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI
Serikali imeandaa mikakati mbalimbali ya kuboresha afya ya wanawake wajawazito ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.
Akijibu swali kwa Niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi, katika
kipindi cha maswali na majibu Bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa
Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Dkt. Pindi Chana amesema moja ya
mikakati hiyo ni mpango mkakati ulioboreshwa wa kuendeleza kasi ya
kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi uliozinduliwa na Rais wa Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete mwaka 2014.
Alisema kuwa mpango huo unawashirikisha wadau mbalimbali ambao
ni World Lung Foundation, Plan International, Care International,
Jhpiego, UNFPA na GIZ wanaochangia katika kupanua vituo vya afya
,kujenga vyumba vya upasuaji na ununuzi wa vifaa na tiba.
“Mkakati huu ni jitihada za serikali katika kuhakikisha afya ya
mama na mtoto inaboreshwa kwa kukomesha vifo vitokanavyo na uzazi na
watoto walio chini ya umri wa miaka mitano” alisema Dkt. Chana.
Alifafanua kuwa Rais Dkt Kikwete ameagiza wakuu wa mikoa
kusimamia masuala ya afya kwa ngazi zote zinahusu afya ya mama na mtoto
na kuhakikisha wanawasilisha taarifa za maendeleo ya utekelezaji kila
baada ya miezi mitatu(3).
Mpango mkakati huo umeanzishwa kutokana na bajeti finyu ya afya
ya mama na mtoto ambayo imekuwa ikipungua kila mwaka wa fedha , hivyo
serikali ikaona umuhimu wa kuangalia njia mbadala ya kuweze kupata fedha
ili kuongeza bajeti.
BUNGE LAENDELEA NA VIKAO VYAKE MJINI DODOMA
Naibu Waziri wa Nishati na Madini,
Charles Mwijage akijibu moja ya maswali yaliyoelekezwa kwenye wizara
yake katika kipindi cha maswali na majibu Januari 30,2015 Bungeni mjini
Dodoma.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Janet Mbene akijibu swali Bungeni mjini Dodoma.
MAGARI MAKUBWA YASOTA BARABARA KWENDA OLOLOSOKWAN .
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali (kushoto) akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues aliyemtembelea ofisini kwake wakati wa ziara ya kikazi ya siku nne kwenye kijiji cha Ololosokwani na halmashauri ya Ngorongoro kwa ajili ya maandalizi ya mradi wa kijiji cha digitali unaoendeshwa na Unesco kwa kushirikiana na Ki-elektronic ya Samsung unaotarajiwa kuwasili kijijini hapo mwezi februari ukitokea jijini Dar.
Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro, Elias Wawa Lali (katikati) akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues (kulia) aliyeambatana na wataalamu wa elimu, afya na mawasiliano pamoja na Mratibu wa Taifa wa tiba asilia na mbadala katika Idara ya Tiba Wizara ya Afya na ustawi wa jamii. Dkt Liggy Vumilia (hayupo pichani) . Kutoka kushoto wa kwanza ni Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias, Afisa mipango ya Elimu wa Shirika la UNESCO, Bi. Jennifer Kotta pamoja na Afisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) Bw. Al Amin Yusuph.
RAIS KIKWETE ALIPOTEMBELEA RAIS WA MALAWI ADDIS ABABA
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,
Rais wa Malawi Profesa Peter Mutharika (kulia) wakikutana na marais
wastaafu, Thabo Mbeki wa Afrika ya Kusini(Kushoto) na Joachim Chissano
wa Msumbiji(wapili kushoto) wakati wa mkutano wa 24 wa kawaida wa wakuu
wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika unaofanyika Addis Ababa Ethiopia
leo
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akiwa na Rais wa Malawi Professa Peter Mutharika jijini Addis Ababa
Ethiopia leo.Viongozi hao wanahudhuria mkutano wa wakuu wa nchi
wanachama wa Umoja wa Afrika.
SIKU YA SHERIA NCHINI ILIVYOSHIRIKISHA MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA NHIF
Emmanuel Sarakyika wa Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya akimpima shinikizo la damu mmoja wa watumishi wa
Mahakama alipotembelea kupata huduma hiyo katika banda la NHIF kwenye
maadhimisho ya Wiki ya Sheria yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi
mmoja Dar es salaam ambapo Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajiwa kuwa
mgeni rasmi katika sherehe za kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria
nchini zitakazo fabika februari 04 2015 katika viwanja vya mnazi mmoja
jijini Dar es Saalam.
Afisa Masoko na Elimu kwa Umma wa
NHIF Bi Hawa Duguza akimpima urefu Bw. Ben Kigongola wa Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu katika banda la NHIF kwenye maadhimisho ya Wiki ya
Sheria yanayofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja Dar es salaam.
Subscribe to:
Posts (Atom)






