Naibu
katibu mkuu wa wizara ya uhusiano wa Afrika mashariki. Bwana Uledi
Mussa akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Ripoti
kuhusu hali ya kijiogrofia katika nchi za jumuiya ya Afrika mashaki
iliyoandaliwa na Benki ya dunia uzinduzi huo ulifanyika katika Hotel ya
Hyatt Regency jijini Dar es salaam leo.
TAN
Bayport
Kikoa
Myway entertainment
FORE PLAN CLINIC
MPINGA CUP 2016
Mashujaa Fm 89.3, Lindi
Wednesday, February 8, 2012
KATIBU MKUU WIZARA YA AFRIKA MASHARIKI AZINDUA RIPOTI YA KIJIOGRAFIA
Naibu
katibu mkuu wa wizara ya uhusiano wa Afrika mashariki. Bwana Uledi
Mussa akiongea na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa Ripoti
kuhusu hali ya kijiogrofia katika nchi za jumuiya ya Afrika mashaki
iliyoandaliwa na Benki ya dunia uzinduzi huo ulifanyika katika Hotel ya
Hyatt Regency jijini Dar es salaam leo.
MIUNDOMBINU YA MIFUGO SOKO LA NYAMATALA MISUNGWI HAIJAKAMILIKA KUWA SOKO LA KIMATAIFA
Mwenyekiti wa wafanyabishara wa mifugo Nyaga wa Nyaga akitoa
mapendekezo ya wafanyabiashara kupinga kuhamia katika soko hilo
kutokana na kutokamikilia kwa miundombinu huku Dkt Mugarula na Dkt
Qwali wakitupia kisogo kamera wakiwa wameweka mikono nyuma kuashiria
kushindwa kwa hoja zao.
Wafanya biashara hao wamesema kama
Wizara ya Mifugo na Uvuvi haitarekebisha kasoro ambazo ziko katika soko
la Nyamatala, hawako tayari kuhama katika soko la Igoma ambako
wanafanyia biashara yao kwa sasa, na kama watalazimishwa kuhama
watasitisha kutoa huduma ya kuuza na kuchinja mifugo ili kuipa serikali
ujumbe kuhusu kutatua tatizo hilo.
Choo kinachotarajiwa kutumiwa na wafanyabiashara wa mifugo pamoja na
wateja mbalimbali watakaofika katika soko la Kimataifa la mnada wa
Nyamatala, Misungwi Mwanza.Choo hicho kina matundu manne mawili kwa
ajili ya wanawake na mengine kwa matumizi ya wanaume.
Trekta
na bolzer la maji likiwa limeegeshwa katika soko la Kimataifa
Nyamatala, Misungwi bolzer hilo linauwezo wa kubeba maji lita 4000,
maji ambayo yatatumika kwa ajili ya kunywesha mifugo pamoja na matumizi
ya choo
Sehemu ya kunyweshea mifugo maji katika soko la mnada wa Kimataifa, Nyamatala wilayani Misungwi kama linavyoonekana.
Dkt Mugarula wa kwanza kushoto akisikiliza maswali kutoka kwa Joseph Sikila, Makamu Mwenyekiti wa MWASIBA aliysimama kulia.
WAZIRI MKUU PINDA KUKUTANA NA MADKTARI UKUMBI WA CPL HOSPITALI YA MUHIMBILI KESHO SAA 3 ASUBUHI
WAZIRI
MKUU MIZENGO PINDA YUPO DAR ES SALAAM KUTOKA DODOMA KUSHUGHULIKIA
MGOMO WA MADAKTARI AMBAO UMEKUWA UKIENDELEA KWA LENGO LA KUUPATIA
UFUMBUZI.
LEO AMEKUTANA NA
UONGOZI WA HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI PAMOJA NA MADAKTARI BINGWA
KUTOKA SEKTA YA UMMA NA BINAFSI NA WASTAAFU.
KESHO SAA 3 ASUBUHI
ATAKUTANA NA MADAKTARI BINGWA, MADAKTARI WALIOSAJILIWA (REGISTRALS) NA
MADAKTARI WALIOKO KWENYE MAFUNZO KWA VITENDO (INTERNS) NA BAADA YA HAPO
SAA 4 ATAKUTANA NA WAFANYAKAZI WA HOSPITALI YA MUHIMBILI, MOI, OCEAN
ROAD NA WAWAKILISHI KUTOKA HOSPITALI ZA MKOA WA DAR ES SALAAM, KWENYE
UKUMBI WA CPL, MUHIMBILI.
MATARAJIO YA SERIKALI NI KWAMBA MAZUNGUMZO HAYO YATAWEZA KUMALIZA
MGOGORO HUU NA
MADAKTARI WOTE KUREJEA KAZINI NA HIVYO KUREJESHA HUDUMA ZA MATIBABU
KATIKA HALI YA KAWAIDA KWA WANANCHI WA TANZANIA.
HIVYO SERIKALI INAWAOMBA WOTE WANAOHUSIKA WAFIKE KATIKA MIKUTANO HIYO BILA YA KUKOSA.
(IMETOLEWA NA OFISI YA WAZIRI MKUU)
WANANCHI ARUSHA WALALAMIKA KUPORWA ARDHI
NA GLADNESS MUSHI - ARUSHA
WANANCHI wa
kjiji cha Olkunjwado kilichopo kata ya Ngarenanyuki wilayani Arumeru wamemlalamikia mwenyekiti wa kijiji
hicho Bw Joseph Loibai kwa kosa la kuuza
ardhi kinyume cha sheria sambamba na kutowasomea mapato na matumizi wananchi hao.
Wakiongea na WAANDISHI WA HABARI baadhi ya
wananchi ambao hawakupenda kutajwa majina yao walisema kuwa mwenyekiti huyo amakuwa na
tabia ya kuuza maeneo ya watu wasiokuwa
na uwezo kwa mzungu anaeishi katika kijiji hicho kwa manufaa yake binafsi Aidha walisema kuwa sheria ya ardhi inasema ardhi
haiuzwi kiholela na hata kama basi
itauzwa kuna asilimia ambayo itaenda serikalini lakini kwa mwenyekiti huyo ni tofauti na sheria hiyo.
Mbali na hilo waliongeza kuwa kwa kipindi cha
mwaka jana walimtaka mwenyekiti huyo
kuwasomea wananchi hao mapato na matumizi kwa ajili ya michango mbali mbali wanaochanga kijijini hapo lakini
hakufanya kama walivyokuwa wanataka
wao. Waliongeza kuwa mapato hayo na
matumizi waliyoomba kusomewa yanatokana na michango waliyochanga kwa ajili ya shule ya kutwa
ya sekondari ya Momela na hadi sasa
fedha hizo hazijulikani zilipo hali ambayo inawatia mashakani na mwenyekiti huyo ambapo hadi
sasa wamekataa kuchanga michango mingine
hadi wasomewe mapato hayo Hata hivyo
walimtaka diwani wa kata hiyo kuitisha mkutano ili waweze kutoa kero zao kwa kuwa mwenyekiti huyo amekataa
kusikiliza kero zao Aidha gazeti hili
liliweza kuongea na mwenyekiti huyo kwa njia ya simu na kueleza kuwa hajauza ardhi kinyume cha sheria
bali ni makubaliano yao wote
waliopitisha kumpatia mzungu huyo eneo. Kwa upande wa kuwasomea mapato na matumizi alisema
kuwa alishawaomea mapato na matumizi kwa
kipindi cha nyuma ila mara ya mwisho koramu haikutimia hivyo kushindikana kusomewa kwa mapato
hayo... .
UCHAGUZI
MDOGO JIMBO LA ARUMERU MASHARIKI KUFANYIKA APRIL MOSI
Na Lydia Churi, MAELEZO
Uchaguzi mdogo
wa ubunge katika jimbo la Arumeru Mashariki unatarajiwa kufanyika April Mosi
mwaka huu.
Uchaguzi huo
utafanyika baada ya jimbo hilo kuwa wazi kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge
wake Marehemu Jeremia Solomon Sumari aliyefariki dunia Januari 19 mwaka
huu.
Taarifa
iliyotolewa na Tume ya Taifa ya uchaguzi leo jijini Dar es salaam imesema pamoja
na uchaguzi huo mdogo pia kutakuwepo na chaguzi ndogo za madiwani katika kata za
Halmashauri mbalimbali nchini.
Taarifa hiyo ya
Tume ya Taifa ya uchaguzi inaonesha kuwa katika uchaguzi mdogo wa ubunge kwenye
jimbo la Arumeru Mashariki uteuzi wa wagombea utafanyika Machi 8, na kampeni
zitaanza Machi 9 hadi 31 mwaka huu.
Aidha, Tume
hiyo pia itafanya chaguzi ndogo za madiwani katika kata nane zilizoko katika
halmashauri mbalimbali nchini kufuatia kuwepo wazi kwa nafasi za viti vya
madiwani ambazo zimetokana na vifo vya madiwani husika.
Katika chaguzi
ndogo za madiwani uteuzi wa wagombea utafanyika Machi 5 na kampeni
zitaanza Machi 6 hadi 31 mwaka huu. Kata zitakazohusika kwenye uchaguzi huo ni
zile vijibweni-Temeke, Kiwanga-bagamoyo, Kirumba-Mwanza, Logangabilili-Bariadi,
Chan’gombe-Dodoma, Kiwira-Rungwe, Lizaboni-Songea na Msambweni-Tanga.
Taarifa hiyo
iliyosainiwa na Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Damian Lubuva imesema kuwa
hakutakuwa na kuandikisha wapiga kura kwa ajili ya chaguzi hizo ila daftari la
kudumu la wapiga kura lililotumika wakati wa uchaguzi mkuu uliopita litatumika.
Tume inawasisitiza wananchi na vyama
vyote vya siasa kuzingatia na kufuata ratiba ya uchaguzi na kujitokeza kwa wingi
kushiriki katika mchakato wa uchaguzi kuanzia siku ya uteuzi wa wagombea,
kampeni za uchaguzi na siku ya kupiga kura. Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa
saa 1.00 asubuhi na kufungwa saa 10.00 alasiri
BUNGE LAAHIRISHWA LEO HUKU HOJA YA MGOMO WA MADAKTARI IKIIBUKA KWA MARA YA SITA BUNGENI,SPIKA KUTOA UFAFANUZI KESHO.
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania wakiwa wamesimama mara baada ya Naibu Spika wa
Bunge Job Ndugay Kuahirisha kikao cha Bunge leo mjini Dodoma.Pamoja na mambo
mengine yaliyojitokeza wakati wa kuahirisha kikao hicho ni hoja ya Mgomo wa
madaktari ambayo iliibuliwa na mbunge wa Kigoma mjini Peter Selukamba ambaye
aliitaka serikali kutoa tamko la hatma ya mgomo huo ambapo Naibu spika Job
Ndugay aliwataka wabunge kuwa na subira ili Ofisi ya spika ikutane na kamati ya
uongozi ya bunge ili kutoa maamuzi hapo kesho kabla ya kuahirisha
mkutano huo wa sita.
Aliyekuwa waziri mkuu na mbunge wa
Monduli Edward Lowasa (kushoto) akijadili jambo na Waziri wa nchi Ofisi ya Rais
Mahusiano na Uratibu Stephen Wasira (katikati) na mbunge wa viti maalum
CHADEMA Leticia Nyerere leo mjini Dodoma.
Picha na Aron
Msigwa – MAELEZO.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira
Dkt. Terezya Huvisa (Kulia) akizungumza na Zainabu Kawawa mbunge wa viti maalum
CCM mara baada ya kumalizika kwa kikao cha saba cha bunge leo mjini
Dodoma. MAANDAMANO YA WANAHARAKATI KUSHINIKIZA SERIKALI KUCHUKUA HATUA JUU YA MGOMO WA MADAKTARI WA MUHIMBILI
Mkurugenzi wa TAMWA, Analilea
Nkya akiwa ameshikilia bango lake wakati wa maandamano hayo jijini Dar es salaam
leo.
Polisi wakiwaamuru waandamanaji watawanyike mara
baada ya kufika katika eneo la Salender Brige jijini Dar es salaam leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Msaada wa Sheria na Haki za Binadamu (YANGA YAIGALAGAZA MTIBWA SUKARI 3 -1 UWANJA WA TAIFA LEO
Refarii wa mchezo huo akinyoosha mkono wake juu
kuashiria timu ya Yanga ipige mpira wa adhabu kuelekea lango la timu ya Mtibwa
Sugar.
Mmoja wa Mashabiki
wa timu ya Yanga akiwa amejipaka masizi usoni mwake ikiwa ni moja ya staili ya
ushangiliaji kwa timu yake.
Mchezaji wa timu ya Yanga Haruna Niyonzima akichuana na beki wa timu ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi kuu ya Vodacom uliofanyika kwenye uwanja wa Taifa jioni hii jijini Dar es salaam, Mpira umekwisha na Yanga imefanikiwa kuitandika Mtibwa Sugar Magoli 3-0 bila huruma katika kipindi cha pili cha mchezo huo. Tuesday, February 7, 2012
YANGA , MTIBWA KESHO NDO KESHO LIGI KUU VODACOM TANZANIA
Ligi
Kuu ya Vodacom ambayo iko katika raundi ya 16 inaendelea kesho kwa
mechi moja kati ya Yanga na Mtibwa Sugar. Mechi hiyo namba 112 itachezwa
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.
Mechi
hiyo itachezeshwa na mwamuzi Ibrahim Kidiwa kutoka Tanga wakati
wasaidizi wake ni Michael Mkongwa kutoka Iringa na Kudura Omary wa
Tanga. Kamishna wa mechi hiyo ni Mohamed Nyange kutoka Dodoma.
Viingilio
katika mechi hiyo vitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya bluu na kijani, sh.
5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 10,000 kwa VIP B na C, na sh.
15,000 kwa VIP A.
Timu
14 za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zitakuwa kwenye viwanja saba tofauti
kesho (Februari 8 mwaka huu) katika mfululizo wa ligi hiyo ambayo iko
katika hatua ya makundi.
Transit
Camp na Mgambo Shooting zitachuana kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini
Tanga katika mechi pekee ya kundi A itakayochezeshwa na mwamuzi Said
Ndege wa Dar es Salaam.
Kundi
B litashuhudia mechi tatu. Tanzania Prisons itakuwa mwenyeji wa Small
Kids kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya, JKT Mlale
itaoneshana kazi na Mbeya City kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea na
Polisi Iringa itacheza na Majimaji kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
Samora mjini Iringa.
Mechi
za kundi C zitakuwa kati ya Polisi Morogoro na Morani FC itakayochezwa
Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro, AFC na Rhino zitacheza kwenye Uwanja
wa Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha na Polisi Tabora itakuwa
mwenyeji wa 94 KJ kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Kiongozi wa Olimpiki London 2012 Bw. Lord Sebastian Ceo atembelea shule ya sekondari kibasila
Kiongozi
wa Olimpiki London 2012 Bw. Lord Sebastian Ceo akiwa katika picha ya
pamoja na watoto baada ya kuwakabidhi vyeti katika ziara maalum
aliyoifanya nchini Tanzania na kutembelea shule ya Sekondari ya
Kibasila, ambako kuliandaliwa kliniki ya watoto kwa kuvumbua vipaji na
kuwaandaa kwa ajili ya michezo ya Olimpiki katika siku za usoni,
iliyojulikana kama Interanational Inspiration Tanzania
na kushirikisha watoto kutoka shule mbalimbali jijini Dar es salaam,
hapa wakionyesha vyeti vyao mara baada ya kukabidhiwa vyeti vyao na
kiongozi huyo.
Kiongozi
wa Olimpiki London 2012 Bw. Lord Sebastian Ceo akiruka viunzi pamoja na
mtoto Aica Nicolaus wakati wa kiliniki hiyo kwenye viwanja vya shule ya
Sekondari ya Kibasila.
Wanafunzi
wa shule ya Sekondari ya Kibasila wakicheza ngoma kumkaribisha kiongozi
wa Olimpiki London 2012 Bw. Lord Sebastian Ceo.
Mmoja
wa watoto akirusha Tufe mbele ya Kiongozi wa Olimpiki London 2012 Bw.
Lord Sebastian Ceo wa tano kutoka kulia, hyuku viongozi wengine kutoka
kamati ya Olimpiki nchini na Baraza la Michezo na ubalozi wa Uingereza
nchini wakishuhudia tukio hilo.
Kiongozi wa Olimpiki London 2012 Bw. Lord Sebastian Ceo kulia
akiangalia watoto wakati walipokuwa wakifanya mazoezi ya kuruka viunzi
anayefuata katika picha ni Dk. Ndee na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Olimpiki Tanzania TOC, Filbert Bay.
WAZIRI MKUU NA MATUKIO YANAYOENDELEA BUNGENI
Rais Dk Shein,Mgeni Rasmi Siku ya Sheria Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,akitoa hutuba yake wakati wa sherehe za siku ya
Sheria,Zanzibar,(kulia) ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe.Omar Othman
Makungu,Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Abubakar Khamis,na Jaji
Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Fakih
Jundu,(kushoto) ambapo "kauli mbiu kuga vita Rushwa katika utowaji wa
haki" ,sherehe hizo zilifanyika katika viwanja vya Victoria Garden
Mjini Unguja leo.
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,(kulia) akifuatana na Jaji mkuu wa Zanzibar Mhe.Omar
Othman Makungu,(katikati) na Jaji Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya
Muungano Mhe.Fakih Jundu,alipowasili katika viwanja vya Victoria
Garden katika sherehe za siku ya Sheria,Zanzibar leo.
Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.
Ali Mohamed Shein,(wa tatu kulia) Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe.Omar
Othman Makungu,Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe,Ali Abdalla
Ali,(kulia) Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mhe. Abdalla Mwinyi
Khamis,(kushoto)Jaji Kiongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Fakih Jundu,na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Abubakar
Khamis, wakiwa wamesimama wimbo wa taifa ukipigwa na kikundi cha
polisi Brass Band katika sherehe za Siku ya Sheria
Zanzibar,zilizofanyika Victoria Gaden Mjini Unguja.
Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe.Omar Othman Makungu,akiongoza
maandamano ya majaji na wanasheria wa serikali na wakujitegemea
wakati wa Sherehe za Siku ya Sheria,ambapo kauli Mbiu ya mwaka huu
"Kupiga vita rushwa katika utowaji wa haki",sherehe hizo zilifanyika
katika viwanja vya Victoria Garden Mjini Unguja leo.
Rais Jakaya Kikwete ashuhudia uwekaji saini makubaliano ya ushirikiano kupambana na maharamia
Rais
Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali washuhudia
awaziri wa ulinzi wa Msumbiji Bw Filipe Jacinto Nyarusi (shoto)na wa
Tanzania Dr Hussein Mwinyi wakibadilishana nyaraka huku wa Afrika
Kusini DKT L.N. Sisulu akitazama baada ya mawaziri hao kutiliana saini
ya mkataba wa makubaliano (moU) katika mapambano dhidi ya maharamia
kati ya nchi zao.
(PICHA NA IKULU)
Rais
Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali
wakishuhudia Mawaziri wa ulinzi wa Msumbiji Bw Filipe Jacinto Nyarusi
(kushoto), wa Tanzania Dr Hussein Mwinyi (wa pili kushoto), na wa
Afrika Kusini DKT L.N. Sisulu wakitiliana saini ya mkataba wa
makubaliano (moU) katika mapambano dhidi ya maharamia kati ya nchi zao.
Rais
Jakaya Kikwete akiongea huku Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali
na Mawaziri wa ulinzi wa Msumbiji Bw Filipe Jacinto Nyarusi (shoto), wa
Tanzania Dr Hussein Mwinyi (wa pili kushoto), na wa Afrika Kusini
DKT L.N. Sisulu baada ya mawaziri hao kutiliana saini ya mkataba wa
makubaliano (moU) katika mapambano dhidi ya maharamia kati ya nchi zao.
Rais
Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali wakiwa
katika picha ya pamoja na na Mawaziri wa ulinzi wa Msumbiji Bw Filipe
Jacinto Nyarusi (shoto), wa Afrika Kusini DKT L.N. Sisulu na wa
Tanzania Dkt Hussein Mwinyi baada ya mawaziri hao kutiliana saini ya
mkataba wa makubaliano (moU) katika mapambano dhidi ya maharamia kati ya
nchi zao.
Rais
Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilali wakiongea
na Mawaziri wa ulinzi wa Msumbiji Bw Filipe Jacinto Nyarusi (shoto), wa
Tanzania Dr Hussein Mwinyi (wa pili kushoto), na wa Afrika Kusini
DKT L.N. Sisulu baada ya mawaziri hao kutiliana saini ya mkataba wa
makubaliano (moU) katika mapambano dhidi ya maharamia kati ya nchi zao.
Rais Jakaya Kikwete amuapisha Dr. James Msekela kuwa balozi Italy leo
Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi nyenzo za kazi Dkt James Msekela baada
ya kuapishwa leo kuwa balozi wa Tanzania Italy ikulu jijini Dar es
salaam .
(PICHA NA IKULU)
Rais Jakaya Kikwete akimuapisha Dkt James Msekela kuwa balozi wa Tanzania Italy leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais
Jakaya Kikwete na Makamu wa Rais Dkt Gharib Mohamed Bilal na Katibu
Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na ushirikiano wa Kimataifa Mh John Haule
(kulia) na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi Penaeli Lyimo (kushoto) na Dkt
James Msekela baada ya kuapishwa kuwa balozi wa Tanzania Italy leo
Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais
Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Dr James Msekela na
Familia yake baada ya kuapishwa kuwa balozi wa Tanzania Italy leo
Ikulu jijini Dar
Subscribe to:
Posts (Atom)












