TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, June 16, 2012

Bajeti 2012/13 kutabiri mengi *Wengi wahofia utekelezwaji wake *Lipumba alia na ugumu wa maisha

Posted: 14 Jun 2012 01:03 AM PDT
Na Godfrida Jola

WAKATI bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2012/13, ikitarajia kusomwa leo mjini Dodoma, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) Taifa, Profesa Ibrahim Lipumba, amesema bajeti ya mwaka 2011/2012 ambayo ilikuwa sh. trilioni 13.5, haijatekelezwa.
Alisema vipaumbele vya bajeti hiyo, vilikuwa na kasoro nyingi pamoja na wafadhili kutotoa fedha walizoahidi.
Prof. Lipumba aliyasema hayo Dar es Salaam jana alipozungumza na Majira kwa njia ya simu juu ya maoni yake kuhusu bajeti iliyopita na inayotajariwa kusomwa leo.
Alisema bajeti iliyopita imeongeza ukali wa maisha ya Watanzania mara mbili zaidi kutokana na ongezeko la matumizi ya ndani.
Aliongeza kuwa, asilimia 39 ya bajeti yote ilikuwa katika sekta ya maendeleo ambayo hadi kufikia Machi mwaka huu, asilimia 32 pekee ndiyo iliyotekelezwa.
“Bajeti ya kesho (leo), maendeleo yametengewa sh. trilioni 4 na bilioni 500 wakati mwaka 2011, ilikuwa trilioni 4 na bilioni 900 hivyo imepungua na haiwezi kufikia wanapotaka, hii inatokana na Serikali kunyimwa fedha na wafadhili,” alisema.
Alisema bajeti hiyo ilishindwa kumaliza tatizo la ajira kwa vijana kwa kutumia sekta binafsi, kufufua viwanda vilivyopo na kuboresha upatikanaji wa nishati ya umeme ili kuongeza uzalishaji viwandani na kuongeza ajira.
“Bajeti ilishindwa kufanikiwa kutokana na utegemezi wa fedha za wafadhili ambao waligoma kutoa fedha na kuipa Serikali wakati ugumu hivyo kuyumba katika matumizi yake.
“Tatizo la msingi Serikali kutokuwa na dira kwa sababu inafuata malengo ya milenia na utekelezaji wa Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA 2), ambavyo vyote vimepitwa na wakati, muhimu kubuni njia nyingine ili kupiga hatua ya maendeleo,” alisema Prof. Lipumba.
Alisema Waziri wa Fedha kwa sasa, Dkt. William Mgimwa hajapata muda wa kutosha kuipitia bajeti iliyopita na hana utaalamu kuhusu uongozi hivyo hawezi kubaini kasoro zilizopo.
“Dkt. Mgimwa hana utaalamu wa kutosha wa 'fiscal policy', ni mwezi mmoja tu, toka aingie katika Wizara hii, atawezaje kujua kinachoendelea,” alihoji.
Wakati huo huo, Watanzania wengi wamekuwa na shauku ya kutaka kujua vipaumbele vilivyotolewa katika bajeti iliyopita vimefanyiwa kazi kwa kiwango gani.
Bajeti iliyopita, ilitaja mambo manne ya msingi ili kupunguza makali ya maisha na kutenga asilimia 14 ya bajeti yote kwa ajili ya kulipa deni la Taifa.
Mambo hayo ni pamoja na maboresho ya sheria za kodi,  kuongeza nguvu za uwekezaji katika sekta ya umeme, kupunguza bei ya mafuta ya petroli, matumizi ikiwamo ukubwa wa misafara ya safari za viongozi na kuongeza fedha katika sekta tano.
Pia bajeti hiyo ilitoa vipaumbele katika sekta ya miundombinu ya barabara, reli, bandari na mkongo wa mawasiliano wa Taifa ambao ulitengewa sh. bilioni 2,781.4.
Katika mchanganuo huo, nishati na madini ilitengewa sh. bilioni 539.3 ambayo kwa kiasi kidogo imepunguza tatizo la mgawo wa umeme.
Maji ilitengewa sh. bilioni 621.6  bilioni ikilinganishwa na sh. bilioni 397.6 mwaka 2010/11, sawa na ongezeko la asilimia 56, kilimo na umwagiliaji sh. bilioni 926.2 ikilinganishwa na sh. bilioni  903.8 mwaka 2010/11, sawa na ongezeko la asilimia 2.5.
Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi walisema wanatarajia kupata unafuu wa ukali wa maisha kwa bajeti ya leo kutokana na hali iliyopo kuzididi kupoteza mwelekeo.
Walisema ni muhimu bajeti ya leo ikaweka vipaumbele ambavyo vitatekelezeka ila kuepuka lawama baada ya kuisha kwa mwaka wa fedha.
“Mwaka 2011 Serikali ilisema itasaidia kuweka mikakati ya kupunguza ukali wa maisha lakini imekuwa tofauti maana maisha yamepanda maradufu na kutuacha njia panda,” alisema Bi. Lenarda Christian, mkazi wa Dar es Salaam.
Alisema bajeti ya leo inatakiwa kuonesha namna ya utekelezaji wa malengo yaliyokusudiwa na pia iendane na mipango ya Serikali ya  ukusanyaji wa mapato na matumizi sahihi ya fedha.
Bw. George Martine, mkazi wa Magomeni alisema kutokana na bei ya mafuta na bidhaa kupanda mara kwa mara, imechangia kuongeza ukali wa maisha kwa wananchi.
Alisema Serikali inapaswa kuwaangalia wananchi wake hasa wa kawaida kwa kupunguza bei za nafaka ili kuwanusuru. “Hivi sasa vyakula vimepanda bei maradufu hivyo kusababisha maisha kuwa magumu,” alisema.
Bei za vyakula zilianza kupanda nchini mwishoni mwa 2011 ambavyo ndiyo hutumiwa na watu wengi ukiwemo mchele, maharage, sukari, unga na viungo vya mboga.
Mchele katika masoko ya Dar es Salaam umepanda na kufikia sh.2,300 hadi 2,500 kwa kilo moja, maharage sh. 2,300, 2,500 hadi 2,600 ambapo awali yalipatikana kwa sh.2,000 hadi Sh. 2,200 kwa kilo, unga umefikia sh. 1,000 hadi Sh.1,200 kwa kilo ambapo bei ya awali ilikuwa 800 hadi sh. 900 kwa kilo.
Posted: 14 Jun 2012 01:02 AM PDT 
 Na Peter Mwenda 

MBUNGE wa Mwibara, mkoani Mara, Bw. Kangi Lugola, amemtaka aliyekuwa Waziri wa Fedha, Bw. Mustapha Mkulo, alithibitishie Bunge juu tuhuma alizozielekeza kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), na kudai imehongwa na Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC).
Bw. Lugola aliyasema hayo Bungeni Mjini Dodoma jana baada ya kuomba mwongozo wa spika na kudai kuwa, katika kikao cha Bunge lililopita, alimtaka Bw. Mkulo athibitishe kauli aliyowahi kuitoa bungeni akidai kamati hiyo ilihongwa sh. milioni 60 na CHC ili kupindisha ukweli lakini hakuwepo bungeni.
Alisema katika tuhuma hizo, Bw. Mkulo alimtaja Mwenyekiti wa POAC, Bw. Zitto Kabwe kuwa ameweka rehani ubunge wake kwa ajili ya rushwa hivyo kuishuka hadhi kamati hiyo.
“Kwa vile Bw. Mkulo yupo hapa, naomba Naibu Spika atoe mwongozo ili afute kauli yake ili kuweka kumbukumbu sawa au alete ushahidi bungeni,” alisema.
Katika majibu yake, Naibu Spika Bw. Job Ndugai alisema amepokea jambo hilo na atalitolea mwongozo kwa wakati muafaka.
Posted: 14 Jun 2012 01:10 AM PDT

Naibu Kamishina wa Polisi (DCP), Issaya Mungulu, akiwaonesha waandishi wa habari, picha ya mtuhumiwa wa ugaidi, raia wa Ujerumani, Emrah Erdogan, au kwa jina lingine Abdulrahaman Othman (24), aliyekamatwa nchini akituhumiwa kuwa mpiganaji wa kundi la Al-Qaeda aliyehusika katika matukio mbalimbali ya ugaidi, Dar es Salaam jana. (Picha na Prona Mumwi)
Posted: 14 Jun 2012 12:46 AM PDT

Na Salim Nyomolelo

JESHI la Polisi nchini, linamshikiria raia wa Ujerumani aliyefahamika kwa jina la Bw. Emrah Erdogan, ambaye aliyekamatwa jijini Dar es Salaam, Juni 10 mwaka huu.
Bw. Erdogan ambaye kwa jina lingine anaitwa 'Abdulrahaman Othman', inadaiwa ni mfuasi wa kundi la kigaidi la Al-Qaeda.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Naibu Kamishna wa jeshi hilo, Bw. Isaya Mngulu, alisema kijana huyo ana umri wa miaka 24.
Alisema Bw. Erdogan anadaiwa kushiriki mapambano mbalimbali nchini Afghanistan na hivi karibuni alishirikiana na Kikundi cha Al-Shabab kufanya ugaidi
Aliongeza kuwa, vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kumuhoji wakishirikiana na mataifa mengine.
“Tunashirikiana na nchi za Uganda, Kenya na Ujerumani kumhoji ili kubaini taarida zake, baada ya hapo tutatoa taarifa kwa Watanzania,” alisema Bw. Mngulu.
Hata hivyo, Bw. Mngulu alisema jeshi hilo linatambua mchango wa wananchi ambao ndio uliosaidia kukamatwa kwa mtuhumiwa na kuongeza kuwa, hiyo ndio dhana halisi ya ulinzi shirikishi.
“Jeshi la Polisi linawahakikishia wananchi kuwa, vyombo vya ulinzi na usalama vipo imara kukabiliana na vitisho vyote vya uhalifu na ugaidi, natoa wito kwa wananchi waendelee kutupa ushirikiano katika vyombo vyetu ili kuimarisha amani na utulivu.
Posted: 14 Jun 2012 12:41 AM PDT

Na Mwandishi Wetu

MWENYEKITI wa Muungano wa Vyama vya Wazalishaji na Wachapishaji Maarifa (KOPITAN), Bw. Abdullah Saiwaad, amesema kanuni na muongozo wa tozo kwa kazi zinazorudiwa utasaidia kuliongozea Taifa mapato.
Bw. Saiwaad aliyasema hayo Dar es Salaam jana katika warsha ya siku moja kuhusu kanuni ya urudufishaji na hakimiliki na kusisitiza kuwa, kanuni hizo zitawasaidia waandishi na wachapishaji wa kazi za maandishi.
“Kanuni hizi zitasaidia ukusanyaji wa kodi kwa Taifa na wenye hakimiliki kunufaika kutokana na kazi zao ambazo muda mrefu zimekuwa zinarudufiwa kinyume na sheria,” alisema.
Katika warsha hiyo, njia mbalimbali za ukusanyaji mapato za kurudufu kazi zenye hakimiliki zilielezwa pamoja na namna ya kutekeleza mifumo hiyo.
Mifumo ya ukusanyaji mirabaha kwa kiasi kikubwa imeletwa ili  kulinda na kuzipa hadhi kazi za wazalishaji ambao ni waandishi na wachapaji mbalimbali.
Aliongeza kuwa, licha ya kuwepo kwa wimbi kubwa la kurudufu kazi za sanaa, Chama cha Hatimiliki nchini COSOTA kinashirikiana beka kwa bega na KOPITAN kuhakikisha mfumo na muongozo wa kanuni hizo ambazo Serikali inatarajia kuzitoa, utakuwa daraja bora la mafanikio ya kuhakikisha kazi za wasanii na waandishi zinalindwa ipasavyo.
“Tuna nia ya kuwa na mfumo bora ambao kila mtu atanufaika, kuja kwa mfumo huu ni mafanikio bora ambayo yatanufaisha watu wote,” alisema Ofisa Mtendaji wa COSOTA, Bw. Yustus Mkinga.
Kwa upande wake, Mwakilishi wa Afrika wa Shirikisho la Kimataifa la Haki za Urudufishaji (IFRRO), Bw. Greenfield Chilongo, aliwataka wamiliki wa haki za kazi mbalimbali za kimaandishi na sanaa nyinginezo, kusimamia haki za umiliki wa kazi zao ili kuzuia urudufishaji wa kazi hizo unaofanyika bila kufuata sheria na kanuni za hakimiliki.
Posted: 14 Jun 2012 01:10 AM PDT

Mbunge wa Tabora Mjini Bw. Aden Rage (kushoto) akimsikiliza Naibu Waziri wa Maji Dkt Binilith Mahenge mara baada ya kipindi cha maswali na majibu Bungeni Mjini Dodoma jana. (Picha na Vicent Tiganya-Maelezo)
Posted: 14 Jun 2012 12:22 AM PDT

Na Willbroad Mathias

TATIZO la ubovu wa miundombinu katika viwanja vya ndege na ukosefu wa mafunzo kwa marubani, linadaiwa kuwa chanzo kikuu cha ajali nyingi za ndege zinazotokea nchini.
Wadau wa sekta ya usafiri wa anga nchini, waliyasema hayo Dar es Salaam jana katika mkutano wao uliolenga kujadili na kutafuta njia mbadala ya kuimarisha usalama wa safari za ndege.
Wakichangia mada inayohusu changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo, wadau hao walisema ajali nyingi za ndege nchini, zinasababishwa na ufinyu wa miundombinu katika viwanja.
Walisema pamoja na kuboreshwa kwa njia za ndege zinazotumika  wakati wa kuruka au kutua, viwanja vingi nchini vimezungukwa na mazingira yasiyo salama.
Akiwasilisha mada katika mkutano huo, Mkaguzi Mkuu wa Ajali za Ndege nchini, kutoka Wizara ya Uchukuzi, Bw. John Nyamwihura, alisema ipo haja ya kuboreshwa miundombinu hiyo ili kuleta ufanisi.
Akizungumzia tatizo la uhaba wa mafunzo ya marumbani nchini Bw. Nyamwihura alisema sekta hiyo kwa sasa inakabiliwa na changamoto hizo baada ya Serikali kujitoa tofauti na ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Alisema awali Serikali ilikuwa ikibeba jukumu la kugharamia masomo ya marubani tofauti na sasa.
“Hali hii inachangia kuwa na marubani wengi vijana tena wa kigeni tofauti na Tanzania ambayo marubani wengi wazee, enzi ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere, tulikuwa na utaratibu wa kusomesha marubani katika nchi mbalimbali,” alisema Bw.  Nyamwihura.
Kwa upande wake, Mwakilishi kutoka Chama cha Wasafirishaji wa Anga (TAOA), Bw. Eva Jackson, alisema ipo haja ya kuwepo  uwazi katika kuchunguza vyanzo vya ajali za ndege nchini.
“Hivi sasa ukienda katika taarifa za Mamlaka ya Anga (TCAA),  hakuna taarifa za matukio ya ajali au ya usalama licha ya kuripotiwa zaidi ya mara 10,” alisema.
Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Bw. Fadhili Manongi, alisema ajali za ndege nchini zimepungua ukilinganisha na miaka ya nyuma.
Alisema mwaka huu kumetokea ajali moja tofauti na miaka iliyopita ambayo zilikuwa zikitokea mara kwa mara.
Posted: 14 Jun 2012 12:21 AM PDT

Na Anneth Kagenda

KAMANDA wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini,  Mohamed Mpinga, amekiri kuwepo vitendo vya uchakachuaji leseni ambavyo ni moja ya sababu inayochangia ongezeko la ajali nchini.
Akizungumza na Majira kwa njia ya simu Dar es Salaam jana, Kamanda Mpinga alisema kuwa madereva wengi wanadanganya kuwa wamesea udereva katika vyuo mbalimbali kikiwemo VETA.
“Kuna matukio ya kufoji vyeti ambayo yamekuwa yakijitokeza katika vyuo mbalimbali kikiwamo VETA, utakuta mtu anafanya udanganyifu na kudai amesema katika chuo hiki wakati katika orodha ya waliohitimu hayumo.
“Tumekuwa tukikemea vitendo hivi na kuvitaka vyuo husika kutuletea orodha ya waliomaliza vyuoni baada ya wanafunzi kumaliza masomo yao ila vitendo hivi vitakoma,” alisema.
Alisema wale wananaondelea na tabia hiyo wakikamatwa sheria itachukua mkondo wake ambapo baadhi ya watu waliozungumza na Majira wakiwamo wamiliki wa vyuo vya udereva, walidai vitendo hivyo bado vinaendelea kwa madereva wengi kupata vyeti bila kuvisomea vyuoni.
Posted: 14 Jun 2012 01:11 AM PDT
Baadhi ya wanahabari wa vyombo mbalimbali kutoka Mikoa ya Iringa,Mbeya na Dar es salaam ambao walishiriki katika utafiti na ukibua kero mbalimbali za wananchi wa kata ya Ijombe wakiwa pamojana Waraghbish wa Mtandao wa Jinsia TGNP hivi karibuni.
Posted: 14 Jun 2012 12:12 AM PDT

Na Kassian Nyandindi, Namtumbo

MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma, wametakiwa kuibua miradi ya kimaendeleo ambayo itakuwa na tija kwa wananchi.
Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Bw. Steven Nana, aliyasema hayo juzi mjini Namtumbo, mkoani hapa wakati akifafanua mambo mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri hiyo.
Alisema hivi sasa halmashauri hiyo inakabiliwa na changamoto nyingi hivyo ni vyema madiwani wawe na upeo mpana wa kutafuta njia mbadala za kuharakisha maendeleo ya wananchi.
Bw. Nana aliongeza kuwa, madiwani wana nafasi kubwa katika hilo kama watashirikiana na wananchi kwenye kata zao badala ya kufanya maamuzi mbalimbali bila kuwashirikisha Alisema halmashauri nyingi nchini zinashindwa kujiendesha kwa sababu ya malumbano yasiyo ya lazima miongoni mwao hasa kwa watendaji hivyo kukwamisha maendeleo.
Posted: 14 Jun 2012 01:11 AM PDT
Samaki waliovuliwa katika nyavu sizizoruhusiwa.Utungaji sheria ndogo za kudhibiti uvuvi haramu zitasaidia kustawisha uvuvi endelevu na wenye tija.(Picha na Mtandao wetu).
Posted: 14 Jun 2012 12:05 AM PDT

Na Heckton Chuwa, Same

BENKI ya Ushirika mkoani Kilimanjaro (KCBL), imeanzisha huduma ya akiba kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 18 ili waweze kupata uelewa wa huduma za kibenki.

Meneja Masoko wa benki hiyo Bw. Ahsanterabi Msigomba, aliyasema hayo hivi karibuni wakati akizungumza na viongozi mbalimbali wa Vyama vya Ushirika vya Msingi na wale wa Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya za Mwanga na Same (VUASU).
“Huduma hii inalenga kuwajengea watoto mazingira ya kuanza kuwa na uelewa wa kujiwekea akiba tangu utotoni,” alisema Bw. Msigomba na kuongeza kuwa, benki hiyo pia imeshirikiana na Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kwa kuanzisha huduma ya M-PESA na wao kuwa wakala wa huduma hiyo.
“Huduma hizi nyongeza ya huduma zingine tunazozitoa ambazo ni pamoja na zile za Western Money Union Transfer na stakabadhi ya mazao ghalani ambazo zimekuwa na mafaniko makubwa,” alisema.
Bw. Msigomba alisema mpango wa stakabadhi ya mazao ghalani umeendelea kuwa na mafanikio makubwa tangu uanzishwe kutokana na huduma wanazotoa kwa wakulima ambao hawana rasilimali zinazowapa uwezo wa kukopa fedha kwa ajili ya kilimo.
Kwa upande wake, Ofisa Masoko wa benki hiyo Bi. Regina Ndesanjo, alitoa wito kwa wanachama wa benki hiyo kukamilisha hisa zao ili zifikie kiwango cha milioni moja ambacho kimewekwa ili waweze kushiriki Mkutano Mkuu unaotarajiwa kufanyika baadae mwaka huu.

Posted: 14 Jun 2012 01:11 AM PDT
Posted: 13 Jun 2012 11:42 PM PDT


MIGOGORO ya ardhi imekithiri katika maeneo mbalimbali nchini, kusababisha umwagaji damu, kuhatarisha amani na utulivu tulionao kutokana na umuhimu wake.
Ni wazi kuwa migogoro hiyo imegawanyika katika makundi mawili, moja likihusisha wakulima na wafugaji, jingine linahusisha wananchi na wawekezaji.
Kimsingi migogoro inayohusisha wananchi na wawekezaji inachangia wananchi kuichukia Serikali yao na kuharibu mali.
Katika maeneo mengi yaliyohusishwa na migogoro ya ardhi, tayari kumetokea vurugu zilizosababisha uvunjifu wa amani na kusababisha vifo vinavyoweza kuzuilika.
Vurugu hizo pia zimetokea katika maeneo ambayo wananchi walioheshimiana muda mrefu, wameamua kuvunja udugu wao kwa sababu kasi ya Serikali kumaliza migogoro husika haiendani na tatizo lililopo.
Hatua zinazochukuliwa na Serikali ni zile za kujaribu kutuliza hasira za wahusika jambo linaloweza kutuletea maafa makubwa baadaye.
Sisi tunasema kuwa, migogoro mingi ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji inatokana na makundi hayo kutotengewa maeneo.
Mtu akipata eneo mahali popote anajenga, kulima au kufuga kwa sababu Serikali haijachukua hatua stahiki ya kutenga maeneo na matumizi yake.
Ili kuepuka mapigano ya mara kwa mara na kutunza mazingira, umefika wakati wa Serikali kutenga maeneo ya kilimo, ufugaji, makazi ya watu na yale ya wazi.
Maofisa ardhi ni miongoni mwa watu wanaochangia migogoro hiyo kwa kuuza maeneo zaidi ya mara moja hivyo kusababisha jamii kugombana hata kuchukiana.
Sababu kubwa inayochangia maofisa hao kusababisha migogoro hiyo ni tamaa ya fedha mbali ya kujua wazi kuwa wanachokifanya ni kinyume na maadili ya kazi zao.
Ardhi ni mali ya mwananchi na Serikali hivyo kila upande unapaswa kushirikishwa wakati wa kuuza au kumtafuta mwekezaji.
Umefika wakati wa maofisa hao kubadilika na kufanya kazi kwa mujibu wa sheria ili kupunguza migogoro hii ambayo inaweza kuharibu historia ya nchi yetu.
Posted: 14 Jun 2012 01:11 AM PDT

Mfanyabiashara wa kuku (jina halikufahamika) akiwalinda huku akisoma gazeti,kama alivyokutwa katika foleni ya kuingia ndani ya Soko la Kisutu Barabara ya Bibi Titi, Dar es Salaam jana. Kuongezeka kwa wafanyabiashara kwenye soko hilo kunasababisha msongamano. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 13 Jun 2012 11:28 PM PDT

Na Suleiman Abeid, Shinyanga

WAKULIMA wa zao la pamba mkoani Shinyanga, wametakiwa kuuza pamba yenye ubora na kushirikisha wadau ili kudhibiti uchafu wa zao hilo unaofanywa kwa makusudi na baadhi ya wakulima wanapokwenda kuiuza sokoni.
Wito huo umetolewa juzi na Meneja Uendeshaji wa Kiwanda cha Kuchambua na Kusindika zao hilo cha Afrisian Ltd, kilichopo mjini hapa, Bw. Hrishikesh Katre, katika hafla fupi ya kukabidhi zawadi kwa vituo vya ununuzi wa pamba vilivyofanya vizuri msimu uliopita.
Alisema kama wakulima na wadau wengine watadhibiti uchafu wa zao hilo unaofanywa kwa makusudi na baadhi ya wakulima ili kuongeza uzito wa pamba wanapokwenda kuiuza sokoni thamani yake katika soko la dunia itaongezeka.
Aliongeza kuwa, baadhi ya wakulima wamekuwa na tabia ya kuweka michanga, maji au magadi katika pamba kabla hawajaenda kuiuza sokoni kitu ambacho mbali ya kushusha ubora wake, pia husababisha hasara kwa kampuni zinazoinunua na serikalini.

“Suala la kurejesha ubora wa pamba yetu lipo mikononi mwetu sisi wenyewe wakulima na wadau wa zao hili, tukidhibiti uchafuzi huu pamba ambayo itanunuliwa itakuwa safi na ubora wake utakuwa mzuri hivyo bei katika soko itapanda na wakulima kufaidika,” alisema Bw. Katre.
Alisema kampuni hiyo imeanzisha utaratibu wa kuvizawadia vituo vyake vya ununuzi ambavyo hununua pamba safi isiyo na uchafu pamoja na kuwapa motisha watu wanaosimamia vituo hivyo kuhakikisha wananunua pamba safi.
Katika hafla iliyofanyika juzi kampuni hiyo ilitoa zawadi mbalimbali kwa wahasibu wa vituo hivyo ikiwemo pikipiki mbili aina ya Toyo, baiskeli mbili aina ya Phoenix, majembe manne ya kukokotwa na ng’ombe na simu tano za mkononi aina ya Nokia vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 4.8.
Bw. Katre alivitaja vigezo vinavyomfanya Mhasibu aweze kushinda na kupewa zawadi kuwa ni pamoja na kufikia lengo la makisio ya ununuzi wa pamba katika kituo chake.
Vigezo vingine ni uaminifu anapokabidhi pamba yake kiwandani na kuhakikisha hanunui pamba iliyochanganywa na mchanga, kokoto au kuwekwa maji ya magadi.
Aliongeza kuwa, kampuni hiyo inanunua pamba katika mikoa ya Tabora, Shinyanga, Simiyu, Mwanza na tayari imeingia mikataba na vikundi 256 vya wakulima ambavyo vitapatiwa pembejeo za kilimo  katika msimu wa mwaka 2012/2013.

No comments:

Post a Comment