TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, June 13, 2012

Watanzania washauriwa kutumia mkutano wa AfDB kujitangaza

Posted: 29 May 2012 12:06 AM PDT

Pamela Mollel na Jane Edward, Arusha

WATANZANIA wametakiwa kujitangaza kiuchumi kupitia mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ulioanza jijini Arusha ambao umewajumuisha marais sita wakiwemo magavana wa nchi mbalimbali za Afrika.

Hayo yalisemwa jana na Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo Kikuu cha Dodoma Bw. Juma Mwapachu mjini hapa ambapo alisema kuwa hiyo ni fursa ya pekee kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika mkutano huo.

Bw. Mwapachu alisema kuwa mkutano huo ni muhimu kwa nchi ya Tanzania na unawajumuisha watu mashuhuri na si vikao vya Magavana tu pia Umoja wa Mabenki ya Biashara ya Afrika pamoja na vyombo vya habari mashuhuri.

Aliongeza kuwa katika mkutano huo pia kuna vyombo vya kupima ubora wa uchumi wa nchi mbalimbali na mfano Tanzania uchumi wake umekuwa ukitolea mfano katika mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Alisema kuwa, kupitia Benki hiyo pia wameweza kufadhili ujenzi wa miundombinu ya Barabara ya Namanga hadi Arusha na bado wapo mbio kuhifadhili barabara ya Moshi hadi Holili.

“Kweli uchumi wetu unabadilika kiharaka sana na ukitazama mtikisiko wa kiuchumi 2008-009 ambao kweli kuna nchi ambazo zimetikiswa kiuchumi," alisema Bw.Mwapachu

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Madini Tanzania Bw.Richard Kasesera alisema kuwa ni fursa adhimu ya kukuza uchumi kwa Mkoa wa Arusha na kuvitaka vyombo vya habari kuwa chachu ya kutangaza uchumi wa Tanzania wakati huu mkutano unapoendelea.

Aliongeza kuwa ni jambo la muhimu kwa vyombo vya habari kuelezea matatizo ya kiuchumi na kuacha kuzipa kipaumbele habari za vurugu za Zanzibar za vikundi vichache kwckuwa kufanya hivyo ni kuwanyima Watanzania kupata taarifa sahihi na kuwatia hofu wahisani.

Mkutano huo wenye kauli mbiu 'Afrika katika Ulimwengu wa Utandawazi, Changamoto na Fursa' unafanyika kwa siku nne na kukusanya zaidi ya washiriki 2,000.
Posted: 29 May 2012 12:04 AM PDT

Posted: 29 May 2012 12:00 AM PDT
WALI ilikuwa ikifikirika kuwa kazi ya uuguzi ni wito, hivyo kila anayefanyakazi hiyo ana sifa ya kuwa na ukarimu, upendo, upole na sifa zingine.
Kadri siku, miezi hadi mwaka inavyokwenda ndivyo sifa hizo zinavyotoweka.
Kutokana na ukosefu wa ajira nchini vijana wamejiamulia kujiingiza katika fani mbalimbali licha ya kutokuwa na sifa zinazostahili kuingia kwenye fani husika.

Hali hiyo imekuwa ikiendelea na kusababisha ukiukwaji wa baadhi ya maadili mbalimbali na kusababisha wananchi kuangamia na wengine kupoteza maisha.
Mwishoni mwa wiki iliyopita mwanamke Bi. Rukia Vulai, mkazi wa Magereza Manispaa ya Mtwara alijikuta akijifungulia ndani ya pikipiki ya miguu mitatu maarufu kama bajaji baada ya wauguzi waliokuwa zamu kumtolea lugha chafu.
Mwanamke huyo alifika kituoni hapo akiwa na uchungu mkali na kumuomba muuguzi mmoja amsaidie kwa kumkimbiza wodini kwa kuwa tayari dalili za kujifungua zilianza kuonekana baada ya chupa kuvunjika.
Badala ya muuguzi huyo kutakiwa kutoa huduma ya kwanza ili kuokoa maisha ya mama huyo anadaiwa kuanza kumtolea lugha chafu mwanamke huyo na kudai kuwa yeye hahusiki na kuwasaidia akina mama wajawazito.
Imedaiwa kuwa licha ya wagonjwa wengine waliokuwa pembeni kumbembeleza muuguzi huyo kumsaidia mama huyo hakuweza kufanya hivyo na badala yake aliendelea kumtolea lugha ya matusi mama huyo.
Kutokana na mabishano hayo kuendelea mgonjwa huyo aliweza kujifungua ambapo alisaidiwa na wanawake wengine ambao walifika hospitalini hapo kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali na kujifungua ndani ya bajaji.
Kwa kweli suala hili limenisikitisha sana hata kama huyo muuguzi mama mjamzito alikuwa ni adui yake kwanza alitakiwa kumpa huduma kisha uadui wake auendeleze.
Wauguzi kama hawa wamekuwa vikwazo vikubwa katika vituo mbalimbali vya afya na hata hospitalini na kusababisha baadhi ya akimama kufariki ama watoto wao kutokana na kukosa huduma zinazostahili.
Imefika wakati sasa hakuna kuwaonea aibu wala kuwaachia wauguzi kama hawa kwa kuwa hawana huruma wala upendo kwa wagonjwa.
Malalamiko kama hayo yamekuwa yakiwapata akinamama wengi na kushindwa mahali pa kwenda kueleza kero hizo na hata wanapokwenda kutoa malalamiko hayo katika ngazi za juu huwaziba midogo kwa kuwadaganya kuwa kero hizo zitatatuliwa.
Hata hivyo hainiingii akilini ni kwanini wauguzi kama hawa waendelee kuwepo kwenye hospitali zetu na kuwa kero kwa jamii, ni bora kukawa na ofisi maalumu kwa ajili ya kupokea malalamiko ya wagonjwa na kufanyiwa kazi na kuchukuliwa hatua zinazostahili bila kuonea haya na kutangazwa.
Ukweli ni kuwa hivi vitendo vya kuwanyanyasa wanawake pindi wanapokwenda kujifungua vikomeshwe kwani vinawasababishia kuathirika kisaikolojia kutokana na kuwaza kubeba tena ujauzito na kuhofia kutukanwa.
Lakini pia matukio ya unyanyasaji kwa asilimia kubwa yamekuwa yakifanywa na wanawake ambao nao wapo katika mstari mmoja wa harakati za kumkomboa mwanamke kimapinduzi hivyo imefika wakati sasa tukashirikiana katika kukomesha vitendo hivyo.
Nionavyo mimi ni kuwa kama kuna wauguzi wa namna hii ni bora wapewe adhabu kali ambazo zitasababisha wauguzi wengine kuogopa na pia kuwepo kwa timu maalumu ya wafanyakazi wanaotembelea wodini na kusikiliza kero za wagonjwa na si kungoja kuletewa maofisini.
Posted: 28 May 2012 11:57 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

SIKU 2 baada ya Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuitaka Klabu ya Yanga kufanya uchaguzi wa viongozi wapya Julai 15 mwaka huu, homa ya uchaguzi huo imeanza kupanda huku viongozi waliowahi kuiongoza klabu hiyo, Francis Kifukwe, Godson Karigo na Ahmed Falcon wakitajwa kuwania nafasi za juu.

Uchaguzi huo umelazimika kufanyika tarehe hiyo kutokana na wajumbe nane wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo kujiuzulu huku mjumbe mwingine kufariki, hivyo kufanya nafasi zijazwe kwa ibara ya 28 ya katiba ya Yanga.

Viongozi hao waliamua kujiuzulu kutokana na kuona klabu hiyo ikiendelea na malumbano kati ya uongozi uliopo chini ya Mwenyekiti, Llody Nchunga na Wazee wa Baraza la Muafaka ambapo wazee hao walitaka Nchunga ang'oke baada ya kudai timu imemshinda.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo gazeti hili imezipata kutoka Makao Makuu ya klabu hiyo, Mitaa ya Twiga na Jangwani, zilieleza kwamba tayari kumeshaanza kufanyika kwa vikao vya siri kati ya viongozi mbalimbali waliowahi kuiongoza timu hiyo huku baadhi ya wanachama wakiwapigia chapuo waliowahi kuiongoza.

“Tayari vikao vimeshaanza na kuna baadhi ya wanachama wameanza kupanga safu zao za uongozi huku wengine wanataka kumrudisha Kifukwe, wengine mara Karigo au Falcon na kwamba inaonekana uchaguzi huu utakuwa na msisimko wa aina yake,” alisema kiongozi mmoja ambaye alijiuzulu katika uongozi uliopita.

Alisema kwa jinsi mwelekeo wa wanachama unavyoonekana, endapo mmojawapo kati ya waliotajwa akionesha nia ya kutaka kugombea hatakuwa na upinzani kwani inaonekana wanakubalika.

Gazeti hili lilifika klabuni hapo na kushuhudia kuwepo kwa vikundi vya wanachama wakiuzungumzia uchaguzi huo, huku wakiyataja baadhi ya viongozi waliopita lakini hawakuwa tayari kueleza zaidi mpaka Kamati ya Uchaguzi ya klabu hiyo, iliyo chini ya Jaji John Mkwawa itakapotangaza rasmi.
Posted: 28 May 2012 11:53 PM PDT

Na Amina Athuman

MICHUANO ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ngazi ya wilaya, Kanda ya Ilala yalimalizika juzi kwa New Team FC kuifunga timu ya Sanry FC kwa mikwaju ya penalti 6-5 katika mechi ya fainali iliyochezwa kwenye Uwanja wa Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo ambao ulivuta umati mkubwa wa mashabiki kutokana na timu zote kuwa jirani, ulianza kwa kasi na ilibidi kipa wa New Team kufanya kazi ya ziada dakika 20 za kwanza kwa kuokoa mabao matatu ya wazi kutoka kwa washambuliaji wa Sanry FC, Twalib Mohammed na Hassan Kamoti.

Hata hivyo baada ya mashambulizi hayo, Sanry FC walitulia na kuanza kupeleka mashambulizi mfululizo langoni mwa wapinzani wao, lakini mabeki walisimama vyema kuondoa hatari zilizoelekezwa kwao.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mashambulizi kwa zamu lakini hadi mwamuzi alipopuliza filimbi ya kumaliza mechi hiyo hakuna timu iliyoliona lango la mwenzake.

Baada timu hizo kutoka suluhu katika dakika 90 za kawaida, mwamuzi alilazimika kutumia sheria ya kupigiana mikwaju ya penalti ili kupata mshindi ndipo New Team FC ilibuika kidedea kwa mikwaju 6-5 dhidi ya wapinzani wao.

Mchezo huo ulikuwa ni hitimisho la kuchangua wachezaji watakaoungana na timu ya kombaini ya Mkoa wa Ilala kisoka, ambayo itaiwaikilisha kwenye fainali za Copa Coca-Cola zitakaoanza Juni Mwaka huu.

Katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu, timu ya Aggrey FC iliifunga Young Stars FC 5-4, mchezo ambao pia uliamuriwa kwa mikwaju ya penati baada ya timu zote kumaliza muda wa kawaida bila kufungana.
Posted: 28 May 2012 11:52 PM PDT

Na Yusuph Mussa, Korogwe

MBUNGE wa Viti Maalum kupitia Mkoa wa Tanga, Mary Chatanda ameiokoa timu ya soka ya Korogwe United kuweza kushiriki mashindano ya Kanda, baada ya kuwasaidia sh. milioni moja za kuwapiga jeki katika michuano hiyo.

Michuano hiyo itatoa timu zitakazopanda Daraja la Kwanza msimu ujao, ambapo timu hiyo imepangiwa kituo cha Musoma,Mara.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana mjini hapa, Mkurugenzi wa Korogwe United ambayo ndiyo mabingwa wa Mkoa wa Tanga, Filbert Mpezya alisema mbunge huyo aliwaingizia fedha hizo kwenye akaunti yao, ambapo pia zitawasaidia kukodisha basi dogo aina ya Coaster kwa ajili ya kwenda Musoma kwenye mashindano hayo.

"Unajua mashindano haya ni gharama hasa ukizingatia hayana udhamini, hivyo kwa kupata msaada wa sh. milioni moja kutoka kwa Mama imetusadia sana sisi kuweza kufika kwenye kituo cha mashindano na timu yetu inacheza mchezo wa kwanza leo na timu ya Red Cross ya Dar es Salaam," alisema Mpezya.

Naye Chatanda alisema ameamua kuisaidia timu hiyo, ili iweze kufanya vizuri kwenye mashindano hayo hatimaye iungane na Coastal Union na Mgambo JKT kucheza Ligi Kuu Tanzania Bara.

"Nimewaingizia sh. milioni moja kama ahadi yangu niliyoitoa kwenye sherehe zao za ubingwa wa mkoa, lakini pia nitaendelea kuisaidia timu hii kama Mbunge na mkazi wa Korogwe kuona inacheza Ligi
Posted: 28 May 2012 11:51 PM PDT

Na David John, Aliyekuwa Shinyanga

SERIKALI imeshauriwa kuwasaidia waandishi wa habari ambao wanaripoti habari za mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na siyo kuwawekea vikwazo vya kuwatisha pindi wanaporipoti habari hizo.

Mwito huo ulitolewa na Mkurugenzi wa Shirika la Under The Same Sun Bw. Peter Ash mkoani Shinyanga baada ya kutembelea Shule ya Msingi Buhangija ambayo imefanywa kuwa moja ya kituo cha kulelea watoto wenye ulamavu wa ngozi.


Kituo hicho kilitengwa na Serikali baada ya kutokea mauaji ya albino miaka sita iliyopita.

Bw. Ash alisema kuwa anatambua kuwa serikali itakuwa inajisikia vibaya hasa kuendelea kuripotiwa kwa habari hizo kwa kutambua kuwa mauaji hayo yametia doa utulivu na amani ya nchi katika nyanja za kitaifa na kimataifa.

"Tanzania kwa muda mrefu imekuwa ikisomeka kuwa ni miongoni mwa nchi ambayo imefanikiwa kulinda amani na utulivu wa nchi, lakini baada ya kutokea mauaji hayo yamechafua uhalisia wa amani ya nchi,"alisema Bw Ash.

Alisema ili serikali ionekane haiungi mkono mauaji ya walemavu wa ngozi inatakiwa kuendelea kuunga mkono waandishi wa habari kupinga mauaji hayo ili kulisafisha taifa liendelee kuonekana kuwa ni kisiwa cha amani na upendo.

Mbali na rai hiyo Bw. Ash alitumia fursa hiyo kutoa vifaa mbalimbali kwa watoto hao ikiwa pamoja na miwani kwa ajili ya kujikinga na jua, kofia, madawa ya ngozi, losheni za kujipaka kwa ajili ya kuzuia miozi ya jua.
Posted: 28 May 2012 11:50 PM PDT

Na Mwandishi Wetu, Lindi

MSHAURI Mkuu wa Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi Bw. James Mbatia, Danda Juju ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho amesema ni hatari wananchi kubadili mitazamo yao kisiasa kutokana na maisha magumu yanayowakabili.


Alisema, kama Chama Cha Mapinduzi (CCM) hakitaki kuondoka madarakani kwa hiari, siku wananchi wakiamua kukiondoa madarakani machafuko yanaweza kutokea.

Hayo aliyasema jana Mjini Liwale Mkoa wa Lindi,alipokuwa akihutubia mkutano wa hadhara.

"Hiki Chama Cha Mapinduzi kimechoka, nasema kimechoka kweli kweli na hakina tena sifa za kutawala nchi hii ingawa viongozi wake hawataki kulikubali hilo.

"Sisi hatutaki kufika huko, Tanzania ni nchi ya amani, Tanzania ndiyo nchi inayoheshimika duniani kwa amani na utulivu, lakini narudia tena, binadamu anapobadilika kwa sababu ya shida zinazomkabili anakuwa mbaya zaidi kuliko hata mnyama," alisema Mjumbe huyo wa Halmashauri Kuu ya NCCR-Mageuzi.

Wakati huo huo, alisema CCM ya sasa siyo CCM ya kuwavutia watu kwa sababu chama hicho hakifuati misingi ya utawala bora na kwamba ili kuondokana na kero zinazosababishwa na utawala wa chama hicho wananchi hawana budi kukikataa kwa vitendo.
Posted: 28 May 2012 11:49 PM PDT


Na Daud Magesa, Mwanza

MABINGWA wa zamani wa soka Tanzania Pamba ya Mwanza, imeondoka jijini hapa ikiwa na matumaini makubwa ya kufuzu fainali za Kanda ili kucheza Ligi Daraja la Kwanza.

Pamba ambao ni mabingwa wa soka Mkoa wa Mwanza, iliondoka juzi kwa basi la kukodi ikiwa na kikosi cha wachezaji wake wote chini ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ramadhan Muzzo na kuahidi ushindi.


Wadau wa soka jijini hapa ambao walifika kuwaaga wachezaji wa timu hiyo, makocha na viongozi, walisema silaha pekee itakayowasaidia kufuzu katika michuano hiyo ni nidhamu kwa kila mchezaji na kutimiza majukumu yao.

Wadau hao waliwataka wachezaji wa timu hiyo iliyowahi kutikisa soka la Tanzania katika miaka ya 1980 na mwishoni mwa 1990, kuwakilisha vyema mkoa na kubwa ikiwa ni kupata nafasi ya juu ili kufuzu kucheza Ligi Daraja la Kwanza.

Walisema wakishikamana na kufuata maelekezo ya makocha na wakizingatia nidhamu katika michuano hiyo ni wazi watafanya vizuri.

"Kikubwa ni kuzingatia nidhamu, kuonesha mshikamano wenu kama timu uwanjani na nje ya uwanja, kila mchezaji atimize wajibu wake pamoja na changamoto mliyonayo ya ukata," alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Waandishi wa Habari ya Kuhamasisha Pamba ishinde, Mashaka Baltazar

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) Jackson Songora, alisisitiza nidhamu kwa wachezaji hao akisema mkoa huo upo pamoja nao kuhakikisha wanafanya vizuri.

Pamba iko katika Kituo cha Kigoma pamoja na wenyeji JKT Kanembwa, Majimaji ya Tabora, Mwadui ya Shinyanga, Mabingwa wa Mkoa wa Singida, CDA ya Dodoma na Bandari ya Kagera.
Posted: 28 May 2012 11:46 PM PDT

Na Elizabeth Mayemba

KAMPUNI ya simu za mikononi ya Airtel Tanzania imekabidhi vifaa vya michezo kwa timu za vijana chini ya miaka 17 zitakazoshiriki mashindano ya Aitel Rising Stars, inayotarajiwa kuanza kutimua vumbi kesho katika mikoa sita.

Mikoa ambayo itashiriki michuano hiyo ni Lindi, Mbeya, Arusha, Ilala, Temeke na Kinondoni, ambapo kwa upande wa Ilala mechi zitakuwa zikichezwa Uwanja wa Airwing, Kinondoni Mwenge na Temeke mechi zitachezwa Uwanja Twalipo.

Akikabidhi vifaa hivyo kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Sanifu Kondo, Afisa Uhusiano Airtel Tanzania Jane Matinde, alisema jumla ya timu 24 zinatarajiwa kushiriki mashindano hayo.

Alisema vifaa vilivyotolewa ni jezi na mipira na kila timu itapatiwa jezi mbili.

"Mwaka huu tumeboresha zaidi michuano hii  ikiwa ni pamoja na kushirikisha timu za wasichana tofauti na hapo awali, ambapo kila mkoa utatoa timu ya wanawake ambayo itakuwa kombaini.

"Mwaka huu mashindano yatashirikisha mikoa sita kwa kuanzia ngazi ya mikoa kabla ya ile ya taifa itakayoanza Juni na timu bingwa itashiriki mashindano ya siku nne nchini Kenya yajulikanayo kama Inter Continental Tourmament yatakayoshirikisha mataifa zaidi ya 16," alisema Jane.

Alisema mbali na timu hiyo pia watateua wachezaji sita bora ambao watashiriki kliniki ya soka maarufu kama Coaching Stars  itakayofanyika nchini Kenya chini ya jopo la makocha kutoka Academy ya soka ya Manchester United ya Uingereza.

No comments:

Post a Comment