TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, June 16, 2012

Mbunge aibana serikali muswada wa ushauri

Posted: 14 Jun 2012 11:35 PM PDT

Kocha wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen akizungumza wakati wa hafla ya kuiaga timu hiyo iliyoondoka leo alfajiri kwenda Msumbiji kucheza mechi ya marudiano ya mchujo wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 14 Jun 2012 11:38 PM PDT

Na Elizabeth Mayemba

TIMU ya Taifa (Taifa Stars) imeondoka nchini leo kwenda Msumbiji kwa ajili ya mechi yao ya marudiano dhidi ya nchi hiyo 'Mambas' kusaka tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON), zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.
Mechi  hiyo inatarajia kuchezwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa ulioko Zampeto nje kidogo ya jiji la Maputo kuanzia saa 9 mchana kwa saa za huko.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete ameitakia kila la kheri timu hiyo ili ifanye vizuri, huku akiwapongeza kwa ushindi katika mechi yao iliyopita dhidi ya Gambia, baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-1.
Akikabidhi bendera ya taifa kwa Stars, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said Mecky Sadik, alisema anaimani timu hiyo itaiwakilisha nchi vyema katika michuano hiyo na Watanzania wapo nyuma yao.
"Mkumbuke kuwa mnakwenda Msumbiji kuiwakilisha nchi, hivyo macho na masikio ya Wanzania wote yapo kwenu kuona mtavuna nini huko, kwa mchezo mzuri mliouonesha mechi iliyopita dhidi ya Gambia bila shaka na huko mtatuwakilisha vizuri," alisema.
Alisema matokeo mazuri waliyoonesha katika mchezo uliopita isiwe ni nguvu ya soda na nidhamu, ambayo wanatakiwa kuionesha huko na ushindi kwao uwe wa kwanza.
Pia Mkuu wa Mkoa huyo alisema kuwa Rais Jakaya Kikwete, ameitakia kila la kheri timu hiyo na kuitaka iwakilishe vyema nchi.
"Wakati nakuja kuiaga timu ya taifa, Rais ametoa salamu zake kuwa anawatakia kila la kheri ili mfanye vizuri na matokeo ambayo yalipita dhidi ya Gambia yamemfurahisha na anawapongeza sana," alisema.
Naye Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen alisema ili kuitoa 'Mambas' kwenye michuano ya Afrika ni lazima timu yake ishinde mechi hiyo.
Alisema maandalizi katika kikosi chake yalikwenda vizuri ingawa ana wachezaji watatu ambao ni majeruhi, kipa Mwadini Ali na mabeki Nassoro Masoud 'Cholo' na Waziri Salum.
Iwapo Taifa Stars itaitoa Msumbiji katika raundi ya mwisho itapangiwa moja kati ya timu 16 zilizocheza Fainali za AFCON zilizofanyika Januari mwaka huu katika nchi za Gabon na Equatorial Guinea.
Katika mechi ya kwanza dhidi ya Msumbiji iliyochezwa Dar es Salaam, Februari 29 mwaka huu timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.
Posted: 14 Jun 2012 11:32 PM PDT

MBUNGE wa Moshi Mjini, mkaoni Kilimanjaro, Bw. Philemon Ndasambulo (CHADEMA), ameitaka Serikali kulieleza Bunge ni lini italeta muswada wa sheria ya Sera ya Taifa ya Ushauri kwenye Viwanda ili iweze kutumika na kuinufaisha nchi kiuchumi.
Bw. Ndesambulo aliuliza swali hilo bungeni mjini Dodoma jana katika kipindi cha maswali na majibu.
Akijibu swali hilo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu, Bw. Stephen Wassira, alisema Serikali ilianza kuandaa mchakato wa sera hiyo ili kuwezesha wataalam elekezi kuishauri Serikali mambo ya kiuchumi na kijamii.
Alisema ulijadiliwa na wadau katika hatua mbalimbali na baada ya kukubaliwa, Aprili 2004 ulipelekwa katika Baraza la Mawaziri.
Baraza hilo lilijadili waraka, kukubalina na kumshauri Rais ili aweze kuusaini na kuwa sera rasmi. Ushauri mwingine waliotoa ili kutekeleza sera hiyo, lazima kianzishwe Chama cha Washauri elekezi ili kitumike kama Sekretarieti ya Baraza la Taifa ambapo Ofisi ya Rais, Mipango na Uwezeshaji, ichukue jukumu la kuandaa mpango mkakati wa sera haraka iwezekanavyo na kuhakikisha inatekelezwa kwa faida ya Watanzania.
Alisema kutokana na mabadiliko ya muundo wa Serikali ambao ulitangazwa Februari 2008, baadhi ya majukumu yaliyokuwa yakisimamiwa na kutekelezwa na Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji, yalihamishiwa katika Wizara nyingine.
Aliongeza kuwa, hivi sasa utekelezaji wa sera hiyo unaenda sambamba na Sera ya Taifa ya Ajira ya mwaka 2008, kwa kuhusisha vyombo vya vitatu ambavyo ni Baraza la Ushauri wa Masuala ya Kazi, Uchumi na Jamii.
Mchakato wa kuandaa rasimu ya sheria ya uanzishwaji Baraza la Kitaifa la Huduma na Ushauri, unafanyiwa kazi pamoja na kupata maoni ya wadau mbalimbali chini ya utaratibu wa Wizara ya Kazi na Ajira.
Kwa kuzingatia maoni ya wadau, Serikali itafanya tathmini ya namna kuendelea na utekelezaji wa sera hiyo.
Posted: 14 Jun 2012 11:30 PM PDT
Posted: 14 Jun 2012 11:28 PM PDT


WAMILIKI wa shule binafsi zisizo za Serikali, wanawajibika kutangaza ajira za walimu kwa njia ya matangazo au nyingine wanazoona zinafaa na kuwaajiri katika shule husika.
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bw. Philipo Mulugo, aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Bi. Elizabeth Batenga (CCM).
Bi. Batenga alitaka kufahamu kwanini shule na vyuo vya Serikali havina walimu wa kutosha lakini katika shule na vyuo binafsi kuna walimu wa kutosha, je, waanawapata wapi?
Akijibu swali hilo, Bw. Mulugo, alisema sera ya elimu na mafunzo ya mwaka 1995, inafafanua wazi kuwa utoaji elimu nchini utakuwa kwa ushirikiano wa Serikali na taasisi au watu binafsi.
Alisema shule zisizo za Serikali, zinapata walimu kwa kutangaza ajira kupitia matangazo na kupata walimu kutoka vyuoni au nje ya nchi kwa kuhakikisha wanatimiza masharti ya ajira.
Aliongeza kuwa, baada ya kufungua milango ya ajira kwa nchi za Afrika Mashariki, walimu kutoka nchi jirani watapata ajira katika shule zisizo za Serikali hivyo upo uwezekano mkubwa wa shule za Serikali kupata walimu wa kutosha.
Akizungumzia suala la utoaji na ukaguaji maendeleo ya elimu kwenye shule na vyuo vya Serikali na binafsi, Bw. Mulugo alisema   jambo hilo linasimamiwa na Wizara yake kupitia idara na taasisi zake ikiwemo ya ukaguzi wa shule, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi pamoaja na Tume ya Vyuo Vikuu.
Posted: 14 Jun 2012 11:27 PM PDT

MBUNGE wa Ole, Zanzibar Bw. Rajabu Mbaruk Mohamed (CUF),  amemtaka Waziri Mkuu, Bw. Mizengo Pinda kutoa tamkoa la kuunda Tume Huru ambayo itafanya uchunguzi wa kina ili kubaini watu waliosababisha vurugu zilizotokea hivi karibuni visiwani Zanzibar zikihusishwa na kundi la Uamsho.
Bw. Mohamed aliyasema hayo bungeni mjini Dodoma jana waakati akiuliza swali kwa Bw. Pinda na kudai kuwa yupo tayari kuunda tume huru iweze kufanya kazi na wahusika ili watakaobainika wachukuliwe hatua.
Akijibu swali hilo, Bw. Pinda alisema Mei 26-27 mwaka huu, vurugu kubwa zilitokea Zanzibar zikihusishwa na kikundi kimoja kilichosajiliwa ili kueneza dini ya Kiisilam mwaka 2001 lakini kikaingia katika masuala mengine yasiyohusiana na dini hiyo.
Alisema kikundi hicho kilianza kupinga Muungano baada ya kuanza mchakato wa Katiba Mpya na kufanya maandamano ambayo polisi hawakuwa na taarifa nayo.
Bw. Pinda alisema, kikundi hicho kinapaswa kudhibitiwa ili kutoa fursa ya kufanikisha mchakato wa uandikaji Katiba Mpya kwani Serikali ikiachia jambo hili bila kuchukua hatua, kukundi hicho kinaweza kuleta madhara makubwa.
Aliongeza kuwa, kutokana na vurugu hizo baadhi ya watu waliohusika wamekamatwa akiwemo kiongozi wao mmoja ambaye ni Shekhe Juma Mussa Issa na kudai kuwa taarifa za kiusalama zinasema kikundi hicho hakitaki Muungano uliopo.
Alisema ombi la kuundwa tume hutu ili kuchunguza chanzo cha vurugu hizo ni zuri na kubainisha kuwa, lazima lifikishwe katika Serikali ya Zanzibar ndipo hatua zingine zichukuliwe.
Posted: 14 Jun 2012 11:35 PM PDT
Mchezaji Goodluck Mabiriki wa Ilala (kulia) akigombea mpira na mshambuliaji wa timu ya Lindi, Khalfan Malibiche wakati wa fainali za michuano ya Airtel Rising Stars inayoendelea kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Posted: 14 Jun 2012 11:21 PM PDT

Na Mwandishi Wetu

TIMU za soka za Mkoa wa Mbeya za wanaume na wanawake zimejihakikishia kucheza nusu fainali ya michuano ya kukuza vipaji wenye umri chini ya miaka 17 ya Airtel Rising Stars inayotarajiwa kuanza leo kwenye Uwanja wa Karume, Jijini, Dar es salaam.
Timu hizo zimefuzu kucheza nusu fainali hiyo baada ya kumaliza katika makundi yao zikiwa zinaongoza.
Nayo Arusha imefanikiwa kupitisha timu zake zote za wanaume na wanawake baada ya kushika nafasi ya pili katika kundi A nyuma ya Mbeya.
Mbali na timu hizo, zingine zilizofuzu kwa upande wa wanaume ni Temeke ilioonesha kuwa tishio katika michuano hiyo kwa kufunga idadi kubwa ya mabao.
Ilianza kwa kuisambaratisha Lindi kwa mabao 12-2 kabla ya kuichakaza tena Ilala kwa mabao 3-0. Wakati wanaume wamefuzu, timu yao ya wanawake inasubiri matokeo kati ya Ilala na Lindi zilizotarajiwa kucheza jana.
Hata hivyo, kwa upande wa wanaume timu ya mwisho itakayoungana na timu hizo inategemea matokeo ya mechi za mwisho za makundi zilizotarajiwa kuchezwa baadaye jana, sambamba na kwa upnade wa wanawake.
Katika mechi zilizochezwa juzi asubuhi timu ya wanawake ya Temeke iliichapa Ilala kwa mabao 2-0.
Kwa upande wa wanaume, Temeke iliendeleza mwendo wake wa kugawa dozi baada ya kuibugiza Ilala kwa mabao 3-0. Goli la kwanza la washindi lilifungwa na Khalid Mwenda dakika ya 28, la pili liliwekwa kimiani na Paulo Balama dakika ya 43 na la mwisho lilpatikana dakika ya 87 kupitia kwa mshambuliaji wake hatari, Bakari Ally.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jioni, timu ya wanawake ya Arusha iliifunga Kinondoni kwa mabao 2-0, kupitia kwa Anitha Antony dakika za pili na 35. Mechi ya mwisho ilizikutanisha Kinondoni na Arusha ambapo zilitoka sare ya mabao 2-2. Wafungaji wa Arusha  ni Nazir Abdul dakika za 22 na 82, wakati yale ya Kinondoni yaliwekwa kimiani na Omar Ramadhani na Jarufu Lutonga katika dakika ya 55
Posted: 14 Jun 2012 11:20 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

KAMPUNI ya Bantu inatarajia kuandaa tamasha la utoaji tuzo za filamu nchini (Bantu Film Awards), litakalofanyika kwa mara ya kwanza Julai jijini Dar es Salaam likiwa na lengo la kutambua kazi za wasanii na kuzitangaza kimataifa.
Akizungumzia tamasha hilo Dar es Salaam jana, Ofisa wa kampuni hiyo, Stewart Kambona alisema maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri na kwamba wapo katika mazungumzo na wadau mbalimbali wa sanaa, wakiwemo waadhiri wa vituo vya sanaa kutoka katika vyuo vikuu mbalimbali nchini.
Alisema tamasha hilo linatarajiwa kufanyika mwezi ujao Dar es Salaam, ambalo litasaidia kutoa motisha kwa wasanii wanaochipukia na hata wale wakongwe katika fani hiyo kuongeza bidii katika kuandaa kazi zao.
"Unajua hili tamasha litakuwa ni chachu ya wasanii kuzidi kupata mafanikio kwani wakiona mwenzao leo amepewa tuzo kutokana na kazi yake fulani, nina hakika atajipanga ili mwakani naye apewe tuzo, tunatarajia tuzo hizi kufanyika kila mwaka," alisema Kambona.
Alisema kwa kuanzia kutakuwa na kategoria 27 ambazo alizitaja baadhi yake kuwa ni tuzo ya muongozaji bora, mtunzi na mpiga picha ambapo watahakikisha wanatoa fursa kwa wadau kutoa michango yao, ili kusiwepo na maneno ya hapa na pale baada ya kutoa tuzo hizo.
Naye Wasanii Jacob Stephen 'JB' na Irene Uwoya wakizungumza kwa niaba ya wasanii wenzao kwa nyakati tofauti, waliishukuru kampuni hiyo kwa kuwa na wazo hilo ambalo wanaamini litasaidia kuinua tasnia ya filamu hapa nchini ndani na nje ya nchi.
JB alisema wamekuwa wakifanya sanaa kwa muda mrefu, lakini hakukuwa na kitu cha kuwatia moyo ila hivi sasa kila mmoja ataongeza ubunifu wake katika kuandaa kazi ili mwisho wa mwaka wapate tuzo.
Naye Uwoya alisema tuzo hizo kwao ni changamoto ya kuzidi kufanya vitu vizuri zaidi, kwani ana imani tuzo hizo zitawatambulisha kimataifa kupitia kazi zao na mwisho wa siku mafanikio ya fani hiyo yataongezeka.
Posted: 14 Jun 2012 11:36 PM PDT
Wanyange wanaowania taji la Redd's Miss Kigamboni 2012 wakiwa katika mazoezi jana, mashindano hayo yanatarajia kufanyika leo katika Ukumbi wa Navy Beach, Kigamboni. (Picha na Victor Mkumbo)
Posted: 14 Jun 2012 11:17 PM PDT

Na Victor mkumbo

MSHINDI wa kwanza wa taji la urembo la Kitongoji cha Kigamboni mwaka huu 'Redd's Miss Kigamboni City 2012', atazawadiwa sh. 500,000 katika mashindano yatakayofanyika leo katika ukumbi wa Navy Beach, Dar es Salaam.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, mratibu wa mashindano hayo, kutoka kampuni ya K&L Media Solutions, Somoe Ng'itu alisema maandalizi yote yamekamilika  na warembo wote wako tayari kwa kinyang'amyiro hicho.
Mratibu huyo alisema mshindi wa pili atazawadiwa  sh. 350,000, wa tatu sh. 300,000, wa nne na watano wataondoka na cha sh. 200,000 kila mmoja na wengine saba waliobaki watapatiwa kifuta jasho sh. 150,000 kila mmoja.
Alisema mgeni rasmi katika mashindano hayo atakuwa ni diwani wa kata ya Kigamboni, Dotto Mawa ambaye ametoa mchango mkubwa katika kufanikisha kinyang'anyiro hicho.
Aliongeza kuwa ili kuboresha shindano hilo bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia maarufu Wazee wa Ngwasuma na msanii na mchekeshaji mahiri hapa nchini, Mpoki watatumbuiza kwenye kinyang'anyiro hicho.
"Tumeboresha zaidi mashindano ya Redd's Miss Kigamboni kwa mwaka huu ambapo warembo wote wana sifa na tunatarajia kuwapata wawakilishi wazuri katika mashindano ya Redd's Miss Temeke pamoja na Redd's Miss Tanzania 2012," alisema.
Aliwataja warembo watakaochuana kuwa ni Susanne Jeremiah, Agness Goodluck, Elizabeth Boniface, Dorothea Kessy, Esther Albert, Edda Silyvester, Sophia Martin, Doreen Kweka, Khadija Kombo, Linnah David, Rosemary Peter na Winnie Karaya.
Aliwashukuru wadhamini ambao wamejitokeza kusaidia mashindano hayo ambao ni Redd's, Dodoma Wine, Hope Country Hotel, Screen Masters, Nobro Collections, Times FM na Kitwe Traders.
Aliongeza kuwa warembo watakaoshika nafasi tatu za juu wataungana na wenzao kutoka vitongoji vya Kurasini na Chang'ombe, ili kuwania taji la Kanda ya Temeke baadaye mwaka huu.
Posted: 14 Jun 2012 11:16 PM PDT

Na Mhaiki Andrew, Songea

SHIRIKA lisilokuwa la Kiserikali la Good Hope Sports Club la mkoani Ruvuma lina mikakati ya kutoa mafunzo ya ukocha na waamuzi kwa wanafunzi wa shule za Sekondari, ikiwa na lengo la kuibua na kuendeleza michezo mkoani hapa.
Akizungumza mjini hapa juzi Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Joseph Mapunda alisema mafunzo hayo yatawalenga wanafunzi wa shule hizo kidato cha kwanza hadi cha tatu ili kuwapatia taaluma ya michezo, badala ya kutegemea makocha kutoka nje ya mkoa kufundisha.
Alisema shirika hilo, limejiwekea malengo endelevu katika kusaidia kuinua michezo ambapo alidai baada ya kukamilika kazi hiyo kwa shule za sekondari pia mafunzo hayo yatatolewa kwa vijana wa shule za msingi kuanzia darasa la tano, ili wajengeke na uelewa kabla ya kuchaguliwa kuanza kidato cha kwanza.
Mapunda alisema kabla ya kuanza kwa utoaji wa mafunzo ya ukocha kwa wanafunzi hao, bodi ya shirika hilo imekutana na kuweka mikakati itakayowezesha kufanikiwa kwa kupendekeza shule za kuanzia, badala ya shule zote kwa pamoja kwa kutumia kanda za kielimu mkoani Ruvuma.
Alisema katika mapendekezo yao, wamekubaliana wataanzia na shule za sekondari katika wilaya mbili za Songea na Namtumbo kabla ya kuamia wilaya nyingine za Nyasa, Mbinga na Tunduru kwa mafunzo hayo ya ukocha na waamuzi ambapo yamelekezwa kutolewa kwa michezo 11 ikiwemo soka, netiboli, ngumi, riadha na mpira wa wavu.
Mkurugenzi huyo alisema programu hiyo ya mafunzo itaanza kutolewa baada ya na kuvutiwa na kituo cha michezo cha Twalipo cha Jijini Dar es Salaam, kilivyofanikiwa kwa kiasi kikubwa kutoa mafunzo ya ukocha na waamuzi kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 20.
Posted: 14 Jun 2012 11:13 PM PDT

Na Victor Mkumbo

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Isihaka Nassoro 'Dogo Aslay', anatarajia kuzindua albamu yake ya kwanza Juni 24 mwaka huu katika Ukumbi wa Dar Live, Mbagala.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja wa kundi la TMK Wanaume Family, Said Fella alisema Dogo Aslay anatarajia kuzindua albamu hiyo, kitabu pamoja na filamu ambapo zote amezipa jina la Naenda Kusema.
Alisema albamu hiyo ina jumla ya nyimbo 10 ambayo ameirekodia katika studio ya Poteza Records chini ya mtayarishaji Suresh pamoja na Alow Nem.
Fella alisema katika uzinduzi huo kutakuwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya, ambao watamsindikiza Aslay.
Alisema wasanii watakaoimba jukwaa moja na Aslay ni pamoja na Mh. Temba, Bi. Cheka, TMK Wanaume Family, Ize Man, Ommy Dimpoz na Mwana FA.
"Tumeandaa onesho maalumu kwa ajili ya Aslay kutambulisha albamu, kitabu pamoja na filamu ambapo pia kutakuwa na burudani ya aina yake kutoka kwa wasanii mbalimbali," alisema.
Alizitaja baadhi ya nyimbo zilizopo katika albamu hiyo kuwa ni Nakusemea, Niwe Nawe aliyoimba na Mh. Temba, Kikombe aliyomshirikisha Ferouz, Umbea ambaye amemshirikisha Chege, Utajuta, Mapendo, Nastrago aliyoimba na Mkubwa na Wanawe pamoja na Hawakai.

No comments:

Post a Comment