TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, June 13, 2012

Serikali yabainika kuchelewesha vitabu vya bajeti 2012 na 2013

Posted: 30 May 2012 01:29 AM PDT
Meya wa Manispaa ya Iringa, Aman Mamwingi akimkabidhi kombe nahodha wa timu ya St. Agustine, Jimmy Nicas baada ya kutwaa ubingwa wa mashindano ya Safari Higher Learning Pool Competition 2012 yaliyomalizika mkoani Iringa mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Pool Tanzania (TAPA) Fred Mushi. Na Michael Machella
Posted: 30 May 2012 01:26 AM PDT

Na Godfrey Ismaely, Dar es Salaam

ZIKIWA zimebakia siku chache kabla ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingia katika vikao vya Bajeti, mwaka wa fedha 2012 na 2013 baadhi ya wanaharakati wamedai kusikitishwa na uwajibikaji mdogo wa Serikali hasa kuchelewa kutoa vitabu vya makadirio hayo.

Kwa mujibu wa Ibara ya 96 ya Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la mwaka 2007) wabunge wanapaswa kupokea vitabu vya makadirio ya bajeti ya Serikali angalau siku 21 kabla ya kikao cha Bunge la bajeti kuanza.

Pamoja na kwamba kikao cha bajeti kinatarajia kuanza Juni 12, mwaka huu hadi Mei 29, 2012 tafiti zinaonesha bado wabunge walikuwa hawajapokea nyaraka hizo muhimu na haijulikani ni lini watazipokea.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana na Taasisi ya Sikika na kusainiwa na Mkurugenzi wake Bw. Irenei Kiria ilieleza kwamba hatua hiyo inatia wasiwasi katika utendaji.

"Tumesikitishwa na hatua ya Serikali kushindwa kutoa vitabu vya makadirio ya bajeti ya mwaka wa fedha 2012/2013, siku 21 kabla ya kikao cha Bunge la Bajeti kuanza, jambo ambalo ni ukiukwaji wa Kanuni za Kudumu za Bunge.

"Hii ni kinyume na kanuni na maazimio mbalimbali yaliyoridhiwa na serikali likiwemo, Tamko la Dar es Salaam la mwaka 2011 lililotolewa na wananchi na Azaki karibu 100 kutoka nchi mbalimbali duniani na mashirika 12 ya Kimataifa," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Hata hivyo, tamko hilo linasisitiza uwazi katika bajeti, uwajibikaji na ushirikishwaji kwa kuzitaka Serikali Kuu na serikali za mitaa kutengeneza na kujadili waziwazi katika muda mwafaka angalau nyaraka nane muhimu za bajeti ambapo kati ya nyaraka hizo mojawapo ni makadirio ya bajeti.

Pia kutolewa kwa wakati kwa vitabu vya makadirio ya bajeti vya mwaka wa fedha unaofuata kwa wabunge na umma kwa ujumla ni hatua muhimu katika kuongeza uwazi, ubora wa bajeti na ufanisi wa ushiriki wa wabunge katika kikao cha kujadili na kuidhinisha bajeti.

Taasisi ya Sikika, ilibaini kuwa ni kawaida kwa wabunge kupokea vitabu vya bajeti kwa kuchelewa na wakati mwingine huvipata baada ya kikao cha bajeti kuanza.

"Hali hiyo pia inaweza kusababisha wabunge kupitisha bajeti bila kufahamu undani wa kile wanachokijadili au kupitisha bajeti isiyo na tija wala kipaumbele kwa taifa," iliongeza taarifa hiyo.

Pamoja na kuchelewa kupatiwa vitabu vya makadirio ya bajeti, Sikika pia imebaini kuwa wabunge hupatiwa vitabu vya makadirio ya bajeti toleo la I-IV ambavyo kwa kawaida huwasilisha jumla kuu za vifungu bila maelezo ya kina.

"Na huwa hawapatiwi kabisa Vitabu vya Muundo wa Matumizi vya Muda wa Kati ya Bajeti (MTEF) kwa kila Wizara, Idara na Mashirika mbalimbali ambavyo ndivyo hubeba maelezo ya bajeti na shughuli zitakazotekelezwa," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

"Sikika imekuwa ikipitia tovuti ya Wizara ya Fedha, Bunge na kubaini kuwa hadi leo (jana) tarehe 29, Mei 2012 vitabu vya bajeti kwa mwaka wa fedha 2012/13 havijawekwa kwenye tovuti hizi mbili," iliongeza taarifa hiyo.

Aidha, tafiti zinaonesha kuwa hali hiyo inawanyima wabunge pamoja na wananchi fursa ya kushiriki kikamilifu katika mjadala wa kuichambua bajeti kabla ya kuidhinishwa na Bunge.

Pia tatizo hilo lilijidhihirisha mwaka jana (2011) ambapo wabunge hawakupata vitabu hivyo kwa wakati mwafaka.

"Sikika inatoa rai kwa Serikali kuhakikisha inatoa vitabu vya bajeti, mwaka wa fedha 2012/13 toleo la I-IV na vitabu vya Muundo wa Matumizi ya Muda wa Kati (MTEF) kwa kila Wizara, Idara na mashirika mbalimbali kwa wabunge kabla ya kuanza kwa kikao cha bajeti. Hii itawapa wabunge muda wa kufanya uchambuzi wa kina na kushiriki kikamilifu katika mjadala na hatimaye kuidhinisha bajeti yenye manufaa kwa wananchi," ilifafanua taarifa hiyo.
Posted: 30 May 2012 01:24 AM PDT
Mchezaji wa mpira wa kikapu anyechezea Ligi ya NBA ya Marekani, Hasheem Thabeet akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kliniki ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 ya Sprite itakayofanyika katika viwanja vya Don Bosco Upanga, Dar es Salaam kuanzia keshokutwa. Na Mpigapicha Wetu
Posted: 30 May 2012 01:21 AM PDT


Na Said Hauni, Lindi

MKAZI wa Kata ya Wailes katika Manispaa ya Lindi Bw. Mwanzaga Mbowi amefikishwa Mahakama ya Mkoa wa Lindi akikabiliwa na shitaka la kumjeruhi mkewe kwa kumchoma na moto wa pasi.

Bw. Mboi ambaye ni Mhasibu katika Manispaa hiyo alipandishwa kizimbani Mei 28, mwaka huu na kusomewa shitaka lake na Mwanasheria wa Serikali, Bi. Mwahija Ahamadi.


Akisomewa shitaka lake mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Bw. Dustan Ndunguru, Mwanasheria wa Serikali alidai kuwa mshitakiwa alitendo kosa hilo Mei 27, mwaka huu, saa 1:30 asubuhi.

Bi. Mwahija alidai kuwa siku hiyo ya tukio huko Wailes iliyopo katika Manispaa ya Lindi mshitakiwa alimjeruhi mke wake wa ndoa Bi. Olifoncia Chembekwa kwa kumchoma na moto wa pasi.

Aliiambia mahakama hiyo kwamba siku na wakati huo mshitakiwa na mke wake kwa pamoja walikuwepo nyumbani kwao na mara kukatokea kidogo mifarakano ambayo ilipelekea mshitakiwa kumpiga na hatimaye kuchukua pasi ya moto na kumuunguza mlalamikaji mkono wake wa kulia na sehemu nyingine.

Mwendesha mashitaka huyo alidai kutokana na kitendo hicho, mshitakiwa alimsababishia mlalamikaji maumivu makali kwenye mwili wake.

Bi. Mwahija aliiambia Mahakama hiyo kwamba kutokana na kitendo hicho mshitakiwa amefanya kosa chini ya kifungu cha 225 Kanuni ya Adhabu Sura ya 16.

Hata hivyo Mshitakiwa alikana kosa linalomkabili na kupelekwa rumande baada ya upande wa mashitaka kupinga dhamana kwa mshitakiwa kutokana na kutopata taarifa ya maendeleo ya mlalamikaji huku kesi hiyo namba 49/2012,itatajwa tena Juni 11, mwaka huu.
Posted: 30 May 2012 01:19 AM PDT

Viongozi wa Kamati inayofuatilia madai ya waliokuwa wafanyakazi wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki kabla ya kuvunjika kwaka 1977, wakitoa taarifa ya kuungana katika madai yao, wakati wa mkutano na waandishi wa habari kwenye Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (HLRC) Dar es Salaam jana. Kushoto ni Bw  Ahmed Kabunga na Alfred Kinondo. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 30 May 2012 01:16 AM PDT

Na Pamela Mollel, Arusha

IMEELEZWA kuwa bajeti nyingi za nchi za Afrika zimekuwa tegemezi kwa wahisani jambo ambalo linachangia uwepo wa matumizi mabaya ya rasilimali za nchi kwa maslahi ya wahisani husika.

Pia Serikali imetakiwa kutumia utawala bora wa fedha kwa wananchi wake na matumizi sahihi ya mali asili ili ziweze kuwa na tija kwa vizazi vijavyo na kuitumia demokrasia katika kukuza pato la wananchi.

Changamoto hiyo ilitolewa jana na Waziri wa Elimu Mafunzo ya Amali kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Ally Juma Shamuhuna wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha kwenye mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

"Tumekuja kujifunza suala zima la demokrasia inavyoweza kukuza uchumi wa nchi yeyote sanjari na utawala bora wa matumizi ya fedha za serikali
na kuwa tunaelekea kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2012-13 ambapo tayari tutakuwa na tumepata uzoefu," alisema Waziri huyo.

Alisema kuwa, Serikali yeyote itakayofuata mambo matatu na kuyajali kwa maslahi ya wananchi wake hususan utawala bora wa fedha, matumizi sahihi ya
demokrasia sanjari na matumizi ya mali asili zitaifanya serikali kutokuwa
tegemezi kwa wahisani.

“Mashirika haya ya fedha ulimwenguni hayatoi fedha bure, lazima watangulize maslahi yao hali inayopelekea nchi zilizofadhiliwa 'kubaka' demokrasia na wananchi wake kuendelea kuwa maskini,” alisema Bw. Shamuhuna
Posted: 30 May 2012 01:14 AM PDT

Posted: 30 May 2012 01:12 AM PDT


Na Sangalwise Abia, Dar es Salaam

SHIRIKA la Posta Tanzania limefungua biashara ya kuuza na kununua
fedha za kigeni (Bureau de change) katika ofisi zake zilizopo Posta
Mpya Mtaa wa Azikiwe jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo ni kati ya mikakati ya shirika hilo ambayo inalenga kuhakikisha linawapatia wateja wake nchini kote huduma mbalimbali zenye tija na ufanisi, kibiashara zikiwa mahali pamoja ili kuwapunguzia kutumia muda mwingi wa kuzitafuta mbali.

Meneja Masoko wa shirika hilo Bw. David George aliyasema hayo jana, wakati akizungumza na gazeti hili juu ya mipango mikakati ya shirika ambayo inalenga kuboresha huduma zake nchini kote.

Alisema, walifikia hatua hiyo baada ya kupewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania hivi karibuni.

"Lengo la kuanzisha huduma hii ni kwamba tunahitaji kuhakikisha Watanzania wanapata huduma mahali pamoja badala ya wateja kuhangaika huku na kule wakitafuta huduma. Kwa hali hiyo sisi posta tukaliona hilo...hivyo tukaamua kuanzisha huduma hiyo,"

"Lengo letu ni kwamba mteja anapoingia katika Ofisi za Posta basi ategemee kupata huduma mbalimbali, hatua hiyo itawasaidia wateja kutopoteza muda mwingi kwa kutafuta mahitaji,” alisema Bw. George.

Alisema, kwa sasa Shirika la Posta limeshaanzisha huduma nyingi zikiwepo huduma za Posta Cash, EMS Courier, EMS Cargo, Post Cargo City urgent mail (pCUM), huduma ya Internent Cafe na sasa huduma ya
kuuza na kununua fedha.

"Hayo yote yakiwa ni malengo ya kusogeza huduma za kibiashara karibu zaidi na jamii ili huduma hizo zipatikane kwa urahisi na mahali pamoja badala ya kutafuta huduma sehemu mbalimbali," aliongeza.

Bw. George alitoa mwito kwa wateja kuhakikisha wanatembelea katika Ofisi ya Posta ili wajipatie huduma ya Posta Bureau de Change sambamba na huduma nyinginezo za shirika hilo kwa kuwa zinatolewa kwa ufanisi wa hali ya juuikiwemo gharama nafuu zaidi.
Posted: 30 May 2012 01:09 AM PDT

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishina Augustino Nanyaro kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akimvisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Nne, Mkaguzi Msaidizi wa Magereza, Bi. Mariam  Kamangu. wakati utoaji nishani hizo, Dar es Salaam jana. (Picha na Peter Twite)
Posted: 30 May 2012 01:03 AM PDT


Na Mwali Ibrahim

WANYANGE wanaotaka kushiriki katika mashindano madogo ya kumsaka mwakilishi wa Tanzania katika mashindano ya Dunia (Miss World 2012) wameombwa kuendelea kuchukua fomu za kuingia katika kinyang’anyiro hicho na kuzirudisha kabla ya Juni 4 mwaka huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana Mkurugenzi wa Lino International Agency ambayo inaandaa mashindano hayo, Hashim Lundenga alisema wanatarajia kufanya mchujo wa washiriki Juni 5, mwaka huu kwa ajili ya kubakiza warembo 10 watakaowania nafasi ya kushiriki mashindano ya Dunia.

Mashindano hayo ya Dunia yamepangwa kufanyika Agosti 18, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Dongsheng Fitness Center, mjini Ordos, Inner Mongolia, China.

Lundenga alisema utaratibu huo ulisimamishwa kutokana na zuio la serikali na wakati huo, jumla ya warembo 12 walikuwa wamekwishachukua fomu za ushiriki.

Alisema muda wa kufanya mashindano hayo, umekaribia na wanatarajia kuitangaza tarehe mpya hivi karibuni.

Mkurugenzi huyo alisema amefurahishwa na kasi ya uchukuaji na kurejesha fomu, hata hivyo wanahitaji warembo wengi zaidi ili kupata wigo mpana kwa ajili ya kumsaka mrembo atakayewania taji la Dunia, ambalo kwa sasa lina mikononi mwa mrembo kutoka Venezuela, Ivian Sarcos.

“Tunakaribia kufanya mashindano madogo hivi karibuni, hivyo ni wajibu wetu kuwakumbusha warembo wanaotaka kuwania taji hilo kufanya hivyo kabla ya Juni 4, mwaka huu ili kuweza kuingia katika mchakato wa mchujo,” alisema Lundenga.

Alisema mpaka sasa jumla ya nchi 84, zimekwishapata wawakilishi wao kwa ajili ya mashindano hayo. Nchi 32 pamoja na Tanzania bado hazijachagua wawakilishi wao katika mashindano hayo.

Lundenga alisema fomu za kuomba kushiriki zinapatikana katika ofisi za Miss Tanzania za jijini na mawakala wote wa mashindano hayo katika mikoa ya Tanzania Bara.
Posted: 30 May 2012 01:00 AM PDT

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Under The Same Sun, Bw. Peter Ash (aliyeinua kofia), akiwahimiza watoto wenye ulemavu wa ngozi (Albino), kuvaa kofia ili kujikinga na jua, alipotembelea kituo chao kilichoko Shule ya Msingi Jumuishi ya Buhangija, mkoani Shinyanga hivi karibuni. (picha na David John)
Posted: 30 May 2012 12:18 AM PDT

Na Mashaka Mhando, Tanga

MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Handeni mkoani Tanga wamesema idara za polisi na mahakama zina wajibu mkubwa wa kumaliza tatizo la utoro na mimba shuleni badala ya kuwatupia lawama watendaji wa vijiji na kata.

Wakizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika jana kwenye ukumbi wa halmashauri hiyo, madiwani hao walisema idara hizo zimekuwa kikwazo kikubwa cha tatizo la mimba katika vijiji vingi wilayani hapa hatua ambayo inachangia kuongezeka siku hadi siku.

Diwani wa Kata ya Ndolwa Bw. Joel Mabula alisema wananchi wakishirikiana na watendaji wa vijiji wamekuwa wakiwakamata wahalifu wanaosababisha mimba kwa wanafunzi, lakini wanapofikishwa katika vyombo vya sheria, kesi hizo zimekuwa zikimalizika bila hatua zozote.

“Serikali za vijiji zina makosa gani jamani? Hadi tuwekeane nao mikataba…Mwenyekiti ningeomba sasa badala ya kuwabana viongozi wa vijiji Serikali Kuu ingetusaidia kuvibana hivi vyombo vya dola watu wakikamatwa wakifikishwa polisi na baadaye mahakamani, washitakiwa wanaachiwa,” alisema Bw. Mabula.

Diwani wa Kata ya Komkonga Bw. Ramadhani Kisatu alitoa mfano wa mtu mmoja (jina tunalo) kuwa alimpa ujauzito mtoto wa shule na kisha kwenda kuishi naye katika Mji wa Kitumbi.

"Walipomkamata na kumfikisha katika Kituo cha Polisi Kabuku, mshitakiwa huyo hakuchukuliwa hatua zozote na matokeo yake yupo huru hadi leo," alidai.

Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw. Hassain Mwachibuzi akifafanua juu ya muswada uliowasilishwa na mwanasheria wa halmashauri hiyo Bw. Mohamed Msemo alisema kuwa mkataba baina ya halmashauri na watendaji utakuwa na manufaa ya ufuatiliaji kwa kuwa watendaji hao watakuwa wakiitisha mikutano shuleni itakayokuwa ikifuatilia mienendo ya wanafunzi.


Posted: 30 May 2012 12:13 AM PDT

Na Eliasa Ally, Iringa

MBUNGE wa Jimbo la Kilolo mkoani Iringa Prof. Peter Msolla amekabidhi msaada wa kompyuta tatu na vitabu vya kiada, msaada wenye thamani ya shilingi milioni tisa uliotolewa na Kampuni ya Simu Airtel Tanzania katika shule tatu za sekondari jimboni humo.

Akikabidhi msaada huo katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Sekondari Mazombe jana Prof. Msolla alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi zake katika kuendeleza elimu kwa wananchi wake.

Prof. Msolla alisema kuwa mbali ya kuwa shule hiyo ya Sekondari Mazombe haina umeme ila ametanguliza kompyuta hizo kama njia ya kuanza mkakati wa kuisaidia shule hiyo kupata umeme wa mionzi ya jua.

Alisema kuwa, shule hiyo ilikuwa ikikabiliwa na tatizo la kompyuta na kupelekea walimu kushindwa kuchapa mitihani ama kuandaa masomo yao kwa kutumia kompyuta na kuishia kuandaa mitihani na vipindi mbalimbali kwa kuandika kwa mkono jambo ambalo lilikuwa likikwamisha shughuli nyingine.

"Napenda kuipongeza sana...Kampuni ya Simu ya Airtel Tanzania kwa kusaidia maendeleo ya elimu katika jimbo langu, ndugu zangu wanafunzi na wazazi moja kati ya vipaumbele vyangu vilikuwa ni elimu na wakati nikiingia madarakani mwaka 2005 Kilolo ilikuwa na shule za sekondari tatu ila sasa tumepiga hatua na kuwa na shule zaidi ya 20, napenda kuwahakikishieni kuwa tutaendelea kupiga hatua katika maendeleo ya elimu," alisema.

Pia aliwataka wanafunzi kutumia vizuri nafasi hiyo waliyoipata kwa kuendelea kusoma kwa juhudi kubwa na kuwa katika dunia ya sasa elimu ndio kila kitu na bila elimu ni vigumu kuweza kufanikiwa
Posted: 29 May 2012 11:54 PM PDT


Na Suleiman Abeid, Shinyanga

IMEELEZWA kuwa maendeleo na mafanikio ya uchumi wa nchi yoyote duniani hutokana na wananchi wake kuwa na afya bora zinazowawezesha kufanya kazi za uzalishali mali pasipo matatizo.

Hali hiyo ilibainishwa juzi na Bw. Billie Edmott ambaye ni Ofisa wa Uchumi na Uzalishaji Mali mkoani Shinyanga katika uzinduzi wa duka namba 103 la Kampuni ya TIENS inayojishughulisha na usambazaji wa virutubisho vya mwili wa binadamu.


Bw. Edmott ambaye katika uzinduzi huo alikuwa amemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bw. Ally Rufunga alisema maendeleo ya nchi yoyote ile yanaletwa na wananchi wenye afya na kwamba wakiwa na afya zenye mgogoro haitokuwa rahisi kwao kufanya kazi kwa ufanisi.

Alisema, Watanzania wengi hufanya kazi zao katika mazingira magumu, lakini hata hivyo baada ya kazi hizo huwa hawapimi afya zao ili kuweza kubaini jinsi gani viungo vyao vimetumika ili viweze kuboreshwa kwa kupatiwa virutubisho.

“Uchumi wa nchi yetu hutegemea sana kilimo na asilimia 85 ya Watanzania ni wakulima ambao wapo vijijini, kwenye maeneo ya uzalishaji wa mazao mbalimbali. Sasa ili maendeleo yapatikane inatakiwa wakulima hawa wa vijijini wapate huduma ya kupima afya zao kila wakati ili waweze kuwa na afya bora,” alisema Bw. Edmott.
Posted: 29 May 2012 11:44 PM PDT


Na Zahoro Mlanzi

BENDI ya muziki wa dansi ya Mashujaa, imetangaza rasmi kumnasa Meneja wa African Stars (Twanga Pepeta), Matrin Sospeter kujiunga na bendi hiyo.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Rais wa bendi hiyo, Charles Gabriel 'Chalz Baba' alisema ana furaha kuona kiongozi huyo amejiunga nao na ana imani itazidi kufanya vizuri katika anga ya muziki wa dansi.


Alisema amefanya kazi na kiongozi huyo kwa miaka sita akiwa Twanga Pepeta, hivyo anamfahamu vizuri kutokana na kujituma kwake kazini na hata nje ya kazi.

"Nina furaha kubwa kukutana tena na Sospeter katika kazi, nina imani tutaisukuma vizuri bendi yetu kutoka hapa ilipo na kusogea mbali zaidi ili kuzidi kuliteka soko la muziki wa dansi," alisema Chaz Baba.

Naye Sospeter alisema ameondoka Twanga kwa ridhaa yake bila kushawishiwa na mtu na kwamba anaishukuru familia ya Asha Baraka (Mkurugenzi wa Twanga Pepeta) kwa muda wa miaka 14 aliokaa nao katika bendi hiyo.

Alisema ameondoka Twanga si kwa lengo la kuipa wakati mgumu bendi hiyo, ila kwa ajili ya maendeleo ya muziki wa dansi ili kuongeza ushindani zaidi miongoni mwa bendi za muziki huo.

Meneja huyo alisema hana kinyongo na Asha, kwani ndiye aliyemfanya afike hapo na kwamba anawaomba mashabiki wa Mashujaa kumpa ushirikiano.

Wakati huohuo, Chaz Baba pia alizungumzia ujio wa nyimbo zao mpya ambazo ni Risasi Kidole, Dunia ya mola, Thamani ya mtu na Usidharau sifuri kwamba zitakuwa ni moto wa kuotea mbali hivyo mashabiki wao wakae mkao wa kula.
Posted: 29 May 2012 11:40 PM PDT

Na Salma Mrisho, Geita

IMEELEZWA kuwa mazingira magumu ya kazi yanayowakabili wauguzi hususan upungufu wa watumishi wa kada hiyo na malipo kidogo ni mojawapo ya changamoto zinazowafanya kutowajibika ipasavyo katika kazi zao.

Hayo yalibainishwa hivi karibuni kwenye kongamano la siku mbili na mkutano wa 12 wa Chama cha Wauguzi (TANNA) Mkoa wa Shinyanga ulioenda sambamba na kuwaaga baadhi ya wauguzi waliohamishiwa mikoa ya Geita na Simiyu.

Mgeni rasmi katika kongamano hilo Bi. Liliani Matinga ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bukombe aliwaomba wauguzi hao waendelee na umoja wao pamoja na baadhi ya wilaya kugeuzwa mikoa mipya.

"Ni vyema sasa kila mmoja akafanye kazi huko anakoenda kwa kuwajibika na kuwa kitu kimoja, ili kuepusha jamii kuwalalamikia kuwa hamfanyi kazi ipasavyo ingawa changamoto ya kufanya kazi katika mazingira magumu bado ipo," alisema Bi. Matinga.

Alisema, anatambua kazi ya uuguzi kuwa ni ngumu, lakini aliwapongeza na kusema baadhi ya uharibu muonekano mzuri wa fani hiyo kwa kuwatukana wateja wao na kuomba rushwa jambo ambalo limekuwa likilalamikiwa kila siku na wananchi wanoenda kupata huduma.
Posted: 29 May 2012 11:39 PM PDT


Na Mwandishi Wetu, Mtwara

CHAMA cha NCCR-Mageuzi mkoani Mtwara kimevuna wanachama wapya 2,517 katika Jimbo la Mtwara Mjini.

Takwimu hizo zilitolewa jana na Mjumbe wa Halmashauri ya chama hicho Bw. Danda Juju alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa.


Alisema kuwa, idadi hiyo imepatikana kuanzia Machi hadi Mei mwaka huu kutokana na jitihada za uhamasishaji ambazo zimekuwa zikifanywa na viongozi wa kitaifa na wa jimbo hilo.

“Chama kinazidi kushika kasi, tumekuwa tukivuna wanachama kila kunapokucha kwa sababu wananchi wanajua NCCR-Mageuzi ndicho chama makini kitakachoweza kuwakomboa.

“Nasema hivyo kwa sababu tangu Machi mwaka huu tulipofanya ziara ya kitaifa mjini hapa, tumeshaingiza wanachama 2,517 na idadi hii itazidi kushika kasi kwa sababu wananchi wa Mtwara wameshaamka, wananchi wa Mtwara wanataka mageuzi kutokana na kuichoka CCM,” alisema  Bw. Juju.

Kwa mujibu wa Juju ambaye pia ni Msaidizi Mkuu wa Mwenyekiti wa chama hicho Bw. James Mbatia alisema wanachama wanaojiunga na chama chao wanatoka Chama cha Wananchi (CUF), wengine Chama cha Mapinduzi (CCM) na CHADEMA.

“Hatutaki mzaha wakati huu, lengo letu ni kuhakikisha tunaifukuza CCM, tunataka Mtwara Mjini na Mtwara kwa ujumla wake, iwe ngome ya NCCR-Mageuzi kwani tunaamini hilo litawezekana kutokana na kasi tuliyonayo.

“Kama tuliweza kuibadilisha Kigoma na kuwa ngome ya NCCR-Mageuzi, kwa nini Mtwara na Mkoa wa Lindi ishindikane? Hilo haliwezekani, lazima tupambane hadi dakika ya mwisho na mbinu tulizotumia kuikomboa Kigoma ndizo hizo hizo tutakazotumia kulikomboa Jimbo la Mtwara Mjini,  Mkoa wa Mtwara na Lindi.
Posted: 29 May 2012 11:36 PM PDT


Na Allan Ntana, Tabora

KATIBU Mwenezi wa CHADEMA Bw. Ali Mwakilima amewataka wananchi kutobweteka na ulaghai wa CCM pindi unapokuja uchaguzi kwa kuwahadaa kwa fulana, kofia na kanga.

Kauli hiyo aliitoa juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika
Kijiji cha Igunda Kata ya Ifucha, Manispaa ya Tabora ambako kulikuwa na
mkutano wa CHADEMA.


Bw. Mwakilima alisema inashangaza kuona wananchi wanafikia wanafikia hatua wanadanganyika na vitu hivyo na baada ya ghiliba hiyo wanatamka CCM imewalea.

”Mkitaka kujiridhisha na hilo kuwa watendaji na mabalozi nao hawaijui Katiba...ni pale mtendaji anapohojiwa juu ya haki za msingi za raia na kuwa mkali. Hiyo ni kiashirio tosha kwamba nao Katiba ya nchi hawaijui,” aliongeza.

Aliwataka wananchi kuwa makini na michango isiyo ya lazima na kusema kwamba michango inakuwa mingi, lakini huduma zinakuwa mbovu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA Bw. Saimon Lameck aliwaomba wananchi kwenye mkutano huo waichague CHADEMA kwani ni chama kitakachoweza kuleta mageuzi na huduma za kweli.

”Ukitaka kujua hali sasa ni tete na ngumu angalia kijana wa miaka 30 utadhani ana umri wa miaka 70, hiyo ni kutokana na gharama za maisha kupanda kila kukicha halafu ndugu zangu mnajitapa kuwa CCM imewalea, badilikeni,”  alisema.
Posted: 29 May 2012 11:34 PM PDT


Na David John, Aliyekuwa Mwanza

IMEELEZWA kuwa jamii ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini Albino wana uwezo mkubwa wa kufanya kazi katika sekta mbalimbali iwapo watawezeshwa ili kuhaakisha maendeleo.

Hayo yalielezwa hivi karibuni mkoani Mwanza na Bi.Vicky Ntetema ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Under The Same Sun hapa nchini, baada ya kutembelea mikoa ya Kanda ya Ziwa ili kujionea changamoto zinazowakabili watu hao.


Alisema, kuna haja kupinga mawazo ama fikra potofu ambazo zimejengeka katika vichwa vya Watanzania kwamba watu wenye ulemvu wa ngozi hawana uwezo wa kufanya kazi na kupelekea kunyimwa fursa katika maeneo mbalimbali wanayokwenda kuomba kazi.

"Kuna changamoto kubwa, kwa watu wenye ulemavu wa ngozi kuweza kukubalika katika jamii na hasa pindi wanapokwenda kuomba kazi katika maeneo tofauti ambapo wanakutana na vikwazo vingi hasa kuonekana kama hawana uwezo mbali na elimu waliyokuwa nayo," alisema.

Alisema, moja ya changamoto zinazowakabili walemavu wa ngozi ni kutokukubalika vema na kuonekana kama wao ni watu watofauti ambao hawawezi kufanya lolote katika jamii kitu ambacho kinawakosesha amani na kuonekana wanatengwa katika nchi yao.

Kwa upande wa elimu darasani alisema, walimu wanapaswa kuwa karibu na watu hao ikiwa pamoja na kuonesha upendo wa hali ya juu pia kuepuka kutoa adhabu ambayo inatokana na kufanya vibaya kwa mwanafunzi mlemavu darasani.

"Najua kuna taasisi nyingi hapa nchini na zinasaidia katika maeneo mengi, lakini binafsi naomba tujikite zaidi katika kuwasaidia watu hawa," alisema.
Posted: 29 May 2012 11:31 PM PDT

Na Suleiman Mbuguni

BAADA ya wanachama wa Yanga, kushinda vita ya kumwondoa Mwenyekiti wa klabu hiyo madarakani na kutakiwa kufanya uchaguzi mdogo Mwenyekiti aliyeondoka kabla ya uongozi huu, Imani Madega amesema ili klabu hiyo kongwe ifanikiwe ni lazima kufanyike marekebisho ya katiba.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Madega alisema katiba hiyo mpya ndiyo itakuwa suluhisho lililobaki pekee na ili klabu hiyo ifanikiwe ni lazima idadi ya Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ipungue kutoka 13 hadi kufikia sita na Mwenyenyekiti atatakiwa kuwa na kura ya veto.

Alisema katika idadi ya wajumbe hao italazimika watatu wawe wa kuchaguliwa na wanachama, na mmoja ateuliwe na Mwenyekiti ambaye atakuwa na mamlaka kutokana na kuwa kura ya veto.

"Kwa hiyo baada ya marekebisho hayo wanachama watatakiwa kuwachagua Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, wajumbe watatu na mjumbe mmoja atateuliwa na Mwenyekiti ambaye atakuwa na kura ya veto.

"Kwa kufanya hivyo itakuwa imepunguza idadi kubwa ya wajumbe ambao wengine mara nyingi wanakuwa hawana kazi ya kufanya, isipokuwa wanasubiri mikutano ya klabu pekee litu ambacho kinaleta majungu wenyewe kwa wenyewe," alisema Madega.

Alisema baada ya mchakato huo, viongozi hao watatakiwa kulipwa kwa mujibu wa sheria za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), ambalo hulipa viongozi wake akiwemo Rais Sepp Blatter.

Madega alisema hatua hiyo ya kuwalipa viongozi mishahara itaongeza uwajibikaji na kuondoa majungu, kwani haiwezekani mchezaji akawa wa kulipwa alafu kiongozi wa ridhaa.

"Haiwezekani hata kidogo kiongozi akawa wa kujitolea, alafu anahaha kumtafutia mchezaji mshahara wa sh. milioni 5, wakati nyumbani kwake hajaacha kitu hivyo ni lazima mfumo huu ubadilike kama kweli tunataka klabu zetu zipige hatua hatuwezi kuwa na mifumo miwili tofauti ndani ya klabu moja," alisema Madega.

Alisema hatua hiyo ya kuwalipa mishahara viongozi, itawaletea heshima kwa wanachama kwani hivi sasa kiongozi akiendesha gari anaonekana amelipata kupitia klabu, lakini kwa mfumo huu utaondoa dhana hiyo.

Kiongozi huyo alisema hatua nyingine muhimu ni kupunguza idadi ya wanachama wa kuingia katika mikutano ya klabu kwani sasa Yanga inakadiriwa kuwa na wanachama zaidi ya 10,000, ambao ni tatizo kama wakifika wote katika Mkutano Mkuu.

Madega alisema hakuna ulazima wa kuwakutanisha wanachama wote katika mikutano kwa kuwa si wote wanaochangia hoja, bali wengine hufuata mkumbo na kuanzisha majungu yasiyokuwa na maana.

"Si lazima wanachama wote wakaingia katika mikutano, wanaweza wakachaguliwa wawakilishi watatu kutoka kila tawi. Kwa mfano akawemo Mwenyekiti, Katibu na Mjumbe mmoja wa kuchaguliwa katika tawi husika.

Mfumo huo hautakuwa tofauti na vyama vya siasa ambavyo hutumia wajumbe maalumu kuingia katika mikutano yao kujadili mambo yao, kwani kama vingeamua kutumia wanachama wake wote ingekuwa ni tatizo kutokana na wingi wao nchi nzima," alisema.

Klabu hiyo inatarajia kufanya uchaguzi mdogo Julai 15, mwaka huu kutokana na baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kujiuzulu pamoja na Mwenyekiti wake Nchunga.
Posted: 29 May 2012 11:21 PM PDT

Na Zahoro Mlanzi

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Kim Poulsen amesema uwezo binafsi wa wachezaji Didier Drogba na Yahya Toure wa Ivory Coast utawapa wakati mgumu katika mechi ya Jumamosi itakayopigwa jijini Abidjan.


Mbali na hilo, Kim ameahidi kufa au kupona pindi watakapokutana nao licha ya kwamba wapinzani wao wana wachezaji wengi wanaocheza ligi kubwa barani Ulaya.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Kim alisema anaiheshimu Ivory Coast kutokana na aina ya wachezaji iliyonayo, lakini kikubwa katika mechi ya Jumamosi atahakikisha wanacheza soka la uhakika.

"Nadhani hakuna asiyewajua akina Drogba, Toure na Kalou (Salomon) ni wachezaji wazuri Ulaya kutokana na kuwa fit kiuchezaji, hivyo tunatakiwa kujituma zaidi ili kupata matokeo mazuri," alisema Kim na kuongeza;

"Drogba na Toure wana 'massive indivudual powers' (nguvu kubwa binafsi) ambayo huweza kusababisha matokeo ya aina yoyote uwanjani na ndiyo maana ninawaheshimu kwa hilo."

Akizungumzia kuhusu upungufu wa kikosi chake, Kim alisema kina ukosefu wa nguvu (fitness) ambapo kwa muda uliobaki wa siku nne kabla ya kukutana na Ivory Coast, hawezi kurekebisha hilo ila atajitahidi wacheze soka la kiushindani.

Alisema watatumia mbinu za kulinda na kutawala mchezo ambapo mbinu hiyo itawafanya wawe na nafasi ya kutengeneza nafasi za kufunga.

Wakati huohuo, Kim alimwagia sifa kiungo Mrisho Ngassa kwa kusema sasa anaonekana kubadilika na kucheza kama alivyokuwa akicheza awali.

"Ngassa amefanya kazi kubwa katika mechi dhidi ya Malawi, kiwango kile sijakiona akicheze kwa muda mrefu hivyo ni mabadiliko makubwa kwake na ametambua thamani yake akiwa na timu ya taifa," alisema Kim.

Katika hatua nyingine, Kim aliliomba Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuwa na mpango maalumu kwa wachezaji wa Ligi Kuu wawe na kiwango fulani cha nguvu (fitness) ili wakiwa Taifa Stars wasipate shida.

Kikosi hicho cha Stars kilipanga kuondoka nchini leo kwenda jijini humo kwa ajili ya mechi hiyo ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2014, zitakazofanyika nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment