TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, June 13, 2012

MBUNGE MBALONI


Posted: 05 Jun 2012 01:20 AM PDT

Mbunge wa Bahi (CCM), Bw. Omary Ahmed Badwel, akiwa chini ya ulinzi wa polisi wakati akifikishwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam jana kwa ajili ya kusomewa mashitaka yanayomkabili ya kukamatwa juzi na maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), akituhumiwa kuomba na kupokea rushwa. (Na Mpigapicha Wetu)
Posted: 05 Jun 2012 01:16 AM PDT



Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Bw. Steve Kilindo (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Bw Raymond Mushi, msaada wa vifaa vya usafi kwa ajili ya Manispaa ya Ilala, wakati wa uzinduzi wa Wiki ya Mazingira Duniani, Dar es Salaam jana. (Na Mpigapicha Wetu)

Posted: 05 Jun 2012 01:12 AM PDT
Ofisa Mkuu wa Biashara wa Kampuni ya Simu za mkononi ya Zantel Bw Ahmed Mokhles akionesha katika runinga moja ya huduma mpya ya Epiq Moto kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam juzi, huduma itakayowawezesha wateja kupiga simu kwa mitandao yote kwa Sh.1 kwa sekunde kwa saa 24 na kutuma sms kwa Sh. 25, pia mteja wa kampuni hiyo atapewa megabaiti 50 za intaneti bila malipo. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 05 Jun 2012 01:10 AM PDT

Mwenyekiti wa Chama cha Kupambana na Dawa za Kulevya na Ulevi, Tanzania (IOGT), Bw. Mohamed Lichonyo (kushoto) akizungumza na vijana wa chama hicho kutoka Shule ya Sekondari Tuliani Kinondoni walipowatembelea vijana wa Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki ili kujifunza shughuli za ulinzi shirikishi polisi jamii. (Picha na Charles Lucas)
Posted: 05 Jun 2012 01:05 AM PDT

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Bi. Sophia Simba (aliyeketi) akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Bw. Joshua Nassari, walipokutana kwenye Kamati za Bunge zinazoendelea, Dar es Salaam jana. (Picha na Peter Mwenda)
Posted: 05 Jun 2012 01:02 AM PDT

Mkuu wa Mahusiano wa Benki ya Standard Chartered, Bi. Juanita Mramba (aliechuchuma katikati) akiongoza wafanyakazi wa benki hiyo kupanda miti katika Kata ya Kivukoni wakati wa kuazimisha wiki ya mazingira Dar es Salaam jana. (Na Mpigapicha Wetu)
Posted: 05 Jun 2012 01:03 AM PDT
Wafanyakazi wa Exim Bank wakichangia damu salama jana, jijini Dar es salaam.(Picha na Mpigapicha wetu)
Posted: 05 Jun 2012 12:13 AM PDT
Mnyange wa Redd's Miss Tabata, Noella Michael anayapungia mkono baada ya kutangazwa mshindi katika mashindano hayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Dar West Tabata juzi.(Picha na Victa Mkumbo)
Posted: 05 Jun 2012 12:03 AM PDT

Na Andrew Ignas

MAANDALIZI ya safari ya Bondia wa timu ya Taifa ya ngumi za riadha Suleiman Kidunda(Kg 69) yapo katika hatua mzuri na anatarajiwa kuondoka kesho.

Akizugumza na Majira jana Dar es salaam jana Rais wa Shirikisho hilo Michael Changalawe alisema maandalizi ya safari ya Bondia ambaye anatarajia kuondoka nchini kesho kuelekea nchini Uigereza kwaajili ya kushiriki michuano ya Olimpic itakayoanza julai 27-Agosti 12 mwaka huu yamefikia katika hatua nzuri.

"Taratibu zote zinaendelea vizuri na hivyo hata hali ya bondia wetu ambaye yupo katika kambi ya Shule ya Filbert Bayi Mkoani Pwani,Kibaha ni nzuri"alisema Changalawe.

Alisema kuwa kambi ya bondia huyo ambaye atakwenda kuiwakilisha nchi katika michauno hiyo ya Olimpiki inayotarajia kushirikisha zaidi ya nchi 184 ipo chini ya kamati ya Olimpiki ambayo inaongozwa na Filbert Bayi.

Wakati huo huo Kocha wa timu ya Taifa ya ngumi za riadha Remy Ngabo alisema anafurahishwa sana na kiwango anachokionyesha kinara wa Masumbwi kwa timu hiyo.

"Natumaini  kupata medali kwani uwezo ambao anauonesha Kidunda unanipa faraja hivyo tumuombee dua kwa siku zilizobakia aepushiwe magonjwa."alisema Ngabo.

Posted: 05 Jun 2012 12:02 AM PDT

Posted: 04 Jun 2012 11:58 PM PDT

Na Victor Mkumbo
DROO ya tano ya shindano la Vumbua Hazina Chini ya Kizibo, imechezeshwa jana ambapo washindi wengine wawili wamepatikana.

Droo hiyo inaendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL), ambapo pia itachezeshwa kwa muda wa wiki 16 mfululizo huku washindi mbalimbali wakijinyakulia zawadi.

Washindi waliopatikana katika droo hiyo ni Isaya Charles kutoka Igoma mkoani Mwanza ambaye amejishindia Jenereta, wakati mshindi mwingine Mariam Karumba mwanafunzi wa mwaka wa tatu Chuo Kikuu cha Saint Agustin pia anatoka mkoani Mwanza amejishindia Bajaj.

Akizungumza katika  hafla ya fupi iliyofanyika jana, Meneja Masoko wa SBL, Ephraim Mafuru, alisema kuwa wameanzisha droo hiyo kwa ajili ya kutoa zawadi mbalimbali kwa wateja wao.

Alisema kuwa droo hiyo inachezeshwa wiki nzima ambapo dhumuni lao kubwa ni kuibua kipato cha Watanzania pamoja na kuwapa ajira.

Alisema washindi mbalimbali wameshapatikana katika mikoa ya Tanzania Bara ambapo pia baadhi yao wameshapewa zawadi zao walizoshinda.

Mafuru alizitaja baadhi ya zawadi ambazo zinashindaniwa kuwa ni bajaj, pikipiki, jenereta, fedha taslim pamoja na gari.

Posted: 04 Jun 2012 11:54 PM PDT
Wazee wa Kamati ya Muafaka ya Yanga wakiwa nyumbani kwa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Davis Mosha Mikocheni kwa ajilin ya kumpa pole baada ya kufiwa na Baba mkwe wake Mzee Malick Said Kiongoli.Mazishi yake yanatarajiwa kufanyika kesho nyumbani kwake Kibaha,Pwani.(Picha na Elizabeth Mayemba)
Posted: 04 Jun 2012 10:16 PM PDT


Na Elizabeth Mayemba

ALIYEKUWA Makamu  Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Davis Mosha amesema kwamba hayupo tayari kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya klabu hiyo katika uchaguzi mdogo wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika Julai 15, mwaka huu.


Mosha alitoa kauli hiyo wakati Wazee wa muafaka wa klabu hiyo wakiongozwa Katibu wake Ibrahim Akilimali walipoenda kumpa pole baada ya Alhamisi kufiwa na baba mkwe wake mzee Malick Said Kiongoli, ambapo pia walitumia fursa hiyo kumshauri mpiganaji huyo ili agombee nafasi moja wapo katika uchaguzi huo.

"Kwanza kabisa nawashukuru sana wazee wangu kwa kuja kunifariji katika kipindi hiki kigumu cha kufiwa na baba mkwe wangu Mzee Malick, na ombi lenu la kutaka nirudi kuiongoza Yanga nimelisikia lakini sitakuwa tayari kufanya hivyo,ila naomba niwaahidi kitu kimoja kuwa mimi ni mwanachama wa Yanga na mwenye mapenzi ya dhati na timu hiyo, nitakuwa tayari kutoa msaada wowote kwa timu hata kama nitakuwa nje ya uongozi," alisema Mosha

Alisema anashukuru kwamba wazee hao wametumia busara na hekima kubwa kwani tangu ajiuzulu wadhifa huo hakuwahi kukutananao, lakini juzi ndiyo kwanza amewaona hivyo hapuuziii ombi lao lakini kwa sasa hatakuwa tayari kuongoza Yanga lakini atakuwa bega kwa bega na timu hiyo.

Mosha alisema kuwa sasa timu hiyo inakabiliwa na michuano ya kombe la Kagame anachoahidi kwa wazee hao ni kushirikiana nao na kuhakikisha timu yao itatetea ubingwa wake ikiwa na kusajili wachezaji bora ambao watawaletea ubingwa.

Pia amewataka wanachama wa klabu hiyo kuwa makini katika kuchagua viongozi, wawachague wale ambao wanamapenzi mema na klabu na pia wenye uwezo kifedha na si wale ambao watataka kuja Yanga ili wanufaike na mapato ya milangoni.

"Chagueni viongozi ambao angalau watakuwa wanauwezo kifedha na hata kiuongozi, sio wale viongozi ambao wanategemea kujiendesha kupitia fedha za Yanga," alisema

Naye Mzee Ibrahim Akilimali alisema kuwa wanatambua kuwa Mosha ni mpiganaji kwani baada ya kujiuzulu alihakikisha anaisaidia timu hiyo na hatimaye ilitwaa ubingwa wa bara msimu uliopita, na ndio maana waaona watumie nafasi hiyo kumshawishi arudi tena Yanga.

"Hakuna ambaye hajui kuwa Mosha ni mpiganaji kila mwanayanga anajua hilo na ndio maana tukatumia fursa hii ili kumshawishi agombee, lakini ilimradi ametuahidi kuendelea kutusaidia hilo tunampongeza sana na sisi tunamuombea kwa Mungu afanikiwe hilo," alisema Akilimali.
Posted: 04 Jun 2012 10:14 PM PDT
Na Andrew Ignas


KAMATI ya utendaji ya Chama cha Riadha Mkoa wa Dar es salaam(DAA),imesema kikosi cha timu ya riadha kinaendelea vizuri na mazoezi.

Akizungumza  Dar es salaam jana Katibu wa chama hicho Lucas Nkungu, alisema kikosi cha timu ya Riadha ya Mkoa wa Dar es salaam kinaendelea kujinoa vyema kwaajili ya kuchuana na klabu mbali mbali za mkoa huu kwa ajili ya mashindano maalum yaliyopangwa kufanyika Juni mwaka huu.


"Hali ya maandalizi yanakwenda vyema na inatoa dira ya kikosi kuchuana vikali na klabu zitakazojitokeza kushiriki mashindano hayo maalum kwa ajili ya kuinoa timu hiyo  tayari wakati wa mashindano ya taifa yanayokuja"alisema Nkungu.

Alisema wanariadha hao wanatakiwa kufanya mazoezi kwa bidii ili kuhakuikisha wanafanya vizuri zaidi katika mashindano hayo na anaimani watafanya vizuri.

"Nakiamini kikosi changu hivyo wanariadha wanatakiwa kujituma ili wafanye zaidi, hata hivyo nawaamini sana kwani ni wazoefu,"alisema

No comments:

Post a Comment