TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, June 8, 2016

LEAT YAWATAKA WANANCHI KUHIFADHI MAZINGIRA NA MALIASILI

Mkuu wa wilaya ya Wanging'ombe Asumpta Mshama akihutubia wananchi wakati wa sherehe za siku ya mazingira duniani, katika kijiji cha Lugodalutali, wilaya ya Mufindi.
kikundi cha sanaa kutoka kijiji cha mapogoro kikihamasisha utunzaji wa mazingira na maliasili ktk sherehe za siku ya mazingira zilizo fanyika tarehe 3 June 2016 kijijini Lugodalutali. Kikundi hiki kinalelewa na Timu ya Wanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT).
LEAT yagawa vitabu na vipeperushi vinavyotoa elimu ya mazingira na maliasili.


"Maeneo mengi ya mijini yamechafuliwa kwa utupaji taka ovyo, hivyo kuharibu mandhari ya miji yetu na kuchangia katika magonjwa ya milipuko ikiwemo kuhara na kipindupindu, alisema Kasuga.Alisema, utupaji taka ngumu na zenye sumu karibu na makazi ya watu au vyanzo vya maji, umeleta athari kubwa kiafya kwakuwa kemikali hizo hupenya ardhini na kudhuru ardhi na vyanzo vya maji, hasa kwa wananchi wanoishi karibu na viwanda na sehemu za uchimbaji madini.

“Inasikitisha kuwa wamiliki wa viwanda vingi na machimbo ya madini wanakiuka sheria ya mazingira lakini pia wameshindwa kuwajibika kwa jamii zinazo wazunguka ambazo ndio wadau wakubwa wa biashara zao, kwa kaidi kuchukua hatua za kuzuia uharibifu wa mazingira hata baada ya athari kutokea”, alisema Jowika

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Wanging’ombe Asumpta Mshama alisema kuwa shirika la LEAT limekuwa mstari wa mbele kwa zaidi ya miaka 20, katika kusimamia mazingira nchini katika sekta ya madini, viwanda, machinjio na mazingira kwa ujumla.Asumpta alisema taarifa ya Shirika la Afya Duniani (WHO) iliyotolewa mwezi Aprili, 2016 inaonesha takribani watu milioni 2 hufa kila mwaka duniani na zaidi ya watu bilioni moja hupatwa na magonjwa yanayo sababishwa na uchafuzi wa mazingira.

No comments:

Post a Comment