TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, October 1, 2014

TANZANIA, ZAMBIA, NA KENYA ZASAINI MKATABA KUJENGA MIUNDOMBINU YA UMEME.

1Mawaziri wanaoshughulikia Nishati kutoka nchi za Zambia, Tanzania na Kenya wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi hizo kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme na kufanya biashara ya kuuziana umeme wa ziada baina ya nchi hizo. Mkataba huo umesainiwa jijini Dar es Salaam leo na Waziri wa Nishati na Madini Tanzania, Profesa Sospeter Muhongo (katikati), Waziri wa Wizara ya Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , Christopher Yaruma (kushoto) na Waziri wa Nishati na Petroli Kenya , Davis Chirchir (kulia) . Wanaoshuhudia kutoka kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Migodi , Nishati na Maendeleo ya Maji Zambia, Charity Mwansa, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini , Tanzania , Eliakim Maswi na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Petroli Kenya, Mhandisi Joseph Njoroge.
2Mawaziri wanaoshughulikia Nishati kutoka nchi za Zambia, Tanzania na Kenya , Waziri wa Wizara ya Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , Christopher Yaruma (kushoto) Waziri wa Nishati na Madini , Profesa Sospeter Muhongo Tanzania (katikati) na Waziri wa Nishati na Petroli Kenya, Davis Chirchir (kulia) wakibadilishana Mkataba wa Makubaliano kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi hizo kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme na kufanya biashara ya kuuziana umeme wa ziada baina ya nchi hizo mara baada ya kusaini.
3Mawaziri wa wanaoshughulikia Nishati kutoka nchi za Zambia, Tanzania na Kenya , Waziri wa Wizara ya Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , Christopher Yaruma (kushoto) Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo Tanzania (katikati) na Waziri wa Nishati na Petroli Kenya, Davis Chirchir (kulia) wakionesha Mkataba wa Makubaliano mara baada ya kusaini.
4Sehemu wa wadau walihudhuria hafla ya kusaini Mkataba wa Makubaliano kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi za Zambia, Tanzania na Kenya kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme na kufanya biashara ya kuuziana umeme wa ziada baina ya nchi hizo. Mbali na Wataalamu kutoka katika nchi hizo, hafla hiyo imehudhuriwa uwakilishi wa COMESA, Mashirika ya Umeme kutoka nchi hizo na baadhi ya washirika wa Maendeleo wakiwemo Benki ya Dunia, Umoja wa Ulaya, Ubalozi wa Norway, Shirika la Maendeleo la Japani (JICA), African Development Bank (AfDB), Ubalozi wa Ufaransa.  
Asteria Muhozya, Dar es Salaam Nchi za Zambia, Tanzania na Kenya zimesaini Mkataba wa Makubaliano kuonesha dhamira ya Serikali ya nchi hizo kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme (ZTK) na kufanya biashara ya kuuziana umeme wa ziada baina ya nchi hizo na nchi nyingine barani Afrika. Akiongea katika hafla hiyo Waziri wa Nishati na Madini, Tanzania Profesa Sospeter Muhongo ameeleza kuwa, mradi huo wa pamoja unalenga kuondoa tatizo la upungufu wa nishati ya umeme baina ya nchi hizo na nchi nyingine barani Afrika jambo ambalo litachangia katika kukuza uchumi wa mataifa hayo. Naye, Waziri wa Migodi, Nishati na Maendeleo ya Maji wa Zambia , Christopher Yaruma ameeleza kuwa, utekelezaji wa mradi huo sio tu utaziwezesha nchi hizo kufanya biashara bali pia utafungua fursa za uwekezaji na kusaidia katika kuondoa umaskini miongoni mwa nchi wanachama kutokana kuzitumia fursa mbalimbali zinazotokana na nishati ya umeme. Kwa upande wake Waziri wa Nishati na Petroli Kenya, Davis Chirchir amewataka washirika wa maendeleo kusaidia katika kuwezesha utekelezaji wa mradi huo wa kujenga miundombinu ya pamoja ya kusafirisha umeme baina ya nchi hizo kutokana na manufaa yake kwa bara la Afrika na kuongeza kuwa, kutokana na uwepo wa rasilimali asilia za kutosha katika nchi hizo hakuna sababu ya kuwepo tatizo la nishati katika nchi hizo na barani Afrika. Naye, Katibu Mkuu Msaidizi wa Jumuiya ya Soko la pamoja la nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika anayeshughulikia miradi (COMESA), Dkt. Kipyego Cheluget amezipongeza nchi hizo kwa kuuendeleza utekelezaji wa mradi huo ambao umechukua kipindi kirefu na kuueleza kuwa, ni miongoni mwa miradi 16 ya kipaumbele na kimaendeleo kwa Afrika. Aidha, kwa upande wao Washirika wa maendeleo waliohudhuria hafla hiyo, wameonesha kufurahishwa kwao na dhamira ya nchi hizo na kuahidi kushirikana na nchi hizo kuhakikisha mradi huo unatekelezwa. Miongoni mwa washirika wa maendeleo waliohudhuria ni pamoja na uwakilishi wa Umoja wa Ulaya, Benki ya Dunia, Ubalozi wa Norway, Shirika la Maendeleo la Japani (JICA), African Development Bank(AfDB) na Ubalozi wa Ufaransa.

PROFESA SOSPETER MUHONGO ASAINI MKATABA WA MRADI WA KUUZIANA UMEME KATIA YA ZAMBIA, TANZANIA NA KENYA.

muhongoWAZIRI wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo jana ametia saini Mkataba wa Mradi kujenga Miundombinu ya kuuziana umeme kati ya Zambia, Tanzania na Kenya (ZTK) katika Mkutano  wa Kumi wa kujadili mradi huo.
Katika utiaji saini Mkataba huo, Profesa Muhongo alisema kuwa mchakato wa kuandaa Mkataba wa mradi huo ulikwishafanyika tangu mwaka 2001 ambapo ulikuwa na vipengele ambavyo kwasasa Mawaziri wa Nishati toka nchi zote tatu wameupitia na umefanyiwa marekebisho. 
Profesa Muhonga alisema kuwa katika marekebisho hayo wamebadili kipengele kilichokuwa kinaeleza juu ya uwepo wa Ofisi moja itakayosimamia mradi huo katika nchi zote tatu, na badala yake wamekubaliana kuwa kila nchi ijisimamie yenyewe badala ya kuwa na Ofisi moja pekee itakayosimamia mradi huo.
“Kwa upande wa Tanzania ujenzi wa mradi huu umeshaanza kazi na mpaka hivi sasa asilimia 90 ya vifaa vya ujenzi wa mradi vimeshawasili katika eneo la ujenzi,”alisema Profesa Muhongo.
Akizungumzia maeneo ambayo mradi huo utapita kwa upande wa Tanzania, Profesa Muhongo alisema kuwa, mradi huo utapita maeneo ya mikoa ya Singida- Arusha-Namanga, na Namanga-Isinya kwa Kenya, kwa upande wa Zambia utapita Mbeya–Iringa na Iringa-Singida-Shinyanga. Ambapo unatarajia kusambaza umeme wa kuanzia 400kV.
Naye Katibu Mkuu wa Nishati nchini Kenya, Mhandisi Joseph Njoroge  alisema kuwa muungano huo wan chi tatu utasaidia kupunguza tatizo la umeme katika nchi zote na Afrika kwa ujumla kwani utapunguza gharama ya umeme pamoja na kuongeza ukuaji wa uchumi katika uzalishaji.
Aidha aliongeza kuwa Serikali yake itahakikisha kuwa Mkataba huo ndani ya siku Thelathini zijazo kabla ya mkutano ujao kuanza, Mwanasheria Mkuu wa Kenya atakuwa umekwisha usaini.
Kwa upande wake Waziri wa Nishati na Madini nchini Zambia, Mh. Christopher Yaruma alisema kuwa nchi yake imeshasaini Mkataba wa kuonyesha dhamira ya kuuziana umeme na nchi ya Malawi, Namibia na Botswana.
Utiaji saini wa Mkataba huo ulihusisha wadau mbalimbali wa maendeleo na wafadhili ikiwemo JICA, COMESA, EU, Korea, Benki ya Dunia, AFD, Ufaransa na Mabalozi wa nchi mbalimbali, ambapo wadau hao wameonyesha nia ya dhati katika kuendelea kuisaidia Serikali hususani katika sekta ya Nishati.
Sambamba na hilo, mkutano wa mwendelezo wa mradi huo badaa ya kuwa umesainiwa na viongozi wa Sheria katika nchi husika unatarajiwa tena kufanyika mwanzoni mwa mwezi wa Kumi na moja nchini Lusaka, Zambia.

PROGRAMU YA KUFUNDISHA HISABATI KWA KUTUMIA SIMU ZA MKONONI YAZINDULIWA DAR ES SALAAM

  Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, John Mgodo akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mtaalamu wa mradi huo kutoka Kampuni ya Nokia, Riita Vanska. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)
 Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez akizungumza katika uzinduzi huo. Kampuni ya Tigo, Nokia na Microsoft ndio wadau  mpango huo.
Meneja Mawasiliano wa Microsoft Mobile Devices, Lilian Nganda akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na 
Teknolojia Dk.Hassan Mshinda akizungumza katika 
uzinduzi huo.
 Viongozi mbalimbali wakiwa meza kuu wakati wa uzinduzi huo.
 Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, John Mgodo (katikati), akiangalia simu wakati akiwaelekeza namna ya kutumia simu wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Azania,  Peter Riima (kushoto) na Mrashani Katebeleza, wakati wa uzinduzi wa Programu ya kuwawezesha wanafunzi kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mkononi na vifaa vingine vya kielektroniki Dar es Salaam leo. Kulia ni Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez.
 Hapa uzinduzi huo ukifanyika.
 ‘ Ni kama anasema’ Niacheni nipo kazini nachukua tukio hili nikawahabarishe wengine, chezea mimi nyiee
 Wadau mbalimbali na wanahabari wakiwa kwenye 
hafla hiyo ya uzinduzi.
Wadau na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana wa Jangwani wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 
Dotto Mwaibale
WANAFUNZI nchini wametakiwa kutumia mitandao hasa ya simu za mikononi kwa ajili ya kujifunzia masomo mbalimbali badala ya kutumia katika matumizi yasiofaa.
Mwito huo umetolewa na Naibu  Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia, John Mgodo wakati wa uzinduzi wa Programu ya kuwawezesha wanafunzi kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mkononi na vifaa vingine vya kielektroniki uliofanyika Dar es Salaam leo.
Alisema progamu hiyo imefika wakati muafaka na itawasaidia wanafunzi kujifunza somo hilo muhimu katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.
Alisema programu hiyo imeletwa nchini na Kampuni ya Nokia, Tigo kwa kushirikiana na Microsoft,  ambapo serikali kupitia Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) inasimamia kwa karibu mpango huo.
Alisema Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi katika programu hiyo imesaidia kupata mahudhui ya kihisabati jambo litakalo wasaidia wanafunzi kuwa makini kitaaluma.
Alisema matumizi hayo ya simu katika kujifunza hisabati yatakuwa yakifanyika katika muda wa ziada baada ya masomo kwa vile licha ya wanafunzi kumiliki simu lakini hawaruhusiwi kuwa nazo mashuleni.
Mgodo alisema mpango huo kwa sasa upo katika majaribio ukifanikiwa wanaweza kuuingiza katika mitaala ya taifa.
Mtaalamu wa mradi huo kutoka Kampuni ya Nokia, Riita Vanska alisema mpango huo umekuwa ukiongeza weredi kwa wanafunzi katika somo la hisabati na ni muhimu katika kipindi hiki cha maendeleo ya Sayansi na Teknolojia.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia Dk.Hassan Mshinda alisema tume hiyo ilifanyamchakato na kuukubali mpango huo ambao ni muhimu hasa katika kipindi hiki ambacho taifa linaupungufu mkubwa wa wataalamu wa sayansi wanaotokana na kufaulu kwa somo la hisabati.
“Mradi huu tuliona unafaa kwani utasaidia kuongeza wanasayansi hivyo tuliupokea kwa mikono miwili” alisema Dk.Mshinda.

Serikali Mkoani Tanga yachukua Tahadhari Mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola

???????????????????????????????Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga Dr. Asha Mahita akizungumza na wajumbe muda mchache  kabla ya Mgeni rasmi kufungua kikao rasmi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Halima Dedengo na kulia Chama cha Watoa Huduma binafsi za Afya Nchini, Dr. Samweli Ogillo.
???????????????????????????????Wajumbe wa Kikao wakisikiliza kwa makini
SERIKALI  imetoa rai kwa wananchi kutoa taarifa kwa mgonjwa yeyote mwenye  dalili ya ugonjwa wa Ebora ili aweze kupati msaada wa kitabibu hali ambayo itapunguza maambuzi kwa watu wengi .
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilya ya Tanga wakati akifungua kikao cha maelekezo huhusu ugonjwa hatari wa Ebola na dhana ya ushirikiano baina ya Sekta binafsi na Sekta ya Umma kwa madaktari na wauguzi kutoka serikalini na sekta binafsi kilichofanyika leo katika ukumbi wa Rodasaksa Hospiali ya Mkoa wa Tanga (Bombo).
Kikao hicho ni moja ya jitihada ambazo zinachukuliwa na Mkoa wa Tanga katika kutoa uelewa  wa ugonjwa huo hatari ambao sasa  umekuwa tishio katika baadhi ya maeneo ya Afrika.  Vile vile ametoa wito kwa sekta ya umma na sekta binafsi kuweka nguvu zao pamoja katika kuhakikisha wanachi wanapata huduma bora za afya.
Akielezea mkakati wa Mkoa dhidi ya jinsi gani Mkoa umejiandaa endapo atapatikana mgonjwa wa Ebola katika Mkoa wa Tanga, Kaimu Mganga  Mkuu wa Mkoa  wa Tanga Dr Asha Mahita amesema kuwa tayari maeneo mbalimbali yenye vifaa maalumu yametengwa ili kutoa huduma ya kitabibu kwa wagonjwa wa aina hiyo. Maeneo hayo ni pamoja na eneo la Masiwani lilipo jengo la Hospitali ya Wilaya ya Tanga na kituo kingine kipo Mpakani Horohoro.
Serikali pia imekuchukua tahadhali katika maeneo ya mpakani hasa eneo la Horohoro  mpaka wa Tanzania na Kenye na uwanja wa ndege kwa kuweka kifaa maalumu cha kuweza kupima na kutambua msafiri mwenye maambukizi ya  Ugonjwa wa Ebola. Hatua ambayo imefikiwa baada ya kusikia kuwepo mlipuko wa ugonjwa huo katika nchi za jirani na hasa Afrika.
Akifafanua dhana ya ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi katika kutoa huduma za afya, Dr.Samweli Ogillo ambaye ni Mtendaji Mkuu kutoka chama cha Watoa huduma Binafsi  Nchini ( APHFTA)amesema ni jambo la msingi iwapo Serikali na Sekta binafsi zitaweka nguvu ya pamoja ili kudhibiti na kuzuia ebola kuingia nchini kwa sababu upande mmoja peke yake hauwezi.
Hadi sasa hakuna mgonjwa yeyote mwenye dalili ya ugonjwa wa Ebola ambaye ameripotiwa kupatikana katika nchi ya Tanzania.  Historia inaonyesha mwaka 2012  Mwezi wa Julai ulitokea mlipuko wa ugonjwa wa Ebola  magharibi mwa Uganda eneo linaitwa Kabaale ambapo zaidi ya watu 14 walipoteza maisha.
Ebola ni ugonjwa hatari unaosababishwa na virusi vijulikanavyo kwa lugha ya kitaalamu “Ebola Virusi na husambaa kwa haraka sana . Dalili zake ni pamoja na homa kali inayoambatana na kutokwa damu katika matundu yote ya mwili kama pua, njia ya haja kubwa na ndogo, mdomoni, machoni kutapika na kuharisha damu. Stori & Picha na Monica Laurent, Afisa Habari Tanga

RAIS KIKWETE AREJEA NCHINI KUTOKA MAREKANI KWENYE MKUTANO WA 69 WA UMOJA WA MATAIFA

jk1 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadik  baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa. jk2Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mnadhimu Mkuu  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi  Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samuel Ndomba mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa. jk3 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na IGP Ernest Mangu, Mnadhimu Mkuu  wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi  Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samuel Ndomba na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Saidi Meck Sadik  baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa. jkk1
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama   baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo Septemba 30, 2014 akitokea Marekani alikohudhuria Mkutano wa 69 wa Umoja wa Mataifa. 
PICHA NA IKULU

Wazee walalamikia kunyanyapaliwa na wahuduma wa Afya

Maadhimisho ya Siku ya Wazee Kitaifa Mkoa wa Katavi tarehe 01 Oktoba 2014 (1)
Wazee wakiwa kwenye kongamano la wazee kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Mpanda kujadili changamoto zinazowakabili wakati wa kupatiwa matibabu.
Na Kibada  Kibada-Katavi.
Wahudumu wa Afya wameendelea kuwanyanyapaa wazee wawapo hospitalini kupata huduma ya Afya kwa kuwaacha wakae asubuhi hadi jioni ,huku wenyewe wakifanya kazi zao nyingine.
Pia wakitibiwa na Daktari  mara nyingi huambiwa wakatafute dawa madukani hata kama zipo hospitalini na ukiuliza kwa nini hujibu hawahitaji usumbufu.
Hayo yameelezwa na Katibu wa Shirika la Wazee saidia lenye makao yake Wilayani  Kasulu Mkoani  Cotlida Kokupima wakati akiwasilisha salamu za wazee kutoka Mkoani kigoma kwenye kongamano la wazee lililofanyika Mjini Mpanda Mkoa wa Katavi.
Bibi Kokupima ameeleza changamoto zinazowakabiliwa wazee katika maeneo mbalimbali zikiwemo na manyanyaso hayo wanayofanyiwa wazee wakiwa katika Zahanati,Vituo vya Afya Pamoja na Kwenye Hospitali mbalimbali hapa nchini.
Changamoto hizo ni kuwa wakienda kutibiwa na wakishaandikiwa dawa wanaambiwa hazipo waende wakanunue madukani wakati mwingine wanakuwa hawana hela matokeo yake wanarudi nyumbani kulala bila kupata dawa na mwisho ni kufa.
Changamoto ya usafiri kutoka nyumba hadi kufika kwenye huduma za jamii hasa matibabu kwa wazee wenye umri mkubwa ni taabu,hawana uwezo wa kuzifuata dawa dukani hata kama watakuwa na fedha.
Kwa Upande wake mwakilishi wa shirika la Afya la Wazee Duniani Athman Daniel ameeleza kuwa shirika lake kwa kusaidiana na wadau mbalimbali na wazee limeweza kuchangia kuisukuma serikali kuona uwezekano wa kuwapatia wazee malipo ya uzeeni na mchakato unaenda vizuri na  wakati wowote suala hilo litafanikiwa.
Akizungumzia Halmashauri ya Mpanda amesifu juhudi zilizofanywa  katika kuwahudumia wazee kwa kutenga chumba cha kiliniki ya wazee na wanapatiwa huduma hapo.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni “WAZEE WASIACHWE NYUMA TUJENGE JAMII SHIRIKISHI KUPITISHA SHERIA YAO.

NYUSI AKUTANA NA WANAMSUMBIJI WA ZANZIBAR

 Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi akipokea zawadi kutoka kwa Jumuiya ya watu wa Msumbiji wanaoishi Zanzibar.
Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi akizungumza na Wananchi wa Msumbiji wanaoishi Tanzania ambapo alitumia fursa hiyo kuwaomba wampigie kura kwani amekuja na mikakati mizuri ya kuboresha uchumi ambapo amedhamiria kuiondoa Msumbiji kwenye orodha ya nchi masikini,pia aliahidi kuwawezesha wakina Mama wa Msumbiji.
Wananchi wa Msumbiji wanaoishi Zanzibar wakisikiliza sera za Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi kwenye mkutano uliofanyika katika Hotel ya Zanzibar Beach Resort.
Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi akiongozana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wa Msumbiji wanaoishi Zanzibar Asilia Lunji baada ya kumaliza mkutano wake wa kampeni kwa wapiga kura wanaoishi Zanzibar,Nyusi aliwaambia kuwa amefanya mkutano wa kwanza nchini Tanzania kwa sababu ya mahusiano mazuri baina ya Msumbiji na Tanzania
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi mara baada ya mgombea huyo kumaliza ziara yake Zanzibar. Mgombea wa Urais wa Msumbiji kupitia chama cha FRELIMO Mh.Filipe Nyusi akiwaaga wananchi wa Zanzibar

DK.SHEIN AWAAPISHA WAKUU WAPYA WA WILAYA PEMBA

IMG_8061Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Amran Masoud Amran kuwa Mkuu wa Wilaya ya Wete Pemba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo jioni,kabla ya uteuzi huo alikuwa Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Pemba,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_8158Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Hemed Suleiman Abdulla kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkoani  Pemba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo jiono,kabla ya uteuzi huo alikuwa Afisa Mdhamini  Wizra ya Biashara,Viwanda na Masoko,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_8173Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Jabu Khamis Mbwana kuwa Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Pemba  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo ,kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkuu wa Wilaya Mkoani Pemba,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_8195Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Bibi SSP Sida Mohamed Himid kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini A Unguja  katika ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo ,kabla ya uteuzi huo alikuwa Afisa Mdhamini Ofi ya Makamo wa Pili wa Rais Pemba,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] IMG_8222Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Mohammed  Faki Mohammed kuwa Mwenyekiti wa Kamisheni ya Utumishi wa Umma katika Ukumbi wa Ikulu Mjini Zanzibar leo ambapo anaendelea na kazi hiyo kwa kipindi chengine cha miaka mitatu,[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Azam yadhamini maonesho makubwa ya Keki Dar

Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan wazamini wa maonesho hayo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan wazamini wa maonesho hayo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan wazamini wa maonesho hayo.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan wazamini wa maonesho hayo.
Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias.
Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan wazamini wa maonesho hayo na kulia ni Meneja Bidhaa za Azam, Abubakar Suleiman.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan wazamini wa maonesho hayo na kulia ni Meneja Bidhaa za Azam, Abubakar Suleiman.
Dar es Salaam
KAMPUNI ya Insights Productions Limited kwa udhamini wa Kampuni ya Azam Tanzania imeandaa maonesho makubwa ya keki yanayotarajia kufanyika jijini Dar es Salaam na kuwakutanisha wadau mbalimbali wa uandaaji na utayarishaji wa keki. Maonesho hayo yatajulikana kama ‘Azam World of Cakes Exhibition’.
Akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Insights Productions Limited, Marion Elias alisema maonesho hayo yanatarajiwa kuwakutanisha wadau mbalimbali binafsi, makampuni na taasisi waandaaji wa keki nchini Tanzania ikiwa ni sehemu ya kubadilishana uzoefu na kujifunza ubunifu zaidi wa shughuli hizo.
Bi. Elias alisema dhumuni la maonesho hayo ambayo yanatarajiwa kufanyika Desemba 6, 2014 jijini Dar es Salaam ni pamoja na kusherehekea taaluma ya uokaji keki kwa kuonesha ubunifu na utaalam wa utengenezaji na upambaji wa keki bidhaa inayopendwa na watu wengi na kutumika katika shughuli anuai za kijamii. Alisema washiriki wa tamasha hilo mbali na kushindanisha na kuonesha bidhaa zao za keki pia wanatarajia kupata semina ya mafunzo juu ya utengenezaji bora wa keki ikiwa na lengo la kuboresha zaidi taaluma zao.
Alisema washiriki hao pia watafanya maonesho ya utayarishaji wa vyombo vya kutengenezea keki, utayarishaji wa unga wa ngano kwa ajili ya kupikia keki, kutambua unga bora wa keki, uchanganyaji wa unga na viungo vingine kwa ajili ya uboreshaji wa radha ya keki.
Alisema maonesho mengine yatakayofanywa na wadau hao wa keki ni pamoja na uhifadhi bora wa keki kwa muda mrefu bila kuharibika na washiriki kuonesha maumbo mbalimbali ya keki yenye mvuto kwa watumiaji wa keki na jamii nzima.
Alisema maonesho hayo yanayodhaminiwa na Azam watengenezaji wa unga bora kwa ajili ya kutengenezea bidhaa hiyo, yatawashindanisha wadau wa uandaaji keki na pia washindi watakao tajwa na majaji wa maonesho watajipatia fedha taslimu na bidhaa mbalimbali.
“…Onesho hili litahusisha jamii yote inayojishughulisha na utengenezaji wa keki, upambaji wa keki, wauzaji wa keki na wanaojishughulisha na bidhaa mbalimbali zinazotumika kutengeneza keki kama vile unga wa ngano wa Azam,” alisema Mkurugenzi wa Insights Productions Limited, Bi. Elias.
Akifafanua zaidi Mkurugenzi huyo alisema onesho hilo litajumuisha bekari na hoteli mbalimbali, Vyuo vya taaluma ya hotelia toka Tanzania na majirani (Afrika Mashariki) pamoja na watengenezaji keki binafsi. Wananchi watakaotembelea maonesho hayo ambayo hayata kuwa na kiingilio watapata fursa ya kujionea aina na mitindo mbalimbali ya utengenezaji wa keki pamoja na kuonja bidhaa hiyo kwenye maonesho ambayo yatafanyika Serena Hoteli jijini Dar es Salaam.
Akizungumzia maonesho hayo Mratibu wa Matangazo na Uhusiano wa Umma wa kampuni ya SSB, Mohammed Ramadhan alisema Azam ikiwa ni kampuni inayotengeneza unga bora wa kutengenezea keki imeamua kudhamini ikiwa ni ishara ya kutambua taaluma hiyo ya uokaji keki nje na ndani ya Tanzania. *Imeandaliwa na www.thehabari.com

ILIVYOKUWA JANA WAKATI WA UPIGAJI KURA BUNGE MAALUM LA KATIBA WAENDELEA

PG4A1469Wahudumu wa Bunge wakibeba masanduku ya kura  ili kuyapeleka kwenye  chaumba cha kuhesabia kura  baada ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kumaliza kazi ya kupiga kura Septemba 30, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
PG4A2397Wajumbe wa Bunge  Maalum la Katiba,  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na  Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka  wakiteta bungeni Mjini Dodoma Septemba  30, 2014. Kushoto ni Spika wa Bunge, Anne Makinda (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

programu ya kujitolea kwa vijana yahitimishwa

IMG_8294Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akiongea na wahitimu wa program ya kujitolea ya Vyuo Vikuu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa VSO International Tanzania Bw. Jean Van Wetter IMG_8331Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel aleyekaa katikati katika picha ya Pamoja na wahitimu wa Programu ya kujitolea kwa Vijana Wahitimu wa Vyuo Vikuu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa VSO International Tanzania Bw. Jean Van Wetter.
IMG_8278Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel katikati akimpa Cheti Dada Ndidi Tumpe wakati wa kuhitimisha Programu ya kujitolea kwa Vijana Wahitimu wa Vyuo Vikuu katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kulia ni Mkurugenzi Mkazi wa VSO International Tanzania Bw. Jean Van Wetter.
Picha na Benjamin Sawe

Shirika la Nyumba la Taifa lakabidhi mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana Kigoma

 Meneja wa Mkoa NHC, Nistas Mvungi akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Issa Machibya mashine 32 za kufyatulia matofali ya kufungamana.
  
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Ujiji akishukuru Shirika kwa kuwapatia vijana mashine ya hydraform.
  
Wafanyakazi wa NHC na kikundi cha Vijana Kwanza Group  na wageni waalikwa wakisubiria Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa Mhe Kanali Issa Machibya.
 Meneja wa Shirika la Nyumba Kigoma Ndg Nistas Mvungi akijadiliana na Mkuu wa Mkoa Mhe Issa Machibya jambo kuhusiana na Mashine ya matofali ya kufungamana kuhusu ufanisi wake na ajira kwa vijana.
 Picha ya pamoja ya wafanyakazi wa Shirika Mkoa wa Kigoma na Mgeni Rasmi Mkuu wa Mkoa Mhe Kanali Issa Machibya.
 Meneja wa Shirika la Nyumba Ndg. Nistas Mvungi akihutubia wananchi wa Kigoma kuhusu mradi wa mashine za kufyatulia matofali ya kufungamana 32 zilizotolewa na Shirika kwa vikundi vya  vijana wa Mkoa wa Kigoma
 Mkuu wa Wilaya Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Ramadhan Maneno akikabidhi mashine za kufungamana kwa Kikundi cha Vijana Kwanza Group. Mwenyekiti wa kikundi Ndg Daniel George  na Katibu wake wakipokea mashine.
 
  Picha ya pamoja ya kikundi cha vijana kwanza group na mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa. 
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ramadhani Maneno kwa makini kuhusiana na maelekezo yake kuhusu umuhimu wa kutumia matofali ya kufungamana na kuondokana na nyumba za matope.