TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Wednesday, January 11, 2012

FILAMU MPYA YA KITANZANIA THE DOCUMENT MBIONI KUTUA SOKONI


Msanii wa Filamu za Kitanzania , Jamal Yahaya(Gamba la Ukweli) 
Filamu Mpya ya Kitanzania iliyotengenezwa na wasanii walioiva katika anga za Filamu hapa nchini, THE DOCUMENT, iko mbioni kukamilika ambayo itaingia sokoni hivi karibuni itakayohusu masula ya mapigano,(ACTION), baada ya kijana Jamal, maarufu kama (GAMBA la Ukweli), baada ya kupotea kwa kipindi kirefu akiwa kambini kwa ajili ya maandalizi katika kuonyesha namna ambavyo Filamu za Action zinavyotengenezwa.
Akizungumzia Filamu hiyo Jamal Maarufu kama Gamba, alisema kuwa "nahitaji kuwaonyesha wacheza filamu za action zinachezwaje, wapenzi watazamaji kaeni mkao wa Paka Kurukia Panya, kwa wale Dada zangu na Mashemeji zangu, ninawataadhalisha kwamba, kabla ya kuanza kuitazama pikeni chakula msije kuunguza na kufukuzwa na waume zenu, maana hii Filamu ni nzuri na ya kusisimua, inayoweza kukufanya usiondoke eneo hilo wakati uiangaliapo, na kwa wale masupa staa wanaotubagua sisi wasanii wachanga(Andergroud), na hakika mwaka huu watatukubali  kwa sababu tumefanya vitu vya Ukweli na kwa uwezo zaidi ili tusiwaongopee wananchi, nakuomba mpenzi mtazamaji wa filamu za ACTION popote utakapokuta filamu ya The Document usisite kuinunua kwani utafurahia radha iliyomo kama ulaya vile, napenda kuwashukuru ndugu yangu James wa shinyanga kwa kunivuta mkono na kuwezesha kazi hii kukamilika, vilevile namshukuru Swaga Production kwa kuitendea haki Filamu hii,  wenzangu tulioshirikiana nao katika kazi nzima baadhi yao wakiwa ni Kitundu (Hong Back), Sakayonsa(Jembe Ulaya), Lucas(Master Lee), Binti Munila(Krishina),na wengine wengi ambao mtawaona baada ya Filamu kuingia Sokoni, wapenzi watazamaji angalieni The Document, ujumbe wangu ni kwamba KAENI MAKINI UNGA ROBO "alisema Gamba
Filamu ambazo ameshiriki Gamba na tayari ziko sokoni ni tatu zikiwemo za Bon to safe, How is Killer, na ile ya Furaha iko Wapi iliyoshirikishwa msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Twent per Cent.

No comments:

Post a Comment