TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Monday, July 28, 2014

Kocha Marcio Maximo ‘The Chosen One’ hataki kubahatisha, anafuata Juma Kaseja halafu Ally Mustapha ‘Barthez’

Yanga wameamua, Maximo hataki kubahatisha

Wachezaji wa timu ya Yanga wakiwa mazoezini. Picha na Michael Matemanga
Katika makabrasha ya Mbrazili huyo kila siku anaingiza jina au kulifuta jingine katika nafasi za uwanjani na anafanya hivyo kutokana na viwango vya
YANGA kweli wameamua. Kocha Marcio Maximo ‘The Chosen One’ hataki kubahatisha na kuanzia sasa kila nafasi katika kikosi chake itakuwa ina watu wa uhakika wasiopungua watatu.
Katika makabrasha ya Mbrazili huyo kila siku anaingiza jina au kulifuta jingine katika nafasi za uwanjani na anafanya hivyo kutokana na viwango vya
wachezaji wake mazoezini. Anayepungua anafutwa katika orodha na ambaye kiwango kinapanda anaingizwa jina. Kocha huyo anayafanya hayo kuhakikisha anakuwa na kikosi imara chenye ushindani uwanjani.
Mwanaspoti lina uhakika na mpango huo wa Maximo ambao utamwezesha kuwa na kikosi imara cha ushindani ambacho kitaweza kupigania pointi tatu katika kila mechi watakayocheza pale pazia la Ligi Kuu Bara litakapofunguliwa.
Tangu alipoanza kuifundisha Yanga Julai Mosi, kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, amekuwa akiwatazama kwa makini wachezaji wote na kuandika majina yao kitabuni pia akifuatilia taarifa za wachezaji wake walio katika timu za taifa; Taifa Stars, Rwanda na Uganda.
Akianzia golini, Maximo katika kabrasha lake amepanga namba moja ni Deo
Munishi ‘Dida’, anafuata Juma Kaseja halafu Ally Mustapha ‘Barthez’ na kinda Said Ally wa kikosi B amewekwa namba nne.
Nafasi nyingine yenye idadi ya wachezaji wanne huku anayetakiwa kucheza akiwa mmoja ni ile ya ushambuliaji ambayo wapo Genilson Santana ‘Jaja’,
Jerry Tegete, Said Bahanuzi na Hussein Javu. Jaja ndiye wa kwanza hapo.
Katika beki ya kulia, Maximo anao Juma Abdul na Salum Telela huku anayeanza akiwa Abdul. Katikati wapo Kelvin Yondani, Pato Ngonyani na Issa
Ngao kutoka Yanga B kama mabeki wa mwisho huku Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Rajab Zahir wakiwa mabeki wa kati wakabaji. Hapo wanaoanza ni Yondani na Cannavaro.
Beki ya kushoto ndipo kuna dosari kidogo kwani Maximo anaye Oscar Joshua na kinda Amos Abel anayetoka kikosi B.

No comments:

Post a Comment