TAN

TAN

Bayport

Bayport

Kikoa

Kikoa

Myway entertainment

Myway entertainment

FORE PLAN CLINIC

FORE PLAN CLINIC

MPINGA CUP 2016

MPINGA CUP 2016

Mashujaa Fm 89.3, Lindi

Saturday, August 2, 2014

WENGER: MESSI ALIMFANYA SANCHEZ AHANGAIKE BARCELONA KAMA ILIVYO KWA NEYMAR

Wenger: Messi made Alexis suffer at Barcelona
NA BARAKA MPEJA
ASERNE Wenger anaamini Alexis Sanchez aliathirika kama anavyoathirika Neymar wakati akiwa Barcelona kutokana na uwepo wa Lionel Messi.
Asernal ilitumia Euro milioni 40 kumsajili nyota huyo wa kimataifa wa Chile majira haya ya kiangazi na leo hii anatarajia kucheza mechi yake ya kwanza ya maandalizi ya msimu mpya.
Licha ya kucheza kama winga akiwa Barca, Alexis atachezeshwa kama mshambuliaji Emirates na Wenger anaamini atang`ara zaidi katika nafasi hiyo kutokana na kutokuwepo kwa ‘mchawi’ wake Messi.
“Kwa mara ya kwanza alitinga katika rada zangu alipokuwa Udinese na baadaye Barcelona”. Alisema Mfaransa huyo alipozungumza na The Dail Mirror.
“Ni mshambuliaji. Ni mmaliziaji mzuri ambaye alikuwa na kiwango kizuri Italia. Nilimuona pale na alikuwa amesimama vizuri. Lakini mambo yalikuwa magumu alipoenda Barcelona kama ilivyo kwa Neymar sahizi”.
“Unapomuona Neymar wa Brazil na Neymar wa Barcelona sio mtu mmoja. Naamini kuwa Alexis anaweza kucheza kushoto, kulia na mbele na ndio maana nilimfuata”.

No comments:

Post a Comment